St.Benedict's Abbey Peramiho

St.Benedict's  Abbey Peramiho Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from St.Benedict's Abbey Peramiho, Convent and monastery, P. O. PERAMIHO, Peramiho.

Monastery founded as a mission station in 1898 Eerected as Abbatia Nullius on 23 December 1931
Raised to Diocese of Songea and reduced to status as simple Abbey on 6 February 1969

02/05/2026

Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Mei 3, 2026
Juma la 5 la Pasaka
Mdo 6: 1-7;
Zab 32: 1-5, 18-19;
1 Pet 2: 4-9;
Yn 14: 1-12.
MIMI NI NJIA, UKWELI NA UZIMA
Je umekombolewa? “ndio” tumekombolewa kwa njia tatu: tumekombolewa kwa njia ya neema ya Ubatizo, tunaendelea kukombolewa kwa njia ya neema za Mungu na huruma tunapo amua kumfuata kwa uhuru kamili, na tunatumaini kokombolewa na kuingia katika utukufu wa Mbinguni.
Imekuwaje tumepokea zawadi ya thamani ya ukombozi? Kwa njia ya maisha, mateso kifo na ufufuko wa Yesu Kristo ambaye ndiye pekee aliye njia ya kwenda kwa Baba. Njia pekee ya Ukombozi ni Yesu. Hivyo Yesu Kristo anapaswa kuwa kiini cha maisha yetu, na tunapaswa kumuona k**a njia, ukweli na uzima. Yeye ni njia pekee ya Mbinguni, yeye ni utimilifu wa ukweli wote ambao tunapaswa kuuamini, na yeye ni uzima ambao tunapaswa kuuishi na yeye ndiye chanzo cha maisha mapya ya neema. Bila yeye sisi si kitu, bali kwa njia yake unapata maisha makamilifu.
Katika somo la pili, Petro analifananisha Kanisa na jengo la kiroho ambalo mjenzi ni Mungu na mawe yanayoishi ni watu. Msingi ulianza kwa mawe imara kwa jengo lote, Kristo ambaye juu yake Mungu ameweka pia mawe mengine, wale wanao mwamini yeye. Wakiwa wameunganika na Yesu, wanatengeneza hekalu moja la Mungu.
Injili inamuonesha Yesu k**a kielelezo cha maisha ‘njia, ukweli na uzima’. Kiini cha ukristo ni Kristo mweyewe. Kazi yetu kwa Yesu na upendo wetu kwa watu, haijalishi tumeitwa katika maisha ya namna ghani, maisha yetu yanatiririka kutoka katika chanzo hiki. Mama Teresa aliulizwa kwanini alifanya aliokuwa akifanya, na alijibu tu “ni kwa ajili ya Yesu”. Hiki ndicho kiini kinacho shikilia ili kusiwe na mtikizo au usumbufu wowote. Ni muunganiko wa ndani na Yesu. Kusoma maisha yake, kupata muda wa kutambua mazingira yake na matukio ya maisha yake, kuwa familia na Injili na kumfahamu katika moyo wa sala, njia yetu ya kuweka msingi wetu na ujasiri wetu kuwa imara kwa Yesu. Hivyo mchague yeye katika hali zote za maisha k**a Bwana wako na mkombozi. Kwa unyenyekevu jitambue kuwa bila yeye wewe si kitu, na jikabidhi kwake ili yeye aweze kukuongoza salama kwa Baba yetu wa mbinguni.
Sala: Bwana na Mkombozi, ninakukubali wewe katika maisha yangu k**a Bwana na Mkombozi. Ninakushukuru kwa zawadi ya ubatizo iliyo anzisha maisha ya neema ninaomba nibadilishe maisha yangu niendelee kukufuata kikamilifu, leo na siku zote, ili uweze kuingia zaidi ndani ya maisha yangu. Ninaomba matendo yangu yote yaongozwe nawe ili niweze kuwa sadaka ilyio unganika na wewe milele, Yesu mpendwa. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

