ELCT SELVD HABARI

ELCT SELVD HABARI TO PREACH THE GOSPER OF JESUS CHRIST

Matukio katika PichaJuni 7, 2026 : Ibada ya Siku ya Bwana ya kwanza baada ya Utatu imefanyika Kanisa Kuu Ebenezer. Katik...
07/06/2026

Matukio katika Picha

Juni 7, 2026 : Ibada ya Siku ya Bwana ya kwanza baada ya Utatu imefanyika Kanisa Kuu Ebenezer.

Katika ibada hiyo, Msaidizi wa Askofu Mteule, Mchungaji Aaron Nchambi, alitambulishwa rasmi kwa Wakristo wa Dayosisi baada ya kuchaguliwa kuwa msaidizi wa Askofu mteule katika Mkutano Mkuu wa Dayosis Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria uliofanyika tar 5-6 Juni 2026.

“Kamwe tusibadilishe Neno la Mungu, bali Neno la Mungu litubadilishe,” amesema Askofu Jackson Mushendwa.Amesema hayo wak...
06/06/2026

“Kamwe tusibadilishe Neno la Mungu, bali Neno la Mungu litubadilishe,” amesema Askofu Jackson Mushendwa.

Amesema hayo wakati akinena kwenye Mkutano Mkuu wa 7 wa Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria uliofanyika Makao Makuu yake, Shinyanga-Bushushu, kuanzia tarehe 5 hadi 6 Juni 2026.

Mkutano huo umehitimishwa tarehe 6 Juni 2026 ambapo Dayosisi imepata Neno Kuu kutoka Yohana 8:31ᵇ lisemalo: “…Ninyi mkikaa katika Neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli.”

Neno hilo litatumika kwa kipindi cha miaka minne ijayo.

Mkutano Mkuu wa Saba wa Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria umeanza tarehe 05 Juni 2026 katika Makao Makuu ya Day...
05/06/2026

Mkutano Mkuu wa Saba wa Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria umeanza tarehe 05 Juni 2026 katika Makao Makuu ya Dayosisi, Bushushu mkoani Shinyanga.

Miongoni mwa agenda za mkutano huo ilikuwa ni uchaguzi wa Msaidizi wa Askofu, ambapo Mchungaji Aron Nchambi amechaguliwa kuwa Msaidizi wa Askofu Mteule.

Kabla ya uchaguzi huo, Mchungaji Aaron Nchambi alikuwa akihudumu k**a Mkuu wa Jimbo la Shinyanga.

Mkutano Mkuu huo unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 06 Juni 2026.

02/06/2026

Kutokana na ukuaji wa kazi ya Injili katika Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, ambapo ifikapo Disemba 2027 inatarajiwa kuanzishwa Dayosisi ya Simiyu na ifikapo Disemba 2029 kuanzishwa Dayosisi ya Kahama.

Dayosisi imeandaa na kurekodi nyimbo maalum zilizoshirikisha kwaya kutoka kanda zote za Simiyu, Shinyanga na Kahama.

Nyimbo hizo zimeandaliwa k**a kumbukumbu ya umoja na ushirikiano wa kanda hizo kabla ya mgawanyiko na Uzinduzi rasmi wa nyimbo hizo utafanyika tarehe 5 Juni 2026 katika Makao Makuu ya Dayosisi, Bushushu.

Ziara ya wanafunzi kutoka Chuo cha Concordia University, Nebraska Marekani ndani ya Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Vi...
28/05/2026

Ziara ya wanafunzi kutoka Chuo cha Concordia University, Nebraska Marekani ndani ya Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria imehitimishwa kwa huduma ya kutembelea nyumba kwa nyumba katika mtaa wa Lyandu , ambapo jumla ya watu 38 walibatizwa na kujiunga na Imani ya Kikristo.

Wanafunzi kutoka Chuo cha Concordia University, Nebraska Marekani  pamoja na Wahadhiri  wao, wameendelea na ziara yao ta...
26/05/2026

Wanafunzi kutoka Chuo cha Concordia University, Nebraska Marekani pamoja na Wahadhiri wao, wameendelea na ziara yao tarehe 26 Mei 2026 ndani ya Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria kwa kutembelea Kituo cha Mafunzo cha Askofu Dkt. Makala Negezi, Shule ya Sekondari Mwadui na Kituo cha Watoto Wenye Ualbino KKKT Mwadui kwa lengo la kujionea kazi mbalimbali za Dayosisi. Ziara hiyo imeongozwa na Askofu Dkt. Yohana Nzelu.

Matukio katika picha yakionyesha wanafunzi kutoka Chuo cha Concordia University, Nebraska pamoja na wahadhiri wao katika...
25/05/2026

Matukio katika picha yakionyesha wanafunzi kutoka Chuo cha Concordia University, Nebraska pamoja na wahadhiri wao katika ziara yao ya kutembelea Dayosisi Kusini Mashariki Ziwa Victoria. Ziara hiyo imeongozwa na Katibu Mkuu, Dkt. Happiness Gefi 25 Mei 2026.

Juma la Misioni katika Jimbo la Kusini Mashariki Kishapu limehitimishwa siku ya Bwana ya Pentekoste kwa Ibada iliyoongoz...
24/05/2026

Juma la Misioni katika Jimbo la Kusini Mashariki Kishapu limehitimishwa siku ya Bwana ya Pentekoste kwa Ibada iliyoongozwa na Askofu Dkt . Yohana Nzelu katika mtaa wa Mihama tarehe 24 Mei 2026, eneo ambalo hapo awali halikuwa na Kanisa wala huduma ya kudumu ya kiroho.

Kupitia kazi ya Uinjilisti iliyofanyika katika juma hili, Kanisa limepandwa katika eneo hilo lililo chini ya Usharika wa Imani Mwamanota.

Zaidi ya watu 1,200 wamebatizwa katika juma hilo la Misioni,na hii ni ishara ya matunda ya Injili na ukuaji wa kazi ya Mungu.

Neema ya Mungu yaendelea kuonekana Jimbo la Kishapu eneo la Nyahwa, watu 260 wakibatizwa katika siku ya tano ya Juma la ...
22/05/2026

Neema ya Mungu yaendelea kuonekana Jimbo la Kishapu eneo la Nyahwa, watu 260 wakibatizwa katika siku ya tano ya Juma la Misioni.

Mwamadulu yaendelea kushuhudia matendo makuu ya Mungu watu 223 wamebatizwa katika siku ya nne ya Juma la Misioni.
21/05/2026

Mwamadulu yaendelea kushuhudia matendo makuu ya Mungu watu 223 wamebatizwa katika siku ya nne ya Juma la Misioni.

Address

Shinynga
Shinyanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELCT SELVD HABARI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to ELCT SELVD HABARI:

Share

Category