19/04/2024
ANZA SIKU NA BWANA
KWA NENO NA MAOMBI
_*NENO LA MUNGU LI HAI*_
_*TENA LINA NGUVU*_
_*(WAEBRANIA 4:12).*_
*MATHAYO 28:19&20.*
19.Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20. na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Mpendwa jifunze;
■ *Kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Yesu.*
■ *Kuwafundisha watu neno la Mungu.*
Mpendwa,
1.Je, wewe unachukua
hatua gani ya kuwafikia
wengine?
2.Je, wewe huwa
unawashirikisha
wengine habari njema
za Yesu Kristo?
*TAFAKARI*
Mpendwa, kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Yesu, ni agizo la Yesu Kristo. Ni agizo ambalo kila mtu aliyemwamini Yesu anapaswa kulifanya kwa sehemu yake na katika uwezo wake bila kutoa kisingizio.
👉🏽Mpendwa, kuenenda ni kwenda, lakini 'enendeni' kunaweza kufanywa kwa namna tofauti k**a ifuatavyo;
●Kutoka na kwenda kuwashuhudia watu habari za Yesu Kristo.
●Kuonesha tabia na mwenendo safi unaotoa uhalisia wa maisha ya Yesu Kristo na kufanyika baraka kwa watu wengine.
●Kuenenda ni pamoja na kuwaombea wengine ili wamjue Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao.
●Ni kuwawezesha watumishi wa Mungu kwa maombi, hali na mali ili waweze kuwafikia watu kwa habari njema za Yesu Kristo.
●Kuwafundisha neno la Mungu ili waijue kweli yote ya Mungu.
👉🏽Mpendwa, kuijua kweli ya Mungu ni pamoja na kulishika neno la Mungu, kujua wokovu na kuukulia wokovu, ubatizo, Roho Mtakatifu na namna ya kuishi maisha matakatifu ya kumpendeza Mungu. Lakini katika hayo yote, jambo la kwanza kabisa ni kumwamini *YESU KRISTO na kumpokea kuwa BWANA NA MWOKOZI* wa maisha yako. Yesu atakusamehe dhambi zako zote na kukupa uzima wa milele.
*Omba sala hii;*
👉🏽 _Eee Bwana Yesu, naomba unisamehe dhambi zangu zote, ninatubu kwako. Nimefungua moyo wangu ingia ndani yangu sasa. Nami ninakukiri *YESU kuwa BWANA NA MWOKOZI* wa maisha yangu. *AMINA*._
👆🏽 *IKIWA UMEOMBA SALA HII KWA IMANI, SASA UMEOKOKA.*
*(WARUMI 10:9&10)*
Barikiwa sana mtu wa Mungu. _*Uwe na Ijumaa njema.*_
_*19 Aprili, 2024.*_~:; Elimringi Ernest Mariki ::~