02/05/2026

JUMAPILI, JUMA LA 5 LA PASAKA
SOMO 1
Mdo. 13:44-52
Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,
Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.
Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 98:1-4 (K) 3
(K) Miisho yote ya dunia imeuona Wokovo wa Mungu wetu.
Au: Aleluya.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.
Mkono wa kuume wake mwenyewe,
Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)
Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka rehema zake,
Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)
Miisho yote ya dunia imeuona
Wokovu wa Mungu wetu.
Mshangilieni Bwana, nchi yote,
Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)
SOMO 2
Mdo. 13:44-52
Paulo na wenziwe wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi. Watu wengi, karibu mji waote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu. Bali Wayahudi walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana. Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa mille, angalieni, twawageukia Mataifa. Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana,
Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.
Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio. Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Yn. 14 : 6
Aleluya, aleluya,
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Aleluya.
INJILI
Yn. 14: 1-12
Yesu aliwaambia wafuasi wake: Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; k**a sivyo, ningaliwaambia, maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaa ndalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. Nami niendakt mwaijua njia. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia? Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. K**a mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba, tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe. Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

24/04/2026

“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Aprili 26, 2026
Juma la 4 la Pasaka
Mdo 2: 14, 36-41;
Zab 23: 1-6;
1 Pet 2: 20-25;
Yn 10: 1-10.
KUKUTANA NA MCHUNGAJI MWEMA!
Jumapili ya nne ya Pasaka inajulikana k**a jumapili ya Mchungaji Mwema, k**a Yesu anavyo jiongelea mwenyewe kuwa ni “Mchungaji mwema”. Yesu anatupa sura ya Mchungaji mwema anaye wafahamu kondoo wake: anawaita, anawalisha na kuwaongoza. Ni kwasababu ya hili Kanisa limeipendekeza kuwa siku ya kuombea miito duniani.
Yesu anaonesha wazi tofauti ya wachungaji. Tofauti anayotoa ni juu ya mchungaji yule anaye wafahamu kondoo wake na kuwajali, na wale wanaofuata tu mkumbo bila sadaka ya upendo. Yesu alitolea sadaka kamilifu k**a Mchungaji wa Kimungu. Alikuwa yupo tayari kutembea nasi katika njia zote, sisi kondoo wake. Alikuwa yupo tayari kutoa sadaka ya kila kitu. Hakutaka mateso, kuonewa, kukataliwa na mambo mengine yamuondoe kutoka katika lengo lake la kuwajali na kuwatunza watu wake katika njia kamili. Inapaswa ituguse na sisi, kutufariji na kutupatia sisi ujasiri na kutambua ni kwa jinsi ghani upendo wake ulivyokuwa mkubwa kwetu.
Wakati upendo aliotoa mmoja kwa ajili yetu ni kamili, tena wakati wa wakati mgumu, huu ni msaada mkubwa. Na upendo unaotolewa kwa mwingine k**a huu unatengeneza muunganiko wa kiroho ambao ni imara kuliko matatizo tunayo weza kukutana nayo. Haijalishi ni kitu ghani kigumu kinachoweza kuja katika njia zetu, tunapaswa kutambua upendo na msaada usio na kikomo kutoka kwa Mchungaji wetu mwema. Na k**a tunaweza kuona upendo huo kamili kutoka kwa wengine, tunakuwa kweli tumebarikiwa mara mbili. Katika hali nyingine Yesu anaongea kuhusu mfano wa mtu mwingine ambaye sio mchungaji mwema, ambaye anaona mbwa mwitu wakija na yeye hukimbia. Tunapaswa kuona ndani ya mtu huyu, vishawishi vyote ambavyo vyaweza kuja katika maisha yetu. Ni vigumu kubaki wakati wa nyakati ngumu. Ni vigumu kuwa karibu na wale wenye shinda wanapo tuhitaji sisi. Ni vigumu kuwa waminifu mpaka mwisho bila kuwa na aibu tunapo kutana na vishawishi vya hofu. Yesu anatupa nguvu na msaada wa upendo kamili yeye akiwa k**a Mchungaji wetu mwema, lakini pia anatuhitaji nasi turudishe upendo huu huu kwake, kwa kuwapatia wengine upendo huu huu mkamilifu. Pale ulipo shindwa na kupungukiwa tunamuomba yeye akuchunge k**a mchungaji ili nawe uweze kuwachunga wengine. Mkimbilie mchungaji mwema na amini upendo wake kwako.
Leo, Kanisa zima linatukumbusha hitaji letu la kuomba, k**a Yesu mwenyewe alivyo waambia wanafunzi wake, hivyo kwamba "mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake" (Lk 10: 2). Tangu hapo awali Kanisa “ kwa asili yake ni umisionari" (Ad Gentes, 2), wito wa Ukristo unazaliwa ndani ya watu kutokana na kazi ya umisionari. Kusikia na kufuata sauti ya Kristo Mchungaji mwema, maana yake ni kuruhusi tuvutwe naye na tuongozwe naye, kujiweka wakfu kwake maana yake kumruhusu Roho Mtakatifu kututumia sisi katika mabadiliko haya ya umisionari, na kuamsha ndani yetu tamaa, furaha na ujasiri wa kutoa maisha yetu wenyewe katika utumishi wa Ufalme wa Mungu.
Katika mz**i wa kila wito wa Kikristo tunaona harakati hii ya msingi, ya kuacha nyuma faraja yetu na mambo yote yanayo tupendezesha nafsi zetu na kujikita katika maisha ya Yesu Kristo. Ina maana ya kuondoka, k**a Abrahimu, na kuacha sehemu yetu ya asili na kwenda mbele kwa uaminifu, tukijua kwamba Mungu atatuonesha njia ya nchi mpya. Hii "kwenda mbele" isi tazamwe k**a ishara ya mpango tu wa maisha ya mtu binafsi, hisia ya mtu, utu wa mtu mwenyewe. Kinyume chake, wale ambao wanamfuata Kristo wanapata uzima kwa wingi kwa kujiweka wenyewe bila kujibakiza katika utumishi wa Mungu na ufalme wake. Wito wa Kikristo kwanza kabisa ni wito wa upendo, upendo ambao hutuvuta sisi na kutuelekeza nje ya sisi wenyewe. Kuitika wito wa Mungu, maana yake kumruhusu yeye atusaidie kujiacha wenyewe kwakuondokana na usalama wetu wa uongo, na kutoka nje na kuenenda kwenye njia inayo ongoza kwa Yesu Kristo, aliye asili na hatima ya maisha yetu na furaha yetu.
Katika siku hizi kwanza tunaombwa tuombee Kanisa liweze kupata wachungaji wema na waadilifu wa kufanya kazi ya Kristo ya kueneza Injili, na kwamba Kanisa liweze kupata vijana wengi wanoitwa kwenye wito wa upadre na utawa ikiwa ni pamoja na watoto wetu wenyewe.
SALA: Baba wa huruma, uliyemtoa mwanao kwaajili ya wokovu wetu na ambaye anatutia nguvu kila wakati kwa zawadi ya Roho wako, tujaliye sisi jumuiya ya Wakristo tulio hai, upendo na furaha, vilivyo vya muhimu kwa maisha ya kindugu, na vinavyojenga ndani ya wadogo mwamko wa wito wakujitoa wenyewe wakfu kwako na kwaajili ya wito wa uenezaji wa neno lako. Dumisha ndani ya jumuiya hizi majitoleo ya kutoa katekesi ya kuitika wito huu wakujitoa wakfu kwako . Wajaliye hekima inayohitajika katika maamuzi ya kufuata wito wako, ili katika yote ukuu wa huruma yako ya upendo iweze kungara. Tunaomba Maria, Mama na uliyekuwa kiongozi wa Yesu, utombee. Yesu tunakutumainia wewe. Amina

