OSB FAITH

OSB FAITH Admin
OSB FAITH ni jukwaa la kiroho lililoanzishwa na Br. Michael Daniel Kitabagala, OSB wa Abasia ya Peramiho. Tukiongozwa na kauli mbiu Ora et Labora,.

Tunashirikisha tafakari, sala na mafundisho ya Kikatoliki ili kusaidia jamii kukua katika imani.

TAFAKARI YA MASOMO YA MISA JUMAMOSI, MACHI 14, 2026Jumamosi ya Juma la 3 la KwaresimaMasomo: Hos 5:15–6:6; Zab 51:3–4,18...
14/03/2026

TAFAKARI YA MASOMO YA MISA JUMAMOSI, MACHI 14, 2026
Jumamosi ya Juma la 3 la Kwaresima

Masomo: Hos 5:15–6:6; Zab 51:3–4,18–21; Lk 18:9–14

Utangulizi
Neno la Mungu la leo linatufundisha ukweli muhimu sana kuhusu maisha ya kiroho: Mungu haangalii sana ibada za nje tunazofanya, bali anaangalia hali ya moyo wetu. Tunaweza kusali, kufunga na kutoa sadaka, lakini k**a moyo wetu umejaa majivuno na kujiona bora kuliko wengine, ibada hizo zinapoteza maana yake. Kwaresima ni wakati wa kutakaswa moyo ili tuweze kumkaribia Mungu kwa unyenyekevu na ukweli.

Katika somo la kwanza kutoka Kitabu cha Hosea, Mungu anawaita watu wake wamrudie kwa moyo wa dhati. Anasema wazi: “Nataka upendo wala si sadaka, na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.” Hapa Mungu anaweka wazi kwamba ibada za nje pekee hazitoshi. Anachotaka kwanza ni upendo wa kweli na uhusiano wa karibu na yeye. Sadaka na ibada vina thamani tu pale vinapotoka katika moyo unaompenda Mungu.

Katika Injili kutoka Injili ya Luka, Yesu anatupa mfano wenye nguvu wa watu wawili waliokwenda hekaluni kusali: Mfarisayo na mtoza ushuru. Mfarisayo alisimama mbele ya Mungu akijisifu kwa matendo yake mema: kufunga, kutoa zaka na kuishi kwa sheria. Lakini sala yake ilikuwa imejaa majivuno na hukumu dhidi ya wengine. Alijiona kuwa mwema kuliko watu wengine. Kwa upande mwingine, mtoza ushuru alisimama mbali, hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni. Aligonga kifua chake na kusema kwa unyenyekevu: “Ee Mungu, unirehemu mimi mwenye dhambi.”

Yesu anatoa hitimisho la kushangaza: yule mtoza ushuru ndiye aliyerudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki mbele za Mungu, si yule Mfarisayo. Hapa Yesu anafunua siri ya kweli ya sala. Sala ya kweli si kujisifu mbele za Mungu, bali ni kujitambua katika mwanga wa Mungu. Kadiri tunavyomkaribia Mungu, ndivyo tunavyozidi kuona udhaifu wetu na kumhitaji zaidi.

Katika maisha ya Kikristo, hatari kubwa ni kuzoea mambo ya Mungu kiasi cha kuanza kujiona wenye haki kuliko wengine. Mtu anaweza kuwa mshiriki wa ibada, mhudumu wa Kanisa au mtu anayejitahidi kuishi maisha ya dini, lakini akawa na moyo wa kujiona bora kuliko wengine. Huo ndio mtego uliomwangusha Mfarisayo katika Injili ya leo. Mungu hapendezwi na moyo wa majivuno hata k**a umejificha nyuma ya ibada nyingi.

Kwa upande mwingine, unyenyekevu wa mtoza ushuru unatufundisha kwamba Mungu yuko karibu sana na mtu anayekiri udhaifu wake. Mungu hapendezwi na dhambi, lakini anapendezwa na moyo unaotubu kwa unyenyekevu. Ndiyo maana Zaburi ya leo inasema: “Sadaka impendezayo Mungu ni roho iliyovunjika; moyo uliovunjika na kunyenyekea hutoudharau.”

Hivyo basi, tafakari ya leo inatualika tujiulize kwa uaminifu: ninaposali ninakuja kwa Mungu kwa roho gani? Je, ninakuja kumweleza Mungu mapungufu yangu na kumwomba huruma yake, au ninakuja kujilinganisha na wengine na kujiona bora kuliko wao? Sala ya kweli hutufanya tumuone Mungu katika utakatifu wake na wakati huo huo hutusaidia kuona udhaifu wetu kwa unyenyekevu.

Kwaresima ni wakati mzuri wa kujifunza tena kusali kwa moyo wa unyenyekevu. Tukijitupa mikononi mwa Mungu k**a yule mtoza ushuru, tutagundua kwamba huruma ya Mungu ni kubwa kuliko udhaifu wetu. Mungu hamkatai mtu anayekuja kwake kwa moyo wa toba na unyenyekevu.

