04/11/2022
*UWAKILI UWAKILI UWAKILI*
“Sisi tu Mawakili wa Mungu tuliokabidhiwa na yeye wakati, fursa, uwezo na mali na mibaraka ya dunia na rasimali zake. Tunawajibika kwake kwa matumizi yake sahihi. Tunakiri umilikaji wa Mungu kwa huduma ya uaminifu kwake na wanadamu wenzetu, na kwa kurudisha zaka na k*toa sadaka kwa ajili yake na kwa utegemezaji na ukuaji wa Kanisa lake. Uwakili ni fursa iliyotolewa kwetu na Mungu kwa ajili ya malezi katika upendo na ushindi dhidi yao choyo na tamaa. Wakili hufurahia mibaraka inayowajia wengine k**a matokeo ya uaminifu wake” (Kanuni ya Kanisa toleo la 17 sura 3-12).
Zaidi ya chochote kingine, kuishi maisha ya kikristo ina maana ya kujitoa – kujisalimisha sisi wenyewe na kumkubali Kristo. K**a vile yeye alivyojitoa kwa ajili yetu, Je sisi tutafanya nini kwa ajili yake?
Mungu hategemei wanadamu kuisukuma kazi yake au kuiendeleza injili. Angeweza kuwatumia malaika kuwa mabalozi wa kweli yake. Angeweza kuwajulisha wanadamu mapenzi yake k**a alivyofanya katika mlima wa Sinai kwa sauti yake mwenyewe. Lakini ili kuendeleza roho ya utoaji kujitoa kwetu, amechagua kuwatumia wanadamu kuifanya kazi yake (Counsels on Steward ship page 20).
Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo na Mawakili wa siri za Mungu. Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu” (1 Kor 3:21- 4:2).
```UWAKILI NINI?```
“ *Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni Hekalu la Roho Mtakatifu…………… wala ninyi si mali yenu wenyewe? Maana mlinunuliwa kwa thamani sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu (1 Kor 6:19,20) kwa gharama kubwa tulinunuliwa na kukombolewa. Sisi ni wa Bwana. Hiyo ni k*tufanya kuwa watu wake kwa mara ya pili kwa kuwa alituumba na k*tukomboa. Biblia hueleza kwa uwazi kabisa kwamba Dunia na vyote vilivyomo ni mali yake na wote wakao humo (Zab 24:1)*
Ni katika uumbaji Mungu alimshirikisha mwanadamu katika kumiliki na aliendelea kuwa mmiliki wa kweli wa ulimwengu, walezi wa vitu vyake (Zab 24:1)
*Wakili ni mtu* “aliyekabidhiwa uangalizi wa mali ya mtu mwingine” Uwakili ni nafasi , majukumu. Kwa mkristo uwakili una maana jukumu la mwanadamu kuwa na matumizi ya chochote alichokabidhiwa na Mungu- Uhai, mwili, muda, talanta na uwezo, mali fursa ya kuwahudumia wengine na ujuzi wake wa kweli. Wakristo hutumika k**a waangalizi ( Mameneja) wa mali za Mungu na kuangalia maisha k**a fursa ya kimbingu, kujifunza kuwa waaminifu katika uwakili,hutufanya tufae kwa uwakili uliotukuka zaidi na umilele wa maisha ya baadae.
```Katika upana wake hivyo basi, uwakili unahusisha matumizi ya busara na k*tokuwa wabinafsi wa maisha.```
*NAMNA YA KUTAMBUA UWAKILI WA MUNGU.*
Maisha yaweza kugawanyika katika sehemu kuu nne za msingi na kila sehemu ni zawadi ya Mungu kwetu.
Mungu ametupatia mwili, uwezo, muda pamoja na umiliki wa mali pamoja na hayo twapaswa k*tunza mazingira ya dunia ambayo Mungu ametupatia.
*SEHEMU YA KWANZA- UWAKILI WA MWILI*
Watu wa Mungu ni mawakili wa wao wenyewe twapaswa kumpenda Mungu kwa mioyo yetu yote na kwa nguvu zetu zote na akili zetu zote (Luka 10:27).
Wakristo wamepewa fursa ya kukuza nguvu zao za kimwili na kiakili kwa ngazi ya juu. Kwa kufanya hivyo huleta heshima kwa Mungu na kuwakilisha baraka kuu wanadamu wenzao.
