AICT Sengerema -Twitange

AICT Sengerema -Twitange Preaching the gospel to everyone

*UNYENYEKEVU NA UJASIRI NDANI YA NDOA* Mtu ambaye ni mnyonge kihisia au kimaisha (mtu ambaye hajikubali), hutafuta kuwap...
01/10/2025

*UNYENYEKEVU NA UJASIRI NDANI YA NDOA*

Mtu ambaye ni mnyonge kihisia au kimaisha (mtu ambaye hajikubali), hutafuta kuwapendeza watu, hawezi kuvumilia pale mwenzi wake au watu wengine wakikasirika kwa sababu yake, kwa hiyo ni mtu ambaye anapenda kumpendeza mwingine ili apate kukubaliwa, hivyo hawezi kumkosoa mwenzi wake kukosoa wengine na kuelezea jinsi gani ameumizwa, lakini mtu k**a huyu kwa sababu hawezi kumkosa mwenzi wake, hivyo hawezi hata kusamehe, ataumizwa lakini ataficha maumivu hayo, na hata hawezi kuwa muwazi kuhusu maumivu ambayo anapitia, hataki kukosoa kwa sababu anaamini upendo kwa mwenzi wake utapotea, kwa hiyo ataona bora amani na upendo vitawale kuliko ukweli, kwa hiyo bora adanganywe au adanganye kuliko kusema Ukweli ambao unaweza kumfanya apoteze penzi linalomuinua kimaisha,

Tunahitaji unyenyekevu lakini pia ujasiri mkubwa ambao hautokani na ulimwengu huu, kwa sababu, k**a unyenyekevu unaotokana na maisha, ujasiri wa ulimwengu huu unaweza kuletwa kwa sababu ya elimu, mafanikio, cheo, n.k. lakini ujasiri huu usiwe na unyenyekevu kwa wakosaji ambao hawajafanikiwa k**a wewe. Hivyo unaweza kusema ukweli hata pasipo kuwathamini na kuonyesha upendo kwa wengine kwa sababu ujasiri wako ni kwa sababu ya maisha yako uliyonayo,

Injili ya Yesu Kristo inatugeuza na kutufanya kuwa wanyenyekevu lakini pia ni wajasiri, kwa sababu injili inasema, "sisi ni waovu na wenye dhambi sana hata Yesu Mwana wa Mungu afe kwa ajili yetu, ni waovu sana kiasi kwamba ni kifo tu cha Mwana wa Mungu ndio kingetosha kutuokoa" lakini pia "tunapendwa sana na kuthaminiwa kiasi kwamba Mwana wa Mungu(Bwana wa dunia hii alitupenda kiasi hiki) alikuwa tayari kufa kwa ajili yetu", hivyo injili inatunyeyekesha hadi mavumbini na wakati huohuo inatuinua hadi mbinguni. Dr Timothy Keller" anasema we are sinners but completely loved and accepted in Christ at the same time"

Hivyo tunaweza kusema Ukweli katika Upendo kwa sababu kuna neema ya Mungu itokanayo na injili, inayotufanya wajasiri katika kusema Ukweli na wanyenyekevu katika kuonyesha upendo na kuthamini wengine.

Hongera sana kwa kujifunza mpaka hapa, TUTAENDELEA, DOTTO JOHN SWEYA,, 0787732433, 25/09/2025, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO,

*UKWELI NA UPENDO* Moja ya uwezo ambao ni muhimu sana mtu kuwa nao kwenye ndoa ni uwezo wa kusema ukweli kuhusu dhambi a...
30/09/2025

*UKWELI NA UPENDO*

Moja ya uwezo ambao ni muhimu sana mtu kuwa nao kwenye ndoa ni uwezo wa kusema ukweli kuhusu dhambi au madhaifu au makosa ya mwenzi(mume au mke) wako na bado ukaweza kuonyesha msamaha kwa upendo pasipo unafiki, pasipo kujihesabia haki, pasipo kujionyesha wewe ni mkuu kuliko yeye, au kumfanya mwenzako awe mnyonge,

Hii haimaanishi hautakiwi kuonyesha hasira, k**a hauwezi kuonyesha hasira kuhusu kosa ambalo limefanywa na mumeo au mkeo, ukweli wako hauwezi kueleweka zaidi, ataona ni k**a kosa la kawaida tu, hataweza kuona uzito wa kosa alilofanya, kumbuka kuna tofauti ya kuonyesha hasira kwa kosa ambalo umetendewa na kuonyesha hasira kwa mwenzi wako.

Pamoja na hasira, tunahitaji neema ya kusamehe kila wakati ambapo hasira huibuka, msamaha unapokuwepo hata k**a kuna hasira, msamaha unakuwa k**a chumvi kwenye nyama, msamaha unaipa hasira breki, isiende kwenye maamuzi mabaya,

Kumbuka Biblia haikatazi kuwa na hasira, hasira tulizonazo, Mungu ameziweka kwa makusudi mema, mara nyingi hasira zinaonekana mbaya kwa sababu hazipo kwenye udhibiti, kwa sababu hasira zinahitaji kuwa kwenye udhibiti wa msamaha, ili zionyeshe ukweli katika upendo,

Ukweli na upendo zinaweza kuwa pamoja kwa sababu, kila mmoja wetu (mume na mke) anaweza kumsamehe mwenzi wake k**a ambavyo Kristo alitusamehe sisi, ni vigumu kuishi maisha ya Ukweli na upendo k**a hujui uzito wa ukweli na upendo ambao Yesu ameonyesha msalabani, ukweli ni kwamba "dhambi zetu zilikuwa mbaya mno kiasi kwamba ilihitajika Mwana wa Mungu atuokoe", na Mungu kaonyesha upendo huu mkuu kuwa "tunapendwa sana kiasi kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya wenye dhambi mmoja wao ni mimi na wewe ili tuhesabiwe haki mbele za Mungu". Je, na wewe utasema ukweli na kuonyesha upendo kwa kusamehe unapokosewa?! K**a Mungu alivyofanya kwako?!

