B.O.J Ministry

B.O.J Ministry B.O.J Ministry ni huduma inayokuletea masomo mbalimbali ya NENO la MUNGU.

28/04/2023

UFALME WA MUNGU - [ADVANCED LEVEL -01]

kuwaza kuingia katika UFALME WA MUNGU basi haya ambayo yameandikwa hapa yanakufaa sana.

📌Shalom!!!, Bwana Yesu Kristo apewe sifa!!! Nakusalimu wewe uliyepata neema ya kuyasikia haya mahali popote pale ulipo, karibu!!!

✍🏽Ni jambo jema kuwa sisi sote tumekuwa na shauku ya kumjua zaidi Bwana Mungu na Ufalme wake na mapenzi yake ndani ya huo Ufalme.

✝️Pamoja na shauku hiyo, si watu wote wanafanikiwa kumjua Mungu na Ufalme wake na mapenzi yake ndani ya UFALME wake , na kuingia ndani ya UFALME WA MUNGU.

📚Tuanze hapa kwa maneno haya ya Bwana Yesu Kristo juu ya UFALME na tutajua hasa nini huwa kinazungumzwa ndani ya UFALME WA MUNGU na hicho ni lengo kuu la fundisho hili. 👇🏽

📖Mathayo 7:21-23

[21] Si kila mtu aniambiaye, Bwana , Bwana , ATAKAYEINGIA katika UFALME WA MBINGUNI ;bali ni yeye AFANYAYE MAPENZI YA BABA YANGU aliye mbinguni.

[22] Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, HATUKUFANYA UNABII kwa jina lako, na kwa jina lako KUTOA PEPO , na kwa jina lako KUFANYA MIUJIZA MINGI ?

[23] Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, NINYI MTENDAO MAOVU .

📚 Nimeanza kwa maneno hayo ambayo Bwana Yesu Kristo anasema kwa namna ya ajabu kidogo , juu ya UFALME WA MUNGU na kwa kweli si maneno ya kuyafurahia kwa anayeambiwa /anayelengwa,,,,,, lakini mambo ambayo nilitaka tuyaone kwenye maandiko hayo ni k**a ifuatavyo;~

[1] UHUSIANO ULIOPO KATI YA UFALME WA MUNGU NA KUYAFANYA MAPENZI YAKE

✍🏽Kulikuwa na haja gani ya hao ndugu kujitetea kwao na kutaka kupata kibali mbele ya Bwana Yesu Kristo kuingia katika UFALME WA MBINGUNI kwa kutumia MAMBO WALIYOYAFANYA K**A UTUMISHI WAO /UTENDAJI WAO ikiwa hakuna Uhusiano wowote wa KUTENDA HUKO NA HABARI ZA UFALME ?!

hivi kuna uhusiano wa namna ya KUTENDA MAPENZI YA MUNGU na kuingia katika UFALME WA MUNGU .

🎓Swali litakuja, je ni yapi hayo mapenzi ya Mungu, ambayo YESU KRISTO alisema hakuna namna ya kuingia katika UFALME WA MBINGUNI /Mungu isipokuwa umeyafanya.

📖Mathayo 7:21
Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni YEYE AFANYAYE MAPENZI YA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI.

👆🏽Baada ya kauli hiyo unaona kundi kubwa la watu watakaokuja kuonesha namna yao ya UTENDAJI wakidhani yalikuwa ni mapenzi ya Mungu, na mambo hayo ni ;-

(a) KUFANYA UNABII KWA JINA LA YESU,

(b) KUTOA PEPO KWA JINA LA YESU,

(c) KUFANYA MIUJIZA MINGI KWA JINA LA YESU.

👆🏽Na Yote hayo YESU KRISTO akatoa kauli kuwa KUFANYA HAYO YOTE SI KUFANYA MAPENZI YA MUNGU nao ni UOVU .

=} Inawezekana ikakushangaza kidogo kuona kauli k**a hiyo ya BWANA YESU, kuwa KUTOA PEPO KWA JINA LAKE, KUFANYA UNABII KWA JINA LAKE, NA KUFANYA MIUJIZA MINGI KWA JINA LAKE, SI MAPENZI YAKE, jambo ambalo machoni pa wapendwa wengi huyaona mambo hayo ndio UTUMISHI / NDIO HASA KUMTUMIKIA MUNGU na ndio MAPENZI YAKE kitu ambacho BWANA WAO YESU KRISTO anasema huo ni UOVU.

👆🏽Yesu Kristo hakatai kuwa HAVIKUFANYIKA (ni kweli walitoa pepo tena kwa jina lake, walifanya unabii na kufanya miujiza mingi k**a kuponya wagonjwa, viwete kuona, n.k)..... Kwa hiyo ni KWELI VYOTE HIVYO VILIFANYIKA tena kwa jina la Yesu Kristo na hao walioyafanya hayo WANAMWITA YESU KRISTO kuwa ni BWANA, BWANA WAO.

📖"SI KILA MTU ANIAMBIAYE BWANA, BWANA...... "
kwa maneno mengine ni watu ambao walimwamini KRISTO k**a BWANA wao. Lakini walifanya uovu katika kuyafanya hayo.

✍🏽NGOJA NILIWEKE HILI WAZI.

MAPENZI YA MUNGU HASA ambayo ndio lengo /target (shabaha) ya Mungu, katika UFALME WAKE NI WATU KUBATIZWA yaani KUINGIA UHUSIANO NA MUNGU na huko ndiko KUZALIWA MARA YA PILI NA KUWA WANA WA MUNGU .

✍🏽Labda utakuwa hujanielewa vizuri,,, niseme hivi MAPENZI YA MUNGU ni wewe KUZALIWA MARA YA PILI na KUWA MWANA WA MUNGU NDANI YA UHUSIANO NA YEYE kwa njia ya KRISTO YESU pekee !!!

👆🏽Na hicho ndicho kinachokupa kuingia NDANI YA UFALME WA MUNGU /MBINGUNI.

✝️Hebu tusome wote maandiko haya

📖Mathayo 28:19-20
[19] Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote KUWA wanafunzi, MKIWABATIZA kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu ;

[20] na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.

✝️👆🏽Mistari hiyo inatupa kuona kuna kufanywa kuwa MWANAFUNZI wa Yesu Kristo lakini hiyo inatosha?! Jibu ni Hapana kuna zaidi unapaswa kufika na mahali hapo ni kwenda KUBATIZWA!!!

✝️👆🏽 KUBATIZWA huko ni kupi? Jibu ni rahisi ni juu ya kuingia kwenye UHUSIANO NA MUNGU kwa njia ya KRISTO YESU.....UHUSIANO au MUUNGANIKO huo huitwa NDOA YA AGANO JIPYA kati ya KRISTO NA WANADAMU.

