Kiseke SDA Church

Kiseke SDA Church TO PREPARE PEOPLE FOR INTERNAL LIFE

25/11/2025

```DIRA YA UINJILISTI```

Usinyamaze ikiwa Bwana Mungu ametoa agizo, amka na fanyia kazi

____🌹🌹____
*Uinjilisti ni moyo wa injili na kiini cha wito wa kanisa la Mungu.* Kanisa halipo kwa ajili ya kujihudumia lenyewe bali kwa ajili ya *“kuhubiri injili kwa kila kiumbe”* (Marko 16:15).

*_Katika teolojia ya Waadventista wa Sabato, uinjilisti ni ushiriki wa mwanadamu katika kazi ya Kristo ya kuokoa wanadamu, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu._*

____🌹🌹____

```DIRA KUU```

*“Kanisa la Mungu lipo duniani kwa kusudi moja kuu, kueneza nuru ya ukweli wa wokovu kwa ulimwengu mzima.”*
— Testimonies for the Church, Vol. 6, uk. 11.

Dira hii inatokana na agizo la Kristo:
*“Basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza...”*
— Mathayo 28:19–20.

Kanisa k**a chombo cha uinjilisti:
*Kila muumini ni sehemu ya mwili wa Kristo na ameitwa kushiriki katika huduma ya injili*
(1 Wakorintho 12:27; Warumi 10:14–15).

____🌹🌹____

```MISINGI YA KIMAANDIKO YA UINJILISTI```

🌹🌹
Mathayo 28:18–20
Agizo Kuu la Kristo ambalo ni wito wa uinjilisti kwa wote.

🌹🌹
Marko 1:17
Yesu aliwaita wafuasi wake wawe *“wavuvi wa watu.”*

🌹🌹
Matendo 1:8
*Uwepo wa Roho Mtakatifu ni nguvu ya Uinjilisti.*

🌹🌹
2 Timotheo 4:2
Hubiri Neno kwa wakati ufaao na usiofaa.

🌹🌹
Ufunuo 14:6–12
*Ujumbe wa malaika watatu, ndiyo msingi wa uinjilisti wa Waadventista wa Sabato.*

____🌹🌹____

Ufafanuzi wa Biblia:

*Uinjilisti wa kweli ni matokeo ya kuishi kwa injili. Biblia inaonyesha kuwa wale waliok*tana na Kristo walihubiri mara moja (Yohana 4:28–30). Uinjilisti sio tukio, ni mtindo wa maisha ya Mkristo.*

____🌹🌹____

*“Kila Mwana wa Mungu amewekwa wakfu kwa kazi ya uinjilisti. Yeye ambaye amepokea nuru anatakiwa kuifanya ing’ae kwa wengine.”*
— The Desire of Ages, uk. 822.

*“Kanisa limepewa kazi ya kuupeleka ulimwenguni ujumbe wa malaika watatu... Hii ndiyo kazi ya mwisho, kubwa, ya rehema.”*
— Evangelism, uk. 119.

*“Uinjilisti wa kweli unahusisha huduma ya mtu kwa mtu, moyo kwa moyo.”*
— Ministry of Healing, uk. 143.

*“K**a kanisa lingetenda kazi ambayo Mungu ameliamuru, ulimwengu wote ungepata onyo kwa siku chache, na Bwana Yesu angekuja haraka.”*
— Christian Service, uk. 111.

____🌹🌹____

*“Huduma ya uinjilisti ni wajibu wa kila mshiriki wa kanisa. Wote wameitwa k*toa ushuhuda wa imani yao katika Kristo, kwa maneno na matendo.”*
(Church Manual, 21st Edition, Kifungu cha 8, “Evangelism and Witnessing.”)

Kanisa linapendekeza aina za uinjilisti:
- Uinjilisti wa nyumbani na ujirani.
- Uinjilisti wa vikundi vidogo (small groups).
- Uinjilisti wa vijana, wanawake, na shule ya Sabato.
- Uinjilisti wa redio, televisheni, na mitandao ya kijamii.
- Uinjilisti wa wagonjwa (Medical Missionary Work).

*“Kazi ya Mungu duniani haitamalizika mpaka wanaume na wanawake wa kawaida, wanaojazwa na Roho Mtakatifu, wafanye kazi ya kuhubiri injili nyumbani na majirani.”*
Acts of the Apostles, uk. 111

____🌹🌹____

Mathayo 28:19–20
*“Amri hii ni ya wote wanaomwamini Kristo. Wale waliopokea wokovu hawapaswi kuutunza wao peke yao. Wameitwa kushirikisha wengine. Hivyo kanisa linakuwa ‘taifa takatifu’ linaloitwa k*toka gizani kwenda katika nuru ya ajabu.”*
— Seventh Day Adventist Bible Commentary, Vol. 5, uk. 641.

Ufunuo 14:6–12
*“Malaika watatu wanaashiria watu wa Mungu wanaotoa ujumbe wa onyo wa mwisho kwa ulimwengu kabla ya kurudi kwa Kristo. Ni uinjilisti wa dunia nzima unaolenga kumrudisha mwanadamu katika ibada ya kweli kwa Muumba.”*
— Seventh Day Adventist Bible Commentary, Vol. 7, uk. 823.

____🌹🌹____