Hongera sana kwa kujifunza mpaka hapa, TUTAENDELEA DOTTO JOHN SWEYA, 0787732433, 23/09/2025, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO,

*NEEMA KATIKA KWELI NA UPENDO*K**a ambavyo tumeona ndoa ina nguvu ya kuonyesha ukweli kuhusu tabia zetu, lakini pia pamo...
24/09/2025

*NEEMA KATIKA KWELI NA UPENDO*

K**a ambavyo tumeona ndoa ina nguvu ya kuonyesha ukweli kuhusu tabia zetu, lakini pia pamoja na ndoa kufunua madhaifu yetu, tunahitaji kuambiana ukweli kuhusu madhaifu katika upendo na kuonyesha upendo katika ukweli, kwa sababu hata k**a kuna upendo mwingi lakini hakuna kuambiana ukweli kati ya mume na mke, huo upendo utakuwa wa kinafiki na hautafika mbali, pia tuliona kuwa pasipo neema ya Mungu ni vigumu kuonyesha haya mawili kwa pamoja,"ukweli katika upendo na upendo katika ukweli"

Tunapoifahamu neema ya Yesu Kristo, inatuwezesha kufanya yote mawili, kwa sababu ili uweze kusema "ukweli katika upendo", unahitaji kuelewa nini maana "kusamehewa dhambi zako katika Kristo Yesu", huwezi kusema ukweli katika upendo k**a haujamsamehe mkeo au mumeo, maana ukweli pasipo upendo, huo ukweli hautakuwa na msaada kwa yule ambaye asikiaye, kwa sababu utakuwa unamwambia ukweli sio kwa sababu unampenda bali unamwambia ukweli kwa ajili yako, sio kwa ajili yake, ili aumie kwa sababu amekuumiza, na matokeo yake ni maumivu zaidi, hivyo unahitaji kusamehe ili kusema ukweli katika upendo,

Pia ili tuweze kuonyesha upendo katika ukweli, lazima tukubali kuwa watu wa kutubu, neema ya Kristo inafunua jinsi ambavyo sisi ni wenye dhambi hata Mwana wa Mungu akafa msalabani kwa ajili yetu, k**a hautambui wewe ni mwenye dhambi kiasi gani hata Yesu Kristo akafa kwa ajili yako, ni vigumu kutubu, kwa sababu ukijua kuwa dhambi zako zilisababisha maumivu kwa Yesu, utaelewa ni namna gani madhaifu yako na dhambi zako zinasababisha maumivu kwa mwenzi wako, hivyo toba itakuwa sehemu ya maisha yetu,

Kwa hiyo tunapokuwa watu wazuri katika kusamehe na kutubu, upendo na ukweli vitakaa pamoja, na hii inawezekana kupitia kuifahamu neema iliyopo katika Yesu Kristo,

Hongera sana kwa kujifunza mpaka hapa TUTAENDELEA, DOTTO JOHN SWEYA, +255787732433, 19/09/2025, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO,

*UKWELI KATIKA UPENDO NA UPENDO KATIKA UKWELI*Sababu inayofanya ndoa iwe na nguvu ya kuonyesha UKWELI kuhusu madhaifu ya...
16/09/2025

*UKWELI KATIKA UPENDO NA UPENDO KATIKA UKWELI*

Sababu inayofanya ndoa iwe na nguvu ya kuonyesha UKWELI kuhusu madhaifu yangu ni kwa sababu mwenzi wangu anaweza kuona madhaifu yangu kuliko hata ambavyo mimi naweza kujiona, kwa hiyo mume wako au mke wako ni mtu mmoja pekee duniani ambaye amebeba moyo wako, ambaye maneno yake mazuri yaani UPENDO wake unauhitaji zaidi, lakini pia ni mtu ambaye anaumizwa zaidi kwa dhambi zako kuliko mtu yeyote duniani.