✝️👆Aina hiyo ya UHUSIANO ndio inayokufanya kuzaliwa katika familia ya MUNGU na Familia hiyo iko kwa namna ya Utawala wa KIFALME ndio huo uitwao UFALME WA MUNGU.

✝️📚Kwa hiyo kwa lugha rahisi kabisa k**a ambavyo ilivyo kwa ndoa ya mfano ya MME na Mme kuwa mwili mmoja ndivyo ilivyo MUUNGANIKO wa mtu na KRISTO YESU na kuwa Roho mmoja na huo ndio UBATIZO unaozungumzwa na biblia ambao pasipo huo huwezi kuzaliwa mara ya pili na kuingia katika UFALME WA MUNGU.

✝️👆🏽Katika maandiko utakutana na maneno k**a haya kueleza UBATIZO huo 👇🏽

📖Warumi 6:3-5
[3] Hamfahamu ya kuwa sisi sote TULIOBATIZWA katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

[4] Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya UBATIZO katika mauti yake, kusudi k**a Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

[5] Kwa maana k**a MLIVYOUNGANIKA naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake;

🎓✍🏽 Hakuna UFUFUO kwa UZIMA WA MILELE isipokuwa umebatizwa,

➡️Hakuna UZIMA WA MILELE isipokuwa UMEBATIZWA,

➡️HAKUNA kuingia katika UFALME WA MUNGU isipokuwa UMEBATIZWA.

[2] Jambo la pili ambalo nilitamani tuone kwa pamoja ni hili :-

➡️ KUNA UWEKANO WA MTU KUMWAMINI YESU KRISTO NA ISIFIKE /ASIKUBALI KUFIKA MAHALI PA YEYE KUBATIZWA NDANI YA KRISTO YESU .


✍🏽K**a nilivyokwisha kueleza maana halisi ya KUBATIZWA k**a inavyozungumzwa ndani ya Biblia, kuwa ni mtu KUKUBALI kuingia katika UHUSIANO na KRISTO YESU kiasi cha yeye na maisha yake yote kumezwa ndani ya KRISTO YESU na UHUSIANO HUO WA KIMAISHA , uletao tokeo la maisha mapya ya KRISTO YESU kwa mtu huyo.

📚 Lakini unaweza ukawa na swali kuwa inawezekanaje mtu akafika mahali pa KUMWAMINI YESU KRISTO na ASIKUBALI / ASIFANIKIWE KUBATIZWA ? ....ok Swali zuri!!

📖 Jambo moja la ajabu ni kuwa mtu yeyote anayefika mahali pa KUBATIZWA kwanza alianza na KUMWAMINI YESU KRISTO k**a BWANA na hitimisho la imani yake ikawa ni maamuzi yake ya KUUNGANA NA KRISTO katika UHUSIANO (USHIRIKA) wa MAISHA kwa yeye kuyaacha maisha yake na aanze kuishi ndani ya maisha ya KRISTO YESU, nikiwa na maana hii AISHI kwa MWELEKEO WA MAISHA YA BWANA wake au k**a ATAKAVYO BWANA YESU KRISTO.

👆🏽➡️ Nimesema kuwa kuna uwezekano wa mtu kumwamini YESU KRISTO lakini aisisalimishe maisha yake kwa Kristo Yesu ndani ya UHUSIANO wa KIAMAISHA na YESU KRISTO UHUSIANO utakaomfanya azaliwe katika uzao mpya wa familia ya UFALME WA MUNGU yaani kuzaliwa mara ya pili ,,,

👆🏽✍🏽Ndio maana agizo la BWANA Yesu Kristo katika [ Mathayo Mt 28 :18-20) kwa wanafunzi wake lilikuwa si tu kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi pakee yake, bali na KUWABATIZA k**a wangefundisha mataifa na wakawa wanafunzi wa YESU KRISTO halafu wasifanye ushirika na KRISTO YESU hapo tutasema mapenzi ya Mungu HAYAFANYIKA (rudia tena kusoma hapa).

✝️👆🏽Maelezo hayo, tunayaona hapa kwa maneno mengine katika kitabu cha MARKO 16, BADO MSISITIZO UKIWA NI WATU KUBATIZWA!!! maana ndio hasa mapenzi ya Mungu.

📖Marko 16:15-16
[15] Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

[16] AAMINIYE na KUBATIZWA ATAOKOKA ; asiyeamini, atahukumiwa.

⬆️Angalia vizuri huo mstari wa 16 Injili ya Marko 16, kuna vitu viwili vikubwa hapo, KUAMINI na KUBATIZWA.......

✍🏽Kwa hiyo, katika hatua za mtu kwenda KUOKOKA haubatizwi ndipo UAMINI , isipokuwa UNAAMINI ndipo UNABATIZWA na hicho kitendo cha KUBATIZWA ndio huzaa WOKOVU unaokupa KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU.

🎓Narudia tena TUNAAMINI KWANZA ndipo TUNAPOENDA KUUNGANA na KRISTO YESU, kwa MUUNGANIKO wa ki-ndoa yaani kuishi maisha MAMOJA yaani maisha yake KRISTO YESU BWANA, KUSUDI MOJA , FAMILIA MOJA YA KIFALME, na WARITHI WA BARAKA ZILE ZA MUNGU KATIKA HUO UHUSIANO - k**a matokeo ya UBATIZO HUO.

📖 "WOKOVU hauji tu kwa KUMWAMINI pekee lakini huja kwa KUBATIZWA baada ya KUMWAMINI"..... Hii ndio inaleta maana ya maneno haya...

" AAMINIYE na KUBATIZWA ATAOKOKA ".......... katikati ya maneno AAMINIYE na KUBATIZWA kuna kiunganishi neno "na" lenye maana sana katika sentensi hiyo kukamilisha au kuleta umaana wa tokeo la mwisho ambalo ni MTU KUOKOKA na tokeo hilo halifikiwi isipokuwa MTU huyo aliyeamini AMEBATIZWA!!! Amen 🙌🏾

➡️ Ndio maana nikasema kuna uwezekano wa mtu kumwamini YESU, na asifanye maamuzi ya kuingia kwenye uhusiano na KRISTO YESU na hili lilitokea kwa unabii katika kitabu cha Injili ya YOHANA MT 8 hebu tusome kwa pamoja habari hii ambayo ni unabii wa mambo yqnayotimia katika nyakati hizi tulizonazo....

