21/11/2023
ZAWADI KUU TATU ZA MUNGU.
Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa,kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utikufu wake na wema wake mwenyewe (2Petro 1:3).
Kuna zawadi kuu tatu za Mungu katka Kristo Yesu tulizopewa kwa kupitia Injili.Nazo ni zawadi ya uzima wa milele,zawadi ya haki,na zawadi ya Roho Mtakatifu.
Warumi 6:23 inatuambia"....bali karama ya Mungu ni Uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu."Uzima wa milele ni uzima wa kiungu uliopewa ulipozaliwa mara ya pili. Uzima huu hauko sawa na uzima wa kibinadamu;ni uzima halisi wa Mungu. Huwezi kuufanyia kazi ili uupate uzima wa milele;huwezi kuupata kwa kulipia gharama yoyote;ni zawadi kutoka kwa Mungu. Bila uzima wa milele huwezi kuwa na asili sawa na ya Mungu; kusingekuwa na ushirika,hivyo kusingekuwa na uhusiano.
Haki pia ni zawadi. Warumi 5:17 inasema, "...zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika Uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo." Haki ni asili ya Mungu ambayo inaezea usahihi wake:Ni asili yake na uwezo wa kuwa sahihi wakati. Huwa hakosei daima;na anapoweka asili hiyo na huo uwezo katika roho yako, ndipo unaweza kutembea sawa sawa na kusudi lake na kumpendeza katika maisha yako, nawe unaweza kusimama mbele zake bila kuwa na hisia zozote za kuhulumiwa,kutojithamini au kujiona mwenye makosa.
Roho Mtakatifu pia ni zawadi ya za Mungu kwetu. Mtumie Mtumie Petro alisema katika Matendi 2:38,"Tubuni mkabatizwe kila Jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu."Roho Mtakatifu ni Mungu akitenda kazi ndani yetu. K**a Mkristo,unamhitaji Roho Mtakatifu ili uishi maisha ya ushindi katika Kristo. Hii ndiyo sababu Bwana Yesu alisema, "Nami nitamuomba baba, naye atawapa msaidizi mwingine..."( Yohana 14:16)
Roho Mtakatifu alikuja ili kukusaidia uishi maisha ya kikristo kwa sababu hakuna mtu wa kawaida awezaye kuishi maisha ya Ukristo. By Rev. Paradiso Lema