DNPC DONGOBESH

DNPC DONGOBESH ⛪ Blessed Valley Church
✨ Neno | Maombi | Kuhubiri
📍 Dongobesh, Manyara

Tumekuwa na Ibada ya Baraka ambayo imejawa na nguvu za Mungu hakika Mungu alitenda na tulipata kibali cha kuwa na wageni...
31/05/2026

Tumekuwa na Ibada ya Baraka ambayo imejawa na nguvu za Mungu hakika Mungu alitenda na tulipata kibali cha kuwa na wageni wengi kutoka maeneo mbalimbali

Tumekuwa na wakati mzuri wa kuwa mbele za Mungu leo katika mafundisho na maombi ya nguvu hakika Mungu alionekana na siku...
23/05/2026

Tumekuwa na wakati mzuri wa kuwa mbele za Mungu leo katika mafundisho na maombi ya nguvu hakika Mungu alionekana na siku ya kesho itakuwa siku rasmi kwaajili ya Roho Mtakatifu kujidhirisha kwa watu wake

Hakikisha hautakosa siku hiyo Baraka kabisa

SIKU YA PILI YA SEMINA REV NELSON KAAYAMika 4:1Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya Bwana ...
21/05/2026

SIKU YA PILI YA SEMINA

REV NELSON KAAYA
Mika 4:1
Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi.

Isaya 2:2
Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi.
-
Katika kipindi hiki cha sikukuu tuombe Roho Mtakatifu ajidhihirishe kwetu maana alishakuja kilichobaki ajiridhihirishe kwetu,

Semina hii wapo watu Mungu amewachagua kuwahudumia, Jiadae vyema maana Mungu anahitaji kukuhudumia wewe sasa

Tunatakiwa tuingie vizuri ndani ya wokovu, kanisa ni dola ya Mungu, Mungu ameliandaa kanisa ili liwe nuru na liwe chumvi katika zama hizi Mungu anatuhitaji zaidi

Ndani ya mtu kuna ukiwa ama pengo ambapo hakuna mtu mwingine anaweza kujaza ila ni Mungu tu peke yake

Ibada ni tendo la heshima ya hali ya juu ambayo hakuna mwingine anaweza kutendewa ila Mungu tu

Kwa unyenyekevu tuchukue nafasi hii kuwakaribisha wote katika semina ya pentekosteMungu awabariki
18/05/2026

Kwa unyenyekevu tuchukue nafasi hii kuwakaribisha wote katika semina ya pentekoste

Mungu awabariki

REV MATHEW JACOBMAANDALIZI YA WATU WA MATAIFA KUPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFUMithali 16:1Maandalio ya moyo ni ya mwana...
17/05/2026

REV MATHEW JACOB
MAANDALIZI YA WATU WA MATAIFA KUPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU
Mithali 16:1
Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.
-
Watu ambao walikua wamepuunzwa walitamani kipawa cha Roho Mtakatifu ndipo wakafanya maandalizi Neema ya Mungu ikawajilia wakapokea kipawa cha Roho Mtakatifu
-
Matendo ya Mitume 10:1-4
1.Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2.Mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.

3.Akaona katika maono waziwazi, k**a saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio!

4.Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.
-
Tuhakikishe katika Ibada zetu tunazofanya ziwe zinazoleta ukumbusho mbele za Mungu, kwa kufanya maandalizi kwa maisha yetu

Roho Mtakatifu anahitaji uwe na maandalizi iliaje kwako, kiuhalisia kila kitu ambacho kinatakiwa kiwe kizuri kinahitaji maandalizi mazuri ili kitokee
Mungu si watu flani tu pekee bali Mungu niwa watu wote dunia na Roho Mtakatifu ni kwa wote waliojiandaa

Ukiandaa moyo wako utakipokea kipawa cha Roho Mtakatifu na atakuwa kwako k**a ilivyotokea kipindi cha mitume itakuwa kwako hivi leo pia.

