George ABEL Mwache

George ABEL Mwache Evangelism

03/06/2026

*JE! UMETAFUTA KWANZA KIBALI?*

KWA SABABU
KINA NGUVU ZAIDI YA UJUZI ULIO NAO!

BWANA YESU KRISTO ASIFIWE!!!

Leo nikushirikishe jambo..
Tambua kuwa kibali kina nguvu zaidi ya ujuzi ulionao, kuwa na ujuzi pasipo kibali haimfanikishi mtu kufika mbali, unaweza kuwa na ujuzi (professional) juu ya Hilo eneo unalolitumikia lakini k**a huna kibali bado Jamii haiwezi kukukubali, mfano mdogo tu ..
Hujawahi kusikia ama kuona watu wanasifa zote za kupata kazi lakini hawapati? Hujawahi kusikia dada ni mzuri na anasifa zote za kuolewa lakini miaka na miaka inapita haolewi.?

Ukikosa kibali maana yake unakuwa unamilikiwa na Roho ya kukataliwa na ndio maana Kuna mambo unaona kuwa ni halali kwako kuyapata lakini huyapati kwasababu tu umekosa KIBALI.

Ninachotamani ujifunze hapa ni kujiombea kibali cha ki Mungu leo kwa kila jambo unalofanya huku ukitambua kuwa juhudi zako binafsi peke yake hazitoshi kukufikisha kule unakotakiwa kufika Ila unamuitaji Yesu akupe kibali kwenye Hilo eneo unalotumika kwalo.

Pasipo kibali unaweza kutumia nguvu nyingi na gharama nyingi sana lakini zisikufikishe kupokea matokeo chanya kwasababu Mungu hajaachilia kibali kwenye Hilo eneo unalotumika kwako..

Tujifunze mifano michache katika Biblia ..

Ukisoma Biblia Inaonesha jinsi mfalme alipokuwa anataka kupata malkia na jinsi mabinti walivyokuwa wakitunzwa ili siku Ile mfalme anapochagua malkia basi waonekane kuwa bora zaidi.. Na Ester alionekana kumvutia sana mfalme.. Na akawa malkia.. Kilichomfanya Ester awe malkia sio kwamba alikuwa mzuri wa sura kuliko wengine, yamkini walikuwepo wazuri zaidi yake..

Lakini kwasababu kibali cha Mungu kilikuwa juu ya Ester ndicho kilichomfanya Ester akakubalika kuwa malkia.. Na Mungu alichokuwa akikiona kwa Ester ni kuwa Ester akiwa malkia atakuja kuwatetea ndugu zake wayahudi ili wasiuwawe..

Daniel_na_wenzake
Ukisoma kitabu cha Daniel utaona jinsi ambavyo mfalme alitoa amri ya vijana wote watunzwe huku wakipewa chakula kizuri na Baada ya majuma kadhaa mfalme atachagua wale vijana wenye sura za mvuto kuliko wengine..

Kina Daniel waligoma kula chakula cha mfalme wakasema kamwe hawatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, na wakamuomba mkuu wa matowashi kuwa wao wale mtama na maji..

Biblia inasema siku Ile mfalme alipokuwa akifanya uchaguzi wa vijana wapi wenye sura nzuri.. Biblia inasema kina Daniel, Abelnego, shedrack walionekana kuwa na Sura nzuri kuliko wengine..
Kilichowafanya waonekane vile kuwa na sura nzuri haikuwa mtama.. Ila ni kibali cha Mungu kilikuwa juu ya Daniel na wenzako..

Mara nyingi tunatumia jitahidi kubwa sana katika maeneo ambayo Mungu bado hajatoa kibali na ndo maana hatupokei matokeo sawa na tunavyotarajia..

Kibali kina nguvu kuliko ujuzi ulionao.. Kibali kina nguvu kuliko UZURI wa sura ulionao..
Kuna mazingira utapita ambayo kwa sifa za kibanadamu usingeweza kupita yote hayo ni kwasababu Mungu ameachilia kibali..
Kibali ni jambo La msingi sana katika huduma Mungu aliyokupa..

Utaalamu ni mzuri sana lakini Utaalamu pasipo kibali cha Mungu ni bure. Utatumia jitahidi kubwa sana lakini bado haitazailisha matokeo unayoyataka.. Leo Muombe Mungu akupe kibali katika kila eneo unalotumika
Mwalimu
Biashara
Mwanasheria
Doctar
N.k

Mpendwa Mwana wa MUNGU, bado tumaini lipo kwa Bwana. Chukua maamuzi leo, nyenyekea mbele za Bwana ambae anaweza kukuheshimisha, Omba kwanza Roho Mtakatifu ashuke akusaidie kupata KIBALI CHA BWANA, nawe utafunguliwa, utapokea neema na Baraka zako, utarudishiwa vyote ulivyopoteza, tena maradufu.
BWANA AKUBARIKI SANA.

SHALOM 🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!!!
AMEN AMEN AMEN!!

