12/11/2025
BARUA KWA VIONGOZI WOTE WA DINI WA MADHEHEBU YA
KIKRISTO NCHINI TANZANIA.
Mitume, Manabii, Maaskofu, Mapadre, Wachungaji, Watawa, Wainjilisti, waalimu, na Viongozi
wote katika Imani ya kikristo, nawasalimu kwa salamu ya Bwana wetu Yesu kristo. Neema na Amani ya
kristo vizidishwe ndani yenu.
Najua sistahili mbele zenu kuyaandika haya kwani mimi ni ndugu yenu mdogo kuliko wote. Nami
nalisubiri wazee waseme, umri na wingi wa siku utoe maarifa, na useme hekima, lakini haikuwa hivyo
kwani wote wamenyamaza hakuna anaeonya wala kukemea, wala kushauri kwa upendo wa bwana.
Lakini imo Roho ya Mungu ndani ya mwanadamu nami nimeona niitii. Niwakumbushe wajibu wenu kwa
nyakati hizi.
Nchi yetu leo ina hadithi mpya inayowasha masikioni mwetu, nikweli huenda vijana wamekosa
hekima, na ikapelekea hali hii, au tuseme basi watawala walikosa hekima, busara na upendo ndio
ikapelekea haya.
Swali najiuliza je wote hawa sio waumini na washiriki wetu. Je hawaji kwenye nyumba zetu za ibada?
Je hawashiriki nasi katika karamu zetu za kila wakati? Je! Nini kilitokea? Jambo hilo lilinitafakarisha sana
nikawaza sawa yameshatokea je! Mungu wetu alituacha? Au kwanini alikaa kimyaa? Akanijibu haku kaa
kimya. Nikajiuliza shida iko wapi? Na haya yafuatayo yakawa majibu.
Watumishi wangu wameacha nafasi zao, leo wanatumikia mali, fedha, na umaarufu. Wanaogopa
KUISEMA KWELI YA INJILI KWANI ITAWAONDOLEA HIVYO WANAVYO VITUMAINIA. Wengi wao
wanajua chakufanya ila hawafanyi kwasababu nao WANAOGOPA. Wanalinda DINI na MAKANISA YAO
KULIKO WATU WANGU.
Watumishi wa Mungu jambo hilo ni la kweli na tafakari hiyo imenifanya nijiulize kwani kati ya kiongozi
wa dini na kiongozi wa kisiasa yupi ni mkuu. Jibu likawa ni kiongozi wa dini/kanisa kwani kiongozi wa
kanisa ni kiunganishi kati ya Mungu na dunia/ulimwengu tena hata kiongozi wa kisiasa ni mshirika katika
kanisa nae anapaswa kufwata kile ambacho Mungu wa mbingu na nchi ameagiza kwa kinywa cha
mtumishi wake. Hii ni kusema kwamba kiongozi wa kanisa ananafasi kubwa hata ya kutuliza hasira ya
Mungu na kuzuia uovu usitendeke.
Ukweli ndio huo ila shida ilianzia hapa. Kwamba sisi wenyewe hatuna umoja wa kweli. Tunaitwa wote
wakristo lakini tumetengana kila mtu anapigania kikundi chake. Na anawaogopa watawala wa
ulimwengu kuliko hata Mungu. Kwamfano kwa yaliotokea Tanzania hayakuanza leo wala jana ni vugu
vugu la muda mrefu, kwani tulisikia na kuona watu wakitekwa au kuuwawa wakati mwingine. Lakini
viongozi wadini wengi walikuwa kimya tena walipata hata na nafasi za kukaa na viongzi wakubwa wa
nchi, ikiwemo Mh. Rais lakini hawakuthubutu kukemea, licha yakuwa miongoni mwa wahanga ni
waumini wetu.
Hata walipoinuka viongozi wa dini wachache kupinga mambo haya, wengi walijitenga nao.
Nakuwaona ni wanasiasa au wana mrengo wa kisiasa kumbe ni sauti ya Mungu ikionya. Mimi binafsi
namfuatilia Baba askofu Bagonza Kalikawe wa KKKT dayosisi ya karagwe. na nimeshuhudia maranyingi akionya na kukemea vitendo hivyo lakini chaajabu hata viongozi wenzie na wakubwa wake wamekaa
kimya. Wakatoliki wakaonya Baba Padri Kitima akanusurika kuuwawa, tukawaachia wakatoliki na
kiherehere chao. Tukanyamaza kimya k**a sio wakristo wenzetu. Askofu Gwajima akaonya na kushauri
kanisa likafungwa na sisi tukanyamaza yasifungwe na ya kwetu. Tukamuacha na kiherehere chake.
Lakini yaliotokea tarehe 29/10/2025 hadi 01/11/2025 yamegusa wapendwa wetu, watoto wetu, ndugu
zetu, na mioyo yetu. Leo kila mahali tunahimizwa tumuombe Mungu anaepoza mioyo apoze mioyo
yetu. Je! Hayatajitokeza tena k**a haya?
Niwaombe viongozi wangu tusirudie makosa ya nyuma tusimame imara upya, Tutubu kwamba
tulikosea na tumuombe MUNGU msamaha wa dhati. Tuache kushikilia vikundi vyetu tuihubiri KWELI
usiku na mchana. Maana KWELI NI NENO LA MUNGU. Na neno la Mungu linaonyesha wazi kuwa HAKI
HUINUA TAIFA kumbe k**a tunataka taifa liinuke tukaihubiri HAKI. Na tusiogope kuwaambia ukweli
viongozi wa kisiasa wanapokosea. Lakini tufahamu neno hili kuwa hakuna AMANI bila HAKI hivyo
tuwaimize watawala kutenda haki, kwani nao niwatoto wetu KIROHO.
Nawatakieni Amani ya kristo na neema yake katika utumishi wenu, na Roho wake akawe mwalimu na
shahidi kati yetu.
Ni mimi mtoto wenu,
Victor Daudi
Mjumbe mdogo wa ufalme wa milele.