Kwa sababu ni mtu pekee anayeumizwa na dhambi au makosa yako kuliko mtu yeyote duniani, madhaifu yako ambayo ni KWELI unayo, yataanza kupelekea kubomoa UPENDO kati yenu, na UPENDO unapoanza kubomoka utasababisha kutokuambiana UKWELI kwa UPENDO, ni kweli mtu amekosea badala ya kumwambia UKWELI KUHUSU TABIA ZAKE kwa sababu UNAMPENDA, utamwambia UKWELI KUHUSU TABIA ZAKE kwa sababu UMEKASIRISHWA AU KUCHUKUZWA, na kwa sababu amekuambia huku AMECHUKIA na KUKASIRIKA, hautaelewa UKWELI unaosemwa, zaidi sana utaona ALIKOVYOKUKASIRIKIA AU KUKUCHUKIA, na wewe badala ya kuonyesha UPENDO kwa sababu UMEKASIRISHWA na namna aliyokuambia utamwambia UKWELI KUHUSU KUKASIRIKA pasipo UPENDO, inakuwa changamoto kutatua kushughulikia ukweli huo,

Kile ambacho ningependa tujifunze ni kuwa KWELI NA UPENDO LAZIMA ZIENDE PAMOJA ILI UKWELI UELEWEKE, NA ILI UPENDO UONEKANE, hamwezi kupendana kwa dhati k**a hamwezi kuambiana ukweli wa madhaifu yenu, hivyo hivyo hamwezi kuambiana ukweli wa madhaifu yenu k**a hamwezi kupendana kwa dhati,

Naelewa ni vigumu sana kusema ukweli kuhusu tabia mbaya za mwenzi wako hasa ukiwa umechukizwa mara nyingi tunatumia nguvu ya ukweli bila upendo, lakini pia kwa sababu unaogopa kumuumiza mwenzi wako kwa sababu ya nguvu ya ukweli, unaweza kujaribiwa kutokumwambia ukweli lakini matokeo yake sio upendo kati yenu, kwa sababu jinsi tulivyo ni kuwa sisi k**a wanadamu "tunahitaji kutambua kuwa tunapendwa sana na wenzi wetu ili wakiwa wanatuambia ukweli kuhusu tabia zetu, tuamini kuwa wanatuambia ukweli kwa sababu wanatupenda sana hivyo inakuwa vyepesi kukili makosa yetu" nisikuchoshe, natumai utakuwa unaelewa kile Waefeso 4:15 "kuishika kweli katika upendo"

Hongera kwa kujifunza mpaka hapa TUTAENDELEA, DOTTO JOHN SWEYA, +255787732433, kumbuka UNAWEZA KUIFURAHIA NDOA YAKO,

*NGUVU YA MANENO MAZURI KWA MWENZI WAKO* Mtu anapoingia kwenye mahusiano ya ndoa, anakuwa amekutana na kauli mbalimbali ...
14/09/2025

*NGUVU YA MANENO MAZURI KWA MWENZI WAKO*

Mtu anapoingia kwenye mahusiano ya ndoa, anakuwa amekutana na kauli mbalimbali kwenye maisha kumhusu yeye, mara nyingi kauli mbaya ndizo zina nguvu kubwa ndani ya moyo wa mtu, ndio maana wanasaikolojia wanasema "msifu mara kumi mtoto ili umkosoe mara moja" ili kujenga mtazamo chanya wa kujikubali kuhusu yeye mwenyewe (good self-appreciation)

Mahusiano ya ndoa yanakuweka mikononi mwa mwezi wako kujenga mtazamo chanya au mbovu kuhusu wewe, maneno mazuri ya upendo ya mume wako au mkeo, yana nguvu ya kuleta uponyaji wa majeraha ya moyo ambayo yametokana na maneno magumu ambayo umepitia huko nyuma,

Kwa sababu, hata ulimwengu wote useme wewe ni mbaya, lakini mumeo au mkeo anakukubali kuwa wewe ni mzuri, utajisikia vizuri, hata k**a moyo unakumbia wewe sio mzuri, lakini neno la mumeo au mkeo lina nguvu kuliko hata maneno yako magumu kuhusu wewe wenyewe, lakini ukijikubali na hata ulimwengu wote useme wewe ni mzuri halafu mkeo au mumeo asikukubali kuwa ni mzuri, inaumiza sana moyo wako,

Unajua kwanini, ukitambua kuwa unapendwa na mtu ambaye unamthamini kuliko wote duniani ni jambo kubwa kuliko yote duniani, jambo linaloumiza sana pia ni ukitambua unachukiwa na mtu wa thamani kuliko wote duniani,

K**a vile ambavyo ukitambua kuwa Bwana wa dunia hii anakupenda, ni jambo ambalo kila mwanadamu anahitaji, na maisha yetu yatabadilika tukitambua gharama ya Mungu juu ya maisha yetu, kwa sababu mwanadamu anahitaji "KUPENDWA NA MTU WA THAMANI KULIKO WOTE DUNIANI",

Natambua ni vigumu kuendelea kusema maneno mazuri kwa mwenzi wako hata wakati akikukosea, lakini UKITAMBUA YESU ALISEMWA VIBAYA KWA AJILI YAKO, inabadilisha moyo wako,haswa ukitambua unapendwa na Kristo Yesu, pamoja na dhambi zako, Kristo alikufa msalabani kwa ajili yako, hakuna namna utaokolewa isipokuwa kwa kifo chake msalabani, ilibidi afe ili uokolowe,

K**a vile ambavyo Adamu alivyokuwa na mahusiano makamilifu na Mungu, bado alikuwa ameumbwa kuonyesha upendo kwa mkewe, na wakati mahusiano ya Adamu na Mungu yalipoharibika, hivyo hivyo mahusiano ya ndoa yakaharibika, wakajiona wako uchi na wote wakajificha, mwanadamu unahitaji "UPENDO MKUU WA MUNGU KWAKE ILI KUONYESHA UPENDO MKUU KWA MWENZI WAKO USIPOUJUA UPENDO MKUU HUWEZI KUUONYESHA, KWA SABABU HUWEZI KUTOA KILE AMBACHO HAUNA"

