Efatha Church - Ruvuma

Efatha Church - Ruvuma Welcome to our social media EFATHA CHURCH RUVUMA
www.tiktok.com/ Efatha Ministry -Ruvuma, its a branch of the Efatha Ministry.

03/06/2026

KINACHO SABABISHA MUNGU AKUINUE NI JINAFASI YAKO NA JUHUDI ZAKO

FAHAMU NJIA ANAZO TUMIA MUNGU KUKUPA BARAKA-Mungu ufata utaratibu anapo taka kukuapa baraka 1WAKORINTHO 3:13-1413: Kazi ...
03/06/2026

FAHAMU NJIA ANAZO TUMIA MUNGU KUKUPA BARAKA
-Mungu ufata utaratibu anapo taka kukuapa baraka

1WAKORINTHO 3:13-14
13: Kazi ya kila mtu itaonekana wazi, kwa maana Siku hiyo itaifunua. Itajaribiwa kwa moto, na moto utaonyesha ubora wa kazi ya kila mmoja.
14: Ikiwa kazi ambayo mtu amejenga juu ya msingi huo itadumu baada ya jaribio, atapokea thawabu.

-Kila mtu kwenye ufalme wa Mungu anakazi za kufanya
-Kila mtu kwenye ufalme wa mungu ni mtenda kazi
-Kila mtu hemani kwa Bwana ana wajibu

UFUNUO5:9
“Nao wakaimba wimbo mpya wakisema: Wewe wastahili kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa maana ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila, na lugha, na jamaa, na taifa.”

-Mbingu ili ingia ghalama kwasababu inakusaidia na wewe
-Mungu akitaka kukubariki hapitishi neno nje na wewe
-Kuna baraka unapata kutokana na nafasi unayotumika
-Juhudi unazo onesha kwenye kazi ya mungu ndo inaamua ikupe nini
-Mungu anapitisha baraka ukiwa kwenye majukumu

FAIDA ZA KUTUMIKA NA MUNGU VIZURI
(1)UTAKULA UTAKUNYWA ,UTAVAA
ISAYA 65:13
“Kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi: Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtaaibika.”
-Biblia haija ruhusu mtumishi wake kuwa na njaa

(2)MUNGU ATAKUHESHIMISHA
ZABURI 111:3
“Kazi yake ina heshima na adhama; na haki yake yakaa milele.”
-Heshima ya kweri inapatika kwenye nafasi yako vizuri utapata heshima

(3)MUNGU ATARUHUSU ULINZI KWENYE MAISHA
ISAYA 54:17
“Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa; na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu, asema BWANA.”
-Ukitumika vizuri mungu atakupa ulinzi

NBMTENDAKAZI WA MUNGU UNATAKIWA UWE MTII.

:BONIPHACE MAKUNDI

03/06/2026

🔴LIVE | IBADA YA UKOMBOZI -03th JUNE 2026

02/06/2026

UKIWA KWENYE MAOMBI USI SAAHU KUMUOMBEA RAFIKI YAKO MAANA ROHO YA MAPEPO YAWEZA KUPITIA KWA RAFIKIAKO ILI KUKUPATA

01/06/2026

USISAHAU ULIPOTOKA
Efatha TV

01/06/2026

LINDA UNACHOAMINI

01/06/2026

MKE, USIMKATISHE TAMAA MUMEO ;MTIE MOYO ASONGE MBELE

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA  31|05|2026MATUKIO KATIKA PICHA
31/05/2026

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA 31|05|2026
MATUKIO KATIKA PICHA

MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
31/05/2026

MEZA YA BWANA
Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.
Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.
Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.
@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe....
31/05/2026

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”
Yohana 1:1-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”
Tunapokubaliana na neno tunakuwa tunapata uzima wa milele, tunaporuhusu Neno ndani yetu tunaruhusu Yesu akae ndani yetu, kwa maana Yesu ndiye uzima wetu. Tukikubali Neno tumemkubali Yesu, na hapo ndipo tunalinda imani yetu, ukiilinda imani yako itakupa kuponyeka, ukiamini kile unachokiamini mtu asikiondoe wala kukiharibu ndipo uponyaji unatokea kwako, Yusufu alilinda imani yake japokuwa alitupwa gereani lakini akaishia kuwa mtu mkuu, Daudi pia alilinda imani yake na akaishia kuwa mfalme. Imani ukiilinda unakuwa salama na kwako kunakuwa kwema.
Zaburi 128:1-4 “Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake, Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema…”
Yule amchaye Bwana atabarikiwa. Kumcha Bwana ni kulinda kile unachokiamini, unapolinda unachokiamini maisha yako yanaonekana yana mpangilio na ndipo Mungu anakufurahia, kwa maana unapolinda hicho unajiponya na mambo au ulimwengu huu na ndipo Mungu anakufurahia na kuruhusu mema yakujilie na kwako kunakuwa kwema.
Zaburi 126:6 “Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”
Tunapolinda imani kuna magumu, machungu kudharauliwa na kusukumwa lakini usiangalie yale yanayoendelea bali angalia kile unachokiamini ili kikupe kile unachokitaka, hakikisha unalinda kile unachokiamini na ndipo kwako kutakuwa kwema na Mungu atakushangaza na kila mtu atakushangaa.
@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Address

Mkuzo
Songea
BOX805

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church - Ruvuma posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church - Ruvuma:

Share