Kisima cha uponyaji church.

Kisima cha uponyaji church. Ukurasa maalumu wa kanisa kwa ajili ya kukutana na watu walio mbali. Church's Official page just to interact with people from a far.

13/07/2026

KUMCHA BWANA KWAONGEZA SIKU ZA MTU

Siri ya kuongeza siku za mtu za kuishi ni kumcha Bwana kwa kumaanisha,nasi ili siku zetu za kuishi zisipunguzwe Bali ziongezwe,tuhakikishe tunamcha Bwana.

Nakutakia siku njema wiki njema yenye ushindi,
Happy New Week.

Mithali 10 : 27 Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.

12/07/2026

TUNAWASHUKURU SANA WAGENI WETU WOTE! πŸ™

Tunawashukuru kwa dhati wageni wetu wote mliofika kuabudu pamoja nasi siku ya leo. Uwepo wenu umekuwa baraka kubwa kwetu, na tunaamini Mungu amewagusa na kuwabariki kupitia ibada ya leo.

Karibuni tena wakati wowote kuabudu nasi katika Kanisa la Kisima Cha Uponyaji. Tunawaombea neema, amani, afya njema, na baraka tele katika maisha yenu.

Mungu awabariki sana! Karibuni tena

12/07/2026

SHANGWE ZA UZINDUZI WA TAWI LA KISIMA CHA UPONYAJI – MWAKA- TUNDUMA
KWA MTUMISHI WA MUNGU JOSHUA MBINDI .

12/07/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI
MHUBIRI:ASKOFU DAVID KAYUNI.
SOMO:KUTEMBEA KUPITIA MLANGO USIOWEZA KUUONA

12/07/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI
KUSIFU NA KUABUDU

BWANA YU KARIBU NA WOTE WAMWITAOBwana hayupo mbali na wote wamwitao kwa uaminifu,maana masikio yake husikia maombi ya we...
12/07/2026

BWANA YU KARIBU NA WOTE WAMWITAO

Bwana hayupo mbali na wote wamwitao kwa uaminifu,maana masikio yake husikia maombi ya wenye haki wake,nasi tusiache kumwita Bwana maana yu karibu na wote wenye haja naye.

Nakutakia siku njema ibada njema, pokea neema ya kuabudu ktk roho na kweli,Shalom.

Zaburi 145 : 18 Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.

MWITE NAYE ATAITIKAKatika magumu,katika shida na katika uhitaji mwite Bwana naye atakuitikia,maana amehidi kuitika na at...
11/07/2026

MWITE NAYE ATAITIKA

Katika magumu,katika shida na katika uhitaji mwite Bwana naye atakuitikia,maana amehidi kuitika na atakukuonyesha mambo magumu usiyoyafahamu,

Nakutakia siku njema yenye ushindi,Shalom .

Yeremia 33 : 3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.

11/07/2026

LAZIMA TUKUBALI KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU

Mpendwa, Mungu anatuita kuishi maisha ya utakatifu kila siku. Ni lazima tukubali kumfuata Kristo kwa moyo wote, tukikataa dhambi, tamaa za mwili, na mambo ya dunia yanayotutenganisha na Mungu.

Utakatifu si chaguo, bali ni wito wa kila mwamini. Tuchague kumpendeza Mungu kuliko kuifuata dunia, kwa sababu thawabu ya uaminifu ni uzima wa milele.

"Msifuatane na namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu." β€” Warumi 12:2Mungu akutie nguvu kuishi maisha ya utakatifu kila siku.

Bishop David Kayuni

Kisima cha uponyaji church.

10/07/2026

SOMO: TUTAFUTE KWA BIDII KUWA WATAKATIFU.

Utakatifu ni maisha ya kujitenga na dhambi na kuishi kwa kumtii Mungu. Ni wito wa kila Mkristo.

1. Mungu anatuagiza kuwa watakatifu – 1 Petro 1:15–16.
2. Utakatifu humkaribisha mtu kwa Mungu – Waebrania 12:14.
3. Utakatifu unahitaji kutii Neno la Mungu – Zaburi 119:9.
4. Roho Mtakatifu hutusaidia kuishi maisha matakatifu – Wagalatia 5:16.

Utakatifu si chaguo bali ni agizo la Mungu. Tuchague kuishi maisha yanayompendeza Bwana kila siku.

10/07/2026

1 Petro 1:15
bali k**a yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
Kisima cha uponyaji church.
Bishop David Kayuni

Address

Sogea Tunduma Songwe
Tunduma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kisima cha uponyaji church. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kisima cha uponyaji church.:

Shortcuts

Share