Sala
Ee Bwana Mungu wangu, mara nyingi ninakuja mbele zako nikiwa na majivuno au kujiona mwenye haki kuliko wengine. Nipe moyo wa unyenyekevu ili nijitambue k**a mwenye dhambi anayehitaji huruma yako kila siku. Nifundishe kusali kwa moyo wa kweli na unyenyekevu ili nipate neema yako.
Yesu, nakuamini wewe. Amina. 🙏📖

MASOMO YA MISA TAKATIFU JUMAMOSI JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 14,2026SOMO 1: Hos.5:15-6:6Bwana asema: Katika taabu yao w...
14/03/2026

MASOMO YA MISA TAKATIFU JUMAMOSI JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 14,2026

SOMO 1:
Hos.5:15-6:6
Bwana asema: Katika taabu yao watanitafuta kwa bidii: Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake. Nasi na tujue, naam, tukaendelee kumjua Bwana; kutokea kwake ni yakini k**a asubuhi; naye atatujilia k**a mvua, k**a mvua ya vuli iinyeshayo nchi. Ee Efraimu, nikutendee nini? Ee Yuda, nikutendee nini? Kwa maana fadhili zenu ni k**a wingu la asubuhi na k**a umande utowekao mapema. Kwa sababu hiyo nimewakata-kata kwa vinywa vya manabii; nimewaua kwa maneno ya kinywa changu na hukumu yangu itatokea k**a mwanga. Maana nataka fadhili wala si sadaka; na kumjua Mungu kuliko sadaka za kuteketezwa.

WIMBO WA KATIKATI: Zab.51:1-2,16-19
1. Ee Mungu, unirehemu,
Sawasawa na fadhili zako.
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
Unioshe kabisa na uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu.

(K) Ninavyotaka ni fadhili, si sadaka.

2. Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,
Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;
Moyo uliovunjika na kupondeka,
Ee Mungu, hutaudharau. (K)

3. Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,
Uzijenge kuta za Yerusalemu.
Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,
Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. (K)

SHANGILIO:
Eze.18:3
Tupilieni mbali nanyi
makosa yenu yote mliyoyakosa yote,
asema Bwana,
jifanyieni moyo mpya na roho mpya.

INJILI:
Lk.18:9-14
Yesu aliwaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si k**a watu wengine, wanyang’anyi, wadhalimu, wazinzi, wala k**a huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

MAOMBI
Ee Mungu, wewe wataka fadhili na siyo sadaka; na kwamba tukujue wewe kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa. Kwa kuwa katika kipindi hiki cha Kwaresima tunahimizwa sana kuyafanya mambo hayo, twakuomba:

Kiitikio: Bwana utusikie, Bwana utusikilize.
1. Umfanye kila mmoja wetu akurudie wewe kwa moyo wake wote.

2. Waamni wote wakumbuke kuwa sala ni ya muhimu kabla na baada ya kazi au tendo lolote linalohitaji msaada wako.

3. Utupe moyo wa unyenyekevu tunaposali, ili sala zetu zisiwe na majivuno wala dharau au hukumu kwa wenzetu.

4. Waamini wako wayaenzi matendo mema k**a vile ya kufunga, kutoa zaka, na kulisaidia Kanisa kwa huduma mbalimbali.

Ee Bwana, uwe radhi kuyapokea maombi yetu. Upokee pia shukrani kwa mema unayotujalia siku zote hasa katika mfungo huu wa Kwaresima. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

MASOMO YA MISA TAKATIFU IJUMAA JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 13, 2026SOMO 1: Hos.14:1-9Bwana asema: Ee Israeli, mrudie Bw...
12/03/2026

MASOMO YA MISA TAKATIFU IJUMAA JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 13, 2026

SOMO 1:
Hos.14:1-9
Bwana asema: Ee Israeli, mrudie Bwana, Mungu wako; maana umeanguka kwa sababu ya uovu wako. Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Bwana; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng'ombe.
Ashuru hatatuokoa; hatutapanda farasi; wala hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu, Ninyi ndinyi miungu yetu; maana kwako wewe wasio na baba hupata rehema. Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha. Nitakuwa k**a umande kwa Israeli; naye atachanua maua k**a nyinyoro, na kuieneza mizizi yake k**a Lebanoni. Matawi yake yatatanda, na uzuri wake utakuwa k**a uzuri wa mzeituni, na harufu yake k**a Lebanoni. Na wao wakaao chini ya uvuli wake watarejea; watafufuka k**a ngano, na kuchanua maua k**a mzabibu; harufu yake itakuwa k**a harufu ya divai ya Lebanoni. Efraimu atasema, Mimi nina nini tena na sanamu? Mimi nimeitika, nami nitamwangalia. Mimi ni k**a mberoshi wenye majani mabichi. Kwangu mimi yamepatikana matunda yako. Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za Bwana zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.

WIMBO WA KATIKATI: Zab.81:6-10,13,16
1. Maneno yake nisiyemjua naliyasikia.
Nimelitenga bega lake na mzigo,
Mikono yake ikaachana na kikapu.
Katika shida uliniita nikakuokoa.

(K) Mimi ndimi Bwana Mungu wako,
Sikiliza sauti yangu.

2. Nalikuitikia katika sitara ya radi;
Nalikujaribu penye maji ya Meriba.
Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,
Ee Israeli, k**a ukitaka kunisikiliza. (K)

3. Usiwe na mungu mgeni ndani yako;
Wala usimsujudie mungu mwingine.
Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,
Niliyekupandisha toka nchi ya Misri. (K)

4. Laiti watu wangu wangenisikiliza,
Na Israeli angeenenda katika njia zangu;
Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano,
Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani. (K)

SHANGILIO:
Zab.95:7,8
Leo msifanye migumu mioyo yenu;
Lakini msikie sauti yake Bwana.