Hongera kwa kujifunza mpaka hapa, TUTAENDELEA, DOTTO JOHN SWEYA, 0787732433, 10/09/2025

*MTU MWINGINE MZURI ZAIDI YA MWENZI WAKO*Moja ya zawadi kubwa iliyomo ndani ya ndoa, ni zawadi ya ukweli kuhusu mapunguf...
09/09/2025

*MTU MWINGINE MZURI ZAIDI YA MWENZI WAKO*

Moja ya zawadi kubwa iliyomo ndani ya ndoa, ni zawadi ya ukweli kuhusu mapungufu ya kila mmoja, lakini zawadi hii hua sio vyepesi kuipokea, mara nyingi tunapoona madhaifu ya mwenzi wetu hua mwitikio wetu unakuwa mbaya,

Kipindi unaanza mahusiano na mwenzi wako ulikuwa unaona yeye ni zaidi ya asali,yeye ni mtu wa thamani zaidi ya mtu yeyote kuwahi kutokea kwenye maisha yako, maneno matamu yalikuwa hayakosi kwenye kinywa chako juu yake, lakini kadri ambavyo muda unakwenda unaanza kuona upande mwingine wa madhaifu, uliona asali sasa unaona nyuki, uliona boga sasa unaona maua, uliona dhahabu sasa unaona uchafu,

Inafikia hatua ya kumchukia mwenzi wako, na kuona k**a tabia yake mbaya haiwezi kubadilika, kwa Mkristo haitakiwi kuwa hivyo kwa sababu ndani yetu tunatambua bado asili ya dhambi inaweza kuendelea kututesa, Warumi 7:14-25, kila ambapo unajitahidi kufanya mema, unajikuta unakosea tena, na kila ambavyo unajitahidi kuna eneo jingine unakosea tena,

Wakati ambapo utaanza kuona madhaifu ya mwenzi wako, wengine hufikia maamuzi ya kuachana, wengine hufikia maamuzi ya kupunguza upendo na yawezekana kuendelea kuvumilia tu, maana ni mpaka kifo kiwatenganishe, wengine hupitia kipindi kirefu cha ugomvi na kulaumiana kuwa mwenzi wako ndio chanzo cha yeye kutokuwa na furaha kwenye ndoa, changamoto hizi zote, zinapelekea kila mtu kwenye ndoa (mme na mke) kufikiri kuwa "KUNA MTU MWINGINE MZURI ZAIDI YA HUYU", k**a ambavyo wewe unawaza juu yake, ndivyo na yeye anawaza hivyo juu yako,

Ni kweli ndani ya kila mtu anatamani apate mtu ambaye hana mapungufu, lakini mtu k**a huyo hayupo, kwa sababu k**a vile ambavyo unaona mapungufu ya mwenzako, ndivyo na mwenzako anaona mapungufu yako, kwa hiyo sio kila kuachana kutatatua changamoto ya ndoa, kwa sababu hata kuachana kwenyewe hakurekebishi madhaifu yako,

Ukweli ni kwamba sote tuna madhaifu ambayo kwa sababu ya ndoa inayaibua kwa nguvu zaidi, lakini hakuna namna ambayo tunaweza kufurahia ndoa pamoja k**a kila mtu, (mme na mke) akimpa nafasi mwenzake ya kumsaidia kurekebisha tabia zake, k**a ambavyo Biblia inatuambia Waebrania 3:13,

Ukiwa kwenye mahusiano kabla ya kuingia kwenye ndoa, pata nafasi kujiuliza Je, mtu huyo ni rafiki yako mkubwa ambaye akiona udhaifu wako na wewe ukiona udhaifu wake badala ya kukimbiana au kuachana mtakuwa pamoja kurekebishana na kusaidiana?! ili kuwa mtu yule ambaye Mungu amemkusudia siku hiyo tukisimama mbele zake Mungu. Ni muhimu kuchagua mtu huyo, epuka kuingia kwenye ndoa na mtu ambaye huoni madhaifu yake, kwa sababu hayupo mtu k**a huyo dunia hii,

Hongera sana kwa kujifunza mpaka hapa TUTAENDELEA, Dotto John Sweya, 08/09/2025, kwa msaada zaidi 0787732433, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO, , ,

*UKWELI KUHUSU TABIA ZAKO BAADA YA KUOA AU KUOLEWA* K**a ambavyo tumeona, ndoa inafunua madhaifu mbalimbali ya tabia zet...
29/08/2025

*UKWELI KUHUSU TABIA ZAKO BAADA YA KUOA AU KUOLEWA*

K**a ambavyo tumeona, ndoa inafunua madhaifu mbalimbali ya tabia zetu, lakini kwanini iwe kwenye ndoa?! Kwa sababu mahusiano ya mume na mke ni mahusiano yenye ukaribu mkubwa kuliko mahusiano yoyote yale kuwepo kwenye maisha yako,

Hivyo, Hakuna mtu yeyote ambaye anaguswa na kuumizwa sana na madhaifu yako k**a mwenzi wako, kwa hiyo mwenzi wako atafahamu maumivu ya madhaifu yako kuliko mtu yeyote, kwa sababu mtu atakaye athiriwa kwanza na hasira zako, uchoyo wako, uzinzi wako, matumizi yako mabaya ya fedha, kiburi chako,(zile tabia zako zote na zile ambazo tuliangalia ujumbe uliopita na nyingine nyingi) ni mkeo au mumeo ndiye atakayekuwa mhanga wa kwanza, ndio maana haishangazi kusikia mme au mke kamuambukiza mwenzi wake UKIMWI,