03/06/2026

*JE! UMEONGEZA KIWANGO CHAKO CHA MAOMBI?*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

✍️Kiwango cha nguvu Za Mungu unayoitumia kwenye Maombi ndicho kinachoruhusu kiwango cha Mungu kujibu Maombi yako!
(Angalia Waefeso 3:20).

👉Mfano Yesu aliwapa mitume mamlaka juu ya pepo wote lakini tunaona walishindwa kumtoa pepo wa kifafa.
(Luka 9:1-2; 38-40 & Mathayo 17:14-21).

👉Kwanini?? Kwasababu roho za kishetani zinatofautiana nguvu, hivyo hata katika maombi, utatumia nguvu tofauti kushughulika nazo!

👉Tumia Nguvu za Maombi Vizuri ili uweze kushughulika na Changamoto/matatizo yanayokusonga!

SHALOM 🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

03/06/2026

*JE! UNAFAHAMU KWAMBA SHETANI ANAWINDA KUKUVURUGA ILI USILIELEWE NENO LA MUNGU?*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

👉Shetani anawinda neno ili watu wasilielewe na kumzalia Mungu matunda.
Yesu alisema, *Kile mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia*
(Mathayo 13:19).

✅Kitu kikubwa ambacho Shetani anawinda ni kupambana ili watu wasipate upako ambao utawasaidia katika maisha yao.

👉 Lengo la adui ni kupambana watu wasielewe neno na kupata nguvu za Mungu kwani anajua watu wakishapata nguvu za Mungu, watamshinda.

👉Shetani hasumbuliwi na watu kuomba, ila anasumbuliwa na watu kuomba ndani ya upako. Shetani hasumbuliwi na watu kusoma Biblia na wasielewe, ila anasumbuliwa na watu kusoma ndani ya upako kwani anajua bila Roho Mtakatifu, hatuwezi kuelewa neno
(Luka 24:45).

✅Kwa sababu hiyo, Shetani wakati wote atapambana watu wasielewe neno na kupata upako wa Roho Mtakatifu kwani anajua kuwa kiwango cha Mungu kujibu maombi yetu kinategemea kiwango cha nguvu ya Roho Mtakatifu ambayo tunaitumia.

Neno linasema *Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu*
(Waefeso 3:20).

Mungu awabariki Sana Sana

SHALOM 🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

03/06/2026

*USIIPUNGUKIE NEEMA YA MUNGU.*

Waebrania 12:15
mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.

Waebrania 4:16
Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

Wimbo
Siri ya maombi yangu ni wewe wajua,
Siri ya maombi yangu ni wewe wajua.
Siri ya uzima wangu ni wewe wajua
Siri ya uzima wangu ni wewe wajua.

Ni wewe wajua x10

SHALOM!

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

02/06/2026

*NENDA KAFANIKIWE KWA UWEZO WAKO HUO HUO ULIONAO!*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

*BWANA akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani* Je! Si mimi ninayekutuma?
(Waamuzi 6:14)

👉Mungu aliposema na Gideon alimtamkia tuu neno moja *Nenda kwa uwezo wako huo*. Gideon hakuona uwezo wake, Mungu aliujua na akamfumbua macho, matokeo yake Israel wakapata Mwamuzi.

✅Watu Wengi Sana tunapenda kuanza na mambo makubwa lakini Mungu anasema haudharau mwanzo mdogo. Maadamu ni mwanzo kwake una NGUVU.

👉Leo nakwambia Nenda Kwa Mtaji huo huo mdogo Utafanikiwa kimaisha kwa Jina la Yesu Kristo

👉Tunasoma Petro mwanafunzi wa Yesu katika injili K**a mtu aliyekuwa hajatulia lakini mwenye shauku ya kujua mengi hata alidiriki kutembea juu ya maji.

✍️Lakini Petro wa Matendo ya Mitume Ni mtu tofauti kabisa, Mwenye NGUVU, mwenye UJASIRI, mwenye kuinena kweli ya injili na kuleta matokeo( Soma Matendo ya Mitume 2:29) nitakumegea uthibitisho hapa tutazame

Matendo 4:
*Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu*
— Matendo ya Mitume 4:13

✍️Ukiwa pamoja na Yesu katika safari Yako ujasiri unaumbika ndani Yako. Tatizo Watu wengi tumekosa uthubutu na kuamini kile Mungu ameweka ndani yetu.

👉Ujasiri Ni Neema tuliyopewa na Mungu na itafaya kazi K**a tutajipa wajibu kuitetea na kuifanyia kazi.

✍️Nikutie moyo wewe uliyekubali kutembea katika njia ya Bwana Yesu. Nenda na uwezo wako huo. Mungu amekupa NGUVU mpya, Mungu amekupa Roho Mtakatifu na zaidi Mungu amekupa Neno lake kukuongoza.

👉Sauli wa Tarso alipokutana na ujasiri huu akaitwa Mtume Paulo na habari zake na kazi alizofanya tunazikiri hata leo.

*akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu*
— Matendo ya Mitume 28:31

✍️MTU mmoja aliitwa Apollo alikuwa mtu wa elimu, lakini alikuwa na shauku ya kujua zaidi uthubutu wake wa kuhubiri alikutanishwa na Prisila na Akila waliomwelekeza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi ( Matendo 18:25-28).
Akawa faida kubwa kwa ufalme wa Mungu.

👉Mungu amekupa hiyo elimu , Fedha,sio kwa ajili Yako, bali uitumie kwa ufalme wake.

✍️Tunahitaji kizazi Cha kina Apolo wengi wenye ushawishi na ujasiri waijuayo njia ya Bwana Yesu Kristo kwa usahihi.

Siku ya leo; *Nakuombea Nenda katika uwezo wako na ukafanye maajabu Katika Jina la Yesu Kristo*

Mungu awabariki sana sana

SHALOM 🙏🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

02/06/2026

*OMBA KIBALI CHA KUFUNGUA VIFUNGO VYOTE VINAVYOKUZUIA KUOLEWA/KUOA.*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

Karibu ujifunze kitu hapa ambacho kitakusaidia kuweza kufuta Vifungo vyote vya kukuzuia kuolewa/kuoa.

Kifungo ni kitu kinachokushika ili usifanye jambo Fulani jema.

Kifungo ni mfano wa ndege aliyefungwa kamba ndefu kwenye mti , hutoka na kupaa karibu tu na kurudi kwenye mti , hawezi kwenda zaidi.

Na mtu mwenye kifungo cha kutokuolewa/kuoa hupata mateso makubwa sana .

Ni k**a yuko huru lakini kuchumbiwa/kuchumbia ni mtihani, na hata akichumbiwa/Kuchumbia kabla ya kuolewa/Kuoa uchumba unavunjika, au akiolewa tu anaachika au mme/Mke anakufa kifo cha ghafla cha mapema.

Kuna haja ya kujifungua kutoka kwenye vifungo vya kutokuolewa/Kuoa.

Kifungo hiki katoa nani?
Yawezekana adui za wazazi wako, yawezekana mababu katika ukoo, yawezekana wachawi, yawezekana maadui wa ukoo wako , yawezekana maadui wa familia yako, yawezekana majini mahaba ya ndotoni, yawezekana waganga wa kienyeji, yawezekana ni mizimu au shetani mwenyewe na yawezekana mtu yeyote mwenye nia mbaya na ukoo wenu au nia mbaya na familia yenu au nia mbaya na uzao wa tumbo la mama yako na wewe ukiwamo ndani yake.

Unaweza kuepuka Vifungo au mikosi ambayo ni kisababisho cha mateso wakati wa kuoa/kuolewa k**a mmoja kati ya wanaooana yuko kwenye mkondo huo.

*NJIA KUMI(10) ZA KUTAMBUA K**A UNA KIFUNGO CHA KUTOKUOLEWA.*

1. Ukiwa na ndugu wa k**e zaidi ya wawili wakubwa, wenye miaka 30 na zaidi, ambao hawajawahi kuchumbiwa kabisa.

2. Kila unapokaribia kuolewa katika zaidi ya matukio mawili, mara zote huishia kukatishwa tamaa na uchumba wako kuvunjika bila sababu za kueleweka.

3. Endapo kuna hali inayoashiria kifo cha ndoa, na ambayo huharibu ndoa kabisa.

4. Hata k**a ni mwanamke mzuri na mwenye mwenendo mzuri na maisha ya maadili mema, utaona kabisa hakuna kijana anayevutiwa na wewe ili kukuchumbia muoane. Hata kwa wale wenye nia ya kukuchumbia hujikuta wakitoweka tu bila sababu.

5. Endapo Baba au Mama yako , au mtu mwingine akitoa laana ya maneno kuhusu wewe kuolewa.

6. Ikiwa msichana yeyote katika familia yako kaolewa katika mazingira magumu au wale ambao hufa vifo visivyoelekea tena muda mfupi tu baada ya kuolewa.

7. Endapo utasikia sauti ikisisitiza kukuambia kuwa ‘’Kamwe hutaolewa’’ au ‘’Kamwe hutapata mafanikio kwenye maisha yako.’’

8. Ikiwa una pepo mume au watoto wa kipepo. Kwa mfano katika ndoto unazoota utaona mwanamume akija na kufanya mapenzi na wewe, au kujiona una ujauzito na hatimaye kuzaa watoto katika ulimwengu wa roho yaani katika ndoto. Wakati mwingine , mtu huyo anaweza hata akajidhuhirisha katika ulimwengu wa Mwili.

9. K**a hupati kabisa siku zako za mwezi(Hedhi).

10. K**a wewe huota ndoto zenye kuogopesha hususani kuota unacheza na nyoka au viumbe wenye kutambaa.

MPENDWA , ukishajua haya, usifadhaike kwani tumaini bado lipo. Rejesha furaha yako, Rejesha uchumba wako, Rejesha upendo WAKO.