INJILI:
Mk.12:28-34
Mmojawapo wa waandishi alifika, akawasikia wakisemezana naye, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza? Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako k**a nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi. Yule mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye; na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani k**a nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhahibu zote pia. Naye Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, alimwambia, Wewe hu mbali na ufalme wa Mungu. Wala hakuthubutu mtu kumsaili neno tena tokea hapo.

MAOMBI
Ndugu, leo tunakumbushwa tena kuishika Amri Kuu ya Mapendo na kualikwa kumrudia Mungu kwa moyo mnyofu. Na hivi tuombe neema yake Mungu tukisema:

Kiitikio: Twakuomba utusikie.
1. Ee Mungu wetu, utujalie Kipindi hiki cha Kwaresima kituongezee ari ya kukupenda wewe zaidi ya chochote.

2. Utukumbushe daima kuwa kukupenda wewe ni kushika amri zako na kuwatendea mema jirani zetu.

3. Utudumishe katika utumishi wako mtakatifu; na kamwe tusithubutu kuanzisha au kuyaendekeza mashindano yasiyotufaa kwa wokovu.

4. Marehemu wetu wapate kitulizo na faraja kwa kuuona uso wako mtukufu huko mbinguni.

Ee Bwana Mungu, amri zako ni dira yetu na kipimo cha uaminifu wetu kwako na kwa jirani zetu. Utupe moyo wa kukupenda zaidi na zaidi. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

MASOMO YA MISA TAKATIFU ALHAMISI JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 12, 2026SOMO 1: Yer.7:23-28Naliwaamuru neno hili, nikisema...
11/03/2026

MASOMO YA MISA TAKATIFU ALHAMISI JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 12, 2026

SOMO 1:
Yer.7:23-28
Naliwaamuru neno hili, nikisema, Sikilizeni sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu; mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru, mpate kufanikiwa. Lakini hawakusikiliza, wala kutega sikio lao, bali walikwenda kwa mashauri yao wenyewe, na kwa ushupavu wa mioyo yao mibaya, wakaenda nyuma wala si mbele. Tokea siku ile baba zenu walipotoka katika nchi ya Misri hata leo, nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu ninyi, nikiamka mapema kila siku na kuwatuma. Lakini hawakunisikiliza, wala kutega sikio lao; bali walifanya shingo yao kuwa ngumu; walitenda mabaya kuliko baba zao. Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza; nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya Bwana, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali vinywa vyao.

WIMBO WA KATIKATI: Zab.95:1-2,6-9
1. Njoni, tumwimbie Bwana,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele zake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi.

(K) Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu.

2. Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba. (K)

3. Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake. (K)

4. Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu;
K**a vile huko Meriba,
K**a siku ya Masa jangwani.
Hapo waliponijaribu baba zenu,
Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)

SHANGILIO:
Zab.51:10,12
Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Unirudishie furaha ya wokovu wako.

INJILI:
Lk.11:14-23
Yesu alikuwa akitoa pepo bubu; ikawa pepo alipotoka, yule bubu akanena, makutano wakastaajabu. Wengine wao wakasema, Atoa pepo kwa Beelzebuli, mkuu wa pepo. Wengine walimjaribu, wakitaka ishara itokayo mbinguni. Naye akajua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme uliofitinika wenyewe kwa wenyewe hufanyika ukiwa; na nyumba juu ya nyumba huanguka. Basi, ikiwa Shetani naye amefitinika juu ya nafsi yake, ufalme wake utasimamaje? Kwa kuwa ninyi mnasema kwamba mimi natoa pepo kwa Beelzebuli, wana wenu je! Huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo, hao ndio watakaowahukumu. Lakini, ikiwa mimi natoa pepo kwa kidole cha Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama; lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyang’anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea, na kuyagawanya mateka yake. Mtu ambaye si pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.

MAOMBI
Ee Bwana, umependa uwe Mungu wetu na sisi tuwe watu wako. Lakini sisi tunaelekea kuukataa mwaliko huo kwa kutenda dhambi. Kwa kuwa twaukiri na kuujutia udhaifu wetu, twakuomba ukubali kuipokea sala yetu tunayokuletea tukisema:

Kiitikio: Twakuomba utusikie.
1. Uamshe ndani ya watu wako moyo wa kuisikia sauti yako inayotujia kwa njia ya manabii wako na kwa Maandiko yako Matakatifu.

2. Uwaonye wanaotafuta ishara na kumdhihaki Kristo wako, ili waukiri ukuu wake juu ya pepo wabaya.

3. Utujalie sote kumtumainia Mwanao Yesu Kristo ili, kwa nguvu yake kuu, tupate kuponywa maradhi ya kimwili na kiroho.

4. Utuimarishie imani yetu kwa Mwanao, ili tusiyumbishwe na mafundisho tofauti na potofu ya kigeni.

Utujalie hayo kwa njia ya Kristo Bwana na Mwokozi wetu daima na milele. Amina.

