Mwalimu Zoeril Bukuku

Mwalimu Zoeril Bukuku lengo ni kuwafikia wengi kwa mafundisho ya Neno la Mungu aliye hai. Sauti kutoka mbali

25/05/2026
19/05/2026

CWI KUMEKUCHA KWA UMOJA WETU TUKUTANE DODOMA KWA UKUBWA WETU.

MKRISTO UJUE UKWELI HUU  ILI UWE SALAMAMambo  ambayo yana upinzani kwa Wakristo walio wengi. Nimeona niyaweke mambo haya...
15/05/2026

MKRISTO UJUE UKWELI HUU ILI UWE SALAMA

Mambo ambayo yana upinzani kwa Wakristo walio wengi.

Nimeona niyaweke mambo haya machache ili kila mmoja ajipime na kugundua nidhamu aliyonayo kwa Mungu anayemwabudu.

Hii ni changamoto ambayo unapaswa kujipima kwayo na kijifanyia tathimini ili kujiona namna ulivyosimama kwa Mungu.

Haijalishi umri wako au cheo chako nafasi yako hii inatuhusu wote.

Sasa hebu pitia dondoo hizi hapa chini:-
1. Shauku ya kusoma Biblia.
2. Kufunga na kuomba kibinafsi.
3. ShUku ya kumtolea Mungu kwa upendo
4. Kushuhudia habari za Yesu kwa wengine.
5. Nidhamu ya kuhudhuria ibada.
6. Shauku ya maombi ndani yako.

Ili iwe rahisi kwetu kujipima naomba dondoo hizi niziwekee mfumo wa namba kuanzia 1 mpaka 5

Alama ya juu ya ubora ni 5
Kwa mtindo huu wa tathmini hakuna aliye 0 hivyo hata 1 ni namba ya ubora.

Lakini maandiko yanatutaka kupandisha thamani yetu ya utendaji mbele za Mungu namna hii.

Hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; Waefeso 4:13

Wengine walikuwa bora inawezekana hata wewe ulikuwa Bora, lakini kwa hila za shetani kiwango chako kimeshuka hata wewe unashangaaa imekuwaje.

Sasa hebu tuweke wazi ili ujipime mwenyewe k**a andiko linavyotutaka .

Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa. 2Korintho 13:3
Kwa Kila swali alama ni moja tu inaweza kuwa 1 au 2,3,4,5
Usiweke alama mbili kwenye swali moja unapojibu.
Sasa endelea

1. Shauku ya kusoma Biblia. 1. 2. 3. 4. 5

2. Kufunga na kuomba kibinafsi. 1. 2. 3. 4. 5

3. ShUku ya kumtolea Mungu kwa upendo.
1. 2. 3. 4. 5

4. Kushuhudia habari za Yesu kwa wengine.
1. 2. 3. 4. 5

5. Nidhamu ya kuhudhuria ibada. 1. 2. 3. 4. 5

6. Shauku ya maombi ndani yako.
1. 2. 3. 4. 5.

Mtindo huu utakusaidia kujua nafasi ya ubora uliyopo kwa habari za kumtumikia Mungu na kicho chako kwake.

Kutunza nidhamu yako ya utumishi mbele za Mungu ni wajibu wako, kumbuka Mungu atalipa utendaji wa mtu uwe bora au uwe wa chini. Hebu soma andiko hili kwa makini,
Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. 1Korintho 3:8

Paulo alitahadharisha aliposema

Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, k**a mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.
Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.
Lakini k**a mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.
Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.
Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu.
Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni k**a kwa moto. 1Koritho 3:10-15.

Baada ya kujipima na kuona hali yako halisi usivunjike moyo bali tafuta namna ya kuberesha hali yako ya kiroho na utendaji wako mbele za Mungu.

Usivunjike moyo na kukata tamaa ukajiona hufai kwasababu ya matokeo ya chini uliyopata. Tathmini hii ikusaidie kujikagua Kisha kujigundua udhaifu wako na hatimaye ujirkebishi kibinafsi.


Nakutakia tathimini njema tena hatua kwa hatua. Ka Kisha kupandisha kiwango chako katika neema ya Yesu Mwokozi
Barikiwa
Mwl Zoeril Bukuku
0713765 777
Sauti kutoka mbali.

Katika Kumbukuzi yako ya KUZALIWA TIMON ZURIEL MWANANGU.Naomba ufahamu mambo yafuatayo namna Mungu alivyokutetea kutokan...
14/05/2026

Katika Kumbukuzi yako ya KUZALIWA TIMON ZURIEL MWANANGU.