```HUDUMA ZA KANISA```

🌹🌹
(a) Kwa Waumini Wote:

- *Kila mshiriki* aone uinjilisti k**a wajibu binafsi, si kazi ya wachungaji pekee.

- *Kila nyumba* iwe kituo cha nuru na ushuhuda (Mathayo 5:14–16).

🌹____🌹
(b) Kwa Viongozi wa Kanisa:

- *Waandae mpango wa Uinjilisti wa kudumu, si wa msimu.*

- *Wapewe mafunzo ya Uinjilisti wa vitendo kwa waumini.*

- Watumie Shule ya Sabato, kwaya, idara ya vijana, wanawake, na Watoto k**a vyombo vya uinjilisti.

🌹____🌹
(c) Kwa Vijana:

- Watumie vipaji vyao (muziki, michezo, mitandao ya kijamii) kufikisha injili.

- Wajifunze kuwa *“mishenari wa kisasa”* kwa k*tumia teknolojia.

____🌹🌹____
Wito:
- Leo Kristo anaita kila Mwumini kuwa shahidi Wake.

*“Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.”*
— Mathayo 9:37.

*Tuamke, tushike kazi, tuhubiri injili ya milele!*

____🌹🌹____
____🌹🌹____

Na
EV. K KUBOJA
0763740320
0656340320

*TUWE NA TAFAKARI NJEMA NA SIKU NJEMA WOTE*

06/09/2025

```KAYA NA FAMILIA```

*NINAWAZA KUHUSU FAMILIA YA ELI*

Naomba tutafakari pamoja;

*"Wana wa Eli walikuwa watu waovu; hawakumjua Bwana. Walikataa kuwasilisha mioyo yao kwa Mungu, na dhambi zao zilitenda juu ya madhabahu ya Bwana. Walidhihaki kafara na walijitia unajisi kwa uasherati. Wote waliokuja kuhani k*tolea sadaka walichukizwa na maovu yao. Hawak*tubu; WALIKUFA KATIKA UASI WAO.”*
— Patriarchs and Prophets, uk. 575–581

*"Eli aliheshimika k**a kuhani na mwamuzi wa Israeli. Lakini kosa lake kuu lilikuwa kulea kwa upole mno na kuachilia watoto wake kufanya maovu. Alikuwa akiwapenda sana kiasi cha k*toshika nidhamu kali. Kwa hivyo, alihesabiwa na Mungu mwenye hatia sawa na wanawe, kwa sababu alishindwa kuwazuia katika maovu yao.”*
— Patriarchs and Prophets, uk. 575–577

*"Moyo wake ulijaa huzuni kuu kwa sababu ya makosa ya wanawe, na alikufa kwa uchungu baada ya kupata habari ya maafa yaliyowapata. Ingawa alishindwa k**a baba na kuhani, alikufa akiwa amejutia udhaifu wake.”*
— Patriarchs and Prophets, uk. 582

🌹🌹____🌹🌹____🌹🌹

1. ```KUHUSU HOFIN NA FINEHASI```

- *_Walipewa nafasi kubwa ya kuhudumu madhabahuni, lakini walidharau utakatifu wa huduma ya Mungu_*
1 Samweli 2:12–17

- *_Walifanya maovu ya wazi (kula sadaka za Bwana kinyume na sheria, uasherati), bila toba_*
1 Samweli 2:22–25).

- *_Biblia inasema: “Bwana alikusudia kuwaua” (1 Sam. 2:25), kwa sababu walikataa onyo._*

*TUNAJIFUNZA*

🌹____🌹🌹____🌹
- Upendeleo wa kuzaliwa katika familia ya Kikristo au ya kiutendaji haumaanishi wokovu. *Wokovu ni maamuzi ya kibinafsi.*

🌹____🌹🌹____🌹
- Ukifanya dhambi bila k*tubu, hata k**a uko karibu na madhabahu, utapotea.

🌹____🌹🌹____🌹
- Uongozi au ibada bila moyo safi ni unafiki mbele za Mungu.

🌹🌹____🌹🌹____🌹🌹

2. ```KUHUSU ELI – KUHANI ALIYE LEGEA```

- *_Alikuwa mtumishi mwaminifu kwa Mungu, lakini dhaifu katika nidhamu._*

- *_Alipenda watoto wake kuliko heshima ya Mungu (1 Sam. 2:29)._*

- *_Alijutia udhaifu wake mwishoni, lakini alihesabiwa mwenye hatia kwa kulea vibaya (PP, 575–582)._*

*TUNAJIFUNZA*

🌹____🌹🌹____🌹
- Wazazi wana wajibu mkubwa wa kulea kwa nidhamu na kumfundisha mtoto kumcha Mungu (Mithali 22:6; Waefeso 6:4).

🌹____🌹🌹____🌹
- Upendo wa kweli si kuachilia, bali kurekebisha kwa upole na uthabiti.

🌹____🌹🌹____🌹
- Kulea vibaya watoto ni kosa kubwa linaloweza kuangamiza vizazi.

🌹🌹____🌹🌹____🌹🌹

3. ```KUHUSU FAMILIA YOTE – HATMA YAO```

- *_Familia nzima ilipata aibu:_*

- *_Sanduku la agano liliibwa (1 Sam. 4:10–11)._*

- *_Hofni na Finehasi waliuawa._*

- *_Eli alianguka na kufa baada ya kusikia habari hizo (1 Sam. 4:18)._*

Historia yao ni mfano wa ukosefu wa nidhamu nyumbani kuathiri taifa zima.

*TUNAJIFUNZA*

🌹____🌹🌹____🌹
- Familia ni shule ya kwanza ya maadili. Taifa zuri huanza na familia yenye nidhamu.

- Kudharau utakatifu wa Mungu na ibada hupelekea hukumu ya waziwazi.

- Mungu ni mwenye rehema, lakini wakati wa rehema ukikataliwa, hukumu inafuata.