TAFAKARI YA MASOMO YA MISA ALHAMISI, MACHI 12, 2026Alhamisi ya Juma la 3 la KwaresimaMasomo: Yer 7:23–28; Zab 95:1–2,6–9...
11/03/2026

TAFAKARI YA MASOMO YA MISA ALHAMISI, MACHI 12, 2026
Alhamisi ya Juma la 3 la Kwaresima

Masomo: Yer 7:23–28; Zab 95:1–2,6–9; Lk 11:14–23

Utangulizi
Neno la Mungu la leo linatukumbusha ukweli mmoja muhimu katika maisha ya kiroho: Mungu anaendelea kusema na watu wake, lakini changamoto kubwa si kwamba Mungu hasemi—bali ni kwamba mara nyingi mwanadamu hasikilizi. Kipindi cha Kwaresima kinatualika kufungua tena masikio ya moyo ili tusikie sauti ya Mungu na kuiruhusu ibadilishe maisha yetu. Ndiyo maana Zaburi ya leo inasisitiza kwa nguvu: “K**a leo mtaisikia sauti yake, msifanye migumu mioyo yenu.” Huu ni mwaliko wa kuacha ukaidi na kurudi katika utii wa kweli kwa Mungu.

Katika somo la kwanza kutoka Kitabu cha Yeremia, Mungu analalamika juu ya watu wake kwa sababu wamekataa kusikiliza sauti yake. Anawakumbusha kwamba tangu mwanzo aliwaagiza jambo moja tu: wamsikilize na kufuata njia zake ili wapate uzima. Lakini badala ya kusikiliza, walifuata misukumo ya mioyo yao migumu. Hapa tunaona tatizo la msingi la dhambi—si ujinga, bali ukaidi wa moyo unaokataa kusikia ukweli wa Mungu. Mungu aliwatuma manabii mara kwa mara kuwaonya, lakini badala ya kusikiliza walizidi kuufunga moyo wao.

Injili kutoka Injili ya Luka inaonyesha wazi vita ya kiroho kati ya nguvu za Mungu na nguvu za uovu. Yesu anamponya mtu aliyekuwa bubu kwa sababu ya pepo. Mara tu pepo anapotolewa, mtu huyo anaweza kuongea tena na watu wanashangaa. Lakini badala ya kutambua nguvu ya Mungu iliyotenda ndani ya Yesu, baadhi ya watu wanamshutumu kwamba anatoa pepo kwa nguvu za mkuu wa pepo. Hii inaonyesha jinsi moyo wa mwanadamu unavyoweza kufungwa na upofu wa kiroho kiasi cha kushindwa kutambua kazi ya Mungu hata inapokuwa wazi mbele yake.

Picha ya mtu bubu katika Injili hii ina maana kubwa sana kwa maisha ya Kikristo. Ububu ule haukuwa tu tatizo la mwili bali pia ishara ya hali ya kiroho. Pepo alimfunga mtu huyo kiasi kwamba hakuweza kuzungumza. Vivyo hivyo katika maisha ya kiroho, mara nyingi yule mwovu anajaribu kuwafunga waamini kwa hofu, mashaka au aibu ili washindwe kushuhudia imani yao. Wapo Wakristo wengi wanaompenda Mungu moyoni lakini wanaogopa kuonyesha imani yao wazi katika jamii, kazini au hata ndani ya familia zao.

Katika ulimwengu wa leo kuna aina nyingi za “ububu wa kiroho.” Wapo wanaonyamaza wanapoona udhalimu kwa sababu wanaogopa kupoteza nafasi zao. Wapo wanaoona maadili ya Kikristo yakidharau lakini hawathubutu kusema ukweli. Wapo wazazi wanaojua wajibu wao wa kuwalea watoto katika imani lakini wananyamaza kwa sababu ya shughuli nyingi au hofu ya kukosolewa. Huo nao ni ububu unaotufanya tushindwe kuwa mashahidi wa Injili.

Lakini Injili ya leo inatupa tumaini kubwa: Yesu ana nguvu ya kutufungua. K**a alivyomfungua yule mtu aliyekuwa bubu, anaweza pia kutufungua sisi kutoka katika hofu na mashaka yanayotufanya tunyamaze. Yesu anataka Wakristo wawe watu wa ujasiri, wanaotangaza ukweli kwa upendo na ushuhuda wa maisha yao. Ukristo hauwezi kuishi katika ukimya wa woga; unaitwa kuangaza k**a nuru katikati ya dunia.

Hivyo basi, Kwaresima ni wakati wa kujiuliza kwa uaminifu: je, mimi nimefungwa na “ububu wa kiroho”? Je, ninaogopa kushuhudia imani yangu? Tukimruhusu Kristo afanye kazi ndani yetu, atatupa ujasiri wa kusema na kuishi ukweli wa Injili bila woga. Na kwa kufanya hivyo tutakuwa vyombo vya Mungu vinavyoleta nuru, matumaini na wokovu kwa wengine.

Sala:
Ee Bwana Yesu, mara nyingi hofu na mashaka hunifanya ninyamaze ninapopaswa kushuhudia ukweli wako. Nakuomba unifungue kutoka katika ububu wa kiroho na unipe ujasiri wa kutangaza neno lako kwa upendo na uaminifu. Nifanye niwe chombo cha amani na mwanga wako katika ulimwengu huu. Amina. 🙏📖

MASOMO YA MISA TAKATIFU JUMANNE JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 10, 2026SOMO 1: Dan.3:25,34-43Ndipo Azaria akasimama akasal...
09/03/2026