📖Yohana 8:31
Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi WALIOMWAMINI , Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;

⬆️ Ohh !!! , mstari huo unaonesha wazi Bwana Yesu akianza kuzungumza na wayahudi, na tunaona hawa watu tayari mioyoni mwao walikuwa tayari WANA-IMANI na YESU KRISTO lakini IMANI yao haikuwapa KUOKOKA na kuzaliwa mara ya pili ili wawe WANA WA MUNGU yaani kuwa ndani ya FAMILIA YA MUNGU kwa njia ya UBATIZO nazungumza UBATIZO k**a MFUMO WA MAISHA sizungumzii ubatizo wa kuzamishwa ndani ya maji mengi tukio la siku moja,.....

⬆️Ukiendelea kusoma habari hiyo, utaona maneno haya

📖Yohana 8:32-33
32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka HURU .

[33] Wakamjibu, SISI TU UZAO WAKE IBRAHIMU , wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?

⬆ Kumbuka Uzao wa IBRAHIMU unatambulika kwa njia ya IMANI (IBRAHIMU anazaa kwa njia ya IMANI) sawa na ⬇️

📖Wagalatia 3:7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa IMANI , hao ndio wana wa IBRAHIMU .


✍🏽Ok sasa turudi hapo juu unaona wayahudi wakijitetea kuwa wao HAWAJAWAHI KUWA UTUMWANI wakati wowote kwa sababu wao ni uzao wa IMANI- IBRAHIMU..... (wamezaliwa katika imani).... lakini YESU KRISTO akawaeleza hiyo hiyo kuwa mtu wa IMANI haitoshi mpaka utakapozaliwa kuwa uzao wa MUNGU na kuwekwa huru mbali na ASILI YA UTUMWA WA DHAMBI kwa njia ya UBATIZO (Ingawa hapo katika Injili ya YOHANA MT 8 hajatumia neno UBATIZO ametumia neno - KUZALIWA KATIKA UZAO MPYA WA MUNGU).

⬇️Chukua mistari hii na uitafakari

📖Yohana 8:34, 36, 41-42, 47, 51
[34] Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.

[36] Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.

41 Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu.

[42] Yesu akawaambia, K**a Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma.

[47] Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi HAMSIKII KWA SABABU NINYI SI WA MUNGU .

[51] Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele .

[3] Jambo la tatu ni hili :-

" Mambo yafanyikayo kwa IMANI hayamfanyi kuwa AMEOKOKA ".

📖 Marko 16:17-18
[17] Na ishara hizi zitafuatana na hao WAAMINIO ; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya ;

[18] watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya .

⬆️ Jambo la ajabu kidogo ambalo si kila mtu anaweza kuliona hapo kwenye mistari hiyo ni kuwa BWANA YESU KRISTO alitoa ruhusa ya mambo kadha wa kadha KUFANYIKA tena KWA JINA LAKE kigezo kikiwa ni IMANI tu katika KWA JINA LAKE juu ya utendaji wa hayo KWA UWEZO /MAMLAKA YA mwenye JINA HILO na si kwa WALIOBATIZWA akasema ISHARA HIZI zitafuatana nao WAAMINIO .

⬇️⬆️ Usifurahie KUTOA PEPO kwa Jina lake , KUFANYA UNABII kwa jina lake, Kuweka mikono juu ya wagonjwa wakapata afya, ukaishia hapo YESU KRISTO anaziita hizo ni ISHARA. Rudia tena kusema ISHARA,,,, ok kwa kifupi kabisa ISHARA huwa ni lugha ya mafumbo, inayozungumza kitu HALISI KWA MFANO .

✝️ Kwa hiyo ISHARA si mambo halisi ila ni kivuli cha MAMBO HALISI.
Unaweza kuweka mkono juu ya mgonjwa akapata AFYA na si UZIMA kuna tofauti kati AFYA NA UZIMA, si kila mwenye AFYA ana UZIMA, kwa hiyo AFYA ni ISHARA inayozungumza juu ya UZIMA WA MILELE ule wenye asili ya MBINGUNI.

⬆️ ISHARA zote zinazosemwa kuwa zitafanywa na wale WAAMINIO kwa lugha rahisi zinazungumza juu ya tendo moja UBATIZO / KUOKOKA/ KUZALIWA KATIKA MAISHA MAPYA NDANI YA FAMILIA YA KIFALME YA MUNGU.

✝️✍🏽Tena kuna uwezekano wa kuyafanya hizo ISHARA hata k**a HUJABATIZWA maadamu tu wewe ni miongoni mwa waitwao " WAAMINIO " ndio maana unaona hao YESU KRISTO anakuja kuwakataa kwenye MATH 7 kwa kuwaambia ⬇️

📖 Mathayo 7:22-23
[22] Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, HATUKUFANYA UNABII kwa jina lako, na kwa jina lako KUTOA PEPO , na kwa jina lako KUFANYA MIUJIZA MINGI?

[23] Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi MTENDAO MAOVU .

⬆️Kuishia tu kufanya ISHARA KWA JINA LAKE kwa sababu ya IMANI na USIINGIE ndani ya UHUSIANO na BWANA YESU KRISTO (KUBATIZWA) huko ndiko KUFANYA MAOVU.

🎓📚 Wanafunzi wa YESU KRISTO nao kidogo waingie kwenye mtego huo ambao wengi wa watumishi hufurahia sana kuona " ISHARA " hizo zikifanyika na wasikumbuke kuwa MAPENZI YA MUNGU ni watu KUBATIZWA na sio kufanywa kwa ISHARA.

📖Luka 10:17-20
[17] Ndipo wale sabini WALIPORUDI KWA FURAHA , wakisema, Bwana, hata pepo WANATUTII KWA JINA LAKO.

[18] Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni k**a umeme.

[19] Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

[20] Lakini, MSIFURAHI KWA VILE PEPO WANAVYOWATII ; bali furahini kwa sababu MAJINA YENU YAMEANDIKWA MBINGUNI .

⬆️ Unaweza kufikiria kuwa FURAHA ya wale watumishi wa YESU KRISTO walipoleta mrejesho wa UTUMISHI WAO juu ya KUTOA PEPO KWA JINSI LAKE hiyo Furaha yao HAIKUWA FURAHA ya YESU KRISTO,...kwa sababu msingi wa FURAHA yao ilikuwa ni PEPO KUWATII waliamuru kwa jina la BWANA YESU KRISTO, huku FURAHA YA KRISTO YESU ikawa juu ya kitu kingine " MAJINA YAO KUANDIKWA MBINGUNI "

⬆️ Furaha ya UTUMISHI wako ni ipi? Furaha ya IMANI yao ni ipi? Je lengo la UTUMISHI wako ndio lengo la MUNGU? Kusudi na mikakati ya UTUMISHI wako kwa Mungu ni sawasawa na BWANA wa huo UTUMISHI?! maana inawezekana kabisa akawa ni Bwana, Bwana katika UTUMISHI wako na akaishia kusema " SI KILA MTU ANIAMBIAYE BWANA, BWANA ATAKAYEINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI....... " kwa Imani yako akawa ni BWANA lakini ukagoma KUBATIZWA.