Kitu kingine ni kwamba, Kabla hujaolewa au kuoa, watu wengine wameona madhaifu yako, hata wazazi wako wanaelewa madhaifu yako, hata wadogo zako, kaka zako au dada zako wanakuelewa baadhi ya tabia zako, roommates wako, marafiki zako pia, na wao wanafahamu baadhi ya tabia zako, na wakati mwingine hata wao waliwahi kukuambia, lakini pia hawakujali sana pale ambapo hukukubali kubadilika, na hawakuona shida, wengine wamekuvumilia tabia zako, kwa sababu haziwaletei changamoto sana k**a ambavyo mwenzi wako zitampa changamoto,

Kwa hiyo sio kwamba tabia zako mbaya ndio zinaonekana ukiwa kwenye ndoa, ila ndoa inaonyesha ubaya wa tabia zako, japo unaweza kumlaumu mkeo au mumeo kwa tabia zake au kwa kugundua tabia zako, lakini pia kitu ambacho unahitaji kuelewa ndoa haiwezi kuficha tabia zako, mkeo au mumeo anakujua zaidi ya mtu yeyote,

Tabia ambazo huwezi kuzingundua zitaendelea kukutumikisha, lakini pia kukataa ukweli kuhusu tabia zako, sio suluhu ya tabia zako, Kwa sababu pia ndoa ina nguvu kubwa ya kufunua ubaya wa tabia zetu, inatuonyesha ukweli kuhusu jinsi tulivyo, mpe nafasi mkeo au mumeo kukuelezea madhaifu yako, itakusaidia kushughulikia tabia hizo, atakuwa unafanya kile Paulo anasema kwenye Waefeso 5:25-27, k**a vile ambavyo Yesu Kristo alikufa msalabani ili atutakase tuwe safi mbele zake Mungu, bila mawaa au makunyanzi, hivyo imetupasa nasi(wanandoa ) imetupasa kusafishana, ili tuwe safi siku hiyo mbele za Mungu.

Nikomee hapa kwa leo TUTAENDELEA, hongera sana kwa kujifunza, ukihitaji jumbe nyingi k**a hizi, +255787732433, DOTTO JOHN SWEYA, kumbuka UNAWEZA KUIFURAHIA NDOA YAKO,29/08/2025

*UKWELI KUHUSU NDOA* Ukweli ni kwamba ndoa inaleta watu wawili tofauti, waliokua tofauti, walioishi mazingira tofauti, w...
27/08/2025

*UKWELI KUHUSU NDOA*

Ukweli ni kwamba ndoa inaleta watu wawili tofauti, waliokua tofauti, walioishi mazingira tofauti, waliolelewa tofauti n.k. kuwa karibu kuliko hata mahusiano yoyote, lakini si tu hivyo ndoa ni zaidi ya mahusiano yoyote ambayo yanayolazimisha ushughulike na changamoto za udhaifu na dhambi za kila mmoja wenu,

Kwa sababu ndoa ina nguvu ya kuonyesha tabia zako mbaya kwa mwenzi wako, ndoa ina nguvu ya kuonyesha baadhi ya tabia mbaya k**a,

1. Yawezekana wewe ni muoga na mtu mwenye mashaka.
2. Yawezekana wewe ni mtu mwenye kiburi, unayatanguliza mbele mambo yako tu,
3. Yawezekana wewe ni mtu mwenye hasira, vyepesi kukosewa, na vyepesi kufanya maamuzi yasiyo sahihi,
4. Yawezekana wewe ni mtu ambaye huwezi kunyambulika, unakasirika usipotendewa hitaji lako.
5. Yawezekana wewe ni mtu ambaye unataka kutimiziwa mahitaji yako tu, unataka mawazo yako ndio yatendewe kazi,
6. Yawezekana wewe ni mtu mkali, (mtu ambaye anapenda kuheshimiwa kuliko kupendwa).
7. Yawezekana wewe ni mtu asiye na nidhamu (mtu asiye na mipango ya maisha).
8. Wewe ni mtu usiyejali,(don't care).
9. Yawezekana wewe ni mtu unayependa kukosoa na kuhukumu wenzako, ila sio wewe,
10. Yawezekana wewe ni mtu ambaye sio mvumilivu wa tabia za watu(unatunza makosa ya mwenzio).
11. Yawezekana wewe ni mtu ambaye unajiona uko juu wengine wako chini yako.
12. Yawezekana wewe ni mtu ambaye unajiona uko chini, wengine wako juu yako.
13. Yawezekana wewe ni mtu ambaye hupendi kuwajibika na mahitaji ya wengine.
14. Yawezekana wewe ni mtu ambaye hupendi kufanya maamuzi ya pamoja, unapenda kutembea pekee yako,
15. Yawezekana wewe mtu ambaye hupendi kuombwa kusaidiwa.
16. Yawezekana wewe ni mtu ambaye kila kitu unahitaji kusaidiwa.
17. Yawezekana wewe ni mtu ambaye unapenda kupendwa na watu kuliko kuheshimiwa.
18. Yawezekana wewe ni mtu ambaye huwezi kutunza siri,unafanya kila jitihada ili kuwapendezesha watu.
19. Yawezekana wewe ni mbanizi sana wa fedha, ni mtunzaji mzuri ila sio mtumiaji mzuri.(Mtunzaji sana).
20. Yawezekana wewe ni mtumiaji mzuri sana wa fedha, ila hauwezi kutunza fedha.(Mtumiaji sana)

K**a vile ambavyo mwenzi wako ataona changamoto k**a hizi ndani yako, hivyo hivyo na wewe utaona changamoto k**a hizi kwa mwenzi wako, ni ukweli ambao unahitaji kuukubali kuwa upo kwenye ndoa.