Naomba ufahamu mambo yafuatayo namna Mungu alivyokutetea kutokana na mpango wa shetani wa kuyaondoa maisha yako.

Shetani alikusudia kuzima ndoto na kipawa chako hapa dunia.

Ulizaliwa katika Hospitali ya Temeke Tarehe 14.05.1999 kwetu ulikuwa muujiza mkubwa sana kupata mtoto wa kwanza wa kiume.

Pamoja na ukweli huu shetani alitaka kukunyonga ukiwa tumboni kwa kutumia kitovu.

K**a hivyo haitoshi muda uliotumika mpaka unazaliwa kwa watalaamu ulikuwa mrefu sana kiasi kwamba ulikunywa maji yaliyokutunza kwa muda wa miezi tisa ukiwa tumboni.

Lakini hatua ya mwisho ulizaliwa na ikawa shangwe kwetu na kwa familia, majirani na kanisa la EAGT Temeke.

Daktari aliyekuhudumia aliaandika ubaki hospitali chini ya uangalizi kutokana na madhara uliyoyapata.

Lakini kitu cha kuogopesha yawezekana bila umakini Muuguzi alimruhusu mama yako Pulkeria kutoka na wewe Hospitali, tukio hili lililooneshwa kuwa ulitoroshwa.

Baada ya shetani kukushindwa hospitali alilenga kukumalizia nyumbani maana kwa siku tano ulizokaa nyumbani hali yako iliendelea kudhoofika siku hadi siku.

Kati yetu hakuna aliyekumbuka kurudi na wewe hospitali tena na hii ilichangia na kukosa udhoefu wa kulea.
Ikumbukwe wewe ndiye ulikuwa mwanetu wa kwanza.

Tulipokea shauri nyingi na mbalimbali zote hakika zilikuwa sio za kusaidia bali kukupoteza.

Baba yako nikiwa kazini mama yako Pulkeria Bukuku pamoja na shangazi yako mkubwa Agape Kalinga walipoona hali inazidi kudorora waliamua kurudi hospitali tena.

Ulipofikishwa hospitali Daktari aliyekuhudumia wakati unazaliwa alikataa kukupokea akimtuhumu mama yako kuwa alitoroka na wewe wakati hajaruhusiwa. Hii nayo ilikuwa ni gia ya shetani kutaka kukatisha maisha yako.

Hata sasa simlaumu Daktari kwa msimamo wake maana haikuwa dhamira yake, japo kwa upande mwingine alipaswa kupima uzito wa tatizo kuliko hukumu aliyotoa kwa mama yako, kwako ambaye hukuwa na kosa.

Hali ilikuwa mbaya machozi yakimtiririka mama asijue la kufanya.

Muuguzi mmoja aliyeona tukio lile alimtuliza mama yako na kumwambia asiogope nakutafutia Daktari mwingine.

Daktari alipopatikana na kukuona mtoto Hali Yako ilivyo mara moja aliamuru gari ya wagonjwa iandaliwe ili uwahishiwe hosptili ya Taifa Muhimbili kwa matibabu na uangalizi wa juu zaidi.

Ulifikishwa Muhimbili ulipokelewa na kupelekwa kwenye chumba cha uangalizi maalumu (ICU) ambapo ulikaa kwenye chumba hicho kwa siku 9 bila mimi baba yako kukuona.

Kilikuwa ni kipindi kigumu na kinachotisha kwangu ambacho siwezi kukisahau kabisa. Ashukuriwe Mungu aliyenishika na kunivusha salama pale.

Nayakumbuka machozi ya mama yako wakati wote nilipokuwa nakuja hospitali kukuona bila mafanikio na kujua hatima yako.
Hakika nilikuwa natiwa nguvu kwa maombi nikijua Mungu. anakutetea

Binafsi nilifanikiwa kukuona baada ya siku ya 9 ulipotolewa ICU, hali yako ikiwa imetengamaa kiasi.

Ashukuriwe Mungu baada ya siku 14 uliruhusiwa kutoka hospitali na tukarudi nyumbani tena kwa furaha.

Mungu awabariki madaktari, wauguzi na wahudumu wote kuanzia hospitali ya Temeke kwa namna ambavyo walitumika kuokoa maisha yako, japo kusudi la shetani lilikuwa baya sana kwako na kwetu pia..

Vita iliendelea miezi mitano baadaye tarehe 31.10.1999 ungetupoteza sisi wazazi wako wote wawili ukiwa mdogo baada kula chakula ambacho kiliwekwa sumu.