FUNGA NA OMBA upate Macho na Masikio ya Rohoni ili ujenge upya mahusiano yako ukiweka ulinzi wa Damu ya Yesu Kristo na kuvunja Vifungo vyote kwa JINA lipitalo majina yote YESU KRISTO MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

Naye anatuahidi leo; "Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu."
- WARUMI 15:13.

BWANA AKUBARIKI.

SHALOM 🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!!!
AMEN AMEN AMEN..

02/06/2026

*OMBA KIBALI ILI UJUE HATMA YA KIKOMBE UNACHOKINYWEA.*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

Saa ya Ayubu ilipofika marafiki walimkimbia, mke wake alimshauri kumkufuru Mungu wake. Lakini yeye alisimama na Mungu bila kukoma.

Suala la kukinywea kikombe haliji k**a ajali ni lazima lije ili uende kwenye utukufu mwingine. Hii unakuwa umekwisha andikiwa. Chembe ya ngano haitaweza kuzaa mpaka ife Vivyo hivyo kwetu wanadamu lazima tupitie hatua hiyo. Ibrahimu aliomba miaka mingi ili apate mtoto lakini Mungu hakumpa mpaka muda ulipofika. Ili aje apitie majaribu ya kumtoa mtoto kuwa sadaka ndipo Mungu alipombariki. Lakini ni baada ya kukinywea kikombe lakini Mungu alijua ni muda gani atamwondolea baada ya kuionyesha ile IMANI na UTII kwa Mungu.

Tunapopita kwenye majaribu tunapaswa tuombe kwa kuwa roho mtakatifu hutusaidia kuomba kwa kuugua ndani yetu na sio kumwacha Mungu. Angalia Hana aliomba miaka mingi katika roho mtakatifu bila kukoma hata Mungu akamsikia na akapata Samweli.

Mambo hayo yaliyompata Yesu alikwisha andikiwa na manabii kuwa lazima yatokee tangu kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake.

Luka 18:31 Akawachukua wale Thenashara, akawaambia, Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yatatimizwa, Mwana wa Adamu aliyoandikiwa na manabii.

Si kila kikombe unachokinywea ni shetani amekileta maana huenda ni Mungu ameruhusu ili uende katika utukufu mwingine.

Tunapaswa kumshukuru Mungu sio tu tunapo pita kwenye mazuri hata tunapo pita kwenye mabaya tunapaswa kumshukuru Mungu maana lazima yatimizwe.

Mathayo 20:18-19
18 Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi; nao watamhukumu afe;

19 kisha watampeleka kwa Mataifa wapate kumdhihaki, na kumpiga mijeledi, na kumsulibisha; na siku ya tatu atafufuka.

~Marko 16:6

Naye akawaambia, Msistaajabu; mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulibiwa; amefufuka; hayupo hapa; patazameni mahali walipomweka.

SHALOM 🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

02/06/2026

*TUNAPASWA KUMJUA ROHO MTAKATIFU ​​SASA BINAFSI KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE KILE!*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

"Basi Bwana ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru" (2 Wakorintho 3:17).

Roho Mtakatifu ni Roho ya Bwana, kulingana na mstari wetu wa ufunguzi. Na ulipojiunga na Bwana, umekuwa Roho moja naye sasa. "Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye" (1 Wakorintho 6:17). Na ukisha kuwa Roho moja naye, ni lazima yeye azidi ndani yako, na wewe upungue (Yohana 3:30).

Unapaswa kupungua hadi wewe usionekanike tena, ili yeye sasa aliye ndani mwako aweze kuishi na kuonekanika. *"Nimesulibiwa pamoja na Kristo. Sio mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye anayeishi ndani yangu. Na uhai nilio nao sasa katika mwili wangu, ninao kwa imani katika Mwana wa Mungu, aliyenipenda na akajitoa mwenyewe kwa ajili yangu ”(Wagalatia 2:20).*

Mabadiliko haya kamili yanapaswa kutokea ndani yako, kwa sababu sasa umepokea Roho mpya k**a mtoto wa Mungu, ambayo inakufanya uwe kiumbe kipya cha Mungu. Umekuwa kiumbe ambaye sio tena k**a Adamu, bali ni k**a Kristo. Umekuwa kiumbe ambaye si mwanadamu tena, bali ni mungu. Roho Mtakatifu huyu uliyepokea kutoka kwa Mungu amekuwa ni Roho yako sasa. Ndio maana ilikuwa ni muhimu sana kwa utu wako wa kwanza (Adamu) kupungua, ili utu wako mpya (Kristo) atokeze na kuchukua nafasi yake juu yako, ili wewe kuwa kiumbe kipya ambacho ni k**a Mungu.

