Xavery Christ's Gospel Messenger

Xavery Christ's Gospel Messenger Lengo la ukurasa huu ni kujifunza neno la Mungu na hasa kujua mwanae Yesu Kristo ambaye pasipo yeye hatuwezi kumjua Mungu baba. Yohana : Mlango 17:3

08/10/2025

Kati ya dhambi zote, *zinaa* ni mojawapo ya dhambi hatari sana inayoweza kumtenganisha mwanadamu na nguvu ya asili (Mungu).

Ndiyo maana hata kwetu wa kristo kwenye Biblia haikuagizwa *kupambana* nayo k**a dhambi nyingine, bali tumeambiwa wazi:
*"Ikimbieni zinaa."*
(1 Wakorintho 6:18)

Maana yake ni kwamba, zinaa si jambo la kujidai kuwa unaweza kulimudu au kulishinda kwa akili zako *hapana*. Ni dhambi yenye ushawishi wa kipekee, inayovuta mwili, nafsi na roho kwa pamoja.

*Mungu hakusema “shindana” na zinaa, alisema “ikimbieni.”*
Kwa sababu ukijaribu kujionesha kuwa hodari mbele yake, utakushinda.
Ni k**a moto *hausumbui ukiukimbia, lakini ukikosea ukaukalia, utakuchoma.*

Hekima ya kweli ni kutii neno la Mungu na kujiepusha mapema na mazingira yanayopelekea zinaa.
*Ushindi halisi ni kwenye kujilinda, si kujaribu kuithibitishia dunia kuwa unaweza kushinda majaribu kwa nguvu zako.*

02/10/2025

thamini wito na kusudi uliloitiwa na Mungu

Kwa Efatha Church - Ruvuma – Nipo kwenye mfululizo wa ufanisi! Nimekuwa shabiki bora kwa miezi 10 mfululizo. 🎉
15/08/2025

Kwa Efatha Church - Ruvuma – Nipo kwenye mfululizo wa ufanisi! Nimekuwa shabiki bora kwa miezi 10 mfululizo. 🎉

2 wakoritho 6:17-18” Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakar...
01/06/2025

2 wakoritho 6:17-18” Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike”hapa ndipo tatizo lilipo na ndipo kasema usiguse kichafu
1 wakoritho 2:9 “lakini, k**a ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. maana yake mungu amendaa kitu kwa hao wampendao nilijaribu nilitaka kujua mstari huu ni halisi kwahiyo nilifanya vipomo nilijitenga na nikasema sitagusa kilicho najisi na nilipokuwa chuo cha biblia nilianza kuona watu wanaanza kunililetea fedha wanani kabidhi ikiwa siwafahamu, nikagundua kumbe Mungu ametuandalia kitu.
Katika Mungu hakuna uchache nilizunguka nikiwa na watu katika injili nilitaka kujua atanipokea, nilitaka kujua wapi tutakula maana yeye nimwenyeji wangu, kwahiyo nilijaribu nijue je nikweli na lifanya kazi? na ikawa. Ili tupate hicho alicho sema kuna mambo mawili tunapasa kufanya, yapasa tujitenge nao na tusiguse kilicho kichafu, inawezekana tusitende dhambi lakini ukagusa na kushirikiana nao ukanajisika. kwasababu yeye ni mtakatifu, utakatifu hauendani na uchafu(unajisi). Na nilipoamua kufanya hivyo niliona Mungu akiniletea watu tofauti, kwaajili ya kusababisha kazi yake iende sikupungukiwa Fedha, chakula wala sehemu ya kulala.
K**a Elia alikuwa narishwa na kunguru walikuwa wanapata wapi,? nikasema kwangu mimi jambo hili ndilo nitakalo lizingatia. Nataka jitenge nao, wakati mwingine ni vigumu maana sikio letu linapenda upuuzi macho yetu yanapenda upuuzi na tunapenda kutenda katika vitu vya kipuuzi, lakini kwangu mimi nilijitengana watu wakaona k**a nichanganyikiwa. Nilikuwa naimba kila wakati kwasababu nilikuwa sitaki kusika maneno yoa, nilifanya maamuzi ya kujitenga nao na nilikuwa peke yangu. Na mimi peke yangu ndio niliyefanikiwa na kufanya vizuri na vya tofauti.

☆☆☆☆☆☆☆☆☆*UKIRI WA LEO | JUMATATU DECEMBER 30, 2024*☆☆☆☆☆☆☆☆☆💡 NAIBARIKI JUMATATU YANGU, KWA KWELI IMEBARIKIWA NA BWANA ...
30/12/2024

☆☆☆☆☆☆☆☆☆
*UKIRI WA LEO | JUMATATU DECEMBER 30, 2024*
☆☆☆☆☆☆☆☆☆

💡 NAIBARIKI JUMATATU YANGU, KWA KWELI IMEBARIKIWA NA BWANA 😋

💡 MIMI NI WA MAMBO MAPYA KWA KUWA MIMI NI MPYA

💡 MIMI NI MSHINDI 💪

💡 NAKATAA KUJINENEA MABAYA JUU YANGU

💡NAKATAA KUJILAANI KWA MANENO YA KINYWA CHANGU

💡 SITAJITAMKIA MANENO AMBAYO HAYAPO KWENYE KWENYE NENO LA MUNGU JUU YANGU

💡 MIMI SIO WA MAMBO MADOGO, MIMI NI WA MAMBO MAKUBWA MAKUBWA

💡 MIMI SIO MKIA, MIMI NI KICHWA, MIMI NI WA JUU TU NA WALA SIO WA CHINI, MIMI NI WA KWANZA NA WALA SIO WA MWISHO!

