02/07/2023
๐๐๐ฉ๐ ๐ช๐๐๐จ๐ ๐๐ช๐๐ก๐๐ก๐ ๐ง๐จ๐ก๐๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ ๐ช๐๐๐๐ง๐ ๐ช๐ ๐ ๐๐ฆ๐?
Kwanza kabisa nianze kwa kusema kwamba, neno "Maandamano" limetokana na neno la Kiingereza "Procession" yaani "Kundi la watu wanaotembea pamoja kwa lengo fulani."
Katika Kanisa Katoliki, maandamano hutafsiriwa k**a msafara wa Waamini wanaotembea pamoja kutoka eneo moja na kwenda eneo lingine, huku wakiimba na kucheza kwa furaha kwa ajili ya kumsifu na kumwabudu Mungu.
Licha ya Kanisa kukopi maandamano yanayofanywa na watu katika jamii zetu, lakini maandamano yanayofanywa na Wakatoliki asili yake ni kutoka kwenye Biblia kabisa, hasa pale Waisraeli walipokuwa wakitembea pamoja kwa furaha kuelekea Kanaani, baada ya kukombolewa kutoka utumwani Misri (Kutoka 13:1-10). Wakiwa njiani, walimchezea Mungu na kumshangilia kutokana na matendo makuu aliyowafanyia (Kutoka 15:1-19).
๐ฆ๐ช๐๐๐: ๐๐ช๐๐ก๐๐ก๐ ๐ช๐๐๐๐ง๐ข๐๐๐๐ ๐๐จ๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ ๐ช๐๐๐๐ง๐ ๐ช๐ ๐ ๐๐ฆ๐?
๐๐๐๐จ: Mpendwa kabla sijajibu swali hili, naomba nielezee kwanza aina za maandamano yanayofanyika wakati wa Misa, ili wale wasiojua nao pia waweze kujua. Na kupitia maelezo hayo nitakayoyatoa hapo chini, basi na majibu yake yatakuwepo. Hivyo jitahidi kusoma kwa umakini, ili uweze kuelewa.
1. ๐ ๐๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ข ๐ฌ๐ ๐๐จ๐๐ก๐๐๐
= Hili ni andamano la kwanza kabisa kati ya matano yanayofanyika katika Misa. Kikawaida kabla ya Misa kuanza kwa ishara ya Msalaba, Kuhani pamoja na Watumishi wa Altare, Wanakwaya, Wasomaji na Waamini baadhi kutoka Jumuiya inayohudumia, huandamana kutoka nje ya Kanisani hadi ya Altareni.
= Lengo kuu la maandamano hayo, ni kumshangilia Kristo ambaye anakuja tena kwetu na kuirudia Sadaka yake ya wokovu, aliyoitoa pale Kalvari kwa njia ya Misa Takatifu, huku akitualika tuungana nae na kumpokea katika Karamu yake Takatifu. Na ndio maana katika mwaliko huo wa furaha na wa kipekee, Kanisa lote huandamana pamoja na Yesu kabla ya Misa kuanza.
2. ๐ ๐๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ข ๐ฌ๐ ๐๐ก๐๐๐๐
= Hili ni andamano la pili kati ya matano yanayofanyika katika Misa. Mara nyingi maandamano haya hutokea wakati wimbo wa Aleluya ukiimbwa huku Padre au Shemasi akiweka ubani katika chetezo na kusema: "Bwana uitakase....." Halafu hukibeba juu kitabu cha Injili kwa taadhima kubwa kutoka Altareni au mlango mkuu wa Kanisa mpaka kwenye Ambo (Mimbari ya kusomea), akisindikizwa mbele na Watumishi wa Altare wenye chetezo na mishumaa.
= Lengo kuu la Maandamano haya, ni kuwafanya Waamini wakae tayari na kusikiliza kwa umakini ujumbe wa Neno la Mungu unaohubiriwa muda huo kutoka kwenye kitabu cha Injili. Na ndio maana muda huu unapofika, Kanisa lote linapaswa kukaa kimya, maana maneno yanayosomwa pale ni ya Kristo mwenyewe, akiongea nasi kwa kinywa cha Kuhani au Shemasi aliyeandaliwa kusoma.
