Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries

Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries Official page of Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries | BEWARE OF FRAUDRISTERS!!

Happy Mathers day my wife Veronica Kibinga, furahia siku hii muhimu Sana, umekuwa mwanamke mwema, mpambanaji, na mwenye ...
10/05/2026

Happy Mathers day my wife Veronica Kibinga, furahia siku hii muhimu Sana, umekuwa mwanamke mwema, mpambanaji, na mwenye hekima na adabu. Nakuombe kwamba ufanikiwe katika.aisha yako uwe baraka kwangu, kwa familia yetu na Kwa jamii yote Kwa ujumla .
Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries

Shalom karibu uabudu nasi Jumapili ( Kesho) hapa The City Of God Ministries, Jiji la Mungu. Kanisa linapatikana Jijini T...
09/05/2026

Shalom karibu uabudu nasi Jumapili ( Kesho) hapa The City Of God Ministries, Jiji la Mungu. Kanisa linapatikana Jijini Tanga. Tumaini karibu na stand ya mwembe mawazo.

Muda ni kuanzia saa tatu 9:30 hadi saa Saba 13:30 Mchana.
Wote mnakaribishwa.

Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212

Injili ni nini?Kwa Mujibu wa Maandiko Matakatifu " Injili ni uwezo wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye" Warumi 1:16...
09/05/2026

Injili ni nini?

Kwa Mujibu wa Maandiko Matakatifu " Injili ni uwezo wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye" Warumi 1:16

Kwa wengi hii ni taarifa tu na siyo uhalisia.

Kwa tafsiri yangu " Injili ni pale Mungu anapofunuliwa katika Tabia zako"

Hii ina maana k**a Mungu katika Kristo hafunuliwi katika Tabia zako injili itakuwa taarifa tu kwenye karatasi na wino.

Ulimwenguni na wenye dhambi hawatishwi na unajua kiasi gani, umesona Biblia mara ngapi, unavitabu elfu 10. Hiyo siyo shida.

Kumbuka wakati wewe Unasoma Biblia yako "watu wanakusoma wewe" Maisha yako ni Biblia kwa dunia.

Yesu anasema...... Vivyo hivyo Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, Wapate kuyaona Matendo yenu Mema , wamtukuze Baba yenu aliye Mbinguni. Mathayo 5:16

Kushika Biblia, kwenda kwenye Ibada kila siku ni jambo jema sana. Lakini unazalisha nini Kwa watu wanaokuzuka?

Je watu wanaona msamaha Kupitia wewe pale Unapo kosewa?

Je watu wanaona Upendo wa Mungu Kupitia wewe?

Kamwe hatupaswi kuwa k**a makaburi yenye rangi mzuri lakini Ndani yamejaa mifupa ya wafu.

Lazima Ile injili ambayo tunaihubiri isiwe katika maneno matupu Lazima Iwe katika tendo pia.

K**a utakuwa unebadilishwa Ndani Lazima tuone matokeo ya nje.

Jamii ya waaminio wanajikita kwenye " Miujiza" na si katika "Tabia" Tabia inanguvu Sana kuliko Miujiza.

Watu wanaweza kusahau Miujiza ila Tabia zinaweza kuishi muda mrefu " Miujiza hukoma "Tabia huishi"

Tabia humfunua Mungu Kwa haraka kuliko Miujiza, tabia ndiyo haswa humfunua mtu alivyo.

Tabia zinauwezo mkubwa kugusa maisha ya watu wanaokuzunguka kuliko Miujiza.

Na ndiyo maana leo kumekuwa na watumishi wamekaza Miujiza Lakini si tabia " naamini katika tabia kwanza kisha Miujiza "

Shetani anaweza kufanya Miujiza Lakini hawezi kuwa na Tabia njema, Mungu ana Tabia na Miujiza"

Imani ya kweli, takatifu huzaa matunda Mema " Tabia"

Ndiyo maana watu makini huvutiwa na mtumishi anayedhihilisha Tabia za Kristo ( Tunda la Roho ) na siyo Miujiza.