```FUNZO KUU LA KIROHO```

*Toba ni nafasi ya kibinafsi – kila mtu atahesabiwa kwa uamuzi wake.*

*Tunapaswa kuheshimu utakatifu wa ibada na huduma ya Mungu.*

*Wazazi na viongozi wa kiroho wanao wajibu wa pekee wa kuwa kielelezo na kusimamia nidhamu.*

*ZINGATIA* 👇
Hatma ya familia ya Eli ni onyo la wazi kwamba:

*"Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.”* (Wagalatia 6:7).

Na
EV. K. KUBOJA
+255763740320
+255656340320

*TUBARIKIWE*

26/08/2025

HAMARTIOLOGY

Somo la Kwanza: ASILI YA DHAMBI

Fungu Kuu:
Warumi 5:12 – “Kwa hiyo, k**a kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti ikawafikia watu wote...”

Muhtasari

1. Ufafanuzi wa dhambi – K*tenda kinyume cha sheria ya Mungu (1 Yohana 3:4).

2. Chanzo cha dhambi – Lusifa (Isaya 14:12-14; Ezekieli 28:12-17).

3. Kuingia kwa dhambi kwa mwanadamu – Hekalu la Edeni (Mwanzo 3).

4. Asili ya dhambi – siyo tu matendo mabaya, bali hali ya moyo (Yeremia 17:9; Marko 7:21-23).

5. Roho ya Unabii – “Dhambi ni uvunjaji wa sheria ya Mungu, na k*toka kwa uvunjaji huo wote huzuni na mateso ya wanadamu yametokana” (Ellen G. White, Steps to Christ, uk. 23).

Malengo

Kuelewa dhambi ni nini.

K*tambua chanzo chake na kuingia kwake kwa wanadamu.

K*tambua uharibifu wa dhambi kwa tabia ya mwanadamu.

---

Somo la Pili: HALI NA ATHARI ZA DHAMBI

Fungu Kuu: Warumi 3:23 – “Kwa maana wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.”

Muhtasari

1. Ulimwengu wote uko chini ya dhambi – Hakuna mwenye haki (Warumi 3:10-12).

2. Athari kwa mwanadamu –

Kiroho: k*tengwa na Mungu (Isaya 59:2).

Kimaumbile: kifo na uharibifu (Warumi 6:23).

Kijamii: chuki, vurugu, uhasama (Yakobo 4:1).

3. Tabia ya dhambi – Hudanganya, huteka mateka, huua (Yohana 8:34, 44).

4. Roho ya Unabii – “Dhambi ni kitu cha k*tisha. Ilichanganya akili za malaika waliokamilika, na kumtesa Mwana wa Mungu” (Great Controversy, uk. 492).

5. Dhambi binafsi na dhambi za kurithi – (K*t. 20:5; Zaburi 51:5).

Malengo

Kuelewa uzito wa hali ya dhambi.

Kuona namna dhambi inavyoathiri kila nyanja ya maisha.

Kuzingatia haja ya wokovu.

