02/09/2026
AINA MBILI ZA WOKOVU
1. Aina ya Kwanza: Wokovu wa Kujitungia
• Andiko Kuu: Waefeso 2:9 – "Wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu."
• Matendo Mema: Unategemea matendo ya kibinadamu ili kukubalika.
o Uthibitisho: Isaya 64:6 – "Tendo letu la haki limekuwa k**a nguo iliyochafuka mbele za Mungu."
• Toba na Vitubio Kila Siku: Unamlazimu mtu kuomba toba kila siku ili kulinda wokovu.
o Uthibitisho: Waebrania 10:11 – Inaonyesha udhaifu wa makuhani wa kale waliotoa dhabihu kila siku ambazo hazikuweza kuondoa dhambi kabisa.
• Jitihada Zako Binafsi: Unasimama juu ya juhudi za mwanadamu badala ya neema.
o Uthibitisho: Wagalatia 2:16 – "Mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria."
• Hofu ya Kupoteza Wokovu: Mwamini anaishi kwa uoga wa kuhukumiwa wakati wowote.
o Uthibitisho: 1 Yohana 4:18 – "Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililokamilika hulifukuza hofu, kwa sababu hofu ina adhabu."
• Duniani Hakuna Kuokoka: Mtazamo kwamba mwanadamu hawezi kuwa na uhakika wa wokovu akiwa hai.
o Uthibitisho: 1 Yohana 5:13 – Uhakika upo: "Nimewaandikia ninyi mambo hayo... ili mjue kwamba mna uzima wa milele."
• Swali: Yesu Amekuja Kufanya Nini? K**a mwanadamu anaweza kujiokoa kwa sheria, kifo cha Kristo hakina maana.
o Uthibitisho: Wagalatia 2:21 – "K**a haki hupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure."
• Maombi ya Msamaha Ndiyo Msingi: Kutegemea sala za kuomba msamaha badala ya kumwamini mtoa wokovu.
o Uthibitisho: Warumi 10:3 – "Kwa kuwa, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitiisha chini ya haki ya Mungu."
• Maombi ya Kiongozi wa Dini: Kuamini kuwa kiongozi wa kibinadamu ndiye mwenye mamlaka ya kuondoa dhambi zako.
o Uthibitisho: 1 Timotheo 2:5 – "Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, mwanadamu Kristo Yesu."
________________________________________
2. Aina ya Pili: Wokovu wa Kristo Mwenyewe
• Andiko Kuu: Mathayo 1:21 – "Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake YESU, kwa kuwa yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao."
• Kristo Ndiyo Msingi: Kristo pekee ndiye msingi imara na thabiti wa wokovu.
o Uthibitisho: 1 Wakorintho 3:11 – "Kwa maana hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine, isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo."
• Njia ya Imani: Wokovu unapatikana kwa kuamini tu, si kwa nguvu zako.
o Uthibitisho: Warumi 5:1 – "Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo."
• Siyo Matendo Mema na ya Sheria: Hautegemei matendo ya sheria wala haki binafsi.
o Uthibitisho: Tito 3:5 – "Siyo kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi, bali kwa rehema yake alituokoa."
• Siyo Jitihada Zako: Ni zawadi ya bure (neema) kutoka kwa Mungu.
o Uthibitisho: Waefeso 2:8 – "Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni zawadi ya Mungu."
• Msamaha ni wa Milele: Kazi ya Kristo ilimaliza kabisa deni la dhambi zilizopita, zilizopo, na zijazo.
o Uthibitisho: Waebrania 10:14 – "Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa."
• Siyo Maombi ya Toba na Kufunga: Msamaha hautegemei matambiko ya kidini au kujitesa kwa kufunga ili kusamehewa.
o Uthibitisho: Wakolosai 2:14 – Alikwisha kuifuta ile hati ya mashtaka iliyokuwa inatukabili, akaiondoa isiwepo, akiigongomea msalabani.
• Imani katika Dhabihu Iliyotolewa Mara Moja: Kristo alikufa mara moja tu na hahitaji kurudia dhabihu yake.
o Uthibitisho: Waebrania 9:28 – "Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja tu azichukue dhambi za watu wengi."
________________________________________
Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
The City Of God Ministries
0746 911291
0785 911 212