💡 MIMI SIO WA BONDENI, MIMI NI WA KILELENI!

HALLELUJAH 🤍

UKAWE NA JUMATATU YENYE BARAKA!!!

AMEN!!!
———————————————
Karibu Yesu anakupenda.
0621135022

MAMBO 10 KUHUSU MKEO YAZINGATIE.. 1. Mkeo sio mkamilifu, msamehe. 2. Mkeo ndio uti wako wa mgongo, usiuvunje.3. Mkeo ni ...
30/12/2024

MAMBO 10 KUHUSU MKEO YAZINGATIE..

1. Mkeo sio mkamilifu, msamehe.

2. Mkeo ndio uti wako wa mgongo, usiuvunje.

3. Mkeo ni tunu, mthamini.

4. Mkeo ni kito adimu, mtunze.

5. Mkeo ni rafiki yako bora, muweke karibu yako.

6. Mkeo ni furaha yako, mnawirishe.

7. Mkeo anatakiwa kuwa bora kabisa, mchangamkie.

8. Mkeo ni pande la mwili wako, mstawishe.

9. Mkeo sio ibilisi, usimpige teke.

10. Mkeo sio mzuri tu kitandani, mshirikishe katika kila jambo lenye maslahi yako na hata yake.

YAFANYE HAYO IWAPO MKEO / MWENZA WAKO ATAKUWA NA HAYA MAMBO 10.

1.Anamuabudu Mungu ( Kufanya ibada )
2. Anakupenda
3.Anakuheshimu
4.Akuthamini / Anakuhisani
5.Akujali
6.Akuchangamkie / Akupambanie
7.Msikivu
8.Kauli yako kwake ni amri kwa hiyari na upendo
9.Awe na upendo na kuwaheshimu NDUGU zako kwa namna yeyote.
10.Hakutukani matusi madogo wala makubwa ni awe ni mwenye kufurahia uwepo wako ( Hatamani ukasirike kwa namna yeyote ).

Jumapili njema.

*Ufunuo 19:9**Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya mwanakondoo. Akaniambia, maneno haya ni manen...
20/11/2024

*Ufunuo 19:9*
*Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya mwanakondoo. Akaniambia, maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu*
Amen.

Sunday teachingZaburi 20:1-4 “Bwana akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka pata...
27/10/2024

Sunday teaching

Zaburi 20:1-4 “Bwana akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni. Azikumbuke sadaka zako zote, Na kuzitakabali dhabihu zako. Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote.”

Bwana akujibu siku ya dhiki, akakuonekanie katika haja ya moyo wako; kile unachopitia akupelekee msaada kutoka patakatifu pake; wewe unayekandamizwa na jambo lolote iwe ni magonjwa, uzao wako au ndoa yako haieleweki, Bwana akupelekee usaidizi.

Unapomtolea Mungu sadaka zako hakikisha unafanya kwa uaminifu ili unapohitaji msaada kutoka kwake akazikumbuke sadaka zako ili akakutendee sawa sawa na haja ya moyo wako.

HABARI WANAFAMILIA FACEBOOK.Nawashukuru kwa wote mlio sehemu kubwa katika maisha yangu.Leo nimekuja kwenu kwa lengo la k...
21/06/2024

HABARI WANAFAMILIA FACEBOOK.

Nawashukuru kwa wote mlio sehemu kubwa katika maisha yangu.

Leo nimekuja kwenu kwa lengo la kuhitaji ule umoja wenu mlionionesha siku zote na upendo mkuu.
Natarajia kufunga ndoa mwaka tarehe 07/09/2024 .
Nawaombeni ndugu/jamaa/marafiki na kila mmoja wakiwamo niliosomanao shule ya msingi Namanguli, sekondari luchili na magagula, advance Kigonsera High school na wale wa chuo cha usafirishaji Mabibo. Mchango wenu wa hali na mali ni muhimu ili niweze kutimiza jambo hili la baraka mbele za Mungu wetu.
Kwa wale watakaoweza kulipia kadi
Single 50,000/=
Double 80,000/=
Shughuli itafanyika hapa Dar es salaam, hivyo kwa waliopo hapa karibuni lakini kwa walio nje ya hapa ukiweza kuja itanipa furaha zaidi lakini ukishindwa kuja nakuomba mchango wako utanisaidia sana.
Kuna Group la whatsapp linaundwa kwa anayehitaji kuja naomba tuwasiliane kwa namba hizi zimesajiriwa kwa majina yangu
XAVEEY ANTON MHAGAMA
Halotel 0621135022
Voda 0747665022
Tigo. 0657105022


TAFADHALI USITUMIE NAMBA YOYOTE NJE YA HIZI KUEPUKA MATAPELI

nawashukulu na karibuni kwa ahadi na ushauri.
MITHALI 18;22
"Apataye mke apata kitu chema naye ajipatia kibali kwa bwana"

Address

Xmhagama@gmail. Com
Songea

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Xavery Christ's Gospel Messenger posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Xavery Christ's Gospel Messenger:

Share