St. Anthony's Cathedral Tanga

St. Anthony's Cathedral Tanga Karibu kufuatilia Matangazo yetu.

HABARI PICHA KANISA KUU.Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Familia Takatifu kutoka ...
29/12/2025

HABARI PICHA KANISA KUU.
Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Familia Takatifu kutoka Kanisa Kuu la Mtakatifu Anthony wa Padua Chumbageni.
Katika Misa hiyo kulikuwa na matukio yafuatayo:-

Utoaji wa Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 60
Kufunga Jubilei Kuu 2025 kwa ngazi ya Jimbo
Ufunguzi na kubariki Jengo la Groto la Mama Bikira Maria na Mtakatifu Yosefu Baba mlishi wa Yesu

Sadaka ya Misa Takatifu imeongozwa na Mhashamu Thomas John Kiangio Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga.

HABARI PICHA KWAMNDOLWA.Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu Sherehe ya Bikira Maria Mki...
08/12/2025

HABARI PICHA KWAMNDOLWA.
Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili somo na Msimamizi wa Shirika la Masista wa Mama yetu wa Usambara (COLU) kutoka Makao Makuu ya Shirika Kwamndolwa- Korogwe Jimbo Katoliki Tanga

Sadaka ya Misa Takatifu imeongozwa na Mhashamu Stephano Lameck Musomba OSA wa Jimbo Katoliki Bagamoyo akisaidiwa na mwenyeji wake Mhashamu Thomas John Kiangio Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga pamoja na Mapadre kutoka Jimbo Katoliki Moshi na Same na wenyeji Jimbo Katoliki Tanga pamoja na Shirika la Mapendo(Rosmin Fathers) na Mapadre wa Shirika la Kazi za Roho Mtakatifu (OSS).

Masista kutoka Mashirika mbalimbali wanaofanya utme wao ndani ya Jimbo na waamini kutoka sehemu mbalimbali za Jimbo Katoliki Tanga, Moshi na Same.

HABARI PICHA KANISA KUU.Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu Dominika ya Pili ya Majilio...
07/12/2025

HABARI PICHA KANISA KUU.

Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu Dominika ya Pili ya Majilio Mwaka A wa Kanisa kutoka Kanisa Kuu la Mtakatifu Anthony wa Padua Chumbageni.

Sadaka ya Misa Takatifu imeongozwa na Mheshimiwa Padre Godfrey Joseph Mushi Paroko Msaidizi wa Kanisa Kuu

HABARI PICHA KANISA KUU.Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu Dominika ya Kwanza ya Majil...
30/11/2025

HABARI PICHA KANISA KUU.
Matukio mbalimbali katika PICHA wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu Dominika ya Kwanza ya Majilio na mwanzo wa Mwaka A wa Kanisa kutoka Kanisa Kuu la Mtakatifu Anthony wa Padua Chumbageni.

Sadaka ya Misa Takatifu imeongozwa na Mheshimiwa Padre Sylvester Nitunga ambaye Mlezi na Mkufunzi wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Paulo iliyopo Kipalapala Jimbo Kuu Katoliki la Tabora

02/06/2025

KARIBU KWENYE KUFUATILIA MATANGAZO YA MASIFU YA JIONI NA MISA TAKATIFU YA DARAJA TAKATIFU YA UPADRE JIMBONI TANGA

31/05/2025

Karibu kwenye Novena ya Roho Mtakatifu siku ya pili tarehe 31.05.2025 siku ya Jumamosi

30/05/2025

Karibu kwenye Novena ya Roho Mtakatifu leo tarehe 30.05.2025 siku ya Ijumaa

TUWAKUMBUKE MAREHEMU MAPADRE WETU WA JIMBO KATOLIKI TANGA. Marehemu Padre Richard Mshami alizaliwa July 1953 na wazazi b...
20/03/2025

TUWAKUMBUKE MAREHEMU MAPADRE WETU WA JIMBO KATOLIKI TANGA.

Marehemu Padre Richard Mshami alizaliwa July 1953 na wazazi baba Joseph Mshami na mama Maria Tupa katika kijiji cha Mkuzi wilayani Lushoto Tanga Tanzania.

