15/10/2024
ASILI YA JINA LA YESU.
Jina la Yesu maana yake ni mwokozi, pia linatambulika k**a Yoshua katika agano la kale, maana yake ni ile ile moja mwokozi, wayahudi au waebrania au waisrael walikuwa na kawaida au utamaduni wa kumpa mtu jina kutokana na wito aliokuwa nao, majina yote waliyokuwa wanatoa yalikuwa yana maana, walikuwa hawampi mtoto jina kwa sababu wanajisikia kumpa, hapana, ilikuwa inategemea sana wito au jukumu alilopewa au kusudiwa na Mungu kuja kufanya hapa duniani.
Kwa hiyo wale watoto waliopewa majukumu makubwa muda mwingine Mungu alikuwa anaingilia kati na kutoa majina Yeye mwenyewe kwa mfano tunaona kwa Ibrahimu, Israel, Yohana mbatizaji na hata Yesu mwenyewe.
Kwa hiyo tunajifunza hapo kabla ya kutoa jina kwa mtoto wako embu fikiri mara mbili, lakini itapendeza zaidi na itakuwa ni busara sana kumuuliza Mungu mwenyewe aliyekupa huyo mtoto, sababu ndiye anayejua amemkusudia huyo mtoto kuja kuwa nani.
Kwa hiyo Yesu aliitwa mwokozi kwa sababu kazi yake kubwa ilikuwa kuja kuuokoa ulimwengu na dhambi yao, alikuja kutuokoa mimi na wewe ili tusiangamie na kuishia jehanamu kwenye moto wa milele, alikuja kutuokoa na mauti na kutupatia uzima wa milele, kivipi? Kwa njia ya kuchukua dhambi zetu na adhabu zake ili sisi turithi uzima wa milele.
Yohana 3:16
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
2Petro 3:9
Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, k**a wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
Picha inaanzia hapa, huu ulikuwa ni mpango kamili wa Mungu, uliosukumwa na nguvu ya upendo aliokuwa nao, ambao ndiyo msingi mkuu au unatakiwa uwe msingi mkuu wa dini zote au imani zote, kwa sababu Mungu aliupenda ulimwengu ulioasi, hakutaka watu aliowaumba waangamie, upendo ukazaa nia, nia yake kubwa ni kuwa watu wote waokolewe, japo huwa hamlazimishi mtu,
Hakuishia kupenda tu na kuwa na nia hapana, upendo huwa unakamilishwa na kitendo, kwa hiyo akamtuma Yesu, na ndiye na aliyetoa jina la Yesu, lenye maana ya mwokozi, kulingana na kusudi alilobeba.
Kwa hiyo nia hii aliyokuwa nayo Mungu Baba akamuambukiza na mwanae pia, kwa hiyo Mungu aliupenda ulimwengu akamtuma mwanae, mwanae pia aliupenda ulimwengu akakubali kuja kutuokoa, kwa hiyo ujio wake duniani ulikuwa maalumu kwa lengo moja tu, kukamilisha mission/mpango wa Mungu Baba, nao ni kutuokoa wanadamu.
Mathayo 1:21
Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.
Yohana 1:29
Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
Isaya 53:5
Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Mathayo 18:11
[Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kukiokoa kilichopotea.]
Luka 9:56
Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.
1Thesalonike 1:10
na kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni Yesu, mwenye kutuokoa na ghadhabu itakayokuja.
Yohana 12:47b
sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu.
Lakini mtu yoyote akishaokolewa na Kristo Yesu, anapewa nia ile ile aliyokuwa nayo Bwana Yesu, ya kusaidia au kutaka watu wengine pia waokolewe, inakuwa ni mwendelezo, kutoka kwa Mungu, kwa Yesu hadi kwetu, ndio wito mkuu tuliokuwa nao watumishi, kwa sababu Roho mtakatifu yule yule aliyekuwa anatenda kazi ndani ya Kristo Yesu ndiye tuliyepewa k**a zawadi kwa kumuamini Yeye, huyo Roho mtakatifu anatenda hata sasa ndani yetu, wito ni ule ule, kazi ni ile ile, nia ni ile ile kuokoa.
1 Wakorintho 2:16
Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.
