01/09/2026
IBADA YA ZONE (KITAI MAGEREZA) 1/09/2026
Mathayo 7:7
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.”
Kuna nyakati unaomba lakini huoni jibu. Unalia kimya, unasubiri, na wakati mwingine unaanza kujiuliza k**a Mungu bado anakusikia.
Lakini kumbuka… Mungu hajawahi kupuuza maombi ya moyo unaomtegemea.
Huenda jibu halijaja kwa wakati unaoutaka, lakini Mungu anajua wakati sahihi, njia sahihi na kile kilicho bora kwako.
Endelea kuomba. Endelea kuamini. Endelea kumtumaini Mungu.
Maombi yako hayapotei.
-BONIPHACE MICHAEL
KIONGOZI WA EFATHA RUVUMA