09/05/2026
Injili ni nini?
Kwa Mujibu wa Maandiko Matakatifu " Injili ni uwezo wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye" Warumi 1:16
Kwa wengi hii ni taarifa tu na siyo uhalisia.
Kwa tafsiri yangu " Injili ni pale Mungu anapofunuliwa katika Tabia zako"
Hii ina maana k**a Mungu katika Kristo hafunuliwi katika Tabia zako injili itakuwa taarifa tu kwenye karatasi na wino.
Ulimwenguni na wenye dhambi hawatishwi na unajua kiasi gani, umesona Biblia mara ngapi, unavitabu elfu 10. Hiyo siyo shida.
Kumbuka wakati wewe Unasoma Biblia yako "watu wanakusoma wewe" Maisha yako ni Biblia kwa dunia.
Yesu anasema...... Vivyo hivyo Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, Wapate kuyaona Matendo yenu Mema , wamtukuze Baba yenu aliye Mbinguni. Mathayo 5:16
Kushika Biblia, kwenda kwenye Ibada kila siku ni jambo jema sana. Lakini unazalisha nini Kwa watu wanaokuzuka?
Je watu wanaona msamaha Kupitia wewe pale Unapo kosewa?
Je watu wanaona Upendo wa Mungu Kupitia wewe?
Kamwe hatupaswi kuwa k**a makaburi yenye rangi mzuri lakini Ndani yamejaa mifupa ya wafu.
Lazima Ile injili ambayo tunaihubiri isiwe katika maneno matupu Lazima Iwe katika tendo pia.
K**a utakuwa unebadilishwa Ndani Lazima tuone matokeo ya nje.
Jamii ya waaminio wanajikita kwenye " Miujiza" na si katika "Tabia" Tabia inanguvu Sana kuliko Miujiza.
Watu wanaweza kusahau Miujiza ila Tabia zinaweza kuishi muda mrefu " Miujiza hukoma "Tabia huishi"
Tabia humfunua Mungu Kwa haraka kuliko Miujiza, tabia ndiyo haswa humfunua mtu alivyo.
Tabia zinauwezo mkubwa kugusa maisha ya watu wanaokuzunguka kuliko Miujiza.
Na ndiyo maana leo kumekuwa na watumishi wamekaza Miujiza Lakini si tabia " naamini katika tabia kwanza kisha Miujiza "
Shetani anaweza kufanya Miujiza Lakini hawezi kuwa na Tabia njema, Mungu ana Tabia na Miujiza"
Imani ya kweli, takatifu huzaa matunda Mema " Tabia"
Ndiyo maana watu makini huvutiwa na mtumishi anayedhihilisha Tabia za Kristo ( Tunda la Roho ) na siyo Miujiza.
Ukristo si kuonyesha Vitu, Mali zetu, elimu zetu, bali ni kuonyesha ulimwengu Mungu alivyo Kupitia Tabia na mwenendo halisi katika maisha yetu.
Je, unajivunia ujuzi wako? Unawaona watu wengine ni bure , kujua Maandiko Matakatifu, kusoma na kuwa na utambulisho wa Dkt, Pof.nk. katika maisha yetu k**a wakriso watumishi wa Mungu siyo Sifa ambayo Mungu anataka .....
Paul Mtume alivyowahi kusema Ujuzi huleta majivuno (Majigambo) bali upendo hujenga.
Watu hawajali unajua Sana kuongea kwenye mc watajali unaonyesha tabia gani halisi za Mungu kila siku.
Yesu aliwahi kufundisha......
Mjihadhari na manabii wa uongo wanaokuja kwenu wakijifanya kondoo wasio na madhara ingawa ni watu hatari k**a mbwa mwitu. Mtawatambua watu hawa kwa matendo yao. Mambo mazuri hayatoki kwa watu wabaya, k**a ambavyo zabibu haitokani na miiba, na tini hazitokani na mbigiri. Vile vile, kila mti mzuri huzaa matunda mazuri na mti mbaya huzaa matunda mabaya. Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, na wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa kwenye moto. Mtawatambua manabii hawa wa uongo kwa matendo yao.
Mathayo 7:15-20
Kwa hiyo Yesu alikuwa anataka tujifunze kwa hawa wanyama wawili " Mbwa mwitu" na kondoo"
Wanyama Hawa wanatabia tofauti, kisha akawema Mfano wa mzabibu na miiba tini na mbaruti" kuonyesha nguvu ya Tabia k**a zao halisi linaloshilikishwa kwa Nje.
" Maisha ya Mkristo ambayo hayana onyesho la Tabia za Kristo kwa Nje ni udanganyifu"
Umebarikiwa Sana
Nabii Ernest Kangajaka JR.
The City of God Ministries.
TANGA, TUMAINI Street.
+255 785911212
+255 677304019
Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
The City Of God Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212