Wafilipi 2:5
Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Watumishi wanaotoka ndani ya wito na nia hiyo na kuanza kutafuta mali na fedha na vitu vingine vya kidunia wanakuwa wametoka nje ya reli, nje ya mpango wa Mungu, wanakuwa wametoka kwenye nia ya Kristo, kunakuwa hakuna nguvu ya upendo nyuma yao inaowasukuma kuanisha na kuendesha huduma zao, bali tamaa ya mali na fedha, uwe na uhakika hata mahusiano na aliyewatuma yanakuwa hayapo tena, ndio hao anaosema siku ya mwisho atawakataa, akisema hawajui, maana kazi yao ilikuwa kujilimbikizia mali na starehe za dunia, ila sio kuokoa watu.
Mathayo 7:21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Binafsi huu ndio wito wangu mkuu kutaka watu wote waokolewe, na mtumishi wa hivi huwezi kumzuia kwa namna yoyote kwa sababu anatembea na nguvu na uweza na kujitoa k**a alivyokuwa Bwana Yesu, na huwezi kumzuia wala kumkatisha tamaa kwa chochote sababu anajua ni nini anafanya na wito wake ni nini.
Unaweza ukashangaa kwanini mtumishi wa hivi anaweza kukutana na mambo mengi ya kumkatisha tamaa lakini akasonga mbele, watu wanaweza kumsema vibaya, kumdharau, kumkatisha tamaa kwanamna tofauti lakini akasonga mbele, na muda mwingine, pengine watu hao hao anaowasaidia ndio wanaweza kutumika kumkatisha tamaa, lakini akavumilia na kusonga mbele na wala asiwe na kinyongo nao ni kwa sababu hii, ya wito na nia ya Kristo Yesu ndani yetu.
Hata Yeye Bwana Yesu alivumilia mengi, kukataliwa, kutukanwa, kusemwa vibaya, alitemewa hadi mate, alipigwa na kusulubiwa tena na watu hao hao aliotumwa awaokoe, lakini hakukasirika, hakuzira , hakulalamika wala hakuacha, sababu yeye ni mwokozi na alikuja duniani kwa sababu hiyo tu, kuokoa, naye alijua, alitambua amekuja kufanya nini duniani, kwa mfano, k**a kweli wewe wito wako ni udaktari huwezi kulalamika ukiletewa wagonjwa sababu ni kazi pia ni wito wako, kuona watu wanapona, mtu anayelalamikia kazi anayofanya ujue kabisa huyo huo sio wito wake, Bwana Yesu naye pia alitambua hilo, kwa hiyo alivumilia yote, aliishia kusema Mungu wasamehe maana hawajui walifanyalo.
Isaya 53:3
Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na k**a mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Luka 9:22
akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa na siku ya tatu kufufuka.
Luka 17:25
Lakini kwanza, hana budi kupata mateso mengi, na kukataliwa na kizazi hiki.
Luka 18: 32-33.
32 Kwa kuwa atatiwa mikononi mwa Mataifa, atafanyiwa dhihaka; atatendwa jeuri, na kutemewa mate; 33 nao watampiga mijeledi, kisha watamwua; na siku ya tatu atafufuka.
Luka 23:34
Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.
Kiukweli huwezi kumchukia au kumkasirikia mtu anayehitaji msaada na hajui k**a anahitaji msaada, sababu anakuwa hajui afanyalo.
Nitoe mfano huu wanasema mtu anayetaka kuzama majini, ukienda kumuokoa msubiri kwanza mpaka aishiwe nguvu ndio umbebe, kwa sababu akiwa na nguvu zake huwa ana tapa tapa anaweza kukuzamisha nawewe pia, sasa hapo inahitajika hiyo busara kwa sababu huwezi kujaribu mara moja akakusumbua ukamuacha sio sawa, sababu kwa muda ule anakuwa hajui afanyalo, au ni sawa na mtoto mdogo unaweza kumbeba mgongoni akakuchana na viwembe huwezi kukasirika na kumtupa sababu anakuwa hajui afanyalo, ndivyo Bwana Yesu alivyokuwa anatutizama, nasisi tunatakiwa kutazama hivyo kwa wengine pia ambao hawajamjua Yesu.