MASOMO YA MISA TAKATIFU JUMANNE JUMA LA 3 LA KWARESIMA MACHI 10, 2026

SOMO 1:
Dan.3:25,34-43
Ndipo Azaria akasimama akasali hivi, akifumbua kinywa chake katikati ya moto na kusema: Usituache kabisa, kwa ajili ya jina lako, wala usilitangue agano lako na kutuondolea rehema zako, kwa ajili ya Ibrahimu umpendaye, na kwa ajili ya Isaka mtumishi wako, na Israeli mtakatifu wako k**a nyota za mbinguni na k**a mchanga wao pwani. Maana sisi, Ee Bwana, tumekuwa duni kuliko mataifa yote, na kudhulumiwa leo katika ulimwengu wote kwa sababu ya dhambi zetu. Sasa hakuna mfalme wala nabii wala kiongozi; hakuna dhabihu wala kafara wala sadaka wala uvumba; wala mahali pa kukutolea dhabihu na kuona rehema. Lakini kwa moyo uliovunjika na kwa roho nyenyekevu tukubaliwe nawe, na sadaka yetu iwe machoni pako leo k**a dhabihu za kondoo waume na ng’ombe, na k**a kondoo wanono elfu kumi. Nasi tukufuate kwa unyofu, maana wanaokutumaini Wewe hawataaibika. Na sasa tunakufuata kwa moyo wote; tunakucha na kuutafuta uso wako. Usitufedheheshe, bali ututendee kwa kadiri ya fadhili zako, sawasawa na wingi wa huruma zako. Utuokoe kwa kadiri ya maajabu yako, na kulitukuza jina lako, Ee Bwana.

WIMBO WA KATIKATI: Zab.25:4-9
1. Ee Bwana unijulishe njia yako,
Unifundishe mapito yako,
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha.

(K) Ee Bwana,
kumbuka rehema zako na fadhili zako.

2. Ee Bwana kumbuka rehema zako na fadhili zako,
Maana zimekuwako tokea zamani.
Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu,
Wala maasi yangu.
Ee Bwana, kwa ajili ya wema wako. (K)

3. Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
Wenye upole atawaongoza katika hukumu,
Wenye upole atawafundisha njia yake. (K)

SHANGILIO:
Yn.11:25,26
Mimi ndimi ufufuo na uzima,
asema Bwana;
Yeye aniaminiye mimi,
hatakufa kabisa na milele.

INJILI:
Mt.18:21-35
Petro alimwendea Yesu akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini. Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake. Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi. Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyonavyo, ikalipwe ile deni. Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni. Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia; akamk**ata, akamshika koo, akisema, Nilipe uwiwacho. Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni. Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka. Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nimekusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi; nawe pia haikukupasa kumrehemu mjoli wako, k**a mimi nilivyokurehemu wewe? Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapolipa deni ile yote. Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.

MAOMBI
Wapendwa katika Kristo, Mungu ni mwenye huruma kwa wakosefu na anataka sisi tuwe tayari kuwasamehe wenzetu. Tunahitaji msaada wa Mungu, ili kulitekeleza hilo. Kwa hiyo, tuombe: Ee Mungu Mwenyezi, twakuomba:-

Kiitikio: Pokea ombi letu.
1. Viongozi wetu wa Kanisa wazidi kuhubiri toba huku wakiwatangulia waamini kwa kuziungama dhambi zao wenyewe.

2. Uwajalie waamini wote kuitikia mwaliko wa toba tunaohimizwa katika mfungo huu wa Kwaresima.

3. Utupe moyo wa kuwasamehe wenzetu makosa yao na kuwatendea mema k**a sisi wenyewe tunavyotamani kutendewa nao.

4. Uwahurumie wote wanaodhulumiwa na kunyanyasika sababu ya unyonge wao; na uwatetee kadiri ya mapenzi yako.

Ee Baba Mwema, tunakushukuru kwa nafasi hii ya mfungo wa Kwaresima, ambayo yatupatia fursa ya kuzitafakari njia zetu na kuunganika zaidi nawe. Utuimarishe katika upendo wako. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

📖ELIMU YA KANISASOMO LA TEOLOJIAMADA: THEOLOGIA BAPTISMI (Theolojia ya Ubatizo)Br. Michael Daniel Kitabagala OSBUTANGULI...
05/03/2026

📖ELIMU YA KANISA

SOMO LA TEOLOJIA

MADA: THEOLOGIA BAPTISMI (Theolojia ya Ubatizo)

Br. Michael Daniel Kitabagala OSB

UTANGULIZI

Baada ya kujifunza kwamba Kanisa ni Sacramentum Universale Salutis (Sakramenti ya ulimwengu ya wokovu), sasa tunaingia katika Sakramenti ya kwanza na ya msingi kabisa:

UBATIZO

Ubatizo ni:

> Ianua Sacramentorum
(Mlango wa Sakramenti zote)

>Hakuna Sakramenti nyingine inayoweza kupokelewa bila Ubatizo.

Katika mpangilio wa Seminari Kuu, Theolojia ya Ubatizo inachunguza:

●Msingi wa Kibiblia

●Maendeleo ya kihistoria

●Kiini chake cha kisakramenti

●Athari zake za neema

Masuala ya wokovu yanayohusiana nayo

■ MSINGI WA KIBIBLIA

(a) Agano la Kale

Ubatizo una vielelezo (Typologia – mifano ya awali) katika:

Gharika ya Nuhu (maji k**a utakaso)

Kuvuka Bahari ya Shamu

Kutahiriwa k**a ishara ya agano

Haya yalikuwa maandalizi ya Sakramenti halisi.