24/04/2026

MASOMO YA MISA, APRILI 26, 2026
DOMINIKA YA 4 YA PASAKA
JUMAPILI YA MCHUNGAJI MWEMA
MWANZO:
Zab. 33:5–6
Nchi imejaa fadhili za Bwana. Kwa neno la Bwana mbingu zilifanyika, aleluya.
SOMO 1
Mdo 2:14, 36– 41
Siku ya Pentekoste Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia,
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyesulibisha kuwa Bwana na Kristo.
Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Krito, mpate kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 23:1 – 6 (K) 1
(K) Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)
Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)
Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika. (K)
Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)
SOMO 2
1Pet. 2:20– 25
Kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu. Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.
Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake. Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogopfya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki. Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti; ili, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa. Kwa maana mlikuwa mnapotea k**a kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi war oho zenu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Yn. 10:14
Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi.
Aleluya.
INJILI
Yn. 10:1 – 10
Yesu aliwaambia Wayahudi, Amin, amin, nawaambieni, Yeye asiyeingia mlangoni katika z**i la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang’anyi. Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo. Bawabu humfungulia huyo, na kondoo humsikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kwa majina yao, na kuwapeleka nje. Naye awatoapo kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake. Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni.
Mithali hiyo Yesu aliwaambia; lakini wao hawakuelewa na mambo hayo aliyowaambia.
Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo. Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia. Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo..