🎓✍🏽Mwisho nihitimishe kwa kusema kuwa yote ulivyojifunua mahali hapa, yalikuwa na lengo la kukuleta mahali pa KUBATIZWA uingie katika NDOA ya Wewe na KRISTO YESU ndoa ya MAISHA YAKO YOTE yasiwe tena yako uishi katika MAISHA YAKE, na UBATIZO HUO ndio UNYAKUO unaozungumzwa ndani ya Biblia yaani KUHAMISHWA TOKA MAUTINI na kuingia UZIMANI......

⬆️Huko ndiko hasa KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU, na jina lako KUANDIKWA katika FAMILIA YA MUNGU maana kila FAMILIA inajulikana kwa majina ya wanafamilia nayo yanawekwa kwenye kumbukumbu.

✝️ Karibu katika familia ya Mungu duniani na uanze kuishi maisha mapya ndani ya mahusiano ya Wewe na KRISTO YESU hapo hapa DUNIANI na KUPOKEA UZIMA WA MILELE......ingekuwa ni mkutano wa nje ningesema 🗣️🔊 "WANAOTAKA KUBATIZWA katika MAISHA haya ningesema wasongee hapa mbele"

❤️Ikiwa uko tayari kwa MAAMUZI HAYA tafadhali wasiliana nasi kwa namba hii
📞 # 0752023082 au 0627975451

✝️Karibu katika karamu ya Mwana-kondoo, vinono vimekwisha kuchinjwa!!!

🙏🏽Namshukuru Mungu aliyetupa kunena habari hizi kwa neema ya ajabu, lakini pia kwa namna ya pekee nikushukuru kwa wewe uliyepata nafasi ya kusoma siri hizi za mbinguni ambazo si kila wakati utakutana nazo. Ni maombi yangu Mungu akupe kuyapokea k**a yalivyokusudiwa!!!

🎓Shalom!!!
Imeandaliwa na sisi FAMILIA YA KIFALME ILE YA MUNGU DUNIANI - B.O.J MINISTRY na kuandikwa na mimi ndugu yenu katika Kristo Yesu
# Benjamin Jacob Hema

All Credits : Norbert Nicolaus Rulanyaga [ Our beloved teacher] .

HEAVEN ON EARTH

26/11/2022

Shalom familia ya Mungu duniani. 🙌🏽

Leo chukua hii.

🌍Ulimwengu ni mnufaika wa mauti ya kristo pekee"

📖 Yohana 3:16-17
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye."

na wala ulimwengu si mnufaika wa utawala/ufalme wa Mungu na kristo wake duniani !!!!

📖Waefeso 1:20-23
20 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;

juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;

akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo
ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

🔊✍🏼 Namaanisha kuwa KANISA AMBALO NDIO WATU WA MUNGU NDIO JAMII ILIYO ULIMWENGUNI AMBAYO NDIYO MNUFAIKA WA MAUTI YA YESU KRISTO(maana kwa mauti yake kanisa likanunuliwa na kutakaswa)NA PIA NI KANISA PEKEE NDIO MNUFAIKA WA UTAWALA NA UFALME WA MUNGU DUNIANI(maana ni kwa kutawala kwake kristo; KANISA pia linapata kutawala pamoja nae).

# Mungu aliupenda Ulimwengu mzima na kwa kumtoa mwanawe wa pekee ni ili huo Ulimwengu mzima uokolewe, lakini ili hilo litimie halitegemeani tena na Upendo wa Mungu bado akadai " *KILA AMWAMINIYE HUYO MWANA ALIYETUMWA*" ndiye atakayeokolewa.

Cheers 🥂

Credit : Norbert
Copyright : . © B.O.J MINISTRY 2022.

22/11/2022

📖Nafasi ya Mungu ktk uhusiano na mtu, hua Mungu yuko kumkamilisha MTU kwa njia ya kuhusiana naye,huku nafasi ya MTU kwenye uhusiano na Mungu,mwanadamu yuko kumthibitisha Mungu kuwa ni Mungu kwa njia ya uhusiano na si kumkamilisha Mungu maana MUNGU NI MKAMILIFU HATA PASIPO KUA NA UHUSIANO NA MWANADAMU.

📚Kwa hiyo nafasi yako katika uhusiano na Mungu ni katika kumruhusu Mungu ajithibitishe kupitia uweza wake kuwa ni Mungu na jukumu la Mungu kuhusiana na mwanadamu ni katika kumkamilisha mwanadamu kwa uweza wake kwenye uhitaji alionao ili mwanadamu awe mkamilifu na asiye na uhitaji wowote ila utoshelevu.

Shalom!!!!

05/10/2022

UZIMA WA MILELE
[EPISODE 03]

UZIMA WA MILELE =KUFUFULIWA KWA MWILI
Shalom!!!! 🙌🏽 nakusalimu mahali popote pale ulipo kwa jina la Bwana Yesu Kristo.

✍🏼Leo nikupe hii, tutaunganisha mistari hii miwili halafu utatafakari pamoja nami, hasa juu ya suala hili la UZIMA WA MILELE......

✍🏼Nami nataka uone jambo hili 👇🏾
=} UZIMA WA MILELE NA JAMBO LA AHADI AMBALO YESU KRISTO AMEAHIDI KUWAPA WOTE WATAKAOUNGANA NAE katika kipindi cha kutawala kwake hapa DUNIANI .

🙌🏽KWA HIYO HUU UZIMA WA MILELE utapokelewa /wataupokea watu wakiwa hapa DUNIANI maana huyu YESU KRISTO ujio wake ni kuujia ulimwengu ili amiliki na kutawala dunia sawa na UFUNUO WA YOHANA 11:15

📖Ufunuo wa Yohana 11:15
Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, UFALME WA DUNIA UMEKWISHA KUWA UFALME WA BWANA WETU na WA KRISTO wake , naye atamiliki hata milele na milele.

✍🏼 Nami habari nzuri ni hii UFUNUO WA YOHANA 11:15 hapo juu imefafanuliwa vizuri hapa kwenye mistari miwili ambayo leo nimetaka twende nayo pamoja.... Na tuanze na huu hapa 👇🏾(kumbuka ni HABARI ZA UZIMA WA MILELE katika ULIMWENGU MPYA kipindi ambacho KRISTO amekuja duniani- rejea UFUNUO WA YOHANA 11:15)

📖Mathayo 19:27-29

[27] Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?