3. ๐ ๐๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ข ๐ฌ๐ ๐ฉ๐๐ฃ๐๐๐
= Hili ni andamano la tatu kati ya matano yanayofanyika katika Misa. Kikawaida, baada ya homilia na maombi kuisha, Waamini hutoa matoleo yao ya pesa, mazao, wanyama au kitu chochote kile na kisha hukusanywa pamoja na kupelekwa Altareni huku wakisindikizwa na Watumishi wa Altare wenye chetezo.
= Lengo kuu la maandamano hayo, ni kumuonyesha Mungu jinsi mioyo yetu ilivyo ya ukarimu k**a alivyo yeye, na kumshukuru kwa zawadi ya ridhiki na baraka mbalimbali alizotujalia. Na ndio maana tunaandamana kwa furaha, kumrudishia Mungu yale yote aliyotuneemesha japo ni kidogo, na kumwomba tena Mungu aweze kutubariki siku nyingine.
4. ๐ ๐๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ข ๐ฌ๐ ๐๐ข๐ ๐จ๐ก๐ฌ๐ข
= Hili ni andamano la nne kati ya matano yanayofanyika katika Misa. Mara nyingi baada ya Sala ya mageuzo kumalizika, Waamini Wakatoliki waliojiandaa, hupata fursa ya kushiriki Meza ya Bwana kwa mistari ili kuepuka vurugu na makelele. Kiukweli andamano hili, ni moja ya maandamano makubwa sana ambayo kusanyiko nzima huweza kushiriki kimwili na kiroho pia.
= Lengo kuu la maandamano hayo, ni kumpokea kwa furaha Kristo anayekuja kwetu katika Maumbo ya Mkate na Divai bila mastahili, na kukaa ndani mwetu. Na ndio maana wakati tunaandamana, tunapaswa wote tuimbe hata k**a tupo kwenye mstari, maana anayekuja ndani mwetu ni Mkuu sana, ni k**a vile unavyompokea mgeni mkubwa nyumbani kwako kwa bashishi.
5. ๐ ๐๐๐ก๐๐๐ ๐๐ก๐ข ๐ฌ๐ ๐๐จ๐ง๐ข๐๐
= Hili ni andamano la mwisho kati ya matano yanayofanyika katika Misa. Kikawaida baada ya Misa kuisha kwa ishara ya Msalaba na maneno ya "Nendeni kwa amani" yanayotamkwa na Padre, Kuhani pamoja na Watumishi wa Altare ndio wanaoruhusiwa kwanza kutoka Kanisani, kisha Waamini wengine hufuata. Ni makosa makubwa sana Muumini kuondoka Kanisani, kabla ya Muongozaji Misa.
= Lengo kuu la maandamano haya, kwanza ni kumpa heshima Padre aliyechukua nafasi ya Kristo kuadhimisha Misa, na kuondoka Kanisani kwa ujasiri na furaha tele baada ya baraka ya mwisho ambayo, Kuhani hutualika huko tuendako tuwe Mabalozi wazuri wa Neno la Mungu tulilolisikia Kanisani. Na ndio maana baadhi ya Mapadre humaliza Misa kwa kusema hivi: "๐ฆ๐ฎ๐๐ฎ ๐ ๐ถ๐๐ฎ ๐ถ๐บ๐ฒ๐ธ๐๐ถ๐๐ต๐ฎ, ๐บ๐ป๐ฎ๐๐๐บ๐๐ฎ ๐ธ๐๐ฒ๐ป๐ฒ๐ป๐ฒ๐๐ฎ ๐๐ป๐ท๐ถ๐น๐ถ." Nasi tunajibu: "๐ง๐๐บ๐๐ต๐๐ธ๐๐ฟ๐ ๐ ๐๐ป๐ด๐".
๐ง๐จ๐ ๐ฆ๐๐๐จ ๐ฌ๐๐ฆ๐จ ๐๐ฅ๐๐ฆ๐ง๐ข...