29/04/2019
Mapendo,.. Mungu ni mwema kila wakati maishani mwetu,kila tumwombapo ,yeye hujibu kwa wakati sahihi zaidi ya tulivyotarajia kupata.Kila mara Yesu katika uhai wake wa mwili,alipenda kutumia mifano kwa taifa lake.Siku moja Yesu alitoa mfano Akasema.Tenga wa angani hawapandi wala hawavuni na wala hawakusanyi gharani mazao ya ulimwengu,ila Baba yetu wa Mbinguni uwategemeza kwa yote.Wanakula na kunywa,wanapendeza na kuishi.Nasi ni k**a ndege wa angani,Bwana Mungu anatupenda kuliko ndege wa angani,anatulisha na kutunywesha ,anatupndezesha,anatupa uhai,.Sasa kidato cha sita tunakaribia kuingia katika mtihani wetu wa Taifa .Tukumbuke ya kuwa sisi ni zaidi ya ndege wa angani, Bwana Mungu atatenda kwa ajili yetu.Atamtuma Roho wake ,aje kuketi nasi katika kiti kimoja cha mtihani,ashike a pen tutakayoshika,atuwazie yaliyo makuu na ukweli na atafanya mtihani kwa niaba yetu,AMINA,. Ila tukumbuke yakuwa, ndege wa angani huruka huku na kule wakitafuta mema ya nchi waliyoandaliwa na Bwana Mungu,hivyo nasi pia kwa kipindi hiki kilichobaki tuendelee kujisomea na kumkumbuka yeye Yesu wetu rafiki na mwalimu wa kweli ili tupate hayo mema aliyotuandalia Bwana Mungu. Tukumbuke ya kuwa, Mungu wetu ni mwaminifu,anatupenda sana,anampenda hata mwenye dhambi ya kutisha bali huchukia ile dhambi tu,tufanye toba ya kweli,tukaungame ,sadaka.💞