Mungu ametuita k**a Wakristo kuwa watu wenye afya tele kwani miili yetu ni hekalu la Roho mtakatifu.
Iko mibaraka tele ambayo Mungu ametupatia kuweza kuwa na afya bora. Mibaraka hiyo ni k**a ifuatavyo:-
- Mibaraka ya mazoezi
- Mibaraka ya mwangaza wa jua
- Mibaraka ya maji
- Mibaraka ya Hewa safi
- Mibaraka ya kuwa na kiasi
- Mibaraka ya kupumzika.
Uwakili wa mwili ni pamoja na kuuvika mwili mavazi yanayostahili. Wakati ulimwengu unakwenda na mavazi yasiyofaa, wakristo mameitwa kuinua hadhi ya mavazi katika kiwango cha Ukristo.
Sisi tu mali ya Mungu , mwili nafsi na Roho kwa hiyo ni wajibu wetu wa kidini kushika sheria za afya, kwa ajili ya vyote, hali njema na furaha yetu sisi wenyewe, na pia kwa ajili ya huduma yenye ufanisi kwa Mungu na kwa wanadamu wenzetu. Hamu ya kula chakula sharti idhibitiwe. Afya hutumiwa kwa kuzingatia akili kwa kanuni za afya zinazohusiana na hewa safi, upitishaji wa hewa safi,nguo zifaazo,usafi,mazoezi ya kufaa na maburudisho,usingizi tosha na pumziko na lishe tosha iletayo siha. Mungu amempa mwanadamu chakula chema cha aina nyingi ili k*tosheleza kila hitaji la lishe; matunda, nafaka, njugu na mboga zilizoandaliwa kwa njia rahisi pamoja na maziwa………………. hufanya lishe yenye afya mno” (Christian Temperancy and Bible Hygene Uk 47).
Wakristo waepuke kuonyesha urembo na madoido mengi ikiwezekana nguo ziwe za namna bora na rangi zinazopendeza na zifaazo kwa huduma. Zichaguliwe k*tokana na kudumu kwake kuliko kwa ajili ya onyesho.Uvaaji udhihirishe na adabu nzuri heshima na zinazofaa kwa onyofu wa asili (Messages to Young people Uk 352).
Neno la Bwana linabakia pale pale, likisema “ Ninyi ni nuru ya Ulimwengu mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango, nayo yawaangaza wote walioko nyumbani. Vivyo hivyo Nuru yenu na iangaze mbele ya watu wapate kuyaona matendo yenu mema wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni” (Matayo 5: 14:16)
Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri, kujisikia na k*tenda kulingana na kanuni za mbinguni. Ili Roho aumbe upya ndani yetu tabia ya Bwana wetu twapaswa kujihusisha tu katika mambo yale ambayo yatazaa katika maisha yetu usafi unaofanana na Kristo, hii italeta afya na furaha katika maisha yetu. Hii inamaanisha kwamba maraha na maburudisho yetu yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji na uzuri wa Kikristo. Huku tukitambua tofauti za Kiutamaduni, mawazo yetu yanapaswa yawe ya kawaida si ya anasa na safi yanayostahili wale ambao uzuri wao wa kweli asili yake sio mambo ya nje bali asili yake ni mapambo yasiyoharibika yenye Roho ya upole na utulivu. Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa miili yetu ni mahekalu ya Roho mtakatifu yatunapasa k*tumia kwa akili. Pamoja na mazoezi tosha na mapumziko, yatupasa kuchagua lishe yenye afya. Kwavyovyote vile twapaswa kuepuka vyakula vilivyo najisi vilivyotajwa kwenye maandiko matakatifu. Kwa vile madawa hudhuru miili yetu, yatupasa kuepukana navyo pia. Badala yake tunapaswa kujishughulisha na chochote kile kinacholeta mawazoni mwetu na miili yetu nidhamu ya Kristo ambaye hutamani uzima wetu , furaha na wema.
