Yesu Ni Njia Ministries

Yesu Ni Njia Ministries Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Yesu Ni Njia Ministries, Christian church, Ouganda, Kampala.

11/06/2022
Tuna Shukuru Mungu kwaku tu saidiya ku anzisha rasmi shirika yetu GOD'S HELP FOUNDATION INTERNATIONAL. Tume anza naku ga...
05/06/2022

Tuna Shukuru Mungu kwaku tu saidiya ku anzisha rasmi shirika yetu GOD'S HELP FOUNDATION INTERNATIONAL.
Tume anza naku gawiya watoto mavazi!

Mungu aendelee ku bariki watu wanaona sapoti maono iyi.

01/06/2022

THIBITISHA UPENDO WAKO KWA KUVUNA NAFSI

Yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho (2 Wakorintho 5:19).

Wajibu wetu wa kiinjilisti ni jambo ambalo mbingu yote inalichukulia kwa uzito. Cha kusikitisha, wengi hawaelewi jinsi hili lilivyo na uzito. Kuna Wakristo ambao bado wanauliza ikiwa mtu ambaye havuni nafsi ataenda mbinguni au la. Swali la kuuliza watu k**a hao ni, “Ikiwa mtu hampendi Mungu, au kumpenda Yesu, je, mtu huyo ataenda mbinguni?” Hilo haliwezi kutokea. Biblia inasema, “…Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye” (1 Yohana 5:1). Ikiwa unampenda Baba, lazima umpende Yesu. 1 Wakorintho 16:22 inasema, “Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maranatha.” Maana yake, na alaaniwe. Uthibitisho wa upendo wako kwa Yesu ni kushika amri Zake—Neno Lake (Yohana 14:15). Neno Lake linasema, “Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe” (Marko 16:15). Kwa hiyo unashika neno hilo kwa kuwa mvunaji nafsi. Mtu anaweza kuuliza, “Vipi kuhusu wale walioishi kabla ya Yesu kuja na hawakuwa na nafasi kabisa ya kuonyesha upendo wao Kwake?” Walikuwa na Neno la Mungu— sheria na amri Zake. Ayubu alisema, “…Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu” (Ayubu 23:12).

Yesu ni Neno (Yohana 1:14). Haleluya! Hivyo, kila mmoja wao alikuwa na nafasi ya wazi ya kuonyesha upendo wake Kwake. Alisema katika Mathayo 28:19; “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi…” Hiyo ina maana kuwafanya wale walio katika ulimwengu wako kuwa wanafunzi; wafundishe juu ya Mungu na maisha ya Ufalme; atausimamisha Ufalme Wake katika nchi.

Upendo wako na kujitolea kwako kwa Bwana lazima kuakisi kujitoa kwako kuihubiri Injili.

God is goodMungu yu mwema
29/05/2022

God is good

Mungu yu mwema

27/05/2022

Mungu awabariki nyote mnaotufwata kwenye page yetu mungu wa yesu ni njiya awe njiya kwenu

26/05/2022

JIFUNZE [JIZOEZE] KUWA PEKE YAKO NA MUNGU

Lakini Yesu mara kwa mara alijitenga akaenda nyikani ili kuomba (Luka 5:16).

Kuna kitu kuhusu faragha. Endapo hauelewi thamani ya faragha, kuna mengi ambayo unaweza kukosa maishani. Ni muhimu sana kuwa na nyakati za kibinafsi peke yako na Mungu. Kabla ya ufunuo hutangulia ufaragha. Unapojifunza thamani ya kuwa na nyakati za faragha za ushirika na Bwana, utastaajabishwa na mabadiliko yatakayotokea katika maisha yako na jinsi utakavyokuwa na ufanisi katika mambo ya Mungu. Kamwe usichukulie kirahisi[kiwepesi] nyakati zako za faragha na Bwana. Labda una baadhi ya watu ambao mara kwa mara wako kwenye mlango wako kwa sababu wanahitaji kukuona au kuzungumza nawe kuhusu jambo moja au lingine. Kuwa mwerevu. Ukitumia muda wako mwingi katika maongezi ya kawaida au yasiyo na maana na wengine, na kutumia muda mdogo kufanya ushirika na Roho, hutoenda kutekeleza mambo makubwa maishani. Yesu alielewa thamani na nguvu ya faragha pamoja na Mungu. Katika Mathayo 14:23, Biblia inasema, “Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani peke yake ili kuomba.” Mstari wetu mkuu unatuonyesha kwamba Alifanya hivi mara kwa mara: “Lakini Yesu mara nyingi aliondoka akaenda nyikani ili kuomba” (Luka 5:16 “NIV”).