[28] Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ULIMWENGU MPYA , ATAKAPOKETI MWANA WA ADAMU KATIKA KITI CHA UTUKUFU WAKE , ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

[29] Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa k**e, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, NA KUURITHI UZIMA WA MILELE .

✍🏼 Saa ya kuketi kwake Kristo Yesu ni saa ya watu kuwa UZIMA WA MILELE na kitabu cha UFUFUO 11:15 kinaonesha eneo la huo utawala wake kuwa ni duniani, lakini MATH 28:18 inafafanua zaidi kuwa ni MBINGUNI NA DUNIANI ndio mipaka ya Utawala wake, ila UFUNUO 11:15 na Daniel 7:13-14 na MATHAYO 25:33 inaonesha huyu Kristo kwa jinsi ya mwili atakuja au ataujia ULIMWENGU / DUNIA, japo eneo la mipaka ya UFALME ni MBINGUNI NA DUNIANI.

✍🏼UFALME WA MUNGU unapokuja duniani unaifanya ile DUNIA ya kwanza kufika ukomo wake na kuruhusu vitu vya mbinguni kufanyika hapa hapa DUNIANI maana mapenzi yake yanatimizwa hapa k**a ilivyo ulimwengu wa roho (mbinguni) = Mathayo 6:9-10

✍🏼KUNA WATU WANAAMINI KUPOKEA UZIMA WA MILELE *hakuondoi kule kufa kwa jinsi ya mwili.* wakiwa na maana kuwa, unaweza KUPOKEA UZIMA WA MILELE baada ya Kuokoka lakini kufa kimwili kupo tu japo una Uzima wa milele ndani ya roho yako.

📌Juu ya jambo hilo ni niseme huo nao ni uongo mwingine uliohubiriwa, iko hivi, HAKUNA USHIRIKA wowote wa MAUTI ya aina yoyote (ya kimwili au kiroho) baada ya mtu KUPOKEA UZIMA WA MILELE.

✍🏼 Ngoja niseme sasa, *HUO UZIMA WA MILELE ndio UFUFUO WA MIILI* hii iliyo katika hali ya kufa na udhaifu k**a ulikuwa hujui.

📌Kwa hiyo k**a unakiri na kuamini kuwa umepokea uzima wa milele na hauna hakika k**a utaishi milele hapa DUNIA basi HUO UZIMA WA MILELE ni batili /sio halisi. Maana *UZIMA WA MILELE ni kuvaa asili ndani ya mwili huu wenye udhaifu ili usiweze kufa tena* .

Utasema nmeitoa wapi?

🔊Soma hapa kwa sauti haya 1,2, 3 Soma 👇🏾

📖Warumi 8:11, 19-21, 23
11 Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu *ATAIHUISHA NA MIILI YENU ILIYO KATIKA HALI YA KUFA , kwa Roho wake anayekaa ndani yenu* .

[19] Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.

[20] Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini;

[21] kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.

[23] Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, *tukikutazamia KUFANYWA WANA , yaani, UKOMBOZI WA MWILI WETU* .

✍🏼 Huko kufanywa kuwa Mwana Wa Mungu ndio *KUHUISHWA MIILI ILIYO KATIKA HALI YA KUFA na KUPOKEA HALI YA UZIMA WA MILELE KWENYE MWILI* .

📌Na bila kusita niseme huo ndio *UFUFUO WA WAFU*. Je ni ajabu sana hivyo?

✍🏼UFUFUO HUO WA WAFU NI BAADA YA TUKIO LA YESU KRISTO KUKAMILISHA mpango wa YEYE kulipa den ya dhambi na makosa ya watu ambayo katika hayo watu waliingia katika *HUKUMU YA KUFA - YAANI KILA MWENYE MWILI KUFA*, Maana KUFA ni matokeo ya dhambi na makosa yao. SASA Yesu Kristo kulipa gharama hiyo, inawapa nafasi mpya watu *KUTOKUHUKUMIWA KUFA MILELE* wakiwa NDANI YAKE.

📖Warumi 8:1-2
[1] Sasa, basi, *hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu* .

[2] Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu *imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti* .

🔊 Huko ndiko kufanywa *MWANA WA MUNGU* , na huo ndio *UFUFUO WA WAFU*...........jambo hili tunaliona kinabii (nasema kinabii kwa sababu lilitangulia kuandikwa kabla halijatimia kwetu kwa jinsi ya mwili),,,, unabii huu wa *KUFUFULIWA KWA WAFU* liko hapa 👇🏾

📖Mathayo 27:50-54
[50] Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, *akaitoa roho yake* .

[51] Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

[52] *makaburi yakafunuka; IKAINUKA MIILI MINGI YA watakatifu waliolala* ;

[53] nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.

[54] Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo yaliyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa *MWANA WA MUNGU .*

✍🏼Angalia huo mstari wa MATH 27 : 52 kinachofufuliwa hapo ni nini? Anasema *"....... IKAINUKA MIILI YA WATAKATIFU WALIOLALA"* .......

🌹Nilitaka japo uone kwa uchache kuwa hakuna Uhusiano wowote wa mtu KUPOKEA UZIMA WA MILELE NA kufa kimwili mwilini,.....

📚Labda hiyo haitoshi, OK tuone tena mahali pengine wanapozungumza juu ya UFUFUO,,, huenda bado una maswali mengi na kiuhalisia, ufahamu wowote ambao watu wanao juu ya mambo haya ni baada ya watu kufundishwa maandiko ya biblia, na kuishia kudanganywa, MIMI kazi yangu ni kutumia maandiko hayo hayo uone kweli iliyojificha ndani ya maandiko hayo.

✍🏼 Ikiwa bado uko na swali juu ya *UFUFUO WA WAFU* kuwa ni kubadilishwa asili ndani yetu inayobadili *MWILI HUU WA KUFA UVAE KUTOKUFA*,,, soma nami hapa,,, tena soma taratibu hata nisipoeleza kwa undani utaelewa hasa kwa picha tuliyotoka nayo juu.

*UFUFUO WA WAFU = UZIMA WA MILELE KATIKA MWILI*

📖1 Wakorintho 15:35, 37, 40, 43-44, 49-55

[35] Lakini labda mtu atasema, *WAFUFULIWAJE WAFU ? Nao huja kwa MWILI GANI* ?

[37] nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;

[40] Tena kuna *MIILI ya mbinguni, na MIILI ya duniani* ; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali.

[43] hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu;

[44] hupandwa *MWILI WA ASILI ; HUFUFULIWA MWILI WA ROHO* . Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko.