17/04/2026

Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Aprili 19, 2026
Juma la 3 la Pasaka
Mdo 2: 14, 22-33;
Zab 15: 1-2, 5, 7-11;
1 Pet 1: 17-21;
Lk 24: 13-35.
KUKUTANA NA YESU MFUFUKA KATIKA MAISHA YETU!
Katika Asia ndogo, mwaka 80-90 AD, karibia mashuhuda wote wa Yesu mfufuka walikuwa wamesha toweka. Wakristo (wa kizazi cha tatu) wanajiuliza wenyewe: je, inawezekana sisi kukutana na Bwana? Inawezekanaje, kutoa ushuhuda kwamba yupo hai wakati sisi hatukumuona kwa macho, hatukumshika kwa mikono yetu, na wala hatukukaa mezani pamoja naye? Je sisi tunaongozwa tu kuamini kile walicho amini na kutuambia sisi? Wakristo wana tamani kumuona Yesu.
Injili ya Luka kuhusu habari ya Emaus huenda ilikuwa ndio uvuvio wa majibu na matarajio ya Wakristo hawa. Mmoja wa wawafuasi aliitwa Cleopa (mtu ambaye alijulikana sana wakati wa Kanisa la mwanzo, kwasababu alikuwa ndugu wa Yosefu, Yosefu “Baba” mlishi wa Yesu) na mwingine hajatajwa jina. Luka anaweza kuwa amefanya hivyo, kumwalika msomaji kuwa mfuasi wa pili. Mwaliko ni wito wa kutembea na Cleopa katika njia ya kumtambua Yesu mfufuka, ili kukusanyika pale ambapo wawili wamekusanyika kwa jina lake.
Hawa wafuasi wawili wana huzuni kwasababu wameona maanguko ya mtarajio yao. Walimtazamia Masiha wa utukufu, mkuu na mfalme lakini wamejikuta wakipoteza. Marabi walifundisha kwamba, Masiha ataishi na kuongoza kwa muda wa miaka elfu moja, na tazama sasa Yesu amekufa. Walikata tamaa na kujikuta wakiona ukweli kwamba ulimwengu uliotangazwa na Yesu haukutimia. Bila Imani ya ufufuko, walioshindwa wameshindwa, maisha mwisho wake kifo, na maisha hayana maana.
Hawa wafuasi wawili wa Emausi hawakuwa na shaka kwamba mawazo yao kuhusu Masiha yalikuwa sio sahihi. Walikuwa wamefungwa katika tamaduni na mapokeo. Walikuwa wamejifungia na kushindwa kufahamu mapya ya Mungu. Yesu hamwachi mtu ambaye anaamua kuchagua mwenyewe kwenda katika njia ya huzuni. Yeye huwa anakuwa pembeni na kuwa msindikizaji. Kutokea kwa Yesu kwa wanafunzi wake inashangaza sana. Yesu “anawafafanulia yote yaliosemwa kuhusu yeye katika Maandiko Matakatifu”. Kwa njia hiyo hawa wafuasi walitambua kwamba huyu mtu ana uelewa na hekima ya hali ya juu, na hivyo walimwalika akae pamoja nao. Yesu alikaa nao na kula nao chakula mezani nyumbani kwao. Walivyokuwa mezani “alichukua mkate, na kuubariki na kuumega na kuwapa vipande”. Macho yao yalifunguliwa na kumtambua Yesu mfufuka. Wale wafuasi baada ya kumtambua Yesu, walikimbia na kwenda kuwapasha habari na kutangaza kwamba “Bwana amefufuka kweli kweli”.
Habari ya wafuasi wa Emausi inarudiwa kila siku katika Liturjia ya Ekaristi (Misa Takatifu). Inaanza kwa kuingia kwa padre, alafu Liturjia ya neno la Mungu na homilia, na mwishowe, “kuumega mkate”. Ni katika wakati wa Ekaristi takatifu macho yetu yanafumbuliwa tunatambua kwamba Yesu mfufuka yupo kati yetu. Bila neno hatuwezi kuja kumtambua Bwana, hatuwezi kumtambua Yesu katika Ekaristi Takatifu. Wakati misa inaisha tunamaliza na wimbo wa mwisho na hatimaye tunaondoka na furaha, kwenda kushirikisha furaha ya Yesu mfufuka.
Misa takatifu ni safari yetu ya Emmaus. Tunapaswa kujikita wenyewe katika kumuona Yesu, na kumtambua na kumwabudu. Tunapaswa kutambua uwepo wa Yesu mfufuka kati yetu. Yupo nasi hapa sasa, anatupenda sisi, anaongea na sisi, na anatuita tumpende yeye. Mtafute na msikilize sauti yake. Tutashangaa ni kwa jinsi ghani Bwana mfufuka atakavyo tufanya tutembee naye katika Maandiko Matakatifu, na kujifunua mwenyewe na kuleta furaha katika huzuni yetu na katika mioyo yetu iliokata tamaa.
Sala: Bwana, ninakushukuru kwa kunipenda mimi sana kiasi kwamba upo na mimi daima. Nipe macho ya Imani niweze kukutana nawe katika Maandiko Matakatifu na kukuona wewe ukiwa ndani ya Ekaristi Takatifu. Ninaomba niweze kutambua uwepo wako katika mambo ya kawaida yanayo tokea katika maisha yangu. Ninakupenda Bwana wangu. Yesu, nakuamini wewe. Amina