Kwa hiyo wakati wewe na Bwana (Roho Mtakatifu) mnapokuwa Roho moja, lazima uanze kuwa na ushirika naye kila siku, na kumtii yeye na neno lake, na kumfuata. Sio kila wiki, bali kuwa na ushirika naye wa kila siku, na kumtii na kumfuata kila siku. Unapoanza kuwa na ushirika naye na kumtii k**a hivyo, unakuwa unajenga urafiki wako naye na unakuwa na nguvu kuliko mwanzo. Inafanya wewe na yeye kutoweza kutengana tena. Wakati Roho huyu anapokuwa Roho yako, ndipo Roho wa Bwana anakuwa juu yako, Roho wa hekima na ufahamu, Roho wa ushauri na uweza, Roho wa maarifa na hofu ya Bwana (Isaya 11:2).

Na unapoanza kuishi na kutembea kwa Roho huyu, ndipo utakapoanza kuishi maisha matakatifu, kwa sababu Roho huyu ni Mtakatifu. Na pia utakuwa na nguvu ya Mungu ndani yako ya kufanya mambo makubwa kwa ajili ya Mungu, kwa sababu yeye ndiye Roho wa nguvu zote za Mungu (Matendo 1:8). Pia utukufu wa Mungu utakuwa juu yako na watu watauona juu ya maisha yako, kwa sababu Yeye ndiye Roho wa Utukufu (Isaya 60:2b).

Na wakati Roho huyu atakapokuwa juu yako, au utakapoanza kuishi kwa Roho huyu, basi utakuwa umetiwa mafuta kwa ajili ya kazi ya Mungu hapa duniani. Hivyo k**a unayo Roho Mtakatifu sasa, na unaishi kwa roho hii sasa, hiyo inamaanisha "Roho ya Bwana MUNGU yu juu yako; kwa sababu Bwana amekutia mafuta uwahubiri wanyenyekevu habari njema; amekutuma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao” (Isaya 61:1).

Hivi ndivyo Yesu alivyotiwa mafuta pia (Matendo 10:38) - "Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye" Vivyo hivyo na Yesu alitutia mafuta sisi pia. (Matendo 1:8) - "Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi." Hatua inayofuata baada ya kutiwa mafuta, ni kwenda tu kufanya kazi ambayo Yesu alikupa. Usingoje upako mwingine wowote zaidi ya huo, kwa sababu hakuna zaidi ya huo.

Roho Mtakatifu ndani yako, ndio upako wote usio kuwa na mwisho wa Mungu uko ndani mwako. Kadiri unavyozidi kumjua Roho Mtakatifu ndivyo unavyozidi kujua upako kiasi gani ulio ndani yako. Na unapozidi kujua upako kiasi gani uliopo ndani mwako, ndivyo unavyozidi kujua ni nguvu kiasi gani ulizo nazo, na ni vitu gani unaweza kufanya. Hivyo jifunze zaidi juu ya Roho wako Mtakatifu, ili ujijue wewe ni nani, na una nguvu kiasi gani. Mungu akubariki sana. Amina!!

SHALOM 🙏🏽

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

01/06/2026

*HUU NI MSIMU MPYA KWAKO!*

HAKIKISHA UNAAMBATANA NA WATU WANAOONA FURSA KATIKATI YA MIJITU!

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

Hesabu 13:27
Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake.
28 Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko.
29 Amaleki anakaa katika nchi ya Negebu; na Mhiti, na Myebusi, na Mwamori wanakaa katika milima, na Mkanaani anakaa karibu na bahari; na kando ya ukingo wa Yordani.

*30 Kalebu akawatuliza watu mbele ya Musa, akasema, Na tupande mara, tukaitamalaki; maana twaweza kushinda bila shaka.*

31 Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi.
*32 Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.*
*33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa k**a mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.*

Bwana asifiwe wateule!!..

Tunapoendelea kutafakari wema Wa Mungu Mwaka huu mpya ..Basi ni vema kuamua kuchagua aina ya watu wa kwenda nao kaanani ..usiende na kila mtu wengine ni wakatishaji tamaa hautafika.

Wengi tunaijua habari hii ya wapelelezi walioenda kuipeleleza nchi ya kaanani walienda wapelelezi 12 lakin 10 wakaleta taarifa mbaya badala ya kuona asali na maziwa wao waliishia kuyaona majitu makubwa ya kutisha na wao wakajiona k**a mapanzi ..

Nataka kusema uwe mwangalifu na aina ya watu unaotaka kuambatana nao Mwaka huu ..ukitaka kufanikiwa ogopa kutembea na watu waoga ..wasiothubutu kufanya mambo ..watu walalamishi kwenye kila jambo ..siku zote wao hawaonagi fursa wanaonaga matatizo tu..kazi yao ni kutazama changamoto tu lakini kuzikabili hawataki..

Marafiki walalamishi achana nao..watu wanaojiona mapanzi achana nao ..watu wanaoona mijitu badala ya asali na maziwa achana nao ..hata k**a ni wengi achana nao mtaishia kukata tamaa na kuendelea kukaa jangwani..

Kuna watu ukikaa nao hawajadili maendeleo kazi kusema watu tu asubuhi mpaka jioni hata ukichart nao wao ni kuelezea maisha ya watu wengine tu umemuona Fulani Mara umesikia habari za Fulani aiseee HAWA NI MIZIGO ACHANA NAO KAA NAO MBALI MWAKA HUU WATAKUFELISHA..