[49] Na k**a tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni.

[50] Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.

[51] *Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote TUTABADILIKA ,*

[52] kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na *wafu WATAFUFULIWA , WASIWE na UHARIBIFU , nasi tutabadilika* .

[53] Maana sharti *HUU UHARIBIKAO UVAE KUTOKUHARIBIKA , nao HUU WA KUFA UVAE KUTOKUFA* .

[54] Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda.

[55] Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?

📌Rudia tena kusoma mistari hiyo. Hasa huo mstari wa 53 mpaka ule wa 54. Angalia anazungumza juu ya *MABADILIKO YA MWILI* ........sema *MWILI*!!!!!

✍🏼Mistari ya 52-54 inaeleza kuwa Parapanda italia na kwa sababu ya Parapanda hiyo WAFU WATAFUFULIWA, sasa hiyo Parapanda ni *INJILI / FUNDISHO / NENO LA KRISTO* siku akija duniani, Kwa fundisho Lake litawapa watu kuwa *HAI*

📖Yohana 5:24-25
[24] Amin, amin, nawaambia, *Yeye ALISIKIAYE NENO LANGU* na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna *UZIMA WA MILELE* ; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka *MAUTINI KUINGIA UZIMANI .*

[25] Amin, amin, nawaambia, *Saa inakuja, na sasa ipo, WAFU WATAKAPOISIKIA SAUTI YA MWANA WA MUNGU , na wale waisikiao WATAKUWA HAI.*

🙌🏽BILA SHAKA maandiko hayo yanajieleza wazi kabisa an, sasa acha nikwambie huyo mwenye KUFUFUA amekuja, hayo tuliyoyasoma kwenye maandiko yalikuwa ni unabii tu utakaotimia siku akija huyo mwenye *PARAPANDA YA MWISHO - YENYE KUFUFUA Yaani YESU KRISTO*.

✍🏼Na sasa *YUPO* duniani saa hii. Utamfahamu kwa aina ya fundisho lake . Hana INJILI nyingine ila kuwafanya *WATU walio katika hali ya kufa na WANA MATARAJIO YA KUFA yeye YESU KRISTO ANAWAFANYA WAWE HAI HAPA DUNIANI MILELE*.

🙌🏽Kwa leo nihitimishe kwa kutoa shukrani zangu kwa yeye aliyenipa ufahamu huu, mwalimu wangu *NOBERT* na kuhakikisha kuwa haya yanakufikia na wewe pia uyasomaye haya. Naamini umebarikiwa.

🙌🏽Mungu aendelee kukutunza na ninakushukuru kwa kuendelea kufuatilia mafundisho haya.

📚Karibu kwa maswali, maoni au jambo lolote la kutushirikisha.

✍🏼Imeandaliwa na sisi *B.O.J MINISTRY*.... na kuandikwa na mimi ndugu yenu katika Kristo,
Benjamin Jacob Hema.

🙌🏽 *hey Church Shalom see you!!! Cheers* 🥂!!!!

28/09/2022

UZIMA WA MILELE [ EPISODE 02 ]

MWANA WA MUNGU HAFI /MAUTI HAINA NGUVU JUU YAKE-

[ HUDUMU MILELE BILA KUONJA MAUTI ].

SHALOM familia ya Mungu, nawasalimu kwa jina lake Mwokozi Yesu Kristo mahali popote mlipo.

Leo nimeona ni vema nikupe kutafakari pamoja nami kile ambacho kipo moyoni mwangu kwa kupewa na Bwana nayo niliyopokea yanawafaa sana. Na moja kati ya hayo ni juu ya jambo la UZIMA WA MILELE ndani yako,.

✍🏼 Kule kusema kwangu UZIMA WA MILELE ni kule kuifuta MAUTI iliyo kinyume cha UZIMA na sio UZIMA tu bali huu uitwao UZIMA WA MILELE.

📌 K**a ulikuwa umesahau acha nikukumbushe kuwa YESU KRISTO kuja kwake ni ili upokee UZIMA WA MILELE ndani yako.
ndio maana halisi ya kauli hii kwenye kitabu cha 👇🏾

📖Yohana 10:10 (KSW) Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; *MIMI NALIKUJA ILI WAWE NA UZIMA , KISHA WAWE NAO (uzima) TELE* .

✝️ Nguvu ya maisha yake Yesu yaani Msalaba, ilikuwa ni kufuta dhambi juu ya watu na kuwapatanisha na Mungu kwa dhabihu ya maisha yake na kwa yeye kufanya hivyo ilikuwa ni kufuta DHAMBI NA MAKOSA YA WATU, kusudi hasa lililomfanya yeye kuja na likabeba maana ya jina 'YESU'

📖Mathayo 1:21
*Naye atazaa mwana, nawe utamwita JINA LAKE YESU , maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na DHAMBI ZAO* .

🌹Jambo hili lilikuja kwa sababu matokeo ya DHAMBI na MAKOSA ya watu kuleta MAUTI ( *KUFA =Kiroho +kiroho* ) sawa na ilivyoandikwa katika

📖Warumi 6:23 (KSW) *KWA MAANA MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI* ; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

📌Leo sitaenda mbali sana juu ya sababu hiyo ya MAUTI lakini nilitaka uone MATOKEO YA KAZI YA KRISTO YESU baada ya kufanya UPATANISHO wa watu na Mungu na kulipiwa adhabu ya *DHAMBI na MAKOSA yao kufutwa*,,,,, ambapo kiuhalisia ni *UZIMA* yaani kazi ya YESU KRISTO ni kuwapa watu *UZIMA WA MILELE* .

📚 K**a wewe waamini na ni hakika yako kuwa umempokea KRISTO na una Uhusiano nae, basi kwako MAUTI haitakutawala maana yeye aliyeshinda *MAUTI YU HAI MILELE WALA HAFI TENA* si tu kuwa YESU KRISTO uliyempokea YU HAI bali *AMEKUWA HUO UZIMA*.

📖Yohana 14:6
*Yesu akamwambia, MIMI NDIMI njia , na kweli , na UZIMA* ; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

📌 Ooh unaona? Hebu angalia na hapa 👇🏾

📖Warumi 6:9-10
[9] *TUKIJUA YA KUWA KRISTO akiisha KUFUFUKA katika wafu HAFI TENA , wala MAUTI HAIMTAWALI TENA* .

[10] Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu.

😁 Hallelujah!!!

📌Kwa hiyo kule kushinda kwake MAUTI YU HAI MILELE WALA HAFI TENA na MAUTI HAINA NGUVU JUU YAKE,,,,,, je hayo yote ILIKUWA kwa ajili yake tu?

