Kanisa La Sauti Ya Kalvari Tanzania

Kanisa La Sauti Ya  Kalvari Tanzania Huduma ya SAUTI YA KALVARI. Ni huduma iliyo anzishwa na mchungaji na mwalimu Daudi Missoji Malulu.

20/01/2026

*Hiyo mistari ni lugha ya picha Kwa kizazi chetu na kanisa.*

Ukitafakari maisha yetu vijana tulio *okoka* utagundua kuwa Huwa tunavutiwa sana na namna ya ulimwengu huu.
Mtindo wa maisha.
Mavazi na muonekano.
Miziki pamoja na nyimbo lakini pia hata wapo vijana ndani ya kanisa wanaowatamani mabinti nje ya kanisa.
Na mabinti vivyo hivyo wapo wanao watamani vijana wakiume nje ya kanisa.

Kituambacho ni hatari
Ukisoma hapo utaona Mungu anakasirika alafu nik**a anaamua kumuacha mwanadamu Sasa afanye anavyotaka.

Usikubali Mungu akuache ufanye unavyotaka. Tamani kuongozwa na Mungu.

19/01/2026

*Utangulizi wa kitabu Cha mwanzo sura ya kwanza Hadi ya tatu.*

Tunajifunza mambo mengi hapo kwenye sura hizo. Lakini yapo mambo kadhaa tutakayoyafafanua.

1. Mungu ni wa utaratibu. Kila jambo limefanyika Kwa mpangilio.
2. Mungu hufanya kazi timilifu Kwa wakati. Ukisoma utaona Mungu nafanya jambo Fulani Kwa wakati Fulani na linakamilika bila mapungufu. Kesho anaanza jambo JIPYA na linakamilika pia
3. Mungu huandaa mazingira kwanza kabla ya kumuweka yeyote Mahali popote. _Ukisoma utaona Mungu alituandalia mazingira kabla ya kutuweka_
4. Mungu alimuumba mtu Ili akatawale.
5. Mungu alimuumba mtu alimuumba mwanamume na mwanamke
6. Uumbaji ulifanyika kwanza katika ulimwengu wa Roho ndio ukaja katika ulimwengu wa mwili Sura ya 2
7. Tunaona Mungu anampa AGANO adamu na namna ya kuishi.
8. Tunasoma katika sura ya 3 na kuona anguko na dhambi inaanza baada ya adamu kuasi AGANO LA MUNGU.
9. Ahadi ya kuja Kwa Yesu inaanza kupatikana hapa sura ya tatu anaposema uzao wa mwanamke utamponda nyoka kichwa. Na tunajua uo uzao wa mwanamke ni YESU KRISTO.
Jamani ni watie moyo TUSOME na badae tushirikiane pamoja kuchangia.

16/01/2026

https://chat.whatsapp.com/JKi1XvFPzrv5BAoQc0KR3t

Karibu HUB OF HOPE TUSOME BIBLIA PAMOJA

Tukiwa mwanzoni kabisa mwa mwaka 2026. Nikukaribishe tushirikiane kuisoma BIBLIA nzima Kwa pamoja.
Jiunge nasi k**a moyo wako uko tayari kutoa sadaka ya muda kwaajili ya kumfahamu Mungu

