19/10/2022
*KESHA LA ASUBUHI.*
Jumatano, 19/10/2022.
*VICHOCHEA MWILI HATIMAE HUTOA MATOKEO MAOVU.*
*Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo, lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. 1 Wakorintho 10:13.*
✍️ Sisi watu, pamoja na kukiri kwetu matengenezo ya afya, tunakula kupita kiasi. Kujihusisha na uchu wa kula ndio sababu kuu ya kudhoofika kwa mwili na akili, na ndio msingi wa udhaifu ambao unaonekana kila mahali.
✍️ Kukosa kiasi kunaanzia katika meza zetu katika matumizi ya chakula kisichokuwa cha afya. Baada ya muda, kwa njia ya kuendelea kula ovyo, viungo vya utumbo huwa dhaifu, na chakula kilicholiwa hakikidhi hamu ya kula. Hali zisizokuwa za afya zinaanzishwa, na kunakuwa na uhitaji sana wa chakula kinachochangamsha mwili zaidi. Chai, kahawa, minofu ya nyama huleta madhara kwa haraka. Katika mvuto wa sumu hizi mfumo wa neva unasisimuliwa, na, katika baadhi ya matukio, kwa wakati huu, akili inaonekana kuwa na nguvu na mawazo kuwa wazi zaidi. Kwa sababu vichocheo hivyo huzalisha matokeo yanayokubalika kwa wakati huo, wengi wanahitimisha kuwa wanavihitaji sana na kuendelea kuvitumia.
✍️ Lakini daima kuna athari. Mfumo wa neva, ukiwa na msisimko usiofaa, ulikopa nguvu kwa matumizi ya sasa kutoka kwenye rasilimali zake za nguvu za baadaye. Uimarishaji huu wote wa mfumo ni wa kitambo tu na unafuatiwa na mfadhaiko. Kwa kadiri vichocheo hivi vinavyochangamsha kwa kitambo, mfumo huo utakuwa wa kushusha nguvu za viungo vilivyosisimka baada ya kichocheo kupoteza nguvu yake. Uchu wa kula unaelimishwa kutamani kitu chenye nguvu zaidi ambacho kitakuwa na tabia ya kuendelea na kuongeza msisimko unaokubalika, hadi anasa inakuwa mazoea, na kunakuwa na hamu ya kuendelea kutaka sana kichocheo chenye nguvu zaidi, k**a vile tumbaku, mvinyo, na vileo....
✍️ *Mwisho mkuu ambao Kristo alistahimili mfungo huo mrefu jangwani ulikuwa ni kutufundisha ulazima