17/04/2026

MASOMO YA MISA, APRILI 19, 2026
DOMINIKA YA 3 YA PASAKA
SOMO 1
Mdo. 2:14, 22 – 28
Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.
Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, k**a ninyi wenyewe mnavyojua; mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkasulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; ambaye Mungu alimfufua, akaufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. Maana Daudi ataja habari zake.
Nalimwona Bwana mbele yangu sikuzote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.
Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi wangu ukafurahi; Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini. Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu; Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu. Umenijulisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 16:1 – 2, 5, 7 – 11 (K) 11
(K) Utanijulisha njia ya uzima.
Mungu unihifadhi mimi,
Kwa maana nakukimbilia Wewe.
Nimemwambia Bwana, Ndiwe Bwana wangu;
Bwana ndiye fungu la posho langu, na la kikombe changu;
Wewe unaishika kura yangu. (K)
Nitamhimidi Bwana aliyenipa shauri,
Naam, mtima wangu umenifundisha usiku.
Nimemweka Bwana mbele yangu daima,
Kwa kuwa yako kuumeni kwangu, sitaondoshwa. (K)
Kwa hiyo moyo wangu unafurahi,
Nao utukufu wangu unashangilia,
Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini.
Maana hutaiachaia kuzimu nafsi yangu.
Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu. (K)
Utanijulisha njia ya uzima;
Mbele za uso wako ziko furaha tele;
Na katika mkono wako wa kuume mna mema ya milele. (K)
SOMO 2
1Pet. 1:17 – 21
Ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa k**a wageni. Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; bali kwa damu ya thamani, k**a ya mwanakondoo asiye na ila, asiye na waa, ya Kristo. Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu; ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata Imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Lk. 24:32
Aleluya, aleluya,
Bwana Yesu, utufunulie maandiko; uwashe mioyo yetu unaposema nasi. Aleluya.
INJILI
Lk. 24:13 – 35
Siku ile watu wawili miongoni mwa wafuasi wa Yesu walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu k**a mwendo wa saa mbili. nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia. Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. Macho yao yakafumbwa wasimtambue. Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.
Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi? Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote; tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha. Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo; tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitush*tusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema, wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai. Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo k**a wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona.
Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.
Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, naye alifanya k**a anataka kuendelea mbele. Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao. Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa. Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao. Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?
Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao, wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni, nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

