13/12/2025
TAFAKARI YA DOMINIKA YA 3 YA MAJILIO – GAUDETE
SOMO LA KWANZA – ISAYA 35:1–6, 10
SOMO LA PILI – YAKOBO 5:7–10
INJILI – MATHAYO 11:2–11.
UTANGULIZI WA MISA
Ndugu wapendwa katika Kristo, leo tunaadhimisha Dominika ya 3 ya Majilio, dominika inayojulikana pia k**a “Gaudete” Furahini” (rej. Flp 4:4), kwa sababu Liturujia inatualika kuona kwamba ujio wa Bwana uko karibu sana. Katika kipindi hiki cha Majilio, tunangoja kwa matumaini, toba, na subira. Na leo katika Maandiko matakatifu hasa somo la kwanza linatufariji kwamba Mungu anageuza jangwa kuwa bustani, Isaya anatuambia, atageuza huzuni kuwa furaha, kilio kuwa kicheko (Is 35:1), katika somo la injili tunasikia Yesu anatenda matendo ya kimasihi huu ni ushuhuda wa Yesu kwa utume wake wa Kimasiha, (Mt 11:5), na katika somo la pili Kanisa linaitwa kusubiri ujio wa Bwana kwa moyo thabiti na uvumilivu mfano wa subira ya mkulima tunapewa mwito na Yakobo Mtume kuwa subira tukisubiri ukamilifu wa wokovu. (Yak 5:7–10).
“FURAHINI: MUNGU ANAKUJA KUHUISHA MIOYO YETU ILIYOKAUKA”
Katika somo la kwanza Nabii Isaya anatupatia picha yenye nguvu sana ya mabadiliko ambayo Mungu analeta anapokuja kututembelea. Anaonyesha dunia iliyokauka na jangwa lililokufa likianza kuchanua maua na kuimba kwa furaha (rej Isaya 35:1–2). Taswira hii inawakilisha mioyo yetu ambayo mara nyingi imekauka kwa sababu ya huzuni, hofu, dhambi au kukata tamaa. Lakini Mungu akija katika maisha ya mtu, jangwa linageuka kuwa bustani. Kumbe hii ni lugha ya kinabii lugha ya picha Jangwa linachanua maua jangwa ni sehemu kame isio na maji ni sehemu isiyoweza kustawisha mazao kumbe ukavu na ukame wa sehemu hii katika ugumu wa mioyo yetu nabii isaya inayoonyesha kwamba Mungu anageuza mahali pa ukiwa kuwa ishara ya uzima mpya. Ni taswira ya wokovu wa Mungu unaoingia katika ulimwengu uliochoshwa na dhambi na mateso.
Nabii anaendelea kusema kwamba mikono iliyolegea na magoti yaliyoanguka yatiwe nguvu (rej. Is 35:3–4). Hapa tunaitwa tusisimame katika woga au uchovu tusiwe na hofu, bali tuinuliwe na tumaini jipya, kwa sababu Mungu mwenyewe anakuja kutuokoa. Kukata tamaa kuishiwa nguvu njiani, kuugua, kujikwaa na kuanguka vyote hivi ni magoti yaliyo legea ni sehemu ya maisha sasa tuna tiwa nguvu na kuimarishwa kwa neno la Mungu watu wasiogope. Mungu anakuja kuokoa si kwa uharibifu, bali kwa upendo na faraja kwa ufupi masiha anakuja kutuokoa na anakuja kutookoa kivipi hapa tunaona akifanya matendo makuu ya Mungu hizi ni Ishara za ukombozi wake ni zile zile ambazo Yesu baadaye atazitaja katika somo la injili Vipofu wanaona, viziwi wanasikia, viwete wanaruka, na ulimi wa bubu wafunguka. Hizi ndizo ishara ambazo Yesu atazitaja moja kwa moja kuwa uthibitisho wa utume wake wa Kimasiha (Mt 11:5). Haya ni matendo yanayodhihirisha kwamba Masiha amefika, na dunia inaanza kubadilika. Hatimaye Isaya anafunga kwa kusema kuwa waliokombolewa wa Bwana watarejea kwa furaha ya milele juu ya vichwa vyao, hawa ni watu wa Mungu watarudi “kwa furaha ya milele juu ya vichwa vyao”, Waliokombolewa watarudi kwa furaha; taswira ya ukombozi wa mwisho, kuingia katika uzima wa milele. Ni picha ya Kanisa likisafiri kuelekea wokovu wa mwisho ( Is 35:10). Kwa hivyo, somo hili linatangaza: Mungu anakuja na ujio wake unabadilisha maisha yaliyokauka maisha yalwalio kata tamaa kuwa maisha yenye uzima, matumaini na amani na furaha ya milele.