(b) Agano Jipya

Yesu Kristo:

Alibatizwa katika Mto Yordani

Aliamuru: “Enendeni mkawabatize mataifa yote…”

Alisema: “Mtu asipozaliwa kwa maji na Roho hawezi kuingia Ufalme wa Mungu.”

Hapa tunaona wazi:

>Ubatizo si desturi ya kibinadamu, bali amri ya Kristo.

■MAANA YA KISAKRAMENTI

Ubatizo ni:

> Sacramentum regenerationis
(Sakramenti ya kuzaliwa upya)

Ni kuzaliwa kwa maji na Roho.

Kwa Ubatizo mtu:

Anaoshwa dhambi ya asili (Peccatum originale – dhambi ya asili)

>Anaingizwa katika Mwili wa Kristo

>Anakuwa mtoto wa Mungu

>Anapokea neema ya utakaso (Gratia sanctificans – neema ya kutakatifuza)

■MATTER NA FORM

Matter (Materia – Kitu kinachotumika)

Maji ya asili.

Form (Forma – Maneno rasmi)

“Ninakubatiza kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.”

Bila maji halisi au bila maneno sahihi ya Utatu Mtakatifu, Ubatizo si halali.

■ MINISTER NA INTENTION

Minister (Mhudumu)

Kwa kawaida ni:

●Askofu

●Padri

●Shemasi

●Lakini katika hali ya dharura, mtu yeyote anaweza kubatiza ikiwa:

Ana nia (Intentio – kusudi la ndani) ya kufanya kile Kanisa linachofanya

Anatumia maji na maneno sahihi

Hii inaonyesha umuhimu wa Ubatizo kwa wokovu.

■EX OPERE OPERATO

Ubatizo hutenda kazi:

> Ex opere operato
(Kwa tendo lenyewe lililofanywa)

Neema haitokani na utakatifu wa mhudumu, bali na Kristo anayefanya kazi kupitia Sakramenti.

Hata hivyo, matunda yake yanategemea pia:

> Ex opere operantis
(Kwa jinsi mpokeaji alivyojiandaa)

Kwa mtoto mchanga, imani ya Kanisa inamwakilisha.

■ ATHARI ZA UBATIZO

Ubatizo huleta:

1. Msamaha wa dhambi

Dhambi ya asili na dhambi zote binafsi (ikiwa ni mtu mzima).

2. Neema ya kutakatifuza

Kumfanya mtu mshiriki wa maisha ya Mungu.

3. Character indelebilis

(Alama ya kiroho isiyofutika)

Ubatizo hauwezi kurudiwa kamwe.

4. Kujiunga na Kanisa

Mtu anakuwa sehemu ya Mwili wa Kristo.

■UBATIZO NA WOKOVU

Kanisa linafundisha:

> Baptismus est necessarius ad salutem
(Ubatizo ni muhimu kwa wokovu)

Lakini pia linafundisha uwezekano wa:
>Baptismus flaminis (Ubatizo wa tamanio – hamu ya ndani ya kubatizwa)

>Baptismus sanguinis (Ubatizo wa damu – kifo cha kishahidi kabla ya kubatizwa)

Hii inaonyesha rehema ya Mungu inayozidi mipaka ya ishara inayoonekana.

■ UBATIZO WA WATOTO

Swali la kitheolojia:
Kwa nini kubatiza watoto wasio na dhambi binafsi?

Jibu:

●Wanarithi dhambi ya asili

●Wanaingizwa katika agano jipya

●Imani ya wazazi na Kanisa inawawakilisha

Hii ina mizizi yake katika Kanisa la Mitume.

■UBATIZO NA MAADILI

Ubatizo si tukio la siku moja.

Ni mwanzo wa:

¤Maisha ya neema

¤Wito wa utakatifu

¤Uwajibikaji wa Kikristo

Ubatizo unaweka msingi wa Maadili ya Kikristo tutakayojifunza baadaye katika Moral Theology

Hivyo nimalize kwa kusema kuwa
Ubatizo ni:
>Mlango wa Sakramenti zote
>Msingi wa ukuhani wa waamini
>Mwanzo wa maisha ya neema
>Muhuri wa milele wa kumilikiwa na Kristo
>Ni kuzaliwa kwa maisha mapya ndani ya Kanisa.

SIKU NJEMA

ELIMU YA KANISA – SOMO LA TEOLOJIAMADA YA SABA: LITURUJIA (LITURGICS)Asili, Maana na Maadhimisho ya Ibada ya KanisaImean...
03/03/2026

ELIMU YA KANISA – SOMO LA TEOLOJIA

MADA YA SABA: LITURUJIA (LITURGICS)

Asili, Maana na Maadhimisho ya Ibada ya Kanisa

Imeandaliwa na Br. Michael Daniel Kitabagala OSB

Mafundisho Mahususi kwa Njia ya Mitandao

UTANGULIZI

Baada ya kujifunza juu ya wokovu na neema, sasa tunafika mahali ambapo wokovu huo unaishiwa na kuadhimishwa:

> Liturujia ni nini, na kwa nini ni muhimu?

Liturujia si mkusanyiko wa taratibu za ibada tu.
Ni tendo takatifu ambalo Kristo mwenyewe anaendelea kulifanya ndani ya Kanisa.

Kwa maneno rahisi:

> Liturujia ni ushiriki wa Kanisa katika kazi ya Kristo ya kuokoa.

Ndiyo moyo wa maisha ya Kanisa.