Hongera kwa kujifunza mpaka hapa TUTAENDELEA, DOTTO JOHN SWEYA, kwa mafundisho k**a haya, 0787732433, 27/08/2025, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO,

*HISIA ZA KIMAPENZI (IN LOVE EXPERIENCE)*  Katika nyakati tulizonazo, watu wengi wanaoa au kuolewa kwa sababu ya hisia z...
25/08/2025

*HISIA ZA KIMAPENZI (IN LOVE EXPERIENCE)*

Katika nyakati tulizonazo, watu wengi wanaoa au kuolewa kwa sababu ya hisia za kimapenzi walizonazo, na mara nyingi hua zinakuwa za moto wakati wanakutana na mwenzi wako, ila takwimu zinaonyesha kuwa hisia hizo hua zinadumu kwa miezi kadhaa hadi miaka miwili, lakini pia hisia za kimapenzi zinakuja na udanganyifu mwingi k**a vile,

1. Unahisi k**a vile mwenzi wako ni mkamilifu kwa kila eneo,
2. Tunavutwa zaidi na uzuri ambao tunauona kwa wakati huo
3. Tunahisi upendo wetu ni jambo la pekee kwenye maisha, ambalo halijawahi kutokea duniani (a love story)
4. Tunaona wale ambao tayari wameoa au kuolewa, wamepoteza hisia za kimapenzi, sisi ndio tunazo,
5. Tunaamini kuwa hisia hizo za mapenzi, hazitapotea na tutazitunza kwa bidii zote.
6. Tunaamini wale, wengine walioko kwenye ndoa, hawana mapenzi k**a yetu, maana yake hawapendani k**a sisi ambavyo tunapendana.
7. Unahisi wengine walikosea kuchagua, ndio maana hawana hisia za mapenzi k**a tuliyonayo sisi.

Hichi kipindi cha hisia za kimapenzi hua kinaisha pale ambapo tunaanza kuona makosa ya mwenzi wetu wakati tunaishi naye ndani, tule tumakosa tudogo dogo, ambato ulikuwa hautuoni mwanzoni, sasa unaanza kuona k**a makosa makubwa, mfano kipindi kuna hisia za kimapenzi ulikuwa haujali k**a anakusalimia au la, lakini sasa hivi unahisi hana heshima, kwa sababu hakusalimii, ulikuwa hauoni k**a ana kovu husoni, lakini sasa unaona makovu mengi, ulikuwa hauoni hasira zake, lakini sasa unaziona vizuri, na mengine mengi, lakini sio tu kwako, hata mwenzi wako anashuhudia baadhi ya tabia ngeni, ambazo hakutarajia k**a wewe unazo,

Tukianza kuona makosa ambayo tulikuwa hatuyaoni, na sasa tunaishi nayo, maana yake tunakutana na mtu ambaye hatukumbuki k**a ndio huyo tulikubaliana kuoana, maana yake tunakutana na tabia tofauti ambazo hatukutalajia kukutana nazo, kwa sababu "HISIA ZA KIMAPENZI" zilificha, hizo tabia,

Hivyo kila mtu anaingia kazini kurekebisha tabia za mwenzake, (kazi ambayo hakutarajia kuifanya, maana alijua mtu aliyemchagua ni mtu sahihi) na changamoto kubwa inakuja pale ambapo unataka kurekebisha za mwongine ambazo yeye mwenyewe hazioni, lakini pia mwenzi wako anataka kurekebisha tabia zako, ambazo hata wewe pia huzioni k**a ni tabia mbaya, maana umeishi nazo ukiwa single bila shida kubwa yoyote ile,(maana kila mtu anaona mwenzake ndio chanzo cha tatizo ndani ya ndoa)

Kila mtu ana muitikio tofauti tofauti akikutana na hali k**a hizi, wengine huchagua kuvumiliana, wengine hasa kwenye kizazi chetu huchagua kuachana, kwa sababu amekuja kugundua kuwa "ulifanya uchaguzi mbaya, haukuchagua mwenzi unayendana naye au haukuchagua mtu sahihi" lakini unasahau kuwa k**a vile ambavyo umeanza kuona makosa ya mwenzako ndivyo na yeye amenza kuona makosa yako.

Nikomee hapa kwa leo TUTAENDELEA, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO, DOTTO JOHN SWEYA, 0787732433, 25/08/2025.