Wakati ambapo kila mtu alikuwa akipiga kelele kupata usikivu Wake, aliondoka kwenda nyikani kusali. Hakika, katika tukio fulani, “Alitoroka” ili kwenda kuomba, na walikuwa wakimtafuta. Biblia inasema, “Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko. Simoni na wenziwe wakamfuata” (Marko 1:35-36). Jifunze jambo hili. Jibidishe kuwa na nyakati zako binafsi na Mungu, kila siku.

26/05/2022

K**a kuna mutu waku omba piya kuna mungu wa kusikiya maombi yeremiya 33,3

24/05/2022

UPENDO WAKE UDHIHIRISHWE NDANI YAKO

Kwa maana sisi tulio hai, siku zote twatolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili uzima wa Yesu nao udhihirishwe katika miili yetu ipatikanayo na mauti (2 Wakorintho 4:11).

Uthibitisho kwamba tunaujua upendo wa Mungu ni jinsi tunavyoushiriki na wengine. Je, umewahi kuacha kufikiri kuhusu hilo? Hatujui upendo wa Mungu hadi tuwashirikishe wengine na kuudhihirisha. Yesu alikuwa dhihirisho la upendo wa Mungu. Alikuwa ni upendo wa Mungu katika mwili. Hiyo ni kusema, Alikuwa “mwili” wa upendo. Injili: Mathayo, Marko, Luka na Yohana zinamwonyesha k**a kielelezo cha upendo. Yesu hakuwa na upendo tu; Alikuwa ni upendo uliofanyika kuwa mwili. Hiyo ni moja ya kweli ya kipekee mno kuwahi kufichuliwa. Yesu ndiye udhihirisho kamili wa upendo. Tunasoma katika Biblia kwamba Mungu ni upendo (1 Yohana 4:8), lakini hii haitakuwa na maana yoyote kwako mpaka upate kumjua Yesu. Wengi hufikiri juu ya Mungu kwa dhana mbalimbali. Lakini Yesu alisema, “Ikiwa umeniona mimi, umemwona Baba” (Yohana 14:9). Haleluya! Biblia inasema jinsi Alivyo, ndivyotulivyo katika ulimwengu huu. Mpango wa Mungu ni kujidhihirisha Mwenyewe—tabia, uwezo, na asili Yake ya upendo na haki kupitia kila mmoja wetu. Udhihirisho wa upendo Wake ndani yako na kwa kupitia kwako ni kiashirio kikuu cha ukuaji wa kiroho. Hakika umekomaa kiroho wakati upendo wa Mungu unadhihirishwa zaidi na zaidi katika maneno, mawazo, mtazamo na matendo yako. Kuenenda katika upendo ni udhihirisho wa uzima na asili ya Kristo ambayo iko ndani ya roho yako. Mungu asifiwe! UKIRI

'Tuna shukuru Mungu ku kazi ana endeleya ku fanya kupitiya uduma yetu YESU NI NJIA. kupitia msaada ya watu wenye moyo wa...
21/05/2022

'Tuna shukuru Mungu ku kazi ana endeleya ku fanya kupitiya uduma yetu YESU NI NJIA. kupitia msaada ya watu wenye moyo wa upendo, tume fanyikiwa kupata machines za kushona nguo ambazo zita saidiya wa mama na wadada zetu kujifunza kushona kwa bure.

We thank God 🙏

Address

Ouganda
Kampala

Telephone

+256781423218

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Yesu Ni Njia Ministries posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share