MAFANIKIO YANAHITAJI WATU WANAOTHUBUTU HUWA HAYAJI KIRAHISI..YANAHITAJI WATU WASIOOGOPA NYUKI...WATU WASIOOGOPA CHANGAMOTO MAFANIKIO YANAHITAJI WATU WATAKAO GEUZA CHANGAMOTO KUWA FURSA..

Hesabu 14:6 Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao;
7 wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.
8 Ikiwa BWANA anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali.

9 Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope 💪💪💪.

Kati ya watu 12 wawili tu ndiyo walioona FURSA katikati ya mijitu..waliamua kuona asali na maziwa haijalishi kuna mijitu au hakuna ..haijalishi kuna nyuki ama hakuna maadamu Mungu amewapa nchi hiyo basi HIYO MIJITU NI CHAKULA CHAO..

NASEMA NA WEWE IKIWA BWANA AMEKUPA NEEMA UMEINGIA MSIMU MPYA WA MWAKA HUU WA BARAKA BASI UWE NA UHAKIKA ZIPO CHANGAMOTO LAKINI ZITAKUWA CHAKULA KWAKO IKIWA UTAAMUA KUONA FURSA KATIKATI YA MIJITU..

Mwaka huu amua kuwa na watu k**a Yoshua na Kaleb watu wanaothubutu watu wanaoona FURSA ..wakati wengine wanaoona uchumi umebana basi wewe uwe miongoni mwa watu watakaosema katikati ya uchumi kubana kuna kufanikiwa...wakati wengine wanalalamika na kunung'unika wewe amua kusimama kuzikabili CHANGAMOTO... O oo Halleluyaaaa!

MAFANIKIO HAYAJI K**A NDOTO...MAFANIKIO HAYAJI KWA KUKIMBIA FURSA..MAFANIKIO HAYAJI KWA KULALAMIKA LALAMIKA..MAFANIKIO YANAWAHITAJI WATU K**A YOSHUA NA KALEB VINGINEVYO KAANANI UTAISHIA KUIONA KWA MACHO WAKATI WENGINE WAKILA ASALI NA MAZIWA WEWE UTABAKI JANGWANI UKIFA NA NJAA.

Mwaka huu epuka watu wanaojua Sherehe zote mjini kitchen party hata isiyo muhusu anashona sare... Sendoff zote anajua ratiba zake...ratiba za mipira zote anazijua mpaka anabet ...vigodoro vyote anajua ratiba zake... LAKINI HAJUI BIASHARA MPYA MJINI..HAJUI VIWANJA VINAUZWA WAPI HAJUI WAPI KUNA FURSA HAJUI WAPI KUNA MIZIGO YA BIASHARA WATU WA AINA HII ACHANA NAOOOOO👌👌👌💪💪💪

Ambatana na watu watakao jua biashara gani sasa inalipa...wapi kuna masoko ya biashara...watu wanaojua wapi utapata mafundisho ya neno la Mungu yatakayo kusaidia kuukulia wokovu na kupata maarifa ya kimungu ya kukuvusha ulipokwama watu wanaojua katikati ya ukame wanaweza kutengeneza chemchem ya maji..watu wanaojua kuimba sifa katikati ya machozi HAO AMBATANA NAO AISEE USIWAACHE. ....!
MARAFIKI WATAABISHAJI TUPA KULEEEEEE👉👉👉👉👉👉👌👌💪💪💪

Bwana awabariki na kuwalinda Bwana awainulie nuru ya USO wake na kuwafadhili...

SAA HII, POKEA NGUVU, POKEA UWEZA NA MAMLAKA, POKEA MAARIFA MAPYA, POKEA KUKUA NA KUONGEZEKA, POKEA NDOA, POKEA AJIRA MPYA, POKEA MAFANIKIO KATIKA KILA ENEO UNALOWEKA MKONO WAKO, POKEA USTAWI, POKEA USHINDI, POKEA VYOTE UNAVYOSTAHILI, POKEA POKEA VYOTE ULIVYOIBIWA, POKEA VILIVYOFICHWA, POKEA ONGEZEKO NA KUKUA KIUCHUMI, KIROHO NA KIMWILI KATIKA JINA LA YESU KRISTO MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

SHALOM 🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

01/06/2026

*MALANGO YA KUZIMU.*

BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏

Tunapojifunza vita vya kiroho ili kuubomoa ufalme wa giza, lengo ni kukuweka katika hali ya kujua mbinu za kivita na Siri za kuomba ili kumshinda adui.

Ayubu 38:17

"16 Je! Umeziingia chemchemi za bahari, Au umetembea mahali pa siri pa vilindi?

17 Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?

Jua ya kwamba kuna malango ya Kuzimu hapa duniani.Na vilevile kuna mahala unaweza kufika au kukaa kumbe ni malango ya kuzimu.