12/11/2025

BARUA KWA VIONGOZI WOTE WA DINI WA MADHEHEBU YA
KIKRISTO NCHINI TANZANIA.
Mitume, Manabii, Maaskofu, Mapadre, Wachungaji, Watawa, Wainjilisti, waalimu, na Viongozi
wote katika Imani ya kikristo, nawasalimu kwa salamu ya Bwana wetu Yesu kristo. Neema na Amani ya
kristo vizidishwe ndani yenu.
Najua sistahili mbele zenu kuyaandika haya kwani mimi ni ndugu yenu mdogo kuliko wote. Nami
nalisubiri wazee waseme, umri na wingi wa siku utoe maarifa, na useme hekima, lakini haikuwa hivyo
kwani wote wamenyamaza hakuna anaeonya wala kukemea, wala kushauri kwa upendo wa bwana.
Lakini imo Roho ya Mungu ndani ya mwanadamu nami nimeona niitii. Niwakumbushe wajibu wenu kwa
nyakati hizi.
Nchi yetu leo ina hadithi mpya inayowasha masikioni mwetu, nikweli huenda vijana wamekosa
hekima, na ikapelekea hali hii, au tuseme basi watawala walikosa hekima, busara na upendo ndio
ikapelekea haya.
Swali najiuliza je wote hawa sio waumini na washiriki wetu. Je hawaji kwenye nyumba zetu za ibada?
Je hawashiriki nasi katika karamu zetu za kila wakati? Je! Nini kilitokea? Jambo hilo lilinitafakarisha sana
nikawaza sawa yameshatokea je! Mungu wetu alituacha? Au kwanini alikaa kimyaa? Akanijibu haku kaa
kimya. Nikajiuliza shida iko wapi? Na haya yafuatayo yakawa majibu.
Watumishi wangu wameacha nafasi zao, leo wanatumikia mali, fedha, na umaarufu. Wanaogopa
KUISEMA KWELI YA INJILI KWANI ITAWAONDOLEA HIVYO WANAVYO VITUMAINIA. Wengi wao
wanajua chakufanya ila hawafanyi kwasababu nao WANAOGOPA. Wanalinda DINI na MAKANISA YAO
KULIKO WATU WANGU.
Watumishi wa Mungu jambo hilo ni la kweli na tafakari hiyo imenifanya nijiulize kwani kati ya kiongozi
wa dini na kiongozi wa kisiasa yupi ni mkuu. Jibu likawa ni kiongozi wa dini/kanisa kwani kiongozi wa
kanisa ni kiunganishi kati ya Mungu na dunia/ulimwengu tena hata kiongozi wa kisiasa ni mshirika katika
kanisa nae anapaswa kufwata kile ambacho Mungu wa mbingu na nchi ameagiza kwa kinywa cha
mtumishi wake. Hii ni kusema kwamba kiongozi wa kanisa ananafasi kubwa hata ya kutuliza hasira ya
Mungu na kuzuia uovu usitendeke.
Ukweli ndio huo ila shida ilianzia hapa. Kwamba sisi wenyewe hatuna umoja wa kweli. Tunaitwa wote
wakristo lakini tumetengana kila mtu anapigania kikundi chake. Na anawaogopa watawala wa
ulimwengu kuliko hata Mungu. Kwamfano kwa yaliotokea Tanzania hayakuanza leo wala jana ni vugu
vugu la muda mrefu, kwani tulisikia na kuona watu wakitekwa au kuuwawa wakati mwingine. Lakini
viongozi wadini wengi walikuwa kimya tena walipata hata na nafasi za kukaa na viongzi wakubwa wa
nchi, ikiwemo Mh. Rais lakini hawakuthubutu kukemea, licha yakuwa miongoni mwa wahanga ni
waumini wetu.
Hata walipoinuka viongozi wa dini wachache kupinga mambo haya, wengi walijitenga nao.
Nakuwaona ni wanasiasa au wana mrengo wa kisiasa kumbe ni sauti ya Mungu ikionya. Mimi binafsi
namfuatilia Baba askofu Bagonza Kalikawe wa KKKT dayosisi ya karagwe. na nimeshuhudia maranyingi akionya na kukemea vitendo hivyo lakini chaajabu hata viongozi wenzie na wakubwa wake wamekaa
kimya. Wakatoliki wakaonya Baba Padri Kitima akanusurika kuuwawa, tukawaachia wakatoliki na
kiherehere chao. Tukanyamaza kimya k**a sio wakristo wenzetu. Askofu Gwajima akaonya na kushauri
kanisa likafungwa na sisi tukanyamaza yasifungwe na ya kwetu. Tukamuacha na kiherehere chake.
Lakini yaliotokea tarehe 29/10/2025 hadi 01/11/2025 yamegusa wapendwa wetu, watoto wetu, ndugu
zetu, na mioyo yetu. Leo kila mahali tunahimizwa tumuombe Mungu anaepoza mioyo apoze mioyo
yetu. Je! Hayatajitokeza tena k**a haya?
Niwaombe viongozi wangu tusirudie makosa ya nyuma tusimame imara upya, Tutubu kwamba
tulikosea na tumuombe MUNGU msamaha wa dhati. Tuache kushikilia vikundi vyetu tuihubiri KWELI
usiku na mchana. Maana KWELI NI NENO LA MUNGU. Na neno la Mungu linaonyesha wazi kuwa HAKI
HUINUA TAIFA kumbe k**a tunataka taifa liinuke tukaihubiri HAKI. Na tusiogope kuwaambia ukweli
viongozi wa kisiasa wanapokosea. Lakini tufahamu neno hili kuwa hakuna AMANI bila HAKI hivyo
tuwaimize watawala kutenda haki, kwani nao niwatoto wetu KIROHO.
Nawatakieni Amani ya kristo na neema yake katika utumishi wenu, na Roho wake akawe mwalimu na
shahidi kati yetu.
Ni mimi mtoto wenu,
Victor Daudi
Mjumbe mdogo wa ufalme wa milele.