ELIMU
1963 – 1970: alipata elimu ya msingi darasa la I – VII katika shule msingi Kionwa Mkuzi, Lushoto, Tanga, Tanzania.
Baada ya kumaliza elimu ya msingi alijiunga na Seminari ndogo ya Mt. Peter huko Morogoro kwa masomo ya sekondari kuanzia mwaka 1971 – 1974 kwa kidato cha 1 – IV.
1975 – 1976: alijiunga na Seminari kuu ya Kibosho Moshi kwa masomo ya Falsafa (Philosophy)
1980: alifanya mwaka wa kichungaji parokiani Gare Lushoto Tanga.
1977 – 1981: alisoma masomo ya Thelojia (Theology) katika seminari kuu ya Kipalapala Tabora Tanzania

USHEMASI NA UPADRE
June 9, 1981: alipewa daraja la ushemasi katika kanisa la Mt. Anthony wa Padua (Cathedral) Tanga, Tanzania
November 22, 1981: alipata daraja takatifu la upadre katika kanisa la Mt. Anthony wa Padua (Cathedral) Tanga, Tanzania

UTUME WAKE KATIKA KANISA
1981 – 1984: alihudumu k**a paroko msaidizi katika parokia ya Mlingano, Tanga, Tanzania
1984 – 1987: Paroko msaidizi parokiani Kilole Korogwe.
1987 – 1988: Paroko msaidizi katika parokia ya Lushoto.
1988 – 1992: Paroko msaidizi parokia ya Mt. Theresia wa mtoto Yesu Bar.20 Tanga, Tanzania
1992 – 1997: Paroko parokia ya Magoma, Korogwe, Tanzania.
1997 – 2002: Diocesan Director for Apostleship of the Sea in Tanga, Tanzania
2002 - 2009: Paroko parokia ya Malindi, Lushoto, Tanga, Tanzania
2009 - 2011: Paroko msaidizi parokia ya Mkuzi, Lushoto, Tanga, Tanzania
2011 - 2014: Paroko msaidizi parokia ya Mlingano, Tanga, Tanzania
2014 - March 10, 2021: Paroko parokia ya Mlingano, Tanga, Tanzania

KIFO
Marehemu Padre Richard Mshami aliugua kifua kwa muda mrefu. Siku za mwisho wa uhai wake ililazimika kulazwa hosipitalini huko Dar Es Salaam. Machi 10, 2021 Mungu alimuita mpendwa wetu Padre Richard Mshami katika makao yake ya milele mbinguni.
Marehemu Padre Richard Mshami alizikwa siku ya Jumatano Machi 17, 2021 kwenye makaburi ya mapadre jimbo parokia ya Kilole, Korogwe.

Tunamshukuru Mungu kwa utume wa Padre Richard Mshami jimboni Tanga. Ameweza kulitumikia kanisa k**a padre kwa muda wa miaka 40.

Raha ya milele umpe ee Bwana: Na mwanga wa milele umwangazie.
Apumzike kwa amani: Amina.

18/03/2025

Kwaya ya Familia Takatifu kutoka Parokia ya Familia Takatifu Kwediboma Jimbo Katoliki Tanga.

HABARI PICHA|| MISA TAKATIFU  YA MAZISHI YA HAYATI PADRE ELIAS LAURENT MAIVAJI KUTOKA PAROKIA YA MAMA BIKIRA MARIA MSHIN...
18/10/2024

HABARI PICHA|| MISA TAKATIFU YA MAZISHI YA HAYATI PADRE ELIAS LAURENT MAIVAJI KUTOKA PAROKIA YA MAMA BIKIRA MARIA MSHINDI, KILOLE KOROGWE- JIMBO KATOLIKI TANGA.

Baadhi ya matukio mbalimbali yaliyojiri leo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Mazishi na Maziko ya hayati Padre Elias Laurent Maivaji
Misa imefanyika leo tarehe 18.10.2024 katika Parokia ya Mama Bikira Maria Mshindi, Kilole Wilayani Korogwe - Jimbo katoliki Tanga na Misa hiyo imeadhimishwa na Mhashamu Thomas John Kiangio Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga na Homilia imetolewa na Mheshimiwa Sana Padre Joseph Mbena Wakili wa Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga.

ikumbukwe kuwa Baba Padre Elias Maivaji alizaliwa mnamo tarehe 2.12.1962 na kupewa Daraja Takatifu ya Upadre Mnamo tarehe 09.07.1997 Katika Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu Rangwi na mapaka umauti unamkuta alikuwa Paroko wa Parokia ya Mt. Fransisco wa Asisi Mtindilo Jimbo Katoliki Tanga

Address

84
Tanga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when St. Anthony's Cathedral Tanga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to St. Anthony's Cathedral Tanga:

Share