Mafungu ya ziada
Warumi 12:1, 2. 1Yoh 2:6, Waef 5:1-2; Waf 4:8 2 Kor 10:5, 6 14-7, 1 Pet 3:1-4; 1 Wakr 6: 19,20 10:31; Walawi 11: 1-4, 7, 3 Yoh 2
*SEHEMU YA PILI-WAKILI WA TALANTA*
Kila mmoja wa watoto wa Bwana amepewa uwezo; mmoja aweza kupewa uwezo wa uimbaji, mwingine uwezo wa Biashara au ufundi wa magari au mmoja aweza k*tengeneza marafiki kwa urahisi lakini mwingine hutenda kazi kwa ukimya lakini k*tenda kazi kwa umakini na kwa uzuri wote.
Kila uwezo waweza k*tumika kumtukuza mwenye k*tumia au kumtukuza yeye aliyeitoa ambaye ni Mungu wa mbinguni.
Maneno ya Yesu mwenyewe aliyoyasema kabla hajapaa kwenda Mbinguni alisema “Enendeni Ulimwenguni mwote” aliwaagiza wanafunzi wake kuhubiri injili kwa kila kiumbe. Mungu anapotoa kazi hutoa pia vitendea kazi, alipowaagiza kuwa watu waende aliwapa uwezo.
Kusudi la vipawa vya Roho kwa Wakristo ni kuwawezesha k*timiza utume wa kanisa pamoja na ukuaji wake.
Mungu huwakirimia washiriki wote wa kanisa lake katika kila kizazi karama za kiroho ambazo kila mshiriki atatumia katika huduma ya upendo kwa ajili ya mema ya kawaida ya kanisa na wanadamu zikitolewa kwa wakala wa Roho mtakatifu, ambaye humgawia kila mshiriki k**a apendavyo yeye, karama hizo hutoa uwezo wote na huduma zinazohitajiwa na kanisa katika k*tekeleza shughuli zake zilizoamuriwa na Mungu kulingana na maandiko, karama hizi hujumuisha huduma k**a imani, uponyaji, unabii, mahubiri, mafundisho na ufadhili kwa ajili ya msaada na faraja kwa watu.
Baadhi ya washiriki huitwa na Mungu na kukirimiwa na Roho kwa ajili ya shughuli zinazotambuliwa na kanisa katika uchungaji,uinjilisti, utume na huduma za kufundisha zinazohitajika hasa kuwapatia zana washiriki kwa ajili ya huduma, kulijenga kanisa hadi ukomavu wa Kiroho na kukuza umoja wa imani na maarifa ya Mungu. Pale washiriki wanapozitumia karama hizi za kiroho k**a mawakili waaaminifu wa neema mbalimbali za Mungu, Kanisa hulindwa dhidi ya mivuto miharibifu ya mafundisho ya uongo na hukua kwa ukuaji unaotoka kwa Mungu na kujengeka imara katika Imani na Upendo (Warumi 12:4-8; Wakor 12:9-11, 27, 28 Waef 4:8, 11:1-6; Mdo 6:1-7; Tim 3:1-13; 1 Pet 4:10,11).
*SEHEMU YA TATU-WAKILI WA WAKATI (MUDA)*
Mungu ametupatia wakati. Muda wapaswa k*tumika kwa angalifu. Biblia inasema “Lolote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, k**a kwa Bwana wala si kwa wanadamu mkijua ya kuwa kwa Bwana kuna ujira wa urithi” (Kol 3,23,24).
Neno la Bwana linatuambia tusiwe wajinga tuwe werevu,tukiukomboa wakati kwa sababu zamani hizi ni za uovu. (Waefeso 5: 15, 16) K**a Yesu twapaswa kuwa kwenye shughuli za Bwana (Luka 2:49).
Muda ni zawadi k*toka kwa Mungu. Muda umetolewa k*tengeneza tabia kwa ajili ya ufalme wa Mbinguni.
Njia nne za kupoteza muda:-
- K*tofanya chochote
- K*tofanya kile ulichopaswa kufanya
- Kufanya vitu kwa uzembe
- K*tofanya vitu kwa wakati.
Ili kuonekana mawakili waaminifu Wakristo wanapswa kujiondoa wenyewe katika hali za namna hiyo.
Wakati ndani ya Biblia Marko 1:15,
- Zawadi ya Mungu kwa wanadamu
- Mungu hufanya kazi kwa wakati
- Kristo mhimili wa wakati
- Mtu hapaswi kufanya lolote atakalo bali apaswa kufanya pale Bwana anapomuagiza.
