26/06/2026
*MUHTASARI WA LESONI*
Robo ya Pili 2026 – Somo la 13:
*KATIKA UMILELE*
June 20–26, 2026
____🌹🌹____
Juma hili linahitimisha robo kwa *kuelekeza kwenye tumaini la milele.*
Tumejifunza kuwa,
- *Ingawa tunaishi katika ulimwengu uliojaa dhambi, mateso na majaribu, Mungu ametuandalia uzima wa milele kupitia Kristo.*
- *Wito mkuu ni kuishi leo katika uhusiano wa karibu na Yesu huku tukisubiri kesho kurudi kwake mkombozi.*
________ ________
*DONDOO*
- _Kuishi tayari kwa ujio wa Yesu._
- _Tumaini la mbingu mpya na nchi mpya._
- _Kumwona Yesu ana kwa ana._
- _Yerusalemu Mpya k**a makao ya waliokombolewa._
- _Wito wa kumfuata Mwana-Kondoo kila siku._
- _Mwaliko wa mwisho wa Mungu: *"Njoo."*_
____🌹🌹____
*MAUDHUI YA SOMO*
```Somo linaonyesha kuwa mwisho wa safari ya Mkristo si kaburi bali uzima wa milele pamoja na Kristo.```
Mungu anawaita watu wake kuendelea kukua katika uhusiano naye hadi watakapomwona uso kwa uso.
____🌹🌹____
*DHAMIRA*
Kuimarisha tumaini la uzima wa milele na kuwatia moyo waumini kuendelee kudumu katika Kristo tukisubiri kurudi kwake.
____🌹🌹____
*FUNGU LA KUKARIRI*
*_“Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona k**a alivyo.”_*
— 1 Yohana 3:2
*"Tutafanana naye"*
Tutafanywa wakamilifu katika tabia na utukufu, si kuwa miungu.
*"Tutamwona"*
Pasipo kizuizi cha dhambi, tukitazamana na Yesu, kuonana, kuongea na kukaa pamoja.
Ahadi hii inawahimiza waamini kuishi maisha ya utakatifu tukilitazamia tumaini hilo.
____🌹🌹____
*MATUMIZI MAISHANI LEO*
- _Dumisha uhusiano wa kila siku na Yesu Kristo Mkombozi._
- _Usiweke tumaini lako katika mali za dunia._
- _Ishi ukiwa tayari kwa kurudi kwa Kristo._
- _Washirikishe wengine tumaini la wokovu._
____🌹🌹____
*MUHTASARI WA KILA SIKU*
________ ________
Jumapili (21 June)
– *KUISHI LEO*
Zaburi 80
Ingawa tunatazamia mbingu, tunapaswa kuishi leo katika toba, maombi na uhusiano wa karibu na Mungu.
________ ________
Jumatatu (22 June)
– *HATIMAYE, ANA KWA ANA*
1 Wathesalonike 4:16-17
Kurudi kwa Yesu Kristo kutawaleta pamoja waliofufuliwa na walio hai ili kukutana na Kristo na kuwa naye milele.
________ ________
Jumanne (23 June)
– *BIBI HARUSI*
Ufunuo 21:9-27
Yerusalemu Mpya ni ishara ya makao ya milele ya waliokombolewa na uhusiano wa karibu kati ya Kristo na kanisa lake.
________ ________
Jumatano (24 June)
– *MFUATE MWANA-KONDOO*
Ufunuo 7:17; Isaya 25:8
Baraka kuu ya mbinguni si uzuri wake pekee bali kuwa na Yesu Kristo milele zote, ambaye ndiye Mchungaji wetu.
________ ________
Alhamisi (25 June)
– *NJOO!*
Mathayo 11:28-30; Yohana 6:44
Mungu bado anatoa mwaliko wa neema: *"Njoo."* kila mmoja anaalikwa kumjia Kristo kabla mlango wa rehema haujafungwa.
____🌹🌹____
*MASWALI NA MAJIBU*
________ ________
Swali 1:
*Ni nini kinakugusa katika maelezo ya mbinguni?*
Jibu:
Upendo wa Mungu, kutokuwepo kwa dhambi, mauti, machozi na kumwona Yesu uso kwa uso.
________ ________
Swali 2:
*Ni somo gani la robo unalotaka kulikumbuka?*
Jibu:
Kuendelea kukua katika uhusiano wa karibu na Mungu kila siku kwa njia ya Neno, maombi na imani.
________ ________
Swali 3:
*Ni nani unapaswa kumshirikisha tumaini hili?*
Jibu:
Wanafamilia, marafiki na wote ambao bado hawajampokea Kristo.
____🌹🌹____
*MASWALI YA ZIADA*
________ ________
*(a) Maswali ya Biblia*
1. Kwa nini Yesu anarudi?
- *Kuwachukua waliokombolewa kwake (Yohana 14:1-3).*
2. Kwa nini tumaini la mbinguni ni muhimu?
- *Hutupa nguvu ya kuvumilia majaribu (Warumi 8:18).*
3. Ni nani watakaoingia mbinguni?
- *Wote waliompokea Kristo Yesu kwa imani (Yohana 3:16).*
________ ________
*(b) Maswali ya Wapinzani*
1. Je, mbinguni ni hadithi?
- *Hapana. Yesu aliahidi kuandaa makao (Yohana 14:2-3).*
2. Kwa nini Yesu Kristo hajarudi bado?
- *Mungu anavumilia ili wengi wapate kutubu (2 Petro 3:9).*
3. Kwa nini waumini bado wanateseka?
- *Dhambi bado ipo duniani, lakini mateso yatakoma Kristo atakaporudi (Ufunuo 21:4).*
____🌹🌹____
*REJEA ZA FAFANUZI ZA ZIADA*
Ujisomee kwa kupata uelewa zaidi
________ ________
Pambano Kuu (The Great Controversy), uk. 354 – Yerusalemu Mpya na Bibi-arusi.
________ ________
Pambano Kuu, uk. 556 – *Utukufu wa mbingu hauwezi kuelezwa kikamilifu.*
________ ________
The Faith I Live By, uk. 363 – *Waamini wajifunze kuzungumza na kutafakari kuhusu mbingu.*
________ ________
________ ________
Na
EV. K. KUBOJA
0763740320
0656340320
*BARIKIWA*