*AJIRA NI CHACHE ILA KAZI NI NYINGI* Huu ni msemo unaotumiwa sana baadhi ya watu walio fanikiwa. Ukililenga kundikubwa l...
18/12/2023

*AJIRA NI CHACHE ILA KAZI NI NYINGI*

Huu ni msemo unaotumiwa sana baadhi ya watu walio fanikiwa. Ukililenga kundikubwa la vijana linalo lalamikia *AJIRA*

umo ukweli mchungu ndani ya huu msemo. Ambao Najaribu kuutafakari kila siku.
Ukweli ni kwamba nikweli Kabisa serikali haiwezi kuzalisha ajira zakutosha vijana wote nchini.

Lakini pia ukweli ni kwamba kazi zipo nyingi sana. Kunawakati siogopi Kabisa kufukuzwa kazi Kwasababu nik**a ninaona sitakosa chakufanya.

Lakini sio vijana wote wanazijua na kuziona hizo kazi zilizopo.
Kwasababu mbili kuu
1. Mfumo wa elimu haumjengi kijana kujitegemea ila unamtengeneza kuja kuwa muajiriwa.

2. Vijana hawana Ufahamu / elimu juu ya FURSA.

HILO LAKWANZA NI LA MFUMO. ILA HILI LA PILI. TUTAJIFUNZA WOTE NAMNA YA KUZIJUA NA KUZIONA FURSA. NA FURSA NI NINI? tukutane humu humu January 2024

WhatsApp Group Invite

*IMANI NA MATENDO* _Ndugu Victor anaandika✍🏻✍🏻✍🏻_victordmalulu@gmail.comNdugu nawasalimu katika jina la Yesu kristo wana...
05/05/2020

*IMANI NA MATENDO*
_Ndugu Victor anaandika✍🏻✍🏻✍🏻_
[email protected]

Ndugu nawasalimu katika jina la Yesu kristo wanazareti.
Niwakaribishe Tena kwenye mfululizo wa makala zangu kwa neema ya Mungu.

Leo na kila jumanne nitakua nikiangazia swala ziama la IMANI NA MATENDO. Hapa hapa kwenye group letu la VIJANA WA INJILI. https://chat.whatsapp.com/HTOIMFb8K4eHRpqSKAbDxn

Kabla sijaenda mbali lazima tujue
*Imani Ni Nini?*
*Na imani na matendo Ni nini*

*IMANI* Ni msukumo mkubwa wa kihisia kuhusu Jambo fulani/mtu/kitu.
*Kibiblia IMANI* nikuwa na hakika ya Mambo yatarajiwayo.
Waebrania 11:1
_[1]Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana._

Biblia inasema kwa na *hakika* ya *Mambo* ya *tarajiwayo*

*Hakika*. _Ni kujua bila shaka kuwa hicho kitu kipo/kimetendeka_
Hivyo basi mtu huyu ana uhakika kwamba Jambo fulani limesha tendeka. Au litatendeka *kwa sababu yupo atakae litenda*
Huwezi sema tuu Jambo hili litafanyika na haujuu namna litakavo fanyikaa. ( Yani hakuna mikakati).

Tena asema. *Nibayana ya Mambo yasio onekana*
_K**a kitu hakija onekana Basi Ni nje ya uweza/fahamu wa kibinadamu_. Ina maanisha Ni katika uweza wa Mungu.

