Mfahamu MUNGU vizuri

Mfahamu MUNGU vizuri K**a Unampenda mungu naomba usiache kulike page hii tujifunze kuhusu mungu wetu na pia cheki page on twitter by MUNGU [email protected]

11/09/2018
11/09/2018
20/11/2017

MWANADAMU K**A JENEZA
Fungu kuu:- Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, kijana, nakuambia Inuka. Luka 7:14
Sifa za jeneza
 Jeneza hutengenezwa kwa mbao, na misumari huku likipakwa vanishi au rangi mbali mbali nzuri za kuvutia.
 Kuna mengine yenye thamani kubwa hunakishiwa kwa madini yenye thamani kubwa k**a dhahabu na hutumiwa na watu matajiri wakubwa Duniani.
 Mengine kwa ndani huwekewa sponge na vitambaa raini vyeupe kulifanya lipendeze zaidi.
 Kwasasa mtu kuzikwa bila jeneza huonekana k**a kumdhalilisha marehemu.
 Lakini pamoja na kupambwa kote huko Jeneza hubeba Maiti.
 Kwa wakristo majeneza hufukiwa ndani ya makaburi lakini kwa waislamu marehemu hutolewa ndani ya jeneza baada ya kufika eneo la kuzikia.
Neno jeneza ndani ya Biblia limeoneka mara mbili pekee ambapo sehemu ya kwanza ni katika 2Samweli 3:31 “Kisha Daudi alimwambia Yoabu, na watu wote waliokua pamoja naye, Rarueni nguo zenu, mkajivike nguo za magunia, mkamlilie Abneri. Naye mfalme Daudi akaifuata jeneza.”
Na sehemu ya pili ni katika Luka 7:14 “Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, kijana, nakuambia Inuka.”
Kwanini mwanadamu k**a jeneza?
Yakobo 2:17 “Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo imekufa nafsi mwake” imani inapaswa kuwa hai ndani ya mwanadamu ili itende kazi lakini imani isipo kua hai imekufa kabisa (Maiti).
Imani ambayo iko hai ikoje?
Yakobo 2:14 “Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? Ukweli ni kwamba huwezi kusema mtu yuko hai ikiwa hana matendo ndani yake, wanasayansi wanazo sifa kuu nane za viumbe hai ambazo ni:-
 Movement/locomotion (kutembea/kujongea). Imani haipaswi kukaa sehemu moja ni lazima itoke kufanya kazi. Yakobo 1:27 “Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.” Fungu hili linatuambia dini yenye imani hai sio kukaa sehemu moja na kumuabudu Mungu bali pia kwenda kuwatazama wasio jiweza.
 Irritability/sensitivity (kuhisi). Imani iliyo hai ni lazima ihisi uwepo wa Mungu katika maisha ya mwanadamu. Yohana 20:29 “Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki.
 Feeding/Nutrition (kula). Imani ili iwe hai nilazima ile chakula ambacho ni mkate wa uzima yaani maandiko matakatifu. Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”.”
 Respiration (upumuaji). Ili mtu awe hai ni lazima awe anapumua, Mungu alipo muumba mwanadamu alimpulizia pumzi ya uhai, Mwanzo 2:7 “BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Wakati fulani Yesu alitoa mfano wa wanawali kumi ambapo watano walikua welevu wenye mafuta ya kutosha lakini wengine wapumbavu hawakua na mafuta ya kutosha.Katika Mathayo 25:1-13. Mafuta pamoja na pumzi ni uwepo wa roho mtakatifu katika imani. Imani bila roho mtakatifun ni sawa na nyumba bila msingi.
 Excretion (utoaji wa taka mwili). Imani iliyo hai ni ile inayo muongoza mtu kutambua makosa yake na kutubu yaani kuondoa taka katika hekalu la roho mtakatifu. Mathayo 3:2 “Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.” Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubili akisema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.” 1yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondelee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
 Reproduction (kuzaa). Yakobo 2:20 “Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai? Luka 3:9 “na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.” Luka 13:7 “Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?.”
 Growth (kukua). Imani inapaswa kukua k**a iko hai, itakua kwa kulishwa neno la Mungu na kufanya mazoezi ya kutoka kufanya kazi ili ikomae iweze kupitia nyakati nzuri na mbaya ikiwa imara.
 Death (kifo). Imani inakufa lakini inakufa kwa wakati maalumu ambapo mwanadamu anakufa na vitu vyote alivyo kua anavifanya vinakufa.
Imani inapokosa sifa hizo hapo juu hiyo itakua imekufa ndani ya mwanadamu na mwanadamu atakua amebeba maiti ya imani ndani yake huku akiwa anaendelea kwenda kanisani kusali na kujipamba kwa nje kuuonyesha ulimwengu jinsi ambavyo ni mzuri wa umbo na sura na kusahau kuonyesha uzuri wa ndani ambao ni matendo ya imani iliyo hai.
Lakini endapo mwanadamu ataacha kutenda matendo ya imani, maiti ya imani itaanza kuharibika kwa maana ya kwamba uchafu utaanza kutoka ndani yake k**a uchafu uwezavyo kutoka ndani ya jeneza lililo beba maiti kwa muda mrefu k**a vile funza na harufu mbaya itakayo pelekea jeneza kufukiwa haraka iwezekanavyo.
vivyo hivyo wizi, ujambazi, ubakaji, ukahaba, ulevi, matusi na mengine mengi yafananayo na hayo yaweza onekana kwa mtu aliye mbeba marehemu imani. Hatima yake huwa kifo kisicho cha matumaini au kuambulia maradhi yasiyo na tiba k**a UKIMWI na magonjwa yaendanayo na huo. Hatima ya mtu huyu huwa ni kifo pekee chenye majuto makubwa ndani yake.
Nini cha kufanya?
Kaa chini ujitathimini k**a wewe ni jeneza au la! Na k**a ni jeneza umebeba maiti ya namna gani? Ukisha kugundua yote hayo piga magoti mwite yesu akuguse k**a alivyo gusa jeneza la kijana na kumwambia ainuke, umwambie akuguse na aipatie pumzi maiti ya imani iliyoko ndani yako nayo itanena tena!!!!!! Wakati ndugu wa Lazaro wakiwa wameanza kumsahau na kutambua ya kwamba ndugu yao atafufuka katika ufufuo wa kwanza lakini Yesu alimfufua pasipo wao kutarajia… alimwita Lazaro kutoka kaburini na Lazaro akatoka akawa hai tena. Imani yako ilyo kufa inaweza kuwa hai tena ukimfanya Yesu kuwa rafiki yako wa karibu k**a Lazaro.
Imeandaliwa na Musa J. Mabula Call:- +255 685 450 410 +255 714 750 576 Whatsapp:- +255 623 863 093 Email:- [email protected]
MUNGU AWABARIKI SANA