■ MAANA YA LITURUJIA

Neno “Liturujia” linatokana na neno la Kigiriki leitourgia linalomaanisha:

> Huduma ya hadhara au kazi kwa ajili ya watu.

Katika Kanisa, Liturujia ni:
>Ibada rasmi ya Kanisa
>Maadhimisho ya fumbo la wokovu
>Kazi ya Kristo na Mwili wake (Kanisa)
>Kristo ndiye mhudumu mkuu wa Liturujia.
>Padre anahudumu katika nafsi ya Kristo.

■ ASILI YA LITURUJIA
Liturujia ina mizizi yake katika:
▪︎Ibada ya Agano la Kale
▪︎Pasaka ya Wayahudi
▪︎Maisha na mafundisho ya Yesu Kristo

Kristo alianzisha Ekaristi katika Karamu ya Mwisho.
Hapo ndipo msingi wa Liturujia ya Kikristo uliwekwa.

Baada ya Ufufuko, Mitume waliendelea kuadhimisha “kuumega mkate” k**a ibada ya Kanisa la kwanza.

■SAKRAMENTI K**A ISHARA ZA NEEMA

Sakramenti ni:

> Ishara zinazoonekana zinazoleta neema isiyoonekana.

Kanisa lina Sakramenti saba:
1. Ubatizo
2. Kipaimara
3. Ekaristi
4. Kitubio
5. Mpako wa Wagonjwa
6. Daraja Takatifu
7. Ndoa

Katika Sakramenti:
▪︎Kristo anatenda
▪︎Neema inatolewa
▪︎Wokovu unagusa maisha ya mwanadamu

■EKARISTI – KIINI CHA LITURUJIA
Ekaristi ni:
>Sadaka ya Msalaba inayofanywa hai
>Chakula cha kiroho
>Ishara ya umoja wa Kanisa

Katika Misa Takatifu:
▪︎Tunashiriki katika sadaka ya Kristo

▪︎Tunapokea Mwili na Damu ya Bwana

▪︎Tunajengwa k**a Mwili mmoja wa Kristo

Ekaristi si kumbukumbu ya kihistoria tu — ni uwepo halisi wa Kristo.

Ndiyo “chemchemi na kilele” cha maisha ya Kanisa.

■MWAKA WA KILITURUJIA
Kanisa huishi fumbo la Kristo katika mwaka wa kiliturujia:

🟣Majilio

⚪️🟡Krismasi

🟣Kwaresma

⚪️🟡Pasaka

🟢Kipindi cha Kawaida

Huu si mzunguko wa kalenda tu, bali ni safari ya kiroho ya kukua katika fumbo la Kristo.

■ LITURUJIA NA MAISHA YA KILA SIKU

Liturujia haimaliziki kanisani.
Inapaswa:
¤Kubadilisha maisha yetu
¤Kutufanya watu wa sala
¤Kutufanya mashahidi wa Kristo
¤Ibada bila mabadiliko ya maisha ni tupu.
¤Liturujia ya kweli huzaa matunda ya upendo.

■UMUHIMU WA LITURUJIA LEO

Katika dunia ya leo:
▪︎Wengine huona ibada k**a desturi
▪︎Wengine huona Misa k**a wajibu
▪︎Wengine hupuuza Sakramenti

Lakini Liturujia ni mahali ambapo:
●Mbingu inagusa dunia
●Wokovu unakuwa halisi
●Kristo anakuwa karibu nasi
●Ni pumzi ya roho ya Kanisa.

Nimalize kwa kusema haya,
Kila Misa Takatifu, Kristo yuko hai.
Si hadithi ya zamani.
Si kumbukumbu tu.
Ni tukio la wokovu linaloendelea.

Tunaposhiriki Liturujia:
●Tunaingia katika fumbo la Kristo
●Tunaguswa na neema
●Tunajiandaa kwa uzima wa milele

Liturujia ni daraja kati ya muda na umilele.
Na swali ni: Je, tunaishi tunachoadhimisha?
Kwa sababu Mkristo wa kweli si anayehudhuria Liturujia tu — bali anayeishi Liturujia.

Nikutakie Siku Njema

MASOMO YA MISA DOMINIKA YA 1 KWARESIMA MWAKA A, 22 FEBRUARI 2026ANTIFONA YA KUINGIA: Zab.91:15-16Ataniita nami nitamwiti...
21/02/2026

MASOMO YA MISA DOMINIKA YA 1 KWARESIMA MWAKA A, 22 FEBRUARI 2026

ANTIFONA YA KUINGIA: Zab.91:15-16
Ataniita nami nitamwitikia; nitamwokoa na kumtukuza, kwa siku nyingi nitamshibisha.

KOLEKTA:
Ee Mungu mwenyezi, utujalie tuzidi kulifahamu fumbo la Kristo, kwa njia ya mazoezi ya kipindi cha Kwaresima tunachojaliwa kila mwaka. Na kwa njia hiyo, tuyafuate yale yanayotokana na fumbo hilo, kwa mienendo inayostahili. Kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo Mwanao, anayeishi na kutawala nawe katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu, milele na milele.

SOMO 1:
Mwa.2:7-9,3:1-7
Bwana Mungu alimfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya. Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu: Msile matunda ya miti yote ya bustani? Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa k**a Mungu, mkijua mema na mabaya. Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.