Kabla sijaendelea. Niseme tuu K**a watu wanachanganya kitu kimoja. Kunaimani ya kumwamini Yesu K**a bwana na mwokozi wa maisha yako uka okoka(hiyo nayo Ni imani)
Lakini kunaimani ya kumwamini Mungu/Yesu k**a muweza wa yote. K**a Mungu wako, K**a bwana wako na K**a baba yako.
Kuamini ukuu wake na mamlaka yake.
Kuamini matendo yake na Nguvu zake.

Imani zote hizi lazima ziambatane na MATENDO.
Huwezi sema umeokoka wakati hatuoni matendo yako ya ipasayo imani ya wokovu.

Lakini wakati huo huo imani pia Ni karama/kipawa ambacho anapewa mtu na Mungu kupitia roho mtakatifu. Ndio maana kunawatu mazingira fulani Wana imani kubwa Sana Tena Sana.

Lakini sote tunapaswa kuwa na imani katika kristo.

*Itaendelea...............*

Unataka kufahamu zaidi. Usikose kila juma tano saa mbili usiku..

WhatsApp Group Invite

*TUMIKA UKU UKIJUA NAFASI YAKO.* Ndugu Victor anaandika✍🏻✍🏻✍🏻    Ndugu nawasalimu katika jina la Yesu kristo wanazareti....
28/04/2020

*TUMIKA UKU UKIJUA NAFASI YAKO.*
Ndugu Victor anaandika✍🏻✍🏻✍🏻
Ndugu nawasalimu katika jina la Yesu kristo wanazareti.
Somo lililopita tuliona vile kila mtu alie amini/ okoka. Ni mtumishi wa Mungu. Na kwamba kila mmoja analo kusudi ambalo Mungu amemkusudia katika maisha yake.
_Leo embu tuendelee kwa kuangalia jinsi ya kutumika huku ukijua nafasi yako._
Tunaongozwa na msitari huu
Warumi 12:5
[5]Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

Biblia inaeleza wazi kwamba sote tulio mwamini kristo na kumkiri kuwa bwana na mwokozi wa maisha yetu.
*Tumefungamanishwa pamoja na kuwa mwili mmoja na Yesu mwenyewe ndio kichwa chetu.*
_Hii nikusema kwamba K**a vile mwili unavyo fanya kazi pamoja nasisi vivyo inatupasa kutumika pamoja_
Hii iko hivyo kwa ujumla wake. Kwamaana ya ndani ya kanisa moja. Na wakristo wote pia. Najua hujaelewa.
Na maanisha hivi. K**a Ni kanisa la CAG magomeni au PAG au KLPK au KLPT. Basi pale kanisani wote imewapasa kuwa mwili mmoja mfanye utumishi wenu pamoja.

Hivyo basi katika kumtumikia Mungu. Kitu muhimu Ni *Upendo* . Bila *Upendo* utumishi wako Ni buree kabisa. Kwanini Upendo Ni kitu muhimu katika utumishi.
*1. Upendo huondoa majivuno.*
Unapo mtumikia Mungu hutakiwi kujivuna. Hatak**a Mungu atajidhihirisha kwaku kwa namna isiyo yakawaida bado unatakiwa kubaki K**a vile mwanzo ulivyo kuwa.
*2. Upendo hujali wengine*
Ukimtumikia Mungu kwa Upendo huta fanya ili mradi umefanya Bali utaangalia je simkwazi mtu. Je wanaoniongoza nawapa nafasi? N.k

1 ```Wakorintho 12:26
[26]Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.```