Unaona hapa Ayubu ameongelea malango ya mauti na malango ya kuzimu, unaweza kujiuliza ni kitu gani ambacho kinatokea mpaka mtu anakuwa na mashetani ndani yake? Kumbe yawezekana mtu huyu alikaa sehemu ambapo ni malango au milango ya kuzimu.

Mwanzo 28:12
"12 Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake. "

Mwanzo 28:13

"13 Na tazama, Bwana amesimama juu yake, akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka; nchi hii uilalayo nitakupa wewe na uzao wako. "

Mwanzo 28:14-17

"14 Na uzao wako utakuwa k**a mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi, na mashariki, na kaskazini, na kusini; na katika wewe, na katika uzao wako, jamaa zote za dunia watabarikiwa.

15 Na tazama, mimi nipo pamoja nawe, nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia.

Mwanzo 28:15

16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.

17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha k**a nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni."

Unatakiwa kujua kwamba pia kuna lango la mbinguni,umeona hapa Yakobo alipo kuwa amelala kumbe eneo hilo ni lango la mbinguni.Jua kwamba hivi unaweza pia kulala mahala kumbe ulipo lala ni lango la kishetani na jua kwamba dunia ya leo watu wengi wanak**atwa na mateso kwa sababu mahala wanapokaa. Maana unakuta mahala pale ni malango ya shetani na mahala hapo panafanya mashetani yaingie ndani yako.

Isaya 5:13-14
"13 Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.
14 Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo."

Unaona hapa kumbe mtu anaweza kuwa na shida kumbe ni kinywa cha kuzimu kimeachia malango yake ndani yake ambayo yanamsababishia shida. Jua kwamba kwenye barabara panaweza kuwa ni malango ya kuzimu pia maana unaweza ukawa unaona ajali mara kwa mara katika eneo fulani kumbe eneo lile ni lango la kuzimu la kumeza watu. Elewa kwamba katika barabara kuna mahala shetani ametega nyavu zake ili anasema watu.

Mahali ambapo kuna weza kuwa na malango ya kuzimu ni:

1.Barabara.

Ambazo Barabara hizi shetani anaweza kutega nyavu zake ili ajali za mara kwa mara zitokee na kuzimu imeze watu.

2.Kwenye majumba.

Unatakiwa kujua majumba haya yanaweza kuwa ni malango ya kishetani pia kwa sababu ya vitu vilivyofanyiwa humo ndani ya nyumba ama uganga, ushirikina au uchawi.

Mithali 7:26-27

"26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.

27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti. "

Umeona hapa kumbe nyumba inaweza kuwa ni njia ya kwenda kuzimu na jua kwamba unapoingia kwenye nyumba ya wakala wa giza badala ya kupata baraka kwenye nyumba uliongia una pata balaa,unaweza ukaenda kwenye hiyo nyumba ukajikuta magonjwa yakaanzia kukuandama ghaflaa usichokijua ni kwamba nyumba hiyo inakuwa imeunganishwa na mashetani na nyumba hiyo ni lango. Elewa kwamba mtu anaweza kufanya uchawi na uganga na mambo ya kishirikina kwenye nyumba na anapokuwa anafanya hivyo nyumba hiyo inakuwa iko wakfu kwa ajili ya mashetani.

Jua kwamba kunasehemu inaweza kuwekwa wakfu kwa ajili ya Bwana

na mahala hapo panakuwa mahala pa Bwana, tambua kwamba kila unapoingia kwa mtu jiulize nyumba hii imeekwa wakfu kwa ajili ya nini.

3. Lango la kuzimu linaweza kuwa ndani ya mtu.

Mtu huyu anafanya uchawi,ushirikina,kuabudu sanamu inakuwa shetani anapata nafasi ndani yake na yeye kutumika na shetani na anakuwa lango.

Tambua ya kuwa malango ya kishetani yana pofusha macho yetu tusione pia, ukiona kitu usikiamini moja kwa moja kwani ni lazima ukiona chochote mbele yako omba Kwanza,Jua kwamba popote unapokwenda popote unapolala elewa kwamba unaweza ukaunganishwa na shetani.

Mwanzo 18:1-2

"1 Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari.
2 Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi, "

Unaona hapa Ibrahim alitokewa na Bwana na aliona mwilini na rohoni,jua kwamba Ibrahim aliona kwa macho ya ulimwengu wa mwili ni watu ila ulimwengu wa roho alikuwa ni Bwana. Jua kwamba unaweza kuona kitu kwenye ulimwengu wa mwili kingine na kumbe katika ulimwengu wa roho ni kitu kingine.

Unaweza kwenda mahala kwenye kikao kumbe mahala hapo ni malango ya kishetani au malango ya giza, Pia unaweza kusalimiana na mtu kumbe umeshikana na mlango wa kuzimu, unaona hapa Ibrahim anasema unaweza karibisha malaika pasipo kujua .Kumbe katika kukaribisha unaweza kukaribisha watu kumbe watu wale ni malango ya kuzimu. Pia katika kuwapa watu mkono unaweza kumpa jini mkono Ila wewe utadhani ni mtu wa kawaida umenipa mkono.

