23/03/2019
UFANYE NINI PALE UNAPOFIKWA NA HALI YA KUKOSA TENA TUMAINI?
Na Steven Mshiu.
Kuna hali inaweza kumpata mtu yeyote, haijalishi kwamba ana nguvu za Mungu kiasi gani, au hata ana upako kiasi gani, mtu huyo anaweza kukosa tumaini la kusonga mbele aidha ni kwa sababu tu ya hali anayoipitia.
Kipindi hicho ndicho ambacho shetani huwa anafanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha kuwa mtu huyo anabaki katika hali ya kukosa tumaini. Humletea hofu na mashaka. Humletea hali ya kuona umauti tuu. Humletea hali ya kuona hakuna tena uzima.
Alikuwepo mfalme mmoja aliyeitwa Hezekia. Mfalme huyu alifanya mambo mengi sana yaliyompendeza Mungu. Katika siku za utawala wake k**a mfalme wa Yuda, hakumuacha Mungu wala kuabudu miungu. Alimtumikia Mungu kwa nguvu zake zote.
Licha ya kutokumtenda Mungu dhambi, Neno la Mungu linakuja kupitia nabii Isaya kwenda kwa Hezekia kuwa atengeneze mambo ya nyumba yake maana atakufa wala hatapona. Mfamle huyu alijikuta katika hali ya kuugua, na kwa kuwa alimuamini Mungu hivyo aliamini kuwa Mungu hataacha kumponya. Mbaya zaidi ugonjwa huo ulimfikisha katika hatari ya kufa.
Ujumbe huu wa Mungu kupitia Isaya inawezekana ulikosesha mfalme huyu tumaini kabisa. Kwa hali ya kibinadamu Hezekia inawezekana alifika mbali sana kimawazo, k**a mtu mwingine angeweza kulalamika sana, mwingine angefikia hatua hata ya kumkufuru Mungu, labda mwingine angetumia na kugawa mali zake zote maana hana tumaini la kuishi tena, na mambo mengine kadha wa kadha.
Lakini kupitia kisa hiki, HEZEKIA anatufundisha mambo kadhaa ya kufanya hususani pale tunapojikuta tumefika katika hali ya kukata tamaa na kukosa matumaini.
Jambo la kwanza la kufanya pale unapofika katika hali ya kukosa tena tumaini ni KUJIGEUZA na KUELEKEZA USO KWA MUNGU na KUMUOMBA MUNGU. Isaya 38:2, Hapa tunajifunza kuwa hakuna sehemu yoyote tunapoweza kupata tumaini isipokuwa kwa Mungu. Nimewahi kushudia baadhi ya watu wanapopita katika hali ngumu, huwa wanaenda kwa waganga na wachawi kutafuta kinga, wanamsahau Mungu, Lakini Hezekia anakua ni kielelezo bora kwetu kuwa tufanye nini pale tunapofikia katika hali ambayo yeye mwenyewe aliipitia.
Lakini jambo la pili alilolifanya Hezekia ni KUMKUMBUSHA BWANA, Isaya 38:3, Alikumbusha Bwana jinsi ambavyo alikwenda mbele zake katika kweli yote na kwa moyo mkamilifu. Alimkumbusha jinsi alivyotenda mema machoni pake(Mungu) Tena hapa anazidi kulia sana. Sio kwamba Mungu ni msahaulifu. La hasha. Sio kwamba alikuwa amesahau mambo ambayo Hezekia aliyatenda. Hapana. Lengo lake alitaka kupima imani ya Hezekia. Je Hezekia angejihesabia haki? Je angekuwa na kiburi cha uzima?
Ni kweli kwamba tuna wajibu wa kumkumbusha Bwana juu ya uhitaji wetu. Sio kwamba yeye hajui uhitaji wetu. Lakini yeye k**a Baba kwetu anataka kutuona sisi k**a watoto wake tukienda mbele zake na kumbusha juu ya uhitaji wetu. Lakini yale ambayo tunayafanya au ile kazi ya Mungu tunayoifanya ndio inayotupa nguvu zaidi ya kuzidai ahadi na Baraka zetu kwake. K**a Hezekia angekuwa ni mlegevu kwenye kazi ya Mungu asingekuwa na ujasiri wa kumlilia na kumkumbusha Mungu juu ya hitaji lake la kurejeshewa uponyaji.
Jambo la tatu, Jifunze kuwa mtu wa shukrani na kujishusha. Isaya 38:9-22. Licha ya Hezekia kurejeshewa tena tumaini la uhai wake hakujikweza wala kuchukua utukufu wa Mungu, bado alizidi kuwa mtu wa shukrani mbele za Mungu. Bado alijishusha hadi chini kabisa. Hakuhesabu ni kwa ajili ya matendo mema aliyotenda ndio maana Mungu amemuongezea miaka.
Kuna watu wengine Mungu akiwabariki kwa kidogo tu, mabega yanapanda juu. Wanajiona k**a walistahili. Wanakuwa na kiburi, wanajivuna. Sio hivyo. Kuna mambo Mungu anatutendea sio kwamba tunastahili, ila ajitukuze kupitia sisi. Vyeo vyetu na nafasi zetu havifai wala haviwezi kulirejesha tumaini letu ambalo ni faraja kwetu.
Lakini jambo lingine ni kutambua Mungu yuko tayari kukupatia tumaini jipya. Vs 20. Mwanadamu anaeishi katika ulimwengu huu uliopotoka na kuanguka anategemea tumaini moja tu la WOKOVU. Ili uweze kuwa mshindi kwenye hii dunia inayokwenda kasi katika zama za ujuaji na uovu ni lazima uwe na TUMAINI la wokovu tu. Kwamba hata katika mambo yote bado Mungu aweza kukuokoa. TUMAINI ni ile hali ya kutegemea na kuuona USHINDI hata k**a hakuna dalili za kibinadamu zinazoashiria USHINDI.
Mwisho kabisa mtegemee Mungu aliye chanzo cha tumaini lako. Wakati Daniel anatupwa kwenye shimo la samba wenye njaa kali bado Tumaini lake lilikuwa kwa Mungu wake kuwa anaweza kumuokoa na samba wenye njaa kali. Kina Meshaki na Shedraki walipotupwa ndani ya tanuru la moto mkali bado walikuwa na Tumaini la kuokolewa na Mungu katika moto ule. Ayubu licha ya kupoteza kila kitu kuanzia mali hadi watoto bado alikuwa na tumaini kwa Mungu wake kuwa anaweza kufanya jambo lingine kubwa zaidi.
Mpendwa rafiki, haijalishi unapitia katika hali gani. Umekata tama kiasi gani. Huoni njia kabisa. Huoni mpenyo. Kila kitu kimekwama. Nakuhakikishia kuwa bado liko tumaini la kuinuka tena. K**a shina la mti laweza kuchipua tena na kutoa matunda na watu wakayala. Hata kwako Mungu aweza kukurejeshea tena yale unayoyaona kuwa haiwezekani tena kutokea.
Mungu akuinue viwango viwango vingine.
Rafiki yako,
Steven Mshiu.
0655-882074
March 23, 2019