REV MATHEW J TSUUTMUHIMU WA KUBATIZWA NA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU ANDIKO KUUMathayo 3:11-12, Matendo ya Mitume 1:8, Warumi...
10/05/2026

REV MATHEW J TSUUT
MUHIMU WA KUBATIZWA NA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU

ANDIKO KUU
Mathayo 3:11-12, Matendo ya Mitume 1:8, Warumi 8:26-28

UTANGULIZI
Katika nyakati hizi watu wengi wanazungumzia mafanikio, miujiza, na baraka, lakini wameacha kuzungumzia habari za Roho Mtakatifu. Yesu mwenyewe aliacha agizo wazi kwamba waamini wanapaswa kubatizwa na kujazwa Roho Mtakatifu ili wawe na nguvu, ujasiri, na maisha ya ushindi.

Kubatizwa na Roho Mtakatifu si jambo la hiari kwa Mkristo; ni hitaji muhimu kwa maisha ya wokovu na huduma.

MAANA YA KUBATIZWA NA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU
1.KUBATIZWA NA ROHO MTAKATIFU
Ni tukio la kwanza ambapo mwamini anapokea nguvu na uweza wa Roho Mtakatifu ndani yake.

Mathayo 3:11
“Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.”
Yesu ndiye mbatizaji wa kweli wa Roho Mtakatifu.

2.KUJAZWA ROHO MTAKATIFU
Ni hali ya kuendelea kujazwa uwepo, nguvu, na uongozi wa Mungu kila siku.

Waefeso 5:18
“... mjazwe Roho.”
Mkristo hawezi kutegemea uzoefu wa zamani pekee; anahitaji kujazwa kila mara.

UMUHIMU WA KUBATIZWA NA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU
1.HUTUPA NGUVU NA UJASIRI
Matendo 1:8
“Mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu.”
Petro aliyemkana Yesu aliweza kusimama kwa ujasiri baada ya kujazwa Roho Mtakatifu.

Bila Roho Mtakatifu:
Tunaogopa,
Tunarudi nyuma,
Tunashindwa kusimama katika kweli

Lakini kwa Roho Mtakatifu:
Tunakuwa mashahidi,
Tunanena kwa ujasiri,
Tunashinda majaribu.

2.HUTUFUNDISHA KWELI YOTE
Yohana 16:13-14
“Atawaongoza awatie kwenye kweli yote.”

Roho Mtakatifu:
Hufungua akili kuelewa Neno,
Hututenga na uongo,
Hutuonyesha mapenzi ya Mungu.
Bila Roho Mtakatifu mtu anaweza kuwa kanisani lakini asiijue kweli.

3.HUTUSAIDIA KUOMBA
Warumi 8:26-27
“Roho naye hutusaidia udhaifu wetu...”
Wakati mwingine:
Hatujui tuombe nini,
Hatuna maneno,
Tunaelemewa na mizigo.

Lakini Roho Mtakatifu:
Hutuamsha kuomba,
Hutufundisha kuomba,
Hutuombea mbele za Mungu.
Bila Roho Mtakatifu maombi yanakuwa ya kawaida na yasiyo na nguvu.

4.HUTUSAIDIA KUMWABUDU MUNGU KATIKA ROHO
Yohana 4:24
“Mungu ni Roho...”
Ni ibada inayotoka moyoni kwa msaada wa Roho Mtakatifu.
Pasipo Roho Mtakatifu:
Ibada inakuwa mazoea,
Huduma inakuwa kazi,
Ukristo unakuwa mzigo.

HITIMISHO
Kanisa la leo linahitaji kurudi katika nguvu za Roho Mtakatifu.

WITO
Je, umebatizwa na Roho Mtakatifu?
Je, bado unajazwa kila siku?
Je, maisha yako yanaonyesha matunda ya Roho?
Leo Mungu yuko tayari kukujaza upya kwa Roho Mtakatifu.

REV MATHEW J TSUUT AGIZO LA KUJAZWA ROHO MTAKATIFUMatendo 4:31Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusany...
03/05/2026

REV MATHEW J TSUUT
AGIZO LA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU
Matendo 4:31
Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.

REV JOSEPHAT KYARUZIUDHIHIRISHO WA NGUVU ZA MUNGU KATIKA MAISHA YA MWANADAMU1 Wakorintho 2:1-15[4] “Na neno langu na kuh...
26/04/2026

REV JOSEPHAT KYARUZI
UDHIHIRISHO WA NGUVU ZA MUNGU KATIKA MAISHA YA MWANADAMU

1 Wakorintho 2:1-15
[4] “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
[5] ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.”