Leo unatufurahia kwasababu Mungu alitutetea na mauti ile. Hapa ndipo andiko hili linatimia,
Marko 16:18
watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

Tukio hili lilitokea katika sherehe ya uhuru wa nchi ya Nigeria ambapo watu wengi waliohudhuria waliathirika na chakula kilicholiwa kwenye sherehe hiyo, mimi sikuwepo kwenye sherehe hiyo lakini mauti ilinifuata nyumbani baada ya kula chakula kilicholetwa na mama aliyehudhuria sherehe hiyo maana alikuwa mwajiriwa.

Kipindi tukiwa tumelazwa hospitali ya Temeke kwa siku 3 Timon Zuriel ulikuwa mikononi mwa mtu muhimu kwa famila hii Da Agnes Changwe ambaye watoto wa nyumba yangu mnamwita mama mdogo.

Mungu alimleta Dada Agnes kwa kipindi sahihi kwaajili yetu na yako pia.

K**a hii haitoshi ukiwa tumboni mama yako alipona na shambulio la mabomu yaliyolenga Ubalozi wa Marekani, uliokuwa umepakana na ubalozi wa Nigeria ambapo mama yako alikuwa anafanya kazi wakati huo.

Mama yako na wafanyakazi wengine wa Ubalozi wa Nigeria waliporomokewa na jengo ambalo ofisi yao ilikuwepo.

Ashukuruwe Mungu alimponya na kifo hiki na hakuna hata mmoja aliyepatwa na umauti zaidi ya majeraha kwa wafanyakazi wa Ubalozi wa Nigeria.

Ukiwa na miaka miwili ulinusurika kufa kwa kukabwa na mtu aliyekubeba mikononi.

Aliyekuwa na wewe alikuwa tunaishi naye, sisi hatukujua kuwa ana tatizo la ugonjwa kifafa.

Shambulio la kifafa lilimpata wakati amekubeba kifuani hivyo alikung'ania kiasi kwamba ilikuwa ni vigumu kukutoa mikononi mwake.

Hata hivyo baada ya maombi na kukemea nguvu hiyo Mungu alikutetea na kukupigania rena.

Pia kutoka wakati huo mpaka kaka yako huyu anaondoka kwetu tatizo hilo halikujirudia tena kwake hata sasa.

Nimeandika haya yote ili kukuhimiza kuendelea kumpenda Mungu na kumtumika kwa hofu na kuichochea karama iliyoko ndani yako.

Waheshimu watu, watumikie kwa moyo bila kujali hali zao. Jari utu wao sio kuwabagua kwa kigezo cha uwezo wao au hali zao.

Hakikisha katika maisha yako yote wewe na mkeo mtarajiwa Wema tarehe 31.05.2025 usimsahau Da Agnes kabisa mimi na mama yako tunalitamka hili toka moyoni.

Habari hii ikuhimize kujua namna Mungu alivyokupigania na kulinda tunu iliyoko ndani yako isife hivyo na wewe usiizike kwa vyovyote vile.
Uwe na amani na mkeo Wema, k**a jina lake lilivyo mtende Wema kwa watu wote.
Yesu mwenye neema akutetee daima, Roho mtakatifu akufunike daima, Mungu mwenye upendo akubariki kwa baraka za mbinguni juu, na kwa unono wa nchi utele wa neema na kibali uwe pamoja nawe katika utukufu wa jina la Yesu.

Baba
Sauti kutoka mbali

Viongozi wa CWI Kanda ya Mashariki wakiongozwa na Mkurugenzi Mch Nikusuma Folosi Mwakaniemba mwenye kaunda suit  wakiwa ...
02/05/2026

Viongozi wa CWI Kanda ya Mashariki wakiongozwa na Mkurugenzi Mch Nikusuma Folosi Mwakaniemba mwenye kaunda suit wakiwa na viongozi wa na walimu wa CWI Jimbo la Bagamoyo baada ya semina Elikezi namna ya kufundisha watoto.

KUHUSU YALIYOTOKEA Usibishe ni kweli yametukia na ukweli ndio huo.1. Hata k**a wanajaribu kuficha lakini ni kweli yalitu...
25/04/2026

KUHUSU YALIYOTOKEA Usibishe ni kweli yametukia na ukweli ndio huo.

