01/06/2026
*MALANGO YA KUZIMU.*
BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏
Tunapojifunza vita vya kiroho ili kuubomoa ufalme wa giza, lengo ni kukuweka katika hali ya kujua mbinu za kivita na Siri za kuomba ili kumshinda adui.
Ayubu 38:17
"16 Je! Umeziingia chemchemi za bahari, Au umetembea mahali pa siri pa vilindi?
17 Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?
Jua ya kwamba kuna malango ya Kuzimu hapa duniani.Na vilevile kuna mahala unaweza kufika au kukaa kumbe ni malango ya kuzimu.
Unaona hapa Ayubu ameongelea malango ya mauti na malango ya kuzimu, unaweza kujiuliza ni kitu gani ambacho kinatokea mpaka mtu anakuwa na mashetani ndani yake? Kumbe yawezekana mtu huyu alikaa sehemu ambapo ni malango au milango ya kuzimu.
Mwanzo 28:12
"12 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake. "
Mwanzo 28:13
"13 Na tazama, Bwana amesimama juu yake, akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako. "
Mwanzo 28:14-17
"14 Na uzao wako utakuwa k**a mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi, na mashariki, na kaskazini, na kusini; na katika wewe, na katika uzao wako, jamaa zote za dunia watabarikiwa.
15 Na tazama, mimi nipo pamoja nawe, nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia.
Mwanzo 28:15
16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.
17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha k**a nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni."
Unatakiwa kujua kwamba pia kuna lango la mbinguni,umeona hapa Yakobo alipo kuwa amelala kumbe eneo hilo ni lango la mbinguni.Jua kwamba hivi unaweza pia kulala mahala kumbe ulipo lala ni lango la kishetani na jua kwamba dunia ya leo watu wengi wanak**atwa na mateso kwa sababu mahala wanapokaa. Maana unakuta mahala pale ni malango ya shetani na mahala hapo panafanya mashetani yaingie ndani yako.
Isaya 5:13-14
"13 Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.
14 Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo."
Unaona hapa kumbe mtu anaweza kuwa na shida kumbe ni kinywa cha kuzimu kimeachia malango yake ndani yake ambayo yanamsababishia shida. Jua kwamba kwenye barabara panaweza kuwa ni malango ya kuzimu pia maana unaweza ukawa unaona ajali mara kwa mara katika eneo fulani kumbe eneo lile ni lango la kuzimu la kumeza watu. Elewa kwamba katika barabara kuna mahala shetani ametega nyavu zake ili anasema watu.
Mahali ambapo kuna weza kuwa na malango ya kuzimu ni:
1.Barabara.
Ambazo Barabara hizi shetani anaweza kutega nyavu zake ili ajali za mara kwa mara zitokee na kuzimu imeze watu.
2.Kwenye majumba.
Unatakiwa kujua majumba haya yanaweza kuwa ni malango ya kishetani pia kwa sababu ya vitu vilivyofanyiwa humo ndani ya nyumba ama uganga, ushirikina au uchawi.
Mithali 7:26-27
"26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.
27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti. "
Umeona hapa kumbe nyumba inaweza kuwa ni njia ya kwenda kuzimu na jua kwamba unapoingia kwenye nyumba ya wakala wa giza badala ya kupata baraka kwenye nyumba uliongia una pata balaa,unaweza ukaenda kwenye hiyo nyumba ukajikuta magonjwa yakaanzia kukuandama ghaflaa usichokijua ni kwamba nyumba hiyo inakuwa imeunganishwa na mashetani na nyumba hiyo ni lango. Elewa kwamba mtu anaweza kufanya uchawi na uganga na mambo ya kishirikina kwenye nyumba na anapokuwa anafanya hivyo nyumba hiyo inakuwa iko wakfu kwa ajili ya mashetani.
Jua kwamba kunasehemu inaweza kuwekwa wakfu kwa ajili ya Bwana
na mahala hapo panakuwa mahala pa Bwana, tambua kwamba kila unapoingia kwa mtu jiulize nyumba hii imeekwa wakfu kwa ajili ya nini.
3. Lango la kuzimu linaweza kuwa ndani ya mtu.
Mtu huyu anafanya uchawi,ushirikina,kuabudu sanamu inakuwa shetani anapata nafasi ndani yake na yeye kutumika na shetani na anakuwa lango.
Tambua ya kuwa malango ya kishetani yana pofusha macho yetu tusione pia, ukiona kitu usikiamini moja kwa moja kwani ni lazima ukiona chochote mbele yako omba Kwanza,Jua kwamba popote unapokwenda popote unapolala elewa kwamba unaweza ukaunganishwa na shetani.
Mwanzo 18:1-2
"1 Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari.
2 Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, "
Unaona hapa Ibrahim alitokewa na Bwana na aliona mwilini na rohoni,jua kwamba Ibrahim aliona kwa macho ya ulimwengu wa mwili ni watu ila ulimwengu wa roho alikuwa ni Bwana. Jua kwamba unaweza kuona kitu kwenye ulimwengu wa mwili kingine na kumbe katika ulimwengu wa roho ni kitu kingine.