Bila shaka ni *HAPANA*
🌹 kwa sababu yeye aliyetufia na kulipa gharama ya adhabu ya dhambi za watu, na makosa yetu, hakufa kwa ajili yake bali kwa ajili yetu na huo *UZIMA WA MILELE NA KWA AJILI YAA HAO AMBAO KWA DHAMBI NA MAKOSA YAO WALISTAHILI KUENDELEA KUFA NA MAUTI ILIKUWA HAKI YAO (MALIPO STAHILI KWAO* ) ......

📚Yeye huyo tena hakuwa na asili ya DHAMBI wala kosa lolote.

📖Isaya 53:5
*BALI ALIJERUHIWA kwa MAKOSA YETU , Alichubuliwa kwa MAOVU YETU ; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona* .

❤️ What a Amazing LOVE.... Je mambo haya ya kubadili sheria ya dhambi na MAUTI KUENDELEA kuwapata au kuwatawala watu ilikuwa ni mpaka lini?!

✝️ Jibu la swali hilo si lingine, ni wakati ambao *HUYO ALIYE NA NGUVU YA KUTUTOA DHAMBINI NA MAKOSANI aje - (wapi? - bila shaka Ulimwenguni tulipo)*

📌 Angalia kwa makini kauli hii aliyosema YESU KRISTO angalia anavyoanza

📖 [Yohana 10:10] " ........... *MIMI NALIKUJA ILI WAWE NA UZIMA* , kisha wawe nao tele.

⏫ Kauli hii kwa watu ambao wako makini wangejiuliza swali moja, *ikiwa YEYE ALIKUJA ILI TUWE NA UZIMA KISHA TUWE NAO TELE (MILELE) na swali lingekuwa hivi " kwanini watu bado wanakufa* ?! "

📌 Utagundua KRISTO YESU kwa jinsi ya mwili wakati hayo maandiko yanaandikwa alikuwa bado hajaja, waandishi walipewa kuyaona mambo atakayoyafanya siku akija huyo *MWENYE KUOKOA* - KRISTO YESU. Na sasa AMEKUJA!!!!!

✍🏼 Ni Neema ya ajabu kwa wewe usomaye haya kuwepo katika kipindi hiki tulichonacho sasa, [ mimi nayaandika haya 2022] maana ndicho kipindi cha KUWEPO KWAKE HUYO aitwaye jina lake *UZIMA* [ Yoh 14:6] - *YESU KRISTO* .


📖 Ni kipindi ambacho injili yake inafufua waliokufa na kuwafanya watu kuingia MBINGUNI HASA na kuwa *WANA WA MUNGU* kwa njia ya Uhusiano wa watu na yeye. Hallelujah!!!!

📚 Na unajua nini? Kwanini nimetangulia kusema kuwa kipindi hiki ndicho KRISTO YESU ameujia ulimwengu na kuupa *UZIMA WA MILELE*,......ni kwa sababu kule kufanywa *MWANA WA MUNGU ndio UFUFUO WA WAFU na KUPOKEA HALI YA KUWA NA UZIMA USIO NA KIKOMO HAPA DUNIANI*.

⏩ K**a uko makini na unafuatilia kwa karibu katika haya nisemayo utagundua kuwa kuna vitu vinaenda pamoja navyo ni hivi, nisikilize katika hivi vitu nami nitahitimisha somo hili kwa Episode hii. Na hakika yangu hautabaki k**a ulivyokuwa kabla ya kusoma haya.

✍🏼 Viko vitu au mambo manne ambayo yanaenda pamoja ndani ya kuja kwake *KRISTO ULIMWENGUNI* .

(1) *KUJA KWA KRISTO ULIMWENGUNI*.


(2) *WATU KUFANYWA WANA WA MUNGU*.

(3) *KUFUFULIWA NA KUPOKEA UZIMA WA MILELE*.

(4) *UFALME WA MUNGU*.

✍🏼 Nami niyaunganishe yote kwa pamoja kwa kusema hivi =

⏩ " *KUJA KWAKE KRISTO YESU Ulimwenguni kwa jinsi ya mwili kunaleta UFALME WA MUNGU DUNIANI, na KUWAPA WATU HALI YA WAO KUFANYWA WANA WA MUNGU na kwa sababu hiyo wanapokea kitu kinachoitwa UZIMA WA MILELE ndani yao wala hawafi tena na huo ndio UFUFUO*".

📌Kwa kusema hivyo k**a unaona hakuna watu wanaoishi MILELE hapa duniani, na MAUTI ina nguvu juu yao,,, basi ujue hakuna WANA WA MUNGU ULIMWENGUNI, HAKUNA UFALME WA MUNGU DUNIANI, hata KRISTO hayupo ULIMWENGUNI na hakuna UFUFUO.

📚Yaani ni kule kusema kuwa UJIO WA YESU KRISTO ULIMWENGUNI unaleta matokeo ya KUWAPA WATU HALI YA WAO KUISHI MILELE HAPA DUNIANI. K**a hujashuhudia hayo na unaambiwa Yesu aliwahi kuja miaka 2000 iliyopita basi ujue hakuwahi kuja.

✍🏼Kwa wanaotaka nithibitishe kauli hizi kwa maandiko wala msijali kuhusu hilo, niko na maandiko mengi hapa na baadhi ya hayo ni k**a ifuatavyo ,,,

📖1 Yohana 3:2 *Wapenzi, SASA TU WANA WA MUNGU , WALA HAIJADHIHIRIKA BADO TUTAKAVYOKUWA ; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, TUTAFANANA NAYE ; kwa maana TUTAMWONA k**a alivyo*.

⏫ Mstari huo hapo juu (1 Yohana 3:2) unatosha kutuonesha kuwa , mwandishi huyu Yohana (na wengi wanajua kuwa aliandika haya baada ya Yesu kuwa amekwisha kuja hiyo miaka 2000 iliyopita) , mwandishi alikusudia kutuonesha kuwa yeye pamoja na wote wenye matarajio ya kumngoja Kristo Yesu atakapokuja kuwa WATAPOKEA HALI YA KUWA WANA WA MUNGU,........anaanza kwa kusema " Wapenzi, Sasa tu wana wa Mungu,......"