1. Hata k**a wanajaribu kuficha lakini ni kweli yalitukia.

2. Watawala wanajaribu kuficha ukweli, lakini yalitukia.

3. Hakimu japo alijua ukweli hata hivyo aliacha yatukie.

4. Pamoja na mawakili wao kukosa nguvu ya kuthibitisha mash*taka yake inasikitisha yalitukia.

5. Pamoja na vilio vya uchungu vya wanawake, hawakuzuia yasitukie.

6. Pamoja na wafuasi wake kuunganisha nguvu kwa kufuatilia haikuzuia yasitukie.

7. Kuna baadhi ya wafuasi kwa masikitiko walivunjika moyo kwa yale yaliyotukia.

8. Mijadala iliendelea nchi nzima kuzungumzia yaliyotukia.

9. Watawala hawakujali madhara yatakayojitokeza walihakikisha yanatukia.

10. Hakimu alihukumu kwa shinikizo la watawala, kwa masikitiko aliruhusu kutukia.

11. Wabezaji hawako nyuma hata sasa wanabeza, wakishabikia yaliyotukia.

12. Hawakuzingatia kuwa yamempata yote haya kwasababu ya kuwatetea wao, bali walishabikia yatukie.

Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?

Ni kuhakikishie yote yaliyompata Yesu si kwajili ya dhambi zake bali zako,
Ili uokolewe. Kuokoka ni lazima.

Mwl Zoeril Bukuku
Sauti kutoka mbali

KWA YEYOTE ANAYEHITAJI MSAADA SOMA  HII.Habari njema na muhimu kwako na kwa maisha yako usiipuuze kabisaNajua nitakukose...
19/04/2026

KWA YEYOTE ANAYEHITAJI MSAADA SOMA HII.

Habari njema na muhimu kwako na kwa maisha yako usiipuuze kabisa

Najua nitakukosea lakini ni bora nikukosee katika ukweli huu,

Najua nitakuudhi lakini sina jinsi bali kukufikishia ukweli huu,

Mara nyingine hutapenda kusikia ujumbe huu kwasababu ya msimamo wako na itikadi yako lakini nijizuieje usijue habari hii njema?

Haaa najizuia nisisema lakini msukumo uliomo ndani yangu na upendo nilionao kwako hauniachi kukaa kimya

Ujumbe huu uko wazi ambao umesemwa na wengi ambao husukumwa na upendo wao kwako japo umekuwa ukiupinga mara kwa mara.

Na sasa Mimi imenilazimu nikwambie kwa wazi kuwa Yesu ni Mwokozi anakupenda, aliteswa kwa ajili yako, alikufa kwa ajili yako, alifufuka kwa ajili yako na Yuko hai milele kwa ajili yako.

Okoka leo ndio salama yako.
Mwl Zoeril Bukuku

Sauti kutoka mbali

Najivunia Mchungaji ADOLPH KWIYANDA MAKOPABaba yangu wa kiroho mtu muhimu sana katika maisha yangu ya kiroho,  alinifund...
17/04/2026

Najivunia
Mchungaji ADOLPH KWIYANDA MAKOPA

Baba yangu wa kiroho mtu muhimu sana katika maisha yangu ya kiroho, alinifundisha kumtumikia Mungu, alipojua nilichonacho ndani kwa ajili ya huduma alinishika mkono. Msingi alioujenga ndani yangu hakika umenifanya nibaki kwa Yesu hata sasa.

Nazikumbuka siku za kwanza za wokovu wangu mikononi mwake, nikiri alikuwa baba bora na sahihi mno wakati wa mapambano yale na atabaki kuwa hivyo daima.

Hakika alinivumilia sana, hasa nilipokuwa na maswali magumu ya imani kwake.
Alinichikua kwenda kutembelea nyumba za washirika, na hii nikajufunza tabia ya kujali.

Nakumbuka tumelala wote porini katika safari za Injili. Sitasahau tulipolala chini kwenye Ghala la kuhifadhi Korosho kwa wiki nzima ufadhiri wa viongozi wa kijiji cha tulipopeleka Injili.

Tulitumia ndoo moja kwa kuoga, na mara zote alitangiliza mimi shirika kuoga, hili lilinifundisha kutanguliza wengine.

Nakumbuka upendo wake kwangu, unyeyekevu wake na ucheshi wake.

Namwomba Mungu aendelee kumpa maisha marefu daima katika Kristo Yesu.

Nimeandika kutambua mchango wake kwangu katika maisha ya wokovu.

Niambie wewe unayemkumbuka katika safari yako ya maisha.
Mwl Zoeril Bukuku
Sauti kutoka mbali

Janga kubwa kwa jamii na Kanisa. Nakuomba usome hatua kwa hatua na Mungu akubariki.Kwa sasa ukiulizwa janga kubwa ni lip...
10/04/2026

Janga kubwa kwa jamii na Kanisa. Nakuomba usome hatua kwa hatua na Mungu akubariki.