*MTU TOFAUTI NDANI YA NDOA*Tunapoamua kuoa au kuolewa, mara nyingi hua tunaamini au tunazani tunamjua/kumfahamu vya kuto...
22/08/2025

*MTU TOFAUTI NDANI YA NDOA*

Tunapoamua kuoa au kuolewa, mara nyingi hua tunaamini au tunazani tunamjua/kumfahamu vya kutosha mtu huyo ambaye tunaingia naye kwenye ndoa, na hata wakati mwingine tunahisi tumeoa mtu sahihi, lakini baada ya muda tunaona mtu huyo ni tofauti na yule ambaye tuliingia naye kwenye ndoa, ni k**a vile amebadilika.

Hata k**a upo kwenye mahusiano ya uchumba kwa muda mrefu, haitoshi kumjua mtu vya kutosha japo utafahamu baadhi ya tabia, ila usizifahamu tabia zote alizonazo, k**a vile ambavyo hata wewe haujifahamu vya kutosha, pia kuna tofauti ya namna ambavyo unamjua mtu ukiwa kwenye uchumba(wakati wa maandalizi ya ndoa, wakati mwingine kuna kuigiza ili lengo la ndoa litimie) na vile ambavyo unakuja kumjua mtu ukiwa kwenye ndoa unaishi naye milele.

Moja ya kitu ambacho ningependa tukubaliane ni kuwa, "mtu ambaye anaingia kwenye ndoa sio mtu yule yule anayeishi kwenye ndoa" hata k**a mtu huyo ni sahihi, kuna tabia ambazo hukuwahi kuziona kipindi mnakutana mara kwa mara mkiwa wachumba, ila kwa sababu unaishi naye kila siku utaziona, lakini pia utagundua hata kuna tabia fulani za kwako ambazo ulikuwa huzijui ataziona mwenzi wako, au hata ulikuwa unazijua lakini hukujua k**a zitaleta shida kwa mwenzi wako wakati sasa ndio mpo kwenye ndoa.

Watu ambao wamekaa kwenye ndoa hata kuanzia mwaka mmoja, huanza kuona tatizo hili, na wengi ambao wamekaa kwenye ndoa muda mrefu watakubaliana na hili, tatizo kubwa hua linaanza hapa "kumpenda mtu mgeni na tofauti, ambaye hukuwahi kumuona kabla ya kuoa au kuolewa naye " si hivyo tu utagundua, ndoa hua inatubadilisha, tabia za mtu ambaye ulikutana naye akiwa single ni tofauti na mtu ambaye umeoa au kuolewa naye, kwa sababu pia kuwa na watoto kunaleta mabadiliko ndani ya ndoa, mabadiliko ya kazi yanabadilisha maisha yetu, umri pia unabadili maisha yetu, isitoshe pia ndoa ina tabia ya kufunua tabia zetu(nzuri na mbaya) ambazo zilikuwa zimejificha kwa kila mtu, na nyingine hata wewe mwenyewe ulikuwa huzijui lakini sasa hivi zinaonekana kwa mtu muhimu kwenye maisha yako, mwenzi wako anaona tabia zako zilizokuwa zimejificha na wewe pia unaona tabia zake ambazo zilikuwa zimejificha, je, ule upendo wakati unaoa au kuolewa utaendelea?! Hapa ndipo utaelewa ule msemo unaosema "watu huwa hawaachani sura zao zikiwa k**a kwenye picha za harusi yao"

Naomba nikomee hapa kwa leo, TUTAENDELEA zaidi, ukihitaji kujifunza zaidi, chukua namba hii, 0787732433, DOTTO JOHN SWEYA, nitumie ujumbe Whatsapp, utapata nafasi ya kuwepo kwenye group la mafundisho k**a haya, na utapata jumbe nyingi za mafundisho k**a haya, na mengine mengi, ambayo yanaweza kukupa hatua kubwa kwenye ndoa yako, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO,

*NGUVU YA NDOA* K**a ambavyo Yesu anataka nafasi ya kwanza ndani ya moyo wako ndio maana anasema, "usiwe na miungu mingi...
20/08/2025

*NGUVU YA NDOA*

K**a ambavyo Yesu anataka nafasi ya kwanza ndani ya moyo wako ndio maana anasema, "usiwe na miungu mingine ila mimi" yaani kitu chochote kisichukue nafasi yake, pia hivyo hivyo na ndoa haiwezi kusonga mbele k**a ndoa na mwenzi wako sio kipaumbele cha kwanza kwenye maisha yako, kumbuka hata mwenzi wako anasema, "usiwe na mwenzi mwingine ila mimi" mtoto asichukue nafasi yangu, wazazi wako wasichukue nafasi yangu, kazi zako zisichukue nafasi yangu, hobby zako zisichukue nafasi yangu,

Waefeso 5:28, inasema "imewapasa waume kuwapenda wake zao k**a miili yao" k**a ambavyo unathamini afya yako, kwa sababu afya ni mtaji wa maisha, "health is wealth" k**a ambavyo unapenda uwe na afya njema kwa kuutunza mwili wako, basi unahitaji kufanya hivyo kwa mkeo au ndoa yako.

Kwa sababu umeingia kwenye ndoa ambayo imeanzishwa na Mungu, ukiamua kuendesha ndoa k**a unavyotaka unajitafutia matatizo, maana yake tunahitaji kuishi kwenye ndoa k**a ambavyo Mungu anasema, kwa sababu pia ndoa inahitaji kipaumbele cha kwanza kwenye maisha yako, kwa sababu ndoa ina nguvu kubwa kuendesha maeneo mengine ya maisha yako.