20/11/2017

KUTUNZA SABATO PEKEE SIO UTAKATIFU
Nina wasalimu katika jina la bwana wetu Yesu Kristo aliye shinda dhambi na mauti. Ni hakika tangu kuondoka kwake hakuja patikana mtu mwingine aliyeweza kufanya aliyo yafanye yeye, nani k**a Yesu? Jibu ni hakuna, aliishi k**a mwanadamu pasipo kutenda dhambi maisha yake yote ya duniani. Huyu ndie taa yetu wakirsto wote duniani, kunawakati ilibidi kutumia nguvu kuwafanya wanadamu wajue thamani ya kumtii Mungu na kuna wakati ilibidi awe mpole, nampenda sana Yesu mtu mwenye Hekima, Busara na Upendo mkuu.
Lakini pamoja na kufanya mengi sana Yesu alihakikisha haachi utata hata kidogo juu ya amri na sheria za Mungu na ndio sababu aliwahi kusema sikuja kuitangua Torati (Matheyo 5:17). Hata wakati flani aliwaeleza watu katika Mathayo 5:19 “Basi mtu ye yote atakaye atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwa fundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakaye zitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni”. Yesu alizidi kusisitiza juu ya utunzwaji wa amri zote iwe ndogo au kubwa.
Lakini tulio wengi leo kwa kua sabato imetajwa kuwa ndio muhuri ama ishara ya Mungu kwa watu wake katika Ezekiel 20:20 basi tumekua tukiijali sana hii kuliko zingine zote, watu tumekua waongo na wasengenyaji ndani ya kanisa na tumesahau kuwa ni dhambi, uzinzi na ulevi vyoote huficha na utunzaji wa Sabato, kutokutoa Dhaka na Sadaka havionekani kisa mtu anatunza sabato.


