24/05/2026
IBADA YA JUMAPILI TAREHE 23/5/2026
IBADA YA SHUHUDA NA SHUKRANI
Zaburi 105:1-5
1. Haleluya mshukuruni Bwana ,liiteni jina ,Wajulisheni watu matendo yake .
2. Mwimbieni,mwimbieni kwa zaburi,Zitafakarini ajabu zake zote.
3. Jisifuni kwa jina lake takatifu, Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
MT: WIRTNESS
Naitwa Witness namshukuru Mungu kwa mengi alionitendea, mmewangu alikua hana kazi , tulikua na maisha magumu .
nimekuwa ni mtu ninaye kuja kanisani kila sku, nikiomba Mungu ampe Mmewangu kazi, Siku moja Mmewangu alipigiwa Simu na rafiki yake aje Singida kusimamia duka faida itakayo patikana watagawana, haikua rahisi,kutokana nahayo sikua tayari tena kubeba ujauzito ,kutokana na ugumu huo wa maisha ,lakini Mungu alivyo Wa ajabu nikashika Ujauzito na Mtoto huyo akawa nibaraka kwa maisha yetu
Pia, nashukuru kwa mtoto wang kuongeza mwaka mwingine haikua rahisi ni miujiza na amekua mtoto wa pekee wa kiume katika uzao wangu hakika Mungu anatenda na kufanya yaliyo makuu AMINA.