14/04/2026
14/04/2026
10/04/2026

TAFAKARI YA PASAKA
Aprili 12, 2026
------------------------------------------------
JUMAPILI, DOMINIKA YA 2 YA PASAKA, JUMAPILI YA HURUMA YA MUNGU.
------------------------------------------------
HURUMA YA MUNGU: MSAMAHA WA DHAMBI
Leo ni siku ya nane naya mwisho katika oktava ya Pasaka. Na siku ya leo tunaadhimisha Jumapili ya huruma ya Mungu. Ni siku ambayo geti la huruma ya Mungu hufunguliwa kwetu na Mungu kutukirimu huruma yake hata zaidi ya jinsi ambavyo tunaweza kudhani au kutumaini. Leo tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu isiyo na mipaka. Injili ya leo inaonesha mamlaka ya Yesu yakuwapa mitume Roho Mtakatifu ambaye ndiye atakaye wasamehe watu dhambi zao. Yesu Mfufuka anakuwa hai tena kati ya wafuasi wake. Anafungua miyo yao na kuitia shauku na kuwafungulia maandiko, na kuumega mkate. Anafungua macho yao na kujidhihirisha kwao.
Sehemu ya kwanza katika Injili Yesu anawahidia Roho Mtakatifu wafuasi wake. Kwa njia hiyo anawapa mamlaka yakuangusha uovu wote na nguvu za muovu. Na sehemu ya pili inaonesha sehemu maarufu ya Tomasi yakutokuamini. Ingawaje inaonekana kuwa katika methali hivi. Tomasi anaonekana kutokutenda chochote kibaya, alitaka tu aone kile kitu ambacho wengine wameona. Injili ya Marko inasema kwamba Yesu aliwatokea wale kumi na mmoja na kuwaonya juu ya ugumu wa mioyo yao, kwasababu hawakuamini kwamba amefufuka” (Mk 16:14). Katika Injili ya Luka Yesu mfufuka anaongea na mioyo ya mitume ambayo ina wasi wasi “kwanini mna wasi wasi mioyoni mwenu?” (Lk 24:38). Katika sehemu ya mwisho ya Injili ya Mathayo inasema pia wakati Yesu alivyo watokea mitume katika mlima wa Galilaya, wenigne walikuwa na wasi wasi (Mt 28:17). Kwahiyo wote pia walikuwa na wasiwasi, sio tu maskini Tomasi.
Yohane Mwinjili anawakilisha habari hii sio kwamba anataka Tomasi aonekane mbaya au kumuweka mtume katika hali mbaya. Alitaka kusisitiza juu ya swali la jumuiya yake ya Kikristo ambalo daima walisisitiza na kuuliza. Iliwawia vigumu sana kuamini, wakajikuta katika msongo wa mawazo yenye mashaka mengi, walitaka kuona na ikiwezekana washike na kuhakikisha ni kweli Bwana amefufuka kweli. Walishangaza: je hata sisi hatuwezi kuwa k**a wao? Haya ni maswali ambayo sisi wenyewe tunauliza kila wakati. Je, inawezekana na sisi tuweze kushuhudia Bwana Mfufuka? Je, kuna chochote cha kuonesha kwamba yuu mzima? Sasa inakuwaje hata atutokei ? Haya ni maswali ambayo sisi tunauliza siku hizi. Yohane anataka kumchukua Tomasi k**a sehemu ya kila mfuasi anayepata shida katika kumwamini Yesu. Yohane anataka kuwafundisha waumini wa jumuiya ya kwanza na sisi kwamba maisha ya Yesu mfufuka yanaenda zaidi ya fahamu zetu, maisha ambayo huwezi kuyashika, kuyanusa, wala kuyaona. Yanaweza kupatikana tu kwa Imani. Mtu hawezi kuwa na Imani kwenye kitu ambacho kinaonekana. K**a mmoja anataka kuona, kupata jibu, kugusa lazima aikatae Imani. Lakini kwa Yesu, wana heri ambao hawajaona lakini wanaamini. Wana heri kwasababu Imani yao ni ya kweli na haina mashaka. Ambaye anaona anauhakika na ushahidi, ana nyenzo zisizopingika. Sasa inakuwaje kwa ambaye hajakutana na Yesu mfufuka? K**a Tomasi atahitaji kuona na ushahidi ili aweze kuamini, lakini ni wazi kwamba hatapa kamwe ushahidi.