K**a ndoa yako ni imara, hata k**a maeneo mengine ya maisha yana changamoto bado utakuwa na nguvu ya kusonga mbele, lakini k**a ndoa yako ni dhaifu hata k**a maeneo mengine ya maisha yanakwenda vizuri, utakosa nguvu ya kusonga mbele kwenye maisha yako,

Unafahamu kuna nafasi kwenye taasisi mbalimbali, huwezi kuongoza k**a hauna ushuhuda mwema kwenye ndoa, mfano: kigezo KIMOJAWAPO cha kuwa kiongozi wa Kanisa ndani ya Biblia, ni ndoa bora, k**a mtu hawezi kuiongoza nyumba yake, atawezaje kuongoza kanisa?!, ndio maana kuna msemo unasema "kosea kujenga, utabomoa au utahama au kupangisha kwingineko au utajenga tena, gharama zake ni ndogo sana, ukilinganisha na kukosea kuoa au kuolewa, gharama za kubomoa au kuhama ni kubwa mno,(kosea kujenga usikosee kuoa au kuolewa)" sio tu hivyo ifanye ndoa ya kuwa ya kwanza kwenye vipaumbele vyako na umpe mwenzi wako nafasi ya kwanza, kumbuka "A happy wife is a happy life" ndoa ina nguvu sana kwenye maisha yako kwa sababu ilianzishwa na Mungu, na kwa sababu ina nguvu kubwa kwenye maisha yetu, lazima tuwekeze huko nguvu zetu kubwa, kwa sababu ndio "engine" muhimu ya maisha.

hongera kwa kujifunza mpaka hapa TUTAENDELEA, DOTTO JOHN SWEYA, 0787732433, 20/08/2025,

*MAHUSIANO YA NDOA YANAZIDI MAHUSIANO YOTE*Mungu hakuweka mahusiano ya baba na mama, au mahusiano ya mzazi na mtoto kwen...
18/08/2025

*MAHUSIANO YA NDOA YANAZIDI MAHUSIANO YOTE*

Mungu hakuweka mahusiano ya baba na mama, au mahusiano ya mzazi na mtoto kwenye bustani ya Edeni, Mungu aliweka mahusiano ya mume na mke, maana yake mtu anapomuacha Baba yake na mama yake, na kuamua kuoa au kuolewa, MAHUSIANO NA MWENZI WAKE, YANATAKIWA KUZIDI MAHUSIANO YOYOTE YALE HATA KUZIDI MAHUSIANO YA WAZAZI, kibiblia hakuna kitu k**a "akitoka mama anafuatia mpenzi", Maana yake mahusiano na mwenzi wako wa ndoa lazima yapewe kipaumbele cha kwanza akitoka Mungu,Mwanzo 2:24,

Ukichana na uhusiano na Mungu wako, mchungaji Dr Timothy Keller, aliwahi kusema "Ndoa yako lazima iwe ya muhimu kwako kuliko kitu chochote kile, hakuna mwanadamu/kiumbe mwingine ambaye anatakiwa apewe upendo wako, nguvu zako, kujitoa kwako, ukaribu wako kuliko unavyofanya kwa mwenzi wako"

K**a kuna mtu yeyote au kitu chochote ambacho nicha muhimu kuliko mwenzi wako, huyo mtu au hicho kitu kitaharibu ndoa yako, isitoshe mwenzi wako akijua kwamba kuna mtu mwingine au kitu kingine ambacho kina umuhimu kuliko hata yeye, mahusiano hayo ya ndoa yana hatari ya kwenda kufa. Ukiwa unataka kuoa au kuolewa, au k**a upo kwenye ndoa, je, mwenzi wako atakuwa wa kwanza kuliko kitu chochote au mtu yeyote baada ya Mungu?!(Jijibu)

Mfano, kwenye eneo la kuacha wazazi, utakuwa umeshindwa kuacha wazazi k**a bado unaongozwa na matarajio yao au matamanio yao kuliko ya mwenzi wako, lakini pia unaweza ukawa haujaacha wazazi wako, k**a bado unachuki au kinyongo nao, kwa sababu kihisia unaendeshwa na wazazi wako, linapokuja suala la kuacha wazazi na kuambatana na mwenzi wako, UNAACHANA NA WAZAZI KATIKA KILA KITU, NA KATIKA KILA KITU UNAAMBATANA NA MWENZI WAKO,

Kwa sababu unapooa au kuolewa, unakuwa umetengeneza taasisi mpya ya maamuzi na unakuwa umeanzisha namna mpya ya kuishi na kufanya mambo, changamoto inakuja ukioa au kuolewa, lakini unataka kuishi k**a ulivyokuwa single au unataka kuishi na kutenda k**a ambavyo familia yenu inafanya, kuliko kushirikiana na mwenzi wako kutengeneza taasisi mpya yenye maamuzi yanayojitegemea, k**a unataka kuishi k**a ulivyokuwa unaishi nyumbani basi wewe hujaacha nyumbani kwenu, utakuwa sana na mtu ambaye amepeleka nyumba yao kwenye ndoa yake,

Tuhitimishe kwa leo hapa, TUTAENDELEA, hongera kwa kujifunza, DOTTO JOHN SWEYA, 0787732433, 18/08/2025, kumbuka UNAWEZA KUFURAHIA NDOA YAKO,

Address

Sengerema

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AICT Sengerema -Twitange posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share