Isaya 38:10

"10 Nalisema, Katika usitawi wa siku zangu kuingia malango ya kuzimu; Nimenyimwa mabaki ya miaka yangu. "

Umeona Kumbe kuzimu inaweza kukuchukua kabla ya siku zako,unatakiwa ufike mahala ujue kazi za kishetani ni kuiba na kuharibu,unakuta mtu anajiuliza nilipataje mapepo kumbe kuna mtu ulisalimiana naye au ulilala kwake bila kuomba kumbe mahala pale ni lango la kuzimu.

Shetani anaweza kuja na kitu chake au mambo ya kawaida na wewe ukaona hichi kitu au hili Jambo ni kawaida kumbe yaleyale ya kawaida yanakuunganisha na giza, kuna mtu Leo unaweza ukumuona ukajua ni mtu wa kawaida kumbe ni mlango wa kishetani.

4.Hospitali pia zinaweza kuwa ni malango ya kishetani.

Unaweza kwenda hospital unamkuta Doctor kapagawa yani shetani anamuingia Doctor anajikuta anakupa majibu ya kishetani au anakuchoma sindano ila ni maagizo ya kishetani,jua kwamba hospitalini shetani anapenda apamiliki ili achukue roho za watu,elewa kwamba kabla hujaenda hospital kuna maombi ya kufanya ili uwe salama,shetani anang'ang'ana kuwazuiya madaktari wasimjue Mungu ili wawe mawakala wake wa kishetani ili waweze kuchukuwa roho za watu,pia tambua ya kwamba shetani anak**ata hospital kwenye ulimwengu wa roho na wewe pia unatakiwa uombe kwa kuk**ata hospital na madaktari, manesi kwamba shetani hata watumia na pia kufunga lango la kuzimu la hospital.

Mathayo 16:18

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

Umeona Yesu anatoa kanisa mamlka, uwezo, nguvu za kufunga mashetani na jua kanisa ndio lenye nguvu na mamlaka za kufunga malango ya kishetani,jua kwamba kuna mtu anaweza kupata ajali na asitoke damu kumbe lango la kuzimu limekunywa ile damu ila tambua nakwamba unayo mamlaka na nguvu ya kupangua malango yote ya kuzimu.

Ufunuo wa Yohana 9:1

"1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. "

Unaona kumbe lango la kuzimu lina ufunguo vile vile unatakiwa kujua kwamba na wewe unaona ufunguo na unayo mamlaka ya kufunga malango ya giza na kuufungua malango ya baraka.

Mathayo 16:19

"19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. "

Jua kwamba afya biashara,ndoa,kazi,mambo ya mtu nyota,maisha ya mtu vinaweza kufungiwa kuzimu na kuzimu inafunga ili wewe usifanikiwe.

Kanuni kuu mbi

li za mlango ni

1.Mlango unaweza kufunguliwa.
2.Mlango unaweza kufunga.

Ufunuo wa Yohana 2:12

"12 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Pergamo andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. "

Ufunuo wa Yohana 2:13

"13 Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuawa kati yenu, hapo akaapo Shetani. "

Elewa kwamba Kumbe mtu anaweza kuwa ana kaa kumbe pale alipo kaa au au eneo lile kumbe ndipo anapokaa shetani. Pia Shetani anaweza kukaa kwenye maeneo ,nyumba ,mali, fedha, ndani ya mtu. Ila uwezo wako wa kumpiga ndio uwezo wako wa kushinda.

Unaposema kiti cha enzi cha shetani ndo sehemu yenye mamlaka ,nguvu za kishetani na shetani huyu anatumia nyumba au mahala k**a mlango wa kukushambulia wewe, hivyo unatakiwa uishinde shetani Kwa jina la Yesu.

UKIRI.

Kwa damu ya Yesu, kwa jina la Yesu na kwenda kinyume na kila mlango wa kishetani uliopo ndani ya nyumba ya mtu na funga malango yote ya kuzimu kwa jina la Yesu, na achia moto kuzimu nafungu kila lango la Barabarani la kuzimu nafunga kwa jina la Yesu. Na kwenda kinyume na malango ya hospital kwa damu ya Yesu na yafunga hayo malango ya kuzimu hospitalini kwa jina la Yesu natuma damu ya Yesu kwenye hospitali zote nasema hayatatumika kuua watu au kunyonga watoto.Eehh shimo la kuzimu achia maisha yangu kwa jina la Yesu. Naachilia mlango wa mbinguni kwenye maisha yangu, mlango wa baraka nasema lazima nifanikiwe kwa jina la Yesu.Amen.

Kwa njia ya Maombi ya Vita na kukomboa nafsi tunapaswa kupambana mno ili adui asipate nafasi.

SHALOM 🙏🙏🙏

ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN.

Address

Usa River

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when George ABEL Mwache posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to George ABEL Mwache:

Share