✍🏼Lakini katika Mstari huo maneno yanayofuata yanabadilisha kauli ya kuwa sasa tu wana wa Mungu kwa kusema kuwa,....... " *WALA HAIJADHIHIRIKA BADO ITAKAVYOKUWA......"* nami ninakuhakikishia kuwa HAKUNA HATMA baada ya KUWA MWANA WA MUNGU, Yaani kuwa *MWANA WA MUNGU* ni mwisho, hakuna asili nyingine, tena mwandishi akaongeza kuwa " *TUTAFANANA NAE* (huyo KRISTO - MWANA WA MUNGU ALIYE HAI) "

📖 Na hakuna sababu ya yeye kusema..... " *LAKINI HAIJADHIHIRIKA BADO........... TUTAFANANA NAE* " k**a tayari alikuwa ndani ya kipindi ambacho watu wanapokea hali ya kuwa *WANA WA MUNGU*. Kwa sababu TUTAFANANA nae katika huko kuwa WANA WA MUNGU ambako ndani yake ndio kuna *UZIMA WA MILELE NA UFUFUO WA MIILI YA WATU NA KUISHI MILELE HAPA DUNIANI*....

✍🏼 Nasema tena kwa herufi kubwa kuwa *MWANA WA MUNGU HAFI*,,,, k**a unajiita na unaamini moyoni mwako kuwa wewe ni MWANA WA MUNGU na hauna hakika k**a *UTAISHI MILELE HAPA DUNIANI* bila kuonja *MAUTI*, basi ninayo sababu ya kusema wewe sio Mwana wa Mungu. Kwa sababu kule kuwa MWANA WA MUNGU, ndio KUFUFULIWA - *KUPOKEA hali ya UZIMA USIO NA KIKOMO* na k**a UMEPOKEA HUO UZIMA HAPA DUNIANI *hatutegemei kufa kwako*,,,,,,,, maana ukifa inathibitisha kuwa MAUTI BADO INA NGUVU JUU YAKO na haukuwahi kuwa na *UZIMA WA MILELE*.

😁 Kuna mtu anauliza " *leta andiko* kuthibitisha hayo" , sawa nikupe sasa andiko hili linalotupa sifa ya *WANA WA MUNGU* na moja ya sifa walizonazo *WANA WA MUNGU* ni, *UZIMA WA MILELE* - [ HAWAFI TENA ] .

🔊Haya tusome kwa sauti hapa 👇🏾

📖Luka 20:35-38 (KSW)
[35] lakini, wale wahesabiwao kuwa *wamestahili kuupata ulimwengu ule, na KULE KUFUFUKA KATIKA WAFU* , hawaoi wala hawaolewi;

[36] *WALA HAWAWEZI KUFA TENA ; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, NAO NI WANA WA MUNGU , kwa vile walivyo WANA WA UFUFUO.*

[37] Lakini, ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya Kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.

[38] Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.

⏫ Ningeweza kueleza mstari mmoja baadaye mwingine lakini kwa ufupi kabisa nilitaka uone *SIFA ZA WANA WA MUNGU, mstari wa 36 wameitwa WANA WA UFUFUO*, na utaona kwenye ( Luka 20 : 35-38) utaona mstari wa 36 mwanzoni anaionesha sifa moja wapo ya hao *WANA WA MUNGU / WANA WA UFUFUO* kwa kusema kuwa ni sifa ya wao *KUTOKUFA*.

🧏🏾‍♂️ Nisikie kutoka kwako wewe ni mwana wa Mungu? Je UNA SIFA YA KUTOKUFA?

📚Andiko lingine ni hili

📖1 Yohana 3:2 (KSW) Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; *LAKINI twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, TUTAFANANA NAYE* ; kwa maana tutamwona k**a alivyo.

⏫Mstari huo, tuliusoma lakini limetaka tuusome tena uone kule kuja kwa KRISTO na kudhihirishwa kwake kwetu Ulimwenguni, kuvyoleta *KUFANANA NAYE YESU KRISTO* kwa sisi ambao tulimngoja na tulingoja kwa imani KUPOKEA hali ya *KUFANYWA WANA WA MUNGU.*

✍🏼 Je tunafanana naye [ Yesu ] kwenye eneo gani? Tunajua yeye - Kristo Yesu ni mwana wa Mungu, kwa hiyo tunafanana nae kule KUITWA NA KUFANYWA *KUWA WANA WA MUNGU* ,,,,,

Je ni hivyo tu, hapana, bali sifa ya *KUTOKUFA KABISA* na kuwa na *UZIMA USIO NA UKOMO* tena hapa hapa DUNIANI kwa sababu ametujia hapa duniani na sio atupe uzima wa MILELE tukifa hapana hakusema hivyo alisema *NAMI NIMEKUJA ILI WAWE NA UZIMA kisha wawe nao TELE.* NA kauli hiyo si ya ahadi baada ya kuja, bali ni jambo la KUPOKEA hapa hapa duniani baada ya yeye kuja.

✍🏼 Naye anayo sifa HIYO YA UZIMA - *KUTOKUFA* ambayo katika hiyo maandiko yanasema na mimi nasema *TUTAFANANA NAYE*.

📖Warumi 6:9 (KSW) tukijua ya kuwa Kristo *akiisha kufufuka katika wafu HAFI TENA , wala MAUTI HAIMTAWALI TENA.*

✍🏼Tena mambo haya yakaelezwa hapa hasa juu ya habari ya ukuhani (nafasi yake mbele za Mungu katika kutupatisha na kutuombea) katika ulimwengu wa roho ,, kwamba hata hiyo nafasi ya ukuhani huo *NI WA MILELE KWA SABABU YA UZIMA ALIO NAO MILELE*.

📖Waebrania 7:14-16, 22-25

[14] Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lo lote juu yake *katika mambo ya ukuhani* .

[15] Tena hayo tusemayo ni dhahiri sana zaidi, ikiwa ametokea kuhani mwingine mithili ya Melkizedeki;

[16] asiyekuwa kuhani kwa sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili, *BALI KWA NGUVU ZA UZIMA USIO NA UKOMO* ;

[22] basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

[23] Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;

[24] *BALI YEYE , KWA KUWA AKAA MILELE , ANAO UKUHANI WAKE USIOONDOKA* .

[25] Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

✍🏼Nihitimishe kwa kusema hivi MUNGU NI PENDO, na ameifunua siri ya asili yake hii ya UPENDO ❤️ wake kwa kumfunua mwanawe wa pekee ili kila ampokeaye awe na *UZIMA WA MILELE* na huyo MWANA PEKEE WA MUNGU hata sasa yuko ULIMWENGUNI kwa jinsi ya mwili na roho. Receive him now!!!

🌹Shalom!!!!! Ubarikiwe 🙌🏽

📚 Imeandaliwa na sisi *B.O.J MINISTRY*
na kuandikwa na mimi ndugu yenu katika KRISTO YESU *BENJAMIN JACOB HEMA*.

Church!!!! Cheers 🥂😁

Address

Ndala, Shinyanga TZ
Shinyanga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when B.O.J Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share