*_Sikuzote mkono utabaki kuwa mkona na kidole kuwa kidole_*
Maranyingi tumeona watu wakipata huduma Fulani kanisani hujitenga na kwenda kuanzisha aidha makanisa au mahema.
Hapa wengi ndipo wanapo ua huduma zao bila kujua wameua na wanaendelea kutumika wakijua bado wako Moto kumbe walisha poa.
Mwili Ni mmoja na kila kiungo kina saidia kingine.
Mungu anapokupa kipawa/karama au huduma Fulani kanisani anataka ukitumie hicho kulisaidia kanisa mahali fulani hivyo Ni jukumu lako Sasa kusikiliza kile viongozi wako watakutaka kufanya. Bila kuathiri huduma yako/ utumishi wako.
Ona mfano huu.

```Mtu mmoja aliondoka kanisa fulani kwa sababu alijiona ana huduma ya kupiga vyombo vya muziki lakini nik**a pale kwenyelile kanisa hawajali Sana kuhusu muziki. Akaenda tafuta kanisa kubwa lenye wanavyombo wanapiga muziki akijua pale atatoka/ atajulikana kirahisi. Lakini alikuja kugundua tayari pale Kuna wanao pendwa na tayari Wana majina. Hivyo akapoteza kipaji/ kipawa chake```
Laiti angebaki pale kanisani na akamsihi Mungu amtengenezee nafasi huenda angefanya vizuri zaidi.

Hivyo tambua utumishi wako hapo ulipo Ni Mungu amekuweka. Cha msingi nikujinyenyekeza kwa Mungu na kujitoa vizuri kwa *Upendo*

*Utumishi sio kuhudumu madhabauni tuu*
Watu wengi wanajua utumishi Ni kuhudumu madhabauni tu.
Hapana. Utumishi Ni kile unafanya kwa ajili ya Mungu (Yesu). Na kwaajili ya kanisa lake na watu wake. Ikiwa Ni kuomba, ikiwani ni kumtolea Mungu, ikiwa ni kukaribisha wageni, ikiwa nikusaidia wasionacho, ikiwa ni uinjilisti, ikiwa ni usafi vyote hivyo kwa *Upendo* huku ukijua unamtumikia Mungu alie mbinguni. Utabata baraka nyingi za Rohoni na mwilini na thawabu kubwa mbinguni.

Utumishi Ni mpana Sana na katika utumishi Kuna huduma na karama na vipawa.
Usikose somo lijalo..
Kwa kujiunga nasi katika link hiyo👇🏽👇🏽
https://chat.whatsapp.com/HTOIMFb8K4eHRpqSKAbDxn

K**a bado huja subscribe kwenye channel yangu nikuombe u subscribe leo kwani kuanzia mwezi ujao kutakua na vipindi muhimu kwa ajili yako
Fuata linki👇🏽👇🏽
https://youtu.be/dt7R1mxvdeo

WhatsApp Group Invite

*KILA ALIE AMINI NI MTUMISHI WA MUNGU.*Na ndugu Victor     Watu wa Mungu nawasalimu katika jina la Yesu kristo.Ni furaha...
26/04/2020

*KILA ALIE AMINI NI MTUMISHI WA MUNGU.*

Na ndugu Victor
Watu wa Mungu nawasalimu katika jina la Yesu kristo.
Ni furaha yangu kuwa Mungu kwa rehema zake amenisaidia. Kwa Mara nyingine Tena kuandika ujumbe huu mahali hapa.
Ashuriwe Mungu kwamba kila siku anazidi kutufungua na kunena nasi kwa namna ya pekee. Hivyo basi Soma hadi mwisho ili unielewe vizuri.

Mungu kwa njia ya mwanae Yesu kristo Ali tuzaa mara ya pili. Kwa mbegu isiyo haribika.
1Petro 1 : 23.

*Aliezaliwa Ni Nani??*
Alie zaliwa Ni yule alie amini kwamba Yesu Ni mwana wa Mungu. Na amekufa kwaajili ya makosa na dhambi zake. Kwa lugha nyingine tunasema *(alie okoka)*
Kwamaana imeandikwa aaminie na kubatizwa ataokoka. Marko 16:16

```Hivyo basi kuamini Ni njia ya kukuleta kwa kristo```
_Lakini je unakuja kwa Yesu kufanya Nini Unaokoka ili iweje?_
Jibu Ni rahisi tuu. *Na kila mtu atakwambia. Naokoka ili niende mbinguni.*
Nisawa ila ukibakia hapo utakosea.