Kwa hiyo na wale anaowaokoa anawapa nia, nguvu na kiu hiyo hiyo ya kutaka watu wengine waokolewe pia, mtumishi wa kweli anayefahamu wito wake hawezi kukata tamaa au kukatishwa tamaa kirahisi, ukifunga mlango mmoja atafungua mwingine, sababu ndio kazi aliyobakiwa nayo kufanya hapa duniani, kuna muda Bwana Yesu aliacha hadi chakula sababu ya wito wake na moto uliokuwa unawaka ndani yake, kiu yake ilikuwa akachape injili ili watu wote waokolewe.
Yohana 4:31
31 Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule, 34 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.
Kati ya silaha alizokuwa nazo kwa msaada wa Roho mtakatifu, ametupatia nasisi pia watumishi wake ni uvumilivu, upole na subira, sababu muda mwingine hao hao uliotumwa uwasaidie wanaweza kukupiga mawe, huwezi kukasirika wala kuacha sababu ndio kazi yako, ndio wito wako, yanaweza pia kutokea mambo mengi ya kutukatisha tamaa, lakini Bwana Yesu alishatutahadharisha mapema,
Mathayo 20:22-23a.
22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza, 23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu;
Mathayo 10:17, 22.
17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga; 22 Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
Mathayo 24:9
Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.
Yohana 15:18
18 Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi, 19 K**a mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.
(Yohana 16:4a) Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia.
1Thesalonike 3:3
mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
Kwa hiyo ukiona mtumishi anakata tamaa au anakatishwa tamaa kirahisi na watu au mazingira basi hajajua bado wito wake.
2Timotheo 2:24-26.
24 Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; 25 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili k**a ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; 26 wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.
Mtumishi wa kweli wa Mungu haiwezekani kabisa kumkatisha tamaa, moto ukishawaka umewaka hakuna awezaye kuuzima, Bwana Yesu alisema,
Luka 12:49
Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?
Silaha nyingine aliyotumia na aliyotupatia Bwana Yesu ni kweli na ujasiri, kuna muda watu wengi walimuacha sababu hawakuwa tayari kusikia kweli na wengine walimchukia sababu ya kuzungumza ukweli lakini yeye hakujali, baadhi ya wanafunzi wake walipoondoka aliwauliza wale waliobaki na nyie mnataka kuondoka? Kwa sababu alikuwa yupo tayari kubaki hata peke yake na kusimamia kweli hata k**a dunia yote ingemkataa,
Muda mwingi alipingana na mafarisayo sababu walikuwa wanafiki watu wasio na kweli, mdomoni wanasema hivi, ila moyoni hawamaanishi, sababu matendo yao ni tofauti na wanachosema, aliwakemea hadharani bila woga,
Mathayo 15: 7-9.
7 Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, 8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami, 9 Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.
Yohana 8:40 -44.
40 Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo, 41 Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu, 42 Yesu akawaambia, K**a Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma, 43 Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu, 44 Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.
Yohana 3: 20-21
20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa, 21 Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika Mungu.
Huo msimamo na huo ujasiri ndio aliotuachia watumishi wake pia, mtumishi wa kweli wa Bwana Yesu yupo tayari kusimamia kweli mpaka mwisho hata k**a watu wote watamchukia, watamkataa na akabaki peke yake, lakini pia anakuwa na ujasiri k**a simba.
Kizazi cha sasa wengi wanapenda injili za mafanikio na miujiza, wanapenda wahubiriwe kile wanachopenda kusikia, ukiwahubiria kweli, ukiwakaripia na kuwaonya hawatakupenda, ndio maana manabii wa uongo wanapata watu wengi sana, wanahubiri na kufanya kile watu wanapenda kusikia.
Lakini nisisitize njia inayoweza kuonekana ni njema na ina watu wengi inaelekea upotevuni, njia iendayo uzimani ni nyembamba na imesonga sio wengi wataiona au kuipenda kuifata, Mungu akusaidie uweze kutambua hili nilisemalo.
Mathayo 7:13-14
13 Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo, 14 Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
Tuishie hapa kwa leo, hiyo ndiyo asili ya jina la Yesu, na Bwana Yesu aliyowaachia pia wale wote waliomuamini, waliozaliwa mara ya pili, jina limebeba wito na utume huo.
Mwl. Gadi J Mbajo.