Katika somo la Injili inatuingiza katika swali la Yohana Mbatizaji, ambaye akiwa gerezani anasikia habari za Yesu na anatuma wanafunzi wake kuuliza k**a kweli Yeye ndiye ajaye (rej. Mt 11:2–3). Katika maisha ya imani, kuna nyakati tunahitaji ushahidi wa hoja (facts, reasoning,and explanations) ili kuwahakikishia watu ukweli fulani. Lakini pia kuna nyakati ambapo matendo yenyewe ndiyo yanakuwa ushahidi mkuu na wa kutosha kuonyesha ukweli kuliko maneno yoyote. Katika Injili ya leo tunaona tofauti hii ikifunuliwa kupitia tukio la Yohane Mbatizaji akiwa gerezani.
swali la utambulisho, la kutaka kujua Masihi anayekuja ni nani ni yupi swali ni linalohitaji fact, ufafanuzi, au hoja ya moja kwa moja: Je, Yesu ni Masihi? Je, ndiye aliyeahidiwa na manabii? Je, ni Yule tuliyeandaliwa kumpokea? Kwa mantiki au fikra ya kibinadamu, tungedhani Yesu angemjibu moja kwa moja Yohana mbatizaji “Ndiyo, Mimi ndiye Masihi.” au“Ndio, ndivyo”. Lakini Yesu hafanyi hivyo. Jibu la Yesu: Ukweli Waonyeshwa Kwa Matendo (Mt 11:4–5) Yesu hajibu kwa hoja, ila kwa matendo yanayoonekana: kuna wakati mwingine acha matendo yako yakutambulishe wewe ni nani au unanafasi gani kati ya watu. Ukristu wetu utambulikane kwa matendo yetu. Jibu la Yesu nila vitendo Yesu hajibu kwa maneno, bali kwa matendo. Anawambia wakamwambie Yohana kwamba “Vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.” (Mt 11:4–5) Haya ni matendo ya Masiha yaliyotabiriwa na nabii Isaya akionyesha kuwa utume wake hauna shaka: Yeye ndiye Masiha wa Mungu. Lakini pia anatoa onyo: “Heri asiyekwazwa nami” (rej. Mt 11:6). Ina maana kwamba wengi wanamkataa Yesu kwa sababu wanatarajia Masiha wa nguvu za kijeshi, wa mlipuko na mabavu, mtizamo hasi wa ujio wa masihi wapo waliofikiri kwa mtazamo wa kidunia hapa Yesu anawaonya wale wanaotaka utawala wa kimabavu, wa kisiasa, au wa miujiza ya kutisha. Ufalme wa Mungu unakuja kwa unyenyekevu na huruma. (rej Isa 35:5–6; 61:1).
Kwa hiyo Yesu anasema kwa kifupi: “Angalia matendo yangu. Ndiyo ushahidi wa mimi ni nani.” Yesu hana haja ya kujitetea kwa maneno kwa sababu kazi zake tayari zinajitetea zenyewe zina mtambulisha kuwa yeye ni nani. Mwisho wa injili tunaona hapa Yesu anajibu moja kwa moja kwa kurejea unabii wa Isaya, Yesu anamsifu Yohana, akisema kuwa si mwanasiasa anayetikiswa na upepo, si mtafuta starehe, bali ni nabii na zaidi ya nabii ndiye mjumbe wa Mungu aliyeahidiwa katika Malaki 3:1.
