16/06/2023
Isaya 59:1-2" Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarakanisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia."
Rehema inakurudisha vigezo vya wewe kumwangalia Mungu. Uovu ukiwa ndani yako hata k**a upako ni mwingi hakuna kitakachotokea. Kazi kubwa ya uovu ni kuleta mafarakano na Mungu. Unapoinua mikono yako juu ni ishara ya kujifunia mbele za Mungu, anaona damu yako. Damu yako inanena mbele zake –nayo imefarakana naye, haipatani naye – kwa sababu ya uovu.
Kazi za uovu;1. Unakufarakanisha na kuweka uadui na Mungu 2. Kukuondoa mbele za Mungu na kukuweka mbali Yeye.
Damu yako ikikombolewa mafarakano na mali za Mungu yanakoma.
Yohana 15:2 – Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha ili lizidi kuzaa. Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. Kuhani anaweza kutamka neno juu yako – Neno la utakaso – na likatimia.
MAOMBI;
1. Amekuja na hati ya nyongeza – mambo yanahusiana na uhai na mapato; Isaya 38:1
2. Wito wa kuinua vipawa, amaekuja kuinua vipawa.
3. Amekuja kutuambia songeni mbele. Upo karibu na hatma yako, upo karibu na ndoto yako upo karibu songa mbele.
4. Bwana anakwenda kurejesha watu wake na kuwaweka kwenye mikono yenu. Yeye atawaleta. Mungu anakwenda kuleta wenye dhambi. Mungu anakwenda kuwarejesha waliokimbia
Unaenda kuwa na kibali. Kabla ya December vitu vinakwenda kutokea.
SEMINA MAALUMU YA MAANDALIZI YA MKUTANO WA MWEZI WA NANE 2023
MCHUNGAJI HERRY NELSON -ZANZIBAR