WIMBO WA KATIKATI: Zab.51:1-4,10-12,15
1. Ee Mungu, unirehemu,
Sawasawa na fadhili zako.
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
Unioshe kabisa na uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu.

(K) Uturehemu, ee Bwana,
Kwa kuwa tumetenda dhambi.

2. Maana nimejua mimi makosa yangu,
Na dhambi yangu i mbele yangu daima.
Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,
Na kufanya maovu mbele za macho yako. (K)

3. Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.
Usinitenge na uso wako,
Wala roho wako mtakatifu usiniondolee. (K)

4. Unirudishie furaha ya wokovu wako;
Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,
Na kinywa changu kitazinena sifa zako. (K)

SOMO 2:
Rum.5:12-19
K**a kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi. Maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria; walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja. Lakini karama ile haikuwa k**a lile kosa; kwa maana ikiwa kwa kukosa kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema yake mwanadamu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale wengi. Wala kadiri ya yule mtu mmoja aliyefanya dhambi si kadiri ya kile kipawa; kwa maana hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja ikaleta adhabu; bali karama ya neema ilikuja kwa ajili ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki. Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. Basi tena, k**a kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima. Kwa sababu k**a kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki.

SHANGILIO:
Mt.4:4
Mtu hataishi kwa mkate tu,
ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

INJILI:
Mt.4:1-11
Baada ya kubatizwa, Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi. Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa. Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. Naye akajibu akasema, Imeandikwa: Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa: Atakuagizia malaika zake; na mikononi mwao watakuchukua; usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. Yesu akamwambia, Tena imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa: Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.

Injili ya Bwana, Sifa kwako Ee Kristo

Nasadiki husemwa.

MAOMBI
Yesu alipangiwa na Mungu Baba kutuletea ukombozi. Shetani alimkaribia Yesu ili amshawishi kumwasi Baba yake na kuchagua njia ya ukombozi inayopingana na mpango wa Mungu.

1. Ee Bwana Yesu, ulishawishiwa kutumia nguvu ya kimungu kwa ubinafsi: Utufungue macho yetu ili tutambue kwamba hatuishi kwa mambo ya dunia tu, ila kwa baraka za Mungu Baba.

2. Ee Bwana Yesu, ulishawishiwa kuchagua njia ya siasa ili kutukomboa. Utufundishe kutambua kwamba Ufalme wa Mungu si ufalme wa kupigania mamlaka na madaraka, bali ni kutimiza amri zako.

3. Ee Bwana Yesu, ulishawishiwa kutegemea umungu wako ili kujionesha k**a mkubwa. Utusaidie tutambue kwamba imani yetu inatufundisha kuvumilia shida za duniani ili kustahili tuzo ya mbinguni.

4. Ee Bwana Yesu, ulimpinga mshawishi kwa imani imara kabisa: Utuimarishe kwa nguvu ya imani ili tuweze kushinda vishawishi tunavyokumbana navyo hasa tamaa ya madaraka na mali.

5. Ee Bwana Yesu, ulisema kwamba hakuna mtu atakayeshawishiwa kupita nguvu zake. Utusaidie tunapokuwa katika hatari za vishawishi na utuimarishe kwa nguvu yako tuvishinde.

Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu.

SALA YA KUOMBEA DHABIHU:
Ee Bwana, tunakuomba utufanye tustahili kukutolea inavyofaa vipaji hivi, vinavyotusaidia kuadhimisha mwanzo wa kipindi hiki kitakatifu cha Kwaresima. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.

UTANGULIZI
Kujaribiwa kwa Bwana
K. Bwana awe nanyi.
W. Na awe rohoni mwako.
K. Inueni mioyo.
W. Tumeiinua kwa Bwana.
K. Tumshukuru Bwana Mungu wetu.
W. Ni vema na haki.

K. Kweli ni vema na haki, tendo la kufaa na la kuleta wokovu, tukushukuru wewe daima na popote, ee Bwana, Baba uliye mtakatifu, Mungu mwenyezi wa milele, kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
Yeye kwa siku arobaini alijinyima chakula cha kidunia, akaonesha hivyo namna ya kufanya kitubio. Yeye, kwa kupindua hila zote za nyoka wa kale, alitufundisha kushinda chachu ya uovu, ili kwa kuadhimisha fumbo la Pasaka kwa mioyo inayostahili, hatimaye tuifikie Pasaka ya milele.
Kwa hiyo, sisi pamoja na umati wa Malaika na Watakatifu, tunakuimbia utenzi wa sifa, tukisema bila Mwisho.
Mtakatifu, Mtakatifu,Mtakatifu, Bwana Mungu wa majeshi.

ANTIFONA YA KOMUNYO: Mt.4:4
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

AU: Zab.91:4
Bwana atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio.

SALA BAADA YA KOMUNYO:
Ee Bwana, tumekula mkate wa mbinguni unaolisha imani, kuhamasisha tumaini na kuyatia nguvu mapendo. Tunakuomba, tujifunze kumtamani Yeye aliye mkate hai na wa kweli, na tuweze kuishi kwa kila neno litokalo kinywani mwako. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.

SALA YA KUWAOMBEA WAAMINI:
Ee Bwana, tunakuomba baraka yako iwashukie kwa wingi watu wako; ili, palipo na taabu, matumaini yaongezeke; palipo na kishawishi, nguvu ithibitishwe; na wajaliwe wokovu wa milele. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.

Address

Peramiho

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when OSB FAITH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share