Unaweza kwenda mahala kwenye kikao kumbe mahala hapo ni malango ya kishetani au malango ya giza, Pia unaweza kusalimiana na mtu kumbe umeshikana na mlango wa kuzimu, unaona hapa Ibrahim anasema unaweza karibisha malaika pasipo kujua .Kumbe katika kukaribisha unaweza kukaribisha watu kumbe watu wale ni malango ya kuzimu. Pia katika kuwapa watu mkono unaweza kumpa jini mkono Ila wewe utadhani ni mtu wa kawaida umenipa mkono.
Isaya 38:10
"10 Nalisema, Katika usitawi wa siku zangu kuingia malango ya kuzimu; Nimenyimwa mabaki ya miaka yangu. "
Umeona Kumbe kuzimu inaweza kukuchukua kabla ya siku zako,unatakiwa ufike mahala ujue kazi za kishetani ni kuiba na kuharibu,unakuta mtu anajiuliza nilipataje mapepo kumbe kuna mtu ulisalimiana naye au ulilala kwake bila kuomba kumbe mahala pale ni lango la kuzimu.
Shetani anaweza kuja na kitu chake au mambo ya kawaida na wewe ukaona hichi kitu au hili Jambo ni kawaida kumbe yaleyale ya kawaida yanakuunganisha na giza, kuna mtu Leo unaweza ukumuona ukajua ni mtu wa kawaida kumbe ni mlango wa kishetani.
4.Hospitali pia zinaweza kuwa ni malango ya kishetani.
Unaweza kwenda hospital unamkuta Doctor kapagawa yani shetani anamuingia Doctor anajikuta anakupa majibu ya kishetani au anakuchoma sindano ila ni maagizo ya kishetani,jua kwamba hospitalini shetani anapenda apamiliki ili achukue roho za watu,elewa kwamba kabla hujaenda hospital kuna maombi ya kufanya ili uwe salama,shetani anang'ang'ana kuwazuiya madaktari wasimjue Mungu ili wawe mawakala wake wa kishetani ili waweze kuchukuwa roho za watu,pia tambua ya kwamba shetani anak**ata hospital kwenye ulimwengu wa roho na wewe pia unatakiwa uombe kwa kuk**ata hospital na madaktari, manesi kwamba shetani hata watumia na pia kufunga lango la kuzimu la hospital.
Mathayo 16:18
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Umeona Yesu anatoa kanisa mamlka, uwezo, nguvu za kufunga mashetani na jua kanisa ndio lenye nguvu na mamlaka za kufunga malango ya kishetani,jua kwamba kuna mtu anaweza kupata ajali na asitoke damu kumbe lango la kuzimu limekunywa ile damu ila tambua nakwamba unayo mamlaka na nguvu ya kupangua malango yote ya kuzimu.
Ufunuo wa Yohana 9:1
"1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. "
Unaona kumbe lango la kuzimu lina ufunguo vile vile unatakiwa kujua kwamba na wewe unaona ufunguo na unayo mamlaka ya kufunga malango ya giza na kuufungua malango ya baraka.
Mathayo 16:19
"19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. "
Jua kwamba afya biashara,ndoa,kazi,mambo ya mtu nyota,maisha ya mtu vinaweza kufungiwa kuzimu na kuzimu inafunga ili wewe usifanikiwe.
Kanuni kuu mbi
li za mlango ni
1.Mlango unaweza kufunguliwa.
2.Mlango unaweza kufunga.
Ufunuo wa Yohana 2:12
"12 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Pergamo andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. "
Ufunuo wa Yohana 2:13
"13 Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuawa kati yenu, hapo akaapo Shetani. "
Elewa kwamba Kumbe mtu anaweza kuwa ana kaa kumbe pale alipo kaa au au eneo lile kumbe ndipo anapokaa shetani. Pia Shetani anaweza kukaa kwenye maeneo ,nyumba ,mali, fedha, ndani ya mtu. Ila uwezo wako wa kumpiga ndio uwezo wako wa kushinda.
Unaposema kiti cha enzi cha shetani ndo sehemu yenye mamlaka ,nguvu za kishetani na shetani huyu anatumia nyumba au mahala k**a mlango wa kukushambulia wewe, hivyo unatakiwa uishinde shetani Kwa jina la Yesu.
UKIRI.
Kwa damu ya Yesu, kwa jina la Yesu na kwenda kinyume na kila mlango wa kishetani uliopo ndani ya nyumba ya mtu na funga malango yote ya kuzimu kwa jina la Yesu, na achia moto kuzimu nafungu kila lango la Barabarani la kuzimu nafunga kwa jina la Yesu. Na kwenda kinyume na malango ya hospital kwa damu ya Yesu na yafunga hayo malango ya kuzimu hospitalini kwa jina la Yesu natuma damu ya Yesu kwenye hospitali zote nasema hayatatumika kuua watu au kunyonga watoto.Eehh shimo la kuzimu achia maisha yangu kwa jina la Yesu. Naachilia mlango wa mbinguni kwenye maisha yangu, mlango wa baraka nasema lazima nifanikiwe kwa jina la Yesu.Amen.
Kwa njia ya Maombi ya Vita na kukomboa nafsi tunapaswa kupambana mno ili adui asipate nafasi.
SHALOM 🙏🙏🙏
ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.