Hata hivyo, Yesu anaongeza kuwa aliye mdogo katika Ufalme wa Mungu ni mkubwa kuliko Yohana (rej. Mt 11:11), akionyesha ukuu wa neema waliyopewa wanaomwamini Kristo na kupokea wokovu wake kikamilifu.
Mtume Yakobo katika somo la pili anatufundisha namna ya kusubiri ujio huu wa Bwana. Tusimame imara Maana Ujio wa Bwana umekaribia anatupa mfano wa subiri ya mkulima , uvumilivu huu wa mkulima Anatuambia tuwe na subira k**a mkulima anayesubiri mvua ya mapema , mvua za mwanzo aweze kupanda kabla ya mavuno, ndivyo Mkristo anavyosubiri ujio wa Bwana. Hii ni subira hai, si uvivu. Huu ni mwito wa kutangaza kwamba ujio wa Kristo haupaswi kutia hofu, bali kututia nguvu za kuvumilia, kuacha manung’uniko na kuishi kwa amani, kwa sababu “Hakimu amesimama mlangoni” (rej. Yak 5:9). Kauli hii inarejea pia sehemu hii ya maandiko (Mt 24:33; Fil 4:5; Ufu 22:12).
Wakristo wa kwanza waliishi kwa matumaini hai ya kurejea kwa Kristo.Yakobo anatutia moyo kwa kutukumbusha mifano ya manabii waliovumilia mateso kwa ajili ya ukweli walipitia majaribu kadhaa waliteswa kwa kuhubiri ukweli lakini walikuwa wavumilivu hawakukata tamaa Waamini nao wanahimizwa au tunahimizwa tusikate tamaa tunapopitia majaribu. (rej. Mat 5:12; Ebr 11:32–38).
(rej. Yak 5:10).
Kwa hiyo Majilio yanakuwa si kipindi cha kukaa tu bali ni kipindi cha kusimama imara, kuacha fitina, na kuishi katika uaminifu, tukitazama mbele kwa macho ya matumaini. Hivyo, somo hili linatufundisha: Majilio si kusubiri kwa hofu, bali kwa matumaini yenye subira, tukiishi katika uadilifu na upendo.
Mwisho
Hivyo tunapoadhimisha Leo, Dominika ya Furaha (Gaudete), tunaalikwa kuangalia tena safari yetu ya Majilio kwa macho ya matumaini. Mungu anayeelezwa na Nabii Isaya si Mungu wa mbali, bali ni Mungu anayekuja kubadilisha maisha yetu jangwa la mioyo kuwa bustani yenye uzima. Ni Mungu anaekuja kubadilisha mioyo yetu .k**a Yesu, katika Injili, anatufundisha na kutukumbusha kwamba utambulisho wa Masiha hauhitaji maneno mengi bali matendo yake yenyewe yanatangaza ukweli wake. Vipofu kuona, viwete kutembea, wenye ukoma kutakaswa, maskini kuhubiriwa hivi ndivyo vitambulisho vya ufalme unaokuja kwa unyenyekevu na huruma, si kwa mabavu ya kidunia.
Na mwisho Mtume Yakobo anatukumbusha kwamba safari ya imani ni k**a mkulima anayesubiri mvua:kuna mvua za mwanzo kwa ajili ya kupandia mbegu na mvua za mwisho kwa ajili ya kustawisha na hatimae mavuno hivyo imani inahitaji subira, moyo thabiti, na kutovunjika moyo. Katika kipindi hiki cha Majilio, Bwana anatuambia tuondoe manung’uniko, tufanye mema, tuishi kwa amani, na tusubiri ujio wake kwa matumaini hai. Ujio wa Bwana si sababu ya kuogopa, bali chanzo cha faraja, nguvu, na furaha ya kweli.
Hivyo, na iwe furaha ya Majilio iguse maisha yetu: tuache Bwana abadilishe mioyo iliyokauka, atuinue kutoka udhaifu wetu, na kutufanya watu wa matumaini, watu wa mwanga, na watu wa Ufalme unaokuja. Amen.