Kwa sasa ukiulizwa janga kubwa ni lipi hakika utajibu vita vinavyoendelea vinavyotesa ulimwengu kwa wakati huu kati ya Iran na Israel na Mshirika wake Marekani.

Hi kweli hili linaweza kuwa ni janga kubwa lakini tiba yake pia ni pamoja na kukaa meza ya mazungumzo

Mimi naomba niende mbali kidogo na mtazamo uliopo.

Janga kubwa la kutisha kwa Kanisa na jamii kwa sasa Ni:-

1. Watoto wamesahaulika kiasi cha kutisha. Maomb 4:4
Hakuna mkakati ulio wazi na endelevu wa kuwalea watoto Kiroho makanisani ili wakue wakiwa na maadili mema.
2. Watoto hawathaminiwi Math 19:13, Mar 10:13-14, Luka 18:15, 1Tim5:8.

Tatizo hili liloanzia kwa mitume, hawakuona uthamani wa watoto kwenda kwa Yesu. Walijijali wao kuwa ndio wa thamani mbele za Yesu.
Uwekezaji mkubwa katika makanisa hauwalengi watoto, Ni makanisa machache sana ambayo yana mpango wa kuwekeza kwa ajili ya watoto.

Inaweza kuwa kati ya makanisa kumi utakayotembelea yawezekana 1 au 2 yakawa na miundombinu kwa ajili ya watoto na pengine usikute hata moja.
Na kati ya makanisa hayo miundombinu yake haikidhi ubora unaitakiwa kwaajili ya malezi ya watoto

3. Wengi hawajui kuwa vita ya mtoto ni vita na shetani. Mw 3:15, Kutoka 1:16,22, 10:10
Shetani kwa nguvu zake nyingi anapambana ili kuhakikisha anawameza watoto katika uharibifu wa dunia hii.

Michezo mingi tunayoiona katika mitandao ya kijamii ni makakati wa shetani kuwapoteza watoto na kuwangamiza.

Shetani, Hawaruhusu wazazi na Kanisa kuwashirikisha watoto katika huduma, Ni rahisi mzazi kwenda Kanisani kuabudu wakati mtoto amemuacha nyumbani mbele ya luninga.

Shetani ameingiza uongo kwa Kanisa kuona kuwa watoto hawawezi, hivyo kwa uongo huu huoni watoto wakipewa nafasi ya kuhudumu Kanisani na k**a wakipewa basi ni k**a vile waigizaji ili wazazi hafurahi.

Kwa kiasi kikubwa Kanisa na familia vimemwachia shetani uwanja mpana wa kutamba k**a apendavyo.

Huoni Kanisa na wazazi wakiwa na mipango madhubuti ya kuwalea watoto ili wamjue Yesu na wawe na uwezo wa kujisimamia. Mith22:6

Wazazi nao hawaoni huu kuwa ni wajibu wao mkubwa kuliko wote, 1Tim 5:8, Kumbukumbu 6:6-7, 31:12-13

Musa alipotambua hila za shetani alisema tutakwenda na watoto wetu hatuachi kitu maana hatujui Ni kwa utumishi gani ambao Mungu ametuamuru kwenda kumtumia.

Nimeleta hoja hii ili upige picha ya Kanisa lako, au Kanisani kwako au Kanisa kwa ujumla wake. Ili uone ni kwa namna gani kuna mikakati kwa ajili ya kuwahudumia watoto Kiroho na kimwili.

Je Kuna miundombinu, K**a madarasa, mbembea, vifaa vya kujifunza na vya michezo n.k vinayowashawishi watoto kupenda kuja Kanisani?

Je Kuna walimu waliojitoa kwa dhati na waliopitia mafunzo kwa ajili ya kuwahudumia watoto?.

Je k**a hayahafanyiki Kanisani kwako unategemea kuacha kizazi cha aina gani ili kibebe Injili?

Je kwa mtindo huu Kanisa limejiandaa kukabidhi kijiti cha Injili kwa kizazi hiki kweli?

Ndio maana nimesema hili ni janga kubwa kuliko majanga yote unayoyafahamu wewe.

Wazazi tusifurahie kuimba pambio tunaelekea mbinguni, huku tumekaa kwenye majengo ya thamani kubwa, na huku tukiwa tumwaacha watoto nyuma kiroho wakiporomokea jehanamu.

Unaweza kushea kwa faida ya Kanisa

Tafakari chukua hatua.
Mwl Zoeril Joseph Bukuku
Sauti kutoka mbali

Address

Vikindu

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwalimu Zoeril Bukuku posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share