Biblia inasema.
1 Yohana 4:10
[10]Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu.
_Yeye alitupenda sisi kwanza_
Kwanini alitupenda _aaa Basi kunakitu kinatupasa kufanya_

Turudi nyuma kidogo.
Huwezi kumuamini mtu usie mpenda haiwezekani kabisa.
Hivyo basi kuamini kunafanya kuumbika kwa kitu kipya nacho Ni upendo katika kristo. Upendo wa kumpenda yule unae mwamini

K**a nilivyo sema hatuku okoka tuu ili twende mbinguni lakini Mungu alikua namakusudi na sisi ndio maana akatuokoa.
Yohana 6:44
[44]Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.
_Kwamba Mungu mwenyewe ndio humvuta mtu_
Ili aje amtumikie. Hakuna alie okoka bahati mbaya Mungu analo kusudi na wewe. Ndio maana akakuokoa.

*KUSUDI HILO NI NINI?*

Mungu alituokoa ili tu mtumikie. *(i.e. haijalishi hali yako)*

```_2 Timotheo 1:9
[9]ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele,_```

1. _Akatuita kwa mwito mtakatifu_
Hatukuja wenyewe kwa Yesu
2. _Kwa kadiri ya makusudi yake_
Kwamba kunakusudi la Mungu katika maisha yetu.
Haipaswi nikae tuu. Nisuburi kwenda mbinguni. La hasha ndugu zangu Mungu anataka tulitumikie kusudi lake.
Anataka tuyatoe maisha yetu kwa kusudi lake.

Usije ukwawa Ni mkristo wa kuja kanisani na kuondoka. Hapana. Hiyo Ni mbaya. Mwambie Mungu nisaidie nilitumikie kusudi lako.

Ukitaka kuheshimiw na Mungu. Njia Ni moja tuu kumtumikia. Haijalishi hali, Wala nyakati. Tafuta kujua kusudi la Mungu katika maisha yako.
Usione K**a Mambo yanaenda ukaridhika.
*Tafuta kulitumikia kusudi la Mungu*
Yohana 12:26
[26]Mtu *akinitumikia* , na anifuate; nami nilipo, ndipo na *mtumishi wangu* atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba *atamheshimu* .

_*Ukitaka Mungu akuheshimu mtumikie*_
*_*Ukitaka kuwa pale Yesu atakapo kuwa mtumikie_**

Tafuta leo. Omba leo kujua kusudi la Mungu ili umtumikie.......

WhatsApp Group Invite

WAPENDWA nafurahi kwasababu Bado bwana ameendelea kutu hifadhi pamoja.  Napenda kuwa taarifu kuwa. RATIBA YA GROUP ITAKU...
10/04/2020

WAPENDWA nafurahi kwasababu Bado bwana ameendelea kutu hifadhi pamoja.
Napenda kuwa taarifu kuwa.
RATIBA YA GROUP ITAKUA HIVI
*Jumapili* --- _itakuwa siku ya kushea moyo. Kile ulicho nacho shiriki nasi bila woga_
*Jumatatu* --- _Siku ya mjadala. Na mada itatolewa kwa ajili ya wiki hiyo (K**a una mada ungependa tushiriki. Tuma kwa admin)_
*Jumanne* --- _siku ya maswali. Ukiwa na swali lolote utauliza na litajibiwa_
*Jumatano* --- _Mjadala ( ule ule wa wiki)_
*Alhamisi* --- _Mafundisho_
*Ijumaa* --- _Mjadala_
*Jumamosi* --- _Maswali na kushare moyo pamoja_

*Muda wa Mjadala Ni kuanzia saa moja na nusu Hadi saa nne na nusu*

*Kumbuka.* ```~Usiache kushiriki nasi kwani tunataka kujengwa pamoja. Sote Ni ndugu na tunasafiri kwenda mbinguni~```
Share nasi na Mungu atakujaza

WhatsApp Group Invite

*MAMBO HATARI KWA AFYA YA ROHO YAKO*     Ndugu wakristo ninawasalimu katika jina la Yesu.   Nina mshukuru Mungu kwa upen...
25/03/2020

*MAMBO HATARI KWA AFYA YA ROHO YAKO*
Ndugu wakristo ninawasalimu katika jina la Yesu.
Nina mshukuru Mungu kwa upendo wake kwetu sisi hata tuwazima na tunakiri uku wake kwetu.
