Jiycaymiy

Jiycaymiy "Maombezi na Ushauri wa Kiroho"

22/03/2026

Wakati mwingine tunaomba na tunaona kimya… lakini ukweli ni kwamba Mungu anasikia kila neno.
Usikate tamaa, muda wako unakuja.
K**a unaamini, andika “Amina”

🇹🇿🇰🇪🇺🇬🇧🇮🇷🇼🇲🇼🇿🇲

20/01/2025
Happy Merry Christmas and Happy New Year
26/12/2024

Happy Merry Christmas and Happy New Year

13/05/2023

*UNAWEZAJE KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU KABLA HUJAFANYA MAAMUZI AU KABLA HUJACHAGUA?*

Paulo anaandika kwa Wakolosai 1:9

Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;

Iko hivi katika maisha haya sisi wanadamu tuna mapenzi yetu tunapotaka kuamua jambo juu yetu au juu ya mambo mbali mbali, pia tuna mapenzi yetu tunapotaka kuchagua mtu gani tuwe naye na nani tusiwe naye. Shida ipo kwenye hili Swali hili

JE! MAAMUZI NA MACHAGUO YETU NI MAPENZI YA MUNGU?

➖Umepata mchumba je! ni mapenzi ya Mungu
➖Biashara
➖Kiongozi
➖Kazi
➖Safari
➖Promotion
➖Schoraships
➖Sponsorships

Kabla hujachagua au kufanya maamuzi una uhakika gani jambo hili ni mapenzi ya Mungu?

NATAKA KUKUPA NJIA 3 ZA KUKUSAIDIA KUNG'AMUA JAMBO K**A LINA MAPENZI YA MUNGU AU LA! ILI USIJE KOSEA UKAJUTA BAADAYE.

1. USHAURI WA NENO LA MUNGU
( Zab 32:8, Yosh 1:8 Zab 119:105)

Kwa kusoma kila siku neno la Mungu utaweza kuyajua mapenzi ya Mungu juu ya jambo lako

*mfano wa 1*
Umepata kesi na mwamini mwenzako , kakukosea umekasirika unajiuliza ufanye maamuzi ya kumshtaki au umuache. Neno la Mungu litakupeleka kwenye 1 kor 6:1
Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kush*taki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?

MAPENZI YA MUNGU HAPA NI USISHTAKI KWA WASIOAMINI SH*TAKI KWA WAAMINI WENZIO WANAOWEZA WASAIDIA KUFIKIA SULUHU.

Mfano wa 2.
➖Uko kwenye kigugumizi juu ya kulipa kodi maana hali ya biashara yako mbaya..na unatafuta mapenzi ya Mungu. Biblia itakuelekeza cha kufanya kupitia Warumi 13:6-7

Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo.

Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima.

MAPENZI YA MUNGU HAPA NI KULIPA KODI SIO KWENDA KUTOA SADAKA WASAHAU KUJA KUKUTOZA KODI.

2. AMANI YA KRISTO KUAMUA NDANI YAKO.
(Kol 3:15)

Amani inayosemwa hapa ni k**a ya refarii wa mpira anayetaka kuchezesha kwa haki bila upendeleo.... Kwa kuona na kwa umakini anaweza ng'amua faulo, mpira kutoka nje ya mstari, goli, matusi na akatumia filimbi, kadi ya njano au nyekundu kufanya maamuzi.

▪️Lazima jambo lako uliamue kutokana na mchezo unavyoenda maana wewe ni refarii wa maisha yako

Mfano
Umepata mchumba kike/kiume unaona kabisa anacheza faulo kwenye uaminifu/simu, kwenye matumizi, kujali, maneno, imani, maombi halafu unatafuta kujua nini mapenzi ya Mungu... Acha kuzubaa una filimbi mdomoni mwako, una kadi ya njano, na UNAYO KADI KUBWA KULIKO KADI NYEKUNDU... Usikubali kulaumiwa kumbuka mashabiki hawatakuacha salama ukiharibu mchezo wa maisha yako, watakuzomea na kukutupia makopo ukiruhusu goli wakati uliona faulo na ukashindwa kufanya maamuzi.

Amani ya Kristo iamue ndani yako... Lakini refarii lazima uwe umepata mafunzo ya Warumi 12:2

Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

3. UTHIBITISHO WA WENGINE
( 2KOR 13:1, Mith 11:14, 1kor 12:8).

▪️Biblia inasema kila neno litathibitika kwa ushahidi wa vinywa vya mashahidi wawili au watatu. 2 Kor 13:1

Hii ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa.

Wanaokuzunguka, wazazi, wenye hekima, marafiki, ndugu, viongozi wa kiroho hata wa kawaida wanaweza kukuambia wanavyoliona jambo unalotaka kufanya maamuzi jinsi lilivyokaa..

Kazi yako itakuwa kuangalia uthibitisho wa jambo, MAANA HAIWEZEKANI WATU WAWILI AU WATU WAONGEE JAMBO MOJA LINALOFANANA NA AMBALO HATA HUJAWASIMULIA NA LINAKUTATIZA. MAANA YAKE MUNGU ANAKUJULISHA MAPENZI YALE JUU YA JAMBO HILO KABLA HUJAFANYA MAAMUZI AU UCHAGUZI.

Ushauri wangu
Usiwe na papara, mihemuko, usiongozwe na hisia na mapenzi yako Tafuta mapenzi ya Mungu juu ya jambo lako kwa kutumia njia 3 nilizokuandikia hapo ILI UYAJUE MAPENZI YA MUNGU JUU YA NDOA YAKO, UCHUMBA WAKO, BIASHARA, KAZI, SHULE, SAFARI, CHEO NK.

Barikiwa sana nakupenda usiache kufuatilia nyimbo hizi youtube

https://youtu.be/6Nz6iFMes_E
https://youtu.be/my2Nl31nmKY
kuomba https://youtu.be/gm-MwdFfhbw

tumia link hizo hapo.

28/03/2023

Bwana Yesu Asifiwe! Tunawakaribisha wanawake wote kwenye Kongamano la Maombi la Wanawake,mkoa wa Mwanza, tarehe 1/4/2023 na 2/4/2023 kwanzia saa 8 mchana hadi saa 12 jioni. Kongamano litafanyika kanisa la KKKT- Usharika wa Imani, Kanisa Kuu-Makongoro, Mwanza Mjini. Wanawake waombaji mnakaribishwa. Mungu awabariki!

Tutubuni wapendwa na kumuludia Masihi Yu njiani kitunyakuaJiycaymiy
06/03/2023

Tutubuni wapendwa
na kumuludia
Masihi Yu njiani kitunyakua

Jiycaymiy

Address

Bima
Tabata

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jiycaymiy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Jiycaymiy:

Share