1Thes 1:5
[5]ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; k**a vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu.

1. UTANGULIZI
Wakristo wengi wanajua habari za Mungu lakini hawajaona madhihirisho ya nguvu za Mungu katika maisha yao. Kanisa limejaa maneno mengi, falsafa nyingi, na elimu nyingi; lakini mara nyingi lina upungufu wa udhihirisho wa nguvu za Mungu.

Nguvu za Mungu si hadithi. Nguvu za Mungu ni uhalisia unaoleta matokeo katika maisha ya mwamini.

Leo tutajifunza jinsi nguvu za Mungu zinavyofanya kazi na matokeo yake katika maisha ya mtu binafsi, kanisa, na jamii.

2. MAANA YA NGUVU ZA MUNGU
Nguvu za Mungu ni ushihirisho wa mabadiliko ya kweli pale:
• Neno la Mungu linapohubiriwa (ms. 4, Mdo 2:37, Ebr 4:11)
• Maombi yanapofanyika;
• Roho Mtakatifu anaposhuka;
• Unabii na karama zinapotenda kazi.

Nguvu za Mungu si kelele, si hisia tu, bali ni uwezo wa Mungu kubadilisha hali.

Rejea:
1Kor 1:18
“Kwa maana neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi; bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.”

SIRI KUBWA: Nguvu ya Mungu imebebwa katika Msalaba wa Yesu Kristo.
• Msalaba huokoa
• Msalaba huponya
• Msalaba huweka huru
• Msalaba hushinda dhambi na nguvu za giza

3. UDHIHIRISHO WA NGUVU ZA MUNGU – SIKU YA PENTEKOSTE

Matendo 2:1-47
Siku ya Pentekoste tunaona matokeo makubwa ya nguvu za Mungu ndani na nje ya Kanisa.

Ndani ya Kanisa:
• Mitume walijawa na ujasiri
• Waliokuwa dhaifu wakawa imara
• Waliojificha wakaanza kushuhudia

Nje ya Kanisa:
• Watu waliingiwa na mshangao
• Watu waliguswa mioyoni
• Watu 3000 wakaokoka siku moja
• Miujiza na ishara zikaonekana

21/04/2026

Nguvu ya kuendelea mbele | Rev Mathew Jacob

BISHOP MATHEW J TSUUTMatendo 1:6-8[6]Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudi...
19/04/2026

BISHOP MATHEW J TSUUT
Matendo 1:6-8
[6]Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?

[7]Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.

[8]Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Kanisa ni mahali pa kupokea nguvu za Mungu. Ni mahali pa kupokea majibu ya maswali yako.

Nguvu ya Mungu ya kuokoa na kuponya.

Yesu kufufuka kweli kweli kulifungua awamu mpya. Wanafunzi walitaka kujua iwapo ni Wakati wa Kupokea Ufalme?

Baada ya Kuokoka na Kubatizwa,

Matendo 10:44-48
[44]Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.

Zaburi 84:4-7
[4]Heri wakaao nyumbani mwako,
Wanakuhimidi daima.
[5]Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako,
Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.

Kanisa tunamwitaji roho Mtakatifu ili kuendelea
Roho Mtakatifu anatusaidia kuvuka toka

Mithali 1:32-33
[32]Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua,
Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
[33]Bali kila anisikilizaye atakaa salama,
Naye atatulia bila kuogopa mabaya.

Tukataa roho ya kurudi.

Kutoka 14:15-16
[15]BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele.
[16]Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya; nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu.

Utapita katika nchi kavu.

Nguvu ni uweza kupita katika ya changamoto na upinzani.

Kataa hali ya Kanisa kurudi nyuma. Mungu anatupa Madaraka na Nguvu ya Kushinda katika maisha yako.

Mtume Paulo alisisitiza kutembea katika Nguvu za Mungu wala usitumaini hekima ya Wanadamu .

1 Wakorintho 2:4-5
[4]Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
[5]ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.

Address

DONGOBESH
Mapumulo

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when DNPC DONGOBESH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to DNPC DONGOBESH:

Share