Ndugu nivizuri kujua kua maisha ya kiroho nayo Yana hitajika kulindwa Sana ili kuhakikisha unakua vizuri kiroho.
K**a vile afya ya mwili wako ilivyo ya muhimu na kwamba huwezi kula kila kitu pakaujue faida yake kwenye mwili. Ndivyo ilivyo Rohoni kwamba lazima tujilinde ili afya yetu iwe imara na salama.
Yafuatayo Ni Mambo ya kuepuka ili afya yako Rohoni iwe imara.
*1. Epuka mazungumzo yasio na maana*
Mazungumzo yasio na maana hukausha hali yako ya roho na kuruhusu maneno maovo kinywani mwako. Kadiri unavyo yasikiliza maneno yasio na maana(maovu) ndivyo unavyo jisogezea kuyanena. Na kukausha kabisa Nguvu yako kiroho.

*2. Kusikiliza miziki ya kidunia (world/ secular music*)
Musiki nikitu kinacho penya haraka kwenye akili na moyo wa binadamu.
Nikweli kwamba miziki yawezatumika K**a tiba wakati mwingine lakini nibora tiba isiyokuletea madhara badae.
Ukweli nikwamba kila muziki hubeba roho ya yule alie uimba. Kamuimbaji Ni mvutaji wa bangi/mlevi wa pombe
kadiri utakavyo kuingia muziki wake ndivyo utakavyo fanana nae kuanzia mavazi Hadi matendo. Epuka kusikiliza miziki ya kidunia

*3. Ku acha maombi.*
Ukipunguza maombi Ni njia ya shetani kushambulia maisha yako. Nguvu ya kushinda ipo katika maombi usipo jizoeza kwenda mbele za Mungu wewe mwenye anae kuombea asipo kuwepo hutakua na Nguvu yakushinda jaribu likija.
Penda kwenda mbele za Mungu wewe mwenyewe.

*4. Mahusiano ya kimapenze(Boyfriend/girlfriends)*
Watu wengi makanisani leo wanataka kufanana na ulimwengu. Yale yanayotendwa na Wana wa dunia na wao wanataka kuyatenda. Chakusikitisha hawaoni shida kufanana na ulimwengu wakati biblia inatuambia "Wala msiifutishe namna ya dunia hii Bali mfanywe upya kwa kugeuzwa Nia zenu". Nia zetu zinapaswa kugeuzwa zisifanane na ulimwengu.
Wapo wanao fikiri nivibaya kufanya NGONO/ Zinaa. Lakini kuwa na mpenzi sio shida.
Ukweli nikwamba unaweza ukazini kabla hujaifunua sketi au hujaivua suruali. Hayo Ni madhihirisho tuu kuwa mlisha itenda hiyo dhambi mioyoni mwenu.
Kuwa na mpenzi kunatoa nafasi kwa shetani kupaka matope maisha yako ya kiroho. Hutakua na Nguvu ya kukabiliana na dhambi. Epuka epuka epuka Mahusiano ya sio sahihi.

*5. Mitindo ya mavazi na nywele*
Niliwahi muuliza mtu wewe unamfahamu mchungaji yeyote alie mwana mitindo na mtindo wake ndio ufiata.
Akaniambia hapana. Hii nikuthibitisha kuwa mitindo ya mavazi na nywele ni mpango wa adui kumfarakanisha mtu na muumba wake.
K**a ilivyo kwa muziki. Hata mitindo pia kila mtindo umebeba roho ambayo nikinyume na roho wa kristo Roho hiyo kusudi lake nikuharibu ibada yako mbele za Mungu inakuondolea uhalali wakupaingia patakatifu pa patakatifu. Na kazi ya roho hizi nikuondo nafasi ya roho mtakatifu ili dhambi iingie maishani mwako na hatimae ufe kiroho.

Mungu atusaidie tuyaone haya na kujitaidi tusiingie kwenya mitego ya adui ili uhai wetu uwe salama.
Na afya yetu ya kiroho izidi kuimarika
Barikiwa.......

WhatsApp Group Invite

Address

P. O BOX TANGA
Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kanisa La Sauti Ya Kalvari Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kanisa La Sauti Ya Kalvari Tanzania:

Share