“Hakuna hata mmoja aliyetengwa na huruma ya Mungu na kanisa linawakaribisha wote bila kumkataa yeyote. Milango yake daima ipo wazi, ili wale wote wanaoguswa na neema ya Mungu waweze kuja kusamehewa. Hata Dhambi ikiwa kubwa vipi, ndivyo kanisa linavyo ongeza upendo wakukupenda na kukuribisha yule anayetubu…” . Maneno haya aliyasema Baba Mtakatifu Fransisko wakati akitangaza mwaka wa huruma ya Mungu (2016)
Alirudia kwakusema “Mungu daima hachoki kutusamehe sisi, bali sisi wanadamu tunachoka kumuomba msamaha na kutafuta huruma yake. Yesu ambaye ametuambia tuwasamehe ndugu zetu saba mara sabini, ametupatia sisi mfano. Mfano ambao daima unatupatia tena sisi furaha yetu, anatufanya sisi tunyanyue tena vichwa vyetu na kuanza maisha mengine. Kwahiyo tusikimbie kutoka katika ufufuko wa Yesu, wala tusikate tamaa, hata lije jambo la namna gani. Tunaomba chochote kisitutie nguvu isipokuwa ufufuko wa Yesu mwenyewe, ambao unatupatia nguvu daima” (FURAHA YA INJILI, 3)
”Jumapili ya huruma ya Mungu imekuwa ikiadhimishwa tangu siku nyingi k**a ibaada binafsi. Lakini mwaka 2000, Baba Mtakatifu, Mt. Paulo wa II, ambaye kwakweli katika hali ya kawaida alionesha mfano mzuri wa huruma ya Mungu, aliiweka Jumapili hii ya huruma ya Mungu wakati alipo mtangaza sister Faustina kuwa Mtakatifu. Ambaye alipata Baraka ya kushuhudia huruma ya Mungu na kuandika katika kitabu chake cha kumbukumbu ambacho alikiita huruma ya Mungu. Alikuwa akiandika kila siku ya nane baada ya Pasaka, undani wa huruma umefunguliwa. Ninamwaga huruma k**a bahari kwa roho zote zile ambazo zinahitaji huruma yangu. Roho ambayo itaenda katika kitubio na kupokea Yesu wa Ekarisi (Komunyo) itapokea msamaha kamili na maondoleo ya adhabu. Siku hiyo milango yote ya huruma ya Mungu hufunguliwa k**a bahari. Msikubali roho yoyote ile kuacha kuja kwangu, hata k**a dhambi zake ni nyekundu kiasi ghani. Huruma yangu ni kubwa kiasi kwamba hata roho ya mwanadamu hata malaika hainauwezo wakuishinda milele yote.”
Leo katika jumapili ya huruma ya Mungu, tunakumbushwa juu ya huruma ya Mungu iliyo kuu. Injili yenyewe inaonesha Yesu akitoa mamlaka kwa mitume wake kwa kuwapatia Roho Mtakatifu kuondolea watu dhambi. Tusiache kukimbilia huruma hii ya Mungu. Lakini sisi pia tunapaswa kuwa mawakala wa huruma ya Mungu. Mungu anatuonesha huruma nyingi, lakini sisi nasi anatuhitaji tuoneshe huruma hiyo kwa wengine. Tukisikia sauti ya Yesu mfufuka ambayo ipo kwa ndugu zetu k**a Tomasi basi tumgeukie Mungu na kuwa naye daima. Tushirikishane mapaji yetu k**a jumuiya ya kwanza ilivyofanya katika somo la kwanza. K**a vile Yesu alivyokuja katikati ya mitume, sisi nasi tukishirikishana mapaji yetu, Yesu naye atakuja kati yetu nasi tutamtambua kwakushirikishana zawadi /mkate anao tujalia kila siku.
Sala: Bwana wa huruma, nisaidie leo niweze kuelewa nini maana ya huruma yako. Nisaidie niweze kuingia katika huruma yako ambayo unataka kunipatia mimi. Nikiwa napokea huruma yako mwenyewe, nisaidie na mimi pia niweze kuwa mjumbe wa huruma hiyo ili wote waweze kuona na kukutukuza wewe. Yesu, ninakutumaini wewe. Amina

Address

P. O. PERAMIHO
Peramiho

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when St.Benedict's Abbey Peramiho posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to St.Benedict's Abbey Peramiho:

Share