Ukristo si kuonyesha Vitu, Mali zetu, elimu zetu, bali ni kuonyesha ulimwengu Mungu alivyo Kupitia Tabia na mwenendo halisi katika maisha yetu.

Je, unajivunia ujuzi wako? Unawaona watu wengine ni bure , kujua Maandiko Matakatifu, kusoma na kuwa na utambulisho wa Dkt, Pof.nk. katika maisha yetu k**a wakriso watumishi wa Mungu siyo Sifa ambayo Mungu anataka .....

Paul Mtume alivyowahi kusema Ujuzi huleta majivuno (Majigambo) bali upendo hujenga.

Watu hawajali unajua Sana kuongea kwenye mc watajali unaonyesha tabia gani halisi za Mungu kila siku.

Yesu aliwahi kufundisha......

Mjihadhari na manabii wa uongo wanaokuja kwenu wakijifanya kondoo wasio na madhara ingawa ni watu hatari k**a mbwa mwitu. Mtawatambua watu hawa kwa matendo yao. Mambo mazuri hayatoki kwa watu wabaya, k**a ambavyo zabibu haitokani na miiba, na tini hazitokani na mbigiri. Vile vile, kila mti mzuri huzaa matunda mazuri na mti mbaya huzaa matunda mabaya. Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, na wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa kwenye moto. Mtawatambua manabii hawa wa uongo kwa matendo yao.
Mathayo 7:15-20

Kwa hiyo Yesu alikuwa anataka tujifunze kwa hawa wanyama wawili " Mbwa mwitu" na kondoo"

Wanyama Hawa wanatabia tofauti, kisha akawema Mfano wa mzabibu na miiba tini na mbaruti" kuonyesha nguvu ya Tabia k**a zao halisi linaloshilikishwa kwa Nje.

" Maisha ya Mkristo ambayo hayana onyesho la Tabia za Kristo kwa Nje ni udanganyifu"

Umebarikiwa Sana
Nabii Ernest Kangajaka JR.
The City of God Ministries.
TANGA, TUMAINI Street.
+255 785911212
+255 677304019

Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
The City Of God Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212

"Kabla miujiza hutangulia Tabia"  Mungu hatambulishwi na miujiza hutambulishwa kwanza na  Tabia kisha Miujiza."Mtawatamb...
08/05/2026

"Kabla miujiza hutangulia Tabia" Mungu hatambulishwi na miujiza hutambulishwa kwanza na
Tabia kisha Miujiza.

"Mtawatambua kwa matunda Yao"

Nabii ES.Kangahaka JR.
Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
The City Of God Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212

Shetani haogopi maombi yako ya masaa matano, haogopi kelele zako kwenye jengo la Ibada (Kanisa) kinachoweza kumfanya She...
07/05/2026

Shetani haogopi maombi yako ya masaa matano, haogopi kelele zako kwenye jengo la Ibada (Kanisa) kinachoweza kumfanya Shetani aogope ni " Utii kwa Mungu na Neno lake" K**a unaweza kutii Neno la Mungu na kufanya kwa vitendo shetani ataanza kuondoka kwenye eneo la maisha yako.

"Mtiini Mungu mpingeni shetani naye atawakimbia"

Nawatakia siku njema.

Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
The City Of God Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212

Misaada wetu ukatika Jina la BWANA.....Tamka maneno haya ....Msaada wangu ukatika Jina la BWANA, na Kwa Msaada wa Bwana ...
04/05/2026

Misaada wetu ukatika Jina la BWANA.....

Tamka maneno haya ....Msaada wangu ukatika Jina la BWANA, na Kwa Msaada wa Bwana nitafanya mambo makuu, Bwana ndiye anisaidiaye sitaogopa mwanada Hana chakunitenda.Bwana Yuko upande wangu hakuna anayeweza kinyume changu, katika Jina la Yesu Kristo nimeshinda. AMEN.

Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
The City Of God Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212

Siku hizi mhubiri akihibiri muda mrefu watu Wanasema naboreka Sana, watu watasinzia, sawa. Hivi unamfahamu kuwa dunia un...
02/05/2026

Siku hizi mhubiri akihibiri muda mrefu watu Wanasema naboreka Sana, watu watasinzia, sawa. Hivi unamfahamu kuwa dunia unapoipatia muda na hisia zako itakuonyesha mambo ya kiroho ni upuuuuuzii?

Yesu aliwahi kufundisha Neno Kwa muda siku tatu, hakuwaza watu wamekula Wala kunywa na hakuna aliyekufa, hakuna aliyelalamika kwamba anasikia njaa au kiu. Paulo aliwahi kufundisha Neno usiku kucha kijana mmoja Eutiko alisinzia akadondoka na kufa lakini Paulo hakufunga mkesha aliendelea.

Swali Unaona kutumia muda mrefu kusikiliza Neno la Mungu ni ushamba, kuomba muda mrefu ni kupoteza muda! Unataka Vitu vyepesi katika maisha yako.

Sikiliza usipokufa katika nafsi yako mambo ya kiroho yatakuwa upuuuuuzii tu,

Ngoja nikushangaze unaweza kutazama movie usiku kucha na huchoki, unaweza kuchati masaa mengi na huchoki, unaweza tazama Mechi ya Simba na Yanga dakika 120 huchoki, una magropu 8 ya kila aina kila group upo active lakini unamlalamikia mhudumu wa injili anatumia muda mwingi kuhubiri, kuongoza maombi, nk.

Kabla hujamlamu mchungaji wako Anza kujilaumu kwa ajili ya mambo yako ya kijinga. Kanisa limejaza wajinga na wenaojifanya wakiroho.

Nimekukumbusha tu karibu Sana Kanisa la THE CITY OF GOD MINISTRIES kesho Jumapili 3 May 2026 hapa Tanga Mjini. Kanisa linapatikana CHUMBAGENI MTAA WA TUMAINI karibu na stand ya mwembe mawazo. Muda ni kuanzia saa tatu kamili 9:00 Asubuhii hadi saa Saba na nusu 13:30. Tunajifunza kwa kina Maandiko na tunaomba Kwa muda mrefu, shuhuda za Matendo makuu utazisikia.

The City of God Ministries ni mahali maisha ya watu hubadilishwa na Tabia za watu Mungu zinapokea mfanano halisi wa Kristo.

Karibu k**a Unahitaji kujifunza na kubadilishwa maisha yako.

Tupigie kwa mamba zifuatazo+255 785911212
+255 677304019
Umebarikiwa

The City of God Ministries, Mungu Yuko nasi nyakati zote ( Mathayo 28:20)

Nabii Ernest Kangajaka JR.
The City Of God Ministries
Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
Nabii Ernest Kangajaka
0785 911 212
David Justine

30/04/2026

Mungu hana dini " Mungu ni UPENDO"

Kwa maana Jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa Pekee ili kila amwaminye asipotee bali awe na uzima wa milele (Yohana 3:16)

29/04/2026

Shule ya Roho haina chuo, Ina Biblia tu. 2Timotheo 3:16 Maandiko Matakatifu yote yamevuviwa.

Punzika kwa Amani mtumishi wa Mungu Marilyn Hickey  1931-2026.
27/04/2026

Punzika kwa Amani mtumishi wa Mungu Marilyn Hickey 1931-2026.

Shalom, karibu Sana uabudu nasi kesho Jumapili 26 April 2026. Hapa The City Of God Ministries  Tutakuwa na Ibada Special...
25/04/2026

Shalom, karibu Sana uabudu nasi kesho Jumapili 26 April 2026. Hapa The City Of God Ministries Tutakuwa na Ibada Special Healing, Tutakuwa na Apostle David Justine . Lete wagonjwa na wenye vifungo sugu, muda saa tatu na nusu 9:30 hadi saa Saba kamili 13:30 Mchana.

Kwa mawasiliano tafadhali tupigie simu zako 0785 911 212, +255 677304019.

Wote mnakaribishwa.
Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries
Nabii Ernest Kangajaka

Address

Tanga
16

Opening Hours

Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Nabii Ernest & Veronica Kangajaka Ministries:

Share