04/09/2026
*JE, UNATAKA KUFANIKIWA KWENYE MAISHA YAKO KIROHO NA KIMWILI?*
BWANA YESU KRISTO APEWE SIFA 🙏
▶️▶️Jifunze Kufanya Yafuatayo;
1️⃣ Hakikisha Unamiliki ,na kutawala na kulitiiisha ANGA la mahali ulilopo!
▶️▶️Iwe ni kwenye Biashara, Huduma, Kazi,Elimu,Kukua Kiroho, ANGA ni Eneo Muhimu Sana kwako!
Kwanini??
Kwasababu;
✅Shetani anaweza Kutumia ANGA la mahali ulilopo kukuzuia Usifanikiwe kabsa!
""ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata *mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi*
(Waefeso 2:2)
✅ Shetani anaweza Kutumia ANGA la mahali ulilopo kukuzuia MAOMBI Yako!
*Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi*
(Danieli 10:13)
2️⃣ Hakikisha Unaomba MBINGU ziwe Upande wako!
✅Mbingu zinaweza kufunguka kwaajili Yako na kukuruhusu kufanikiwa
✅Lakini pia Mbingu zinaweza kufungwa kwaajili Yako!
✅K**a Mbingu zisipokuwa Upande wako kufanikiwa kwako itakuwa ni NGUMU Sana
*Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka k**a hua, akija juu yake*
(Mathayo 3:16)
*Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake*
Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.
(Ayubu 26:13)
✅ Mbingu zikiwa Upande wako, Maana yake ni kwamba ROHO wa YESU yupo Upande wako pia!
3️⃣ Hakikisha ARDHI unayofanyia Biashara,Kazi ,Kujenga nyumba,au Huduma Iko Upande wako pia
✅ ARDHI ni Silaha Muhimu sana kwetu Katika kutusaidia kufanikiwa Kiroho na Kimwili pia
*Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake*
(Ufunuo wa Yohana 12:16)
Mungu wangu awabariki Sana Sana
SHALOM 🙏
ONLY CHRIST CAN ACCOMPLISH IT WITHIN US!
AMEN