Mungu ndie mtoaji wa muda Zab: 10: 12 “ Utufundishe kuzihesabu siku zetu
Mungu yuko makini na muda Zab: 31: 16 muda wangu u mkononi mwako, Daniel 2:21 Yeye ndie anayeweza kubadili nyakati.
Kila jambo na wakati wake. Muhub 3:1, 8:6
*SEHEMU YA NNE-UWAKILI WA MALI*
Mungu aliwapatia wazazi wetu wa kwanza jukumu la kuitawala Dunia k*tawala wanyama kwa aina zake pia k*tunza Bustani ya Eden (Mwan 1:28; 2:15) Hii yote ilikuwa sio kufurahia bali pia kuangalia (Manage), jambo moja lilikuwa k**a sharti kwao lilikuwa k*tokula mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mti huu ulikuwa kwa ajili ya kuwa kumbusha kuwa Mungu mmiliki na wenye mamlaka ya mwisho Duniani hapa. Kwa k*tunzasharti hili wawili hawa walionyesha imani yao na utii wao kwao.
Baada ya kuanguka Mungu hakuweka kipimo cha utii katika mti. Lakini bado wanadamu walihitaji kukumbushwa kuwa Mungu ni chanzo cha vitu vyote vyema (Yakobo 1: 17) na kuwa yeye ametupatia nguvu kupata tulivyo navyo. (Kumbku 8:18) Ili k*tukumbusha kuwa yeye ni chanzo cha kila mbaraka, Mungu alianzisha mfumo wa zaka na sadaka.
*Zaka* – k**a vile moja ya saba ya muda wetu tunavyouweka kwa Bwana, vivyo moja ya kumi ya mali zetu twaziweka kwa Bwana pia. Biblia inatuambia zaka ni “Takatifu kwa Bwana” ikiashiria kuwa yeye ni mmiliki wa kila kitu. (Kumb 27:30,32)
Mungu anapoitisha zaka (Mal 3:10) hafanyi hivyo k**a shukrani au ukarimu. Ingawa shukurani yapaswa kuwa sehemu ya kumwonyesha Mungu. Tunatoa zaka kwa kuwa Mungu ameamuru hivyo. Zaka ni ya Bwana na ameagiza tumrudishie.
- Mifano ya utoaji wa zaka
Mwan 14:20 – Abraham alitoa zaka wa Melkzedeki
Mwab 28:22 – Yakobo pia alitoa zaka.
Kumb 27:30 – 32
Heb 18:24,26,28 Israel wanaagizwa k*toa zaka.
Nyakati 12:6,11,17
*Sadaka* - Wakristo wenye shukurani hawawekewi mipaka katika michango yao kanisani.
👉🏼Katika Israel hekalu lilijengwa kwa sadaka za hiari ya moyo (k*t 36:2 -7), Nyakati 29:14).
👉🏼Sadaka maalumu zilisaidia kufanya matengenezo katika sehemu za Ibada (K*to 30:12 – 16) 2 Falme 12:4,5; Kumb 24:4 -13; Nehemia 10:32,33).
_Leo pia Mungu anatuita k*toa kwa kadri tulivyobarikiwa. Sadaka zahitajiwa kujenga na kukarabati makanisa. Hii ikiwa ni pamoja na kuendesha shughuli mbalimbali za kanisa katika k*timiza utume._
*SEHEMU YA TANO-UWAKILI WA KUTUNZA DUNIA.*
Katika miaka ya hivi karibuni wanasayansi na wana mazingira wamegundua kuwa Dunia inaharibiwa na hivyo k**a matokeo ya uharibifu huu Dunia itakuwa sio mahali pa kuishi.
*MIBARAKA YA UWAKILI.*
Mungu ametupatia jukumu la uwakili kwa ajili ya manufaa yetu na wala sio kwa manufaa yake.
- *Mibaraka binafsi.*
- ```Uwakili hutusaidia kuondoa tabia za uchoyo ambazo Yesu amezikemea. (Luke 12:15).```
*Kwa habari ya zaka na sadaka Bwana ameahaidi baraka tele hata isiwemo nafasi ya k*tosha au la,*