Hivi unaifahamu hesabu ya kumi toa moja ni sawa na sifuri, Yakobo 2:10 “Maana mtu awaye yeyote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa katika yote”.


Sasa k**a ndivyo kwanini tuzisahau zingine na kazana na moja tu? Nadhani hapa panafaa sasa kuanza kuelewa ya kwamba katika mwili kila kiungo kina faida yake na ukiondoa kimoja basi vingine vitafanya kazi kwa shinda shida sana, jaribu kuwaza gari bila kita cha Dereva, au gari bila taili moja itaweza kwenda ama itapinduka? Bado tuna safari na Yesu ndiye kiongozi wa safari na Amri kumi ni alama za barabara tupitayo na ndio sababa sisi tunapaswa kuzifuata k**a afanyavyo Dereva Yesu Kristo.
Tukiacha kupuuza amri zingine na kuzitii zote kasha tukaitunza sabato ya Mungu vizuri ni hakika Huu muhuri wa Mungu hauta futika kamwe na yesu atakapo kuja kuchukua walio wake Sabato itabaki kuwa ishara kubwa sana ya watakatifu.
Mwisho niwatakie safari njema ya imani na utii kwa Mungu wetu.
Musa Joel Mabula
0714750576
[email protected]

18/10/2016

k**a una swali lolote unahisi linakuchanganya kuhusu Mungu wa mbinguni, nitumie kwenye hii page au niandikie kupitia [email protected] au nitumie kwa njia ya sms kawaida kupitia 0714750576 nami nitakujibu kupitia hapahapa katika hii page.

26/11/2015

Mwenye Haki atasitawi k**a mtende atakuwa k**a mwerezi wa rebanoni. (zaburi 92 :1)
Ndugu msomaji zaburi inapo Sema juu ya mtende ndipo nafikia hatua ya kuanza kutaja sifa za mtende ili tujifunze kwazo
1.Mtende huota jangwani
Dunia tuliyo nayo ni k**a jangwa, mimi na wewe tunakiwa tukubali kuishi kwenye Dunia hii ambayo imejaa dhiki na shida k**a jangwani, vifo, magonjwa, na
Shida nyingine nyingi tukiwa tunasitawi kiroho k**a mtende jangwani

08/01/2015

Watu wengine wakikumbwa na matatizo husema ni mipango ya mungu huku wakifanikiwa na kujisifu wenyewe. Hivi ni baba yupi ambaye huzaa mtoto ama mama yupi pia huzaa mtoto ili ateseke?! Hii haiwezi kutokea hata kwa kichaa mwenye mtoto. Shetani hututia katika majaribu na masumbuko ili tumkufuru Mungu tu, siku zote wakulaumiwa kutokana na matendo mabaya ni shetani wala so Mungu. Mungu ni baba mwema kwetu na anahitaji watoto waliokamilika na ndo maana akaruhusu majaribu yatupate lakini yakitokea kwa shetani wala so Mungu. Tulimpokea shetani wenyewe katika busitani ya edeni huku katika sayari zingine akiwa amekataliwa kwa kuwa ni mwovu.
Soma kitabu cha yakobo chote kisha utaelewa zaidi nini namaanisha.
Hivi ndivyo tulivyo uanza mwaka 2015 tutaendelea kupeana masomo mbalimbali kupitia ukurasa huu.
K**a unamaswali ya kuliza usisite kutumia ukurasa wetu huu au tuma swali lako kupitia Namba 0763505185.
Mungu akubaliki

isaya 58:1 piga kelele, usiache, paza sauti yako k**a tarumbeta; uwahubiri watu wangu kosa lao na nyumba ya yakobo dhamb...
15/05/2014

isaya 58:1
piga kelele, usiache, paza sauti yako k**a tarumbeta; uwahubiri watu wangu kosa lao na nyumba ya yakobo dhambi zao.

Address

Tanga
Tanga

Telephone

0714750576

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mfahamu MUNGU vizuri posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share