---

Somo la Tatu: SULUHISHO LA MUNGU DHIDI YA DHAMBI

Fungu Kuu: Yohana 1:29 – “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”

Muhtasari

1. Ahadi ya wokovu – Mwanzo 3:15 (proto-evangelium).

2. Kifo cha Kristo msalabani – fidia ya dhambi (Isaya 53:5-6; 2 Wakorintho 5:21).

3. Ukombozi kwa neema kwa imani – Efeso 2:8-9.

4. Nguvu ya Kristo dhidi ya dhambi – Roho Mtakatifu hutupa uwezo wa kushinda (Warumi 8:1-4).

5. Roho ya Unabii – “Kwa kifo chake Kristo aliharibu nguvu za Shetani juu ya wanadamu” (Desire of Ages, uk. 490).

6. Ushindi wa mwisho dhidi ya dhambi – Ufunuo 21:4, 27.

Malengo

Kuonyesha upendo wa Mungu kwa mwanadamu mwenye dhambi.

Kufundisha kuwa wokovu ni kwa neema kupitia Kristo pekee.

K*tilia mkazo ushindi dhidi ya dhambi kwa nguvu ya Kristo.

---

Maswali ya Kujadili (Kwa Kila Somo)

Somo la 1: Asili ya Dhambi

1. Je, dhambi ni tendo tu au pia ni hali ya moyo?

2. Kwa nini Mungu alimruhusu Lusifa kuchagua uasi badala ya kumwangamiza mara moja?

3. Je, dhambi ya Adamu na Hawa inatufundisha nini kuhusu uhuru wa kuchagua?

Somo la 2: Hali na Athari za Dhambi

1. Kwa nini hata watoto wachanga huchukuliwa kuwa katika hali ya dhambi?

2. Je, ni namna gani dhambi inavyoathiri familia na jamii leo?

3. Kwa nini watu wengi hawaoni uzito wa dhambi hadi madhara yake yajitokeze?

Somo la 3: Suluhisho la Mungu Dhidi ya Dhambi

1. Kwa nini Kristo pekee ndiye anayeweza k*tuokoa k*toka dhambini?

2. Neema ya Mungu inamaanisha nini kwako binafsi?

3. Tunawezaje kuishi maisha ya ushindi juu ya dhambi katika ulimwengu huu uliojaa vishawishi?

04/11/2022

*UWAKILI UWAKILI UWAKILI*


“Sisi tu Mawakili wa Mungu tuliokabidhiwa na yeye wakati, fursa, uwezo na mali na mibaraka ya dunia na rasimali zake. Tunawajibika kwake kwa matumizi yake sahihi. Tunakiri umilikaji wa Mungu kwa huduma ya uaminifu kwake na wanadamu wenzetu, na kwa kurudisha zaka na k*toa sadaka kwa ajili yake na kwa utegemezaji na ukuaji wa Kanisa lake. Uwakili ni fursa iliyotolewa kwetu na Mungu kwa ajili ya malezi katika upendo na ushindi dhidi yao choyo na tamaa. Wakili hufurahia mibaraka inayowajia wengine k**a matokeo ya uaminifu wake” (Kanuni ya Kanisa toleo la 17 sura 3-12).

Zaidi ya chochote kingine, kuishi maisha ya kikristo ina maana ya kujitoa – kujisalimisha sisi wenyewe na kumkubali Kristo. K**a vile yeye alivyojitoa kwa ajili yetu, Je sisi tutafanya nini kwa ajili yake?

Mungu hategemei wanadamu kuisukuma kazi yake au kuiendeleza injili. Angeweza kuwatumia malaika kuwa mabalozi wa kweli yake. Angeweza kuwajulisha wanadamu mapenzi yake k**a alivyofanya katika mlima wa Sinai kwa sauti yake mwenyewe. Lakini ili kuendeleza roho ya utoaji kujitoa kwetu, amechagua kuwatumia wanadamu kuifanya kazi yake (Counsels on Steward ship page 20).

Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo na Mawakili wa siri za Mungu. Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu” (1 Kor 3:21- 4:2).

```UWAKILI NINI?```

“ *Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni Hekalu la Roho Mtakatifu…………… wala ninyi si mali yenu wenyewe? Maana mlinunuliwa kwa thamani sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu (1 Kor 6:19,20) kwa gharama kubwa tulinunuliwa na kukombolewa. Sisi ni wa Bwana. Hiyo ni k*tufanya kuwa watu wake kwa mara ya pili kwa kuwa alituumba na k*tukomboa. Biblia hueleza kwa uwazi kabisa kwamba Dunia na vyote vilivyomo ni mali yake na wote wakao humo (Zab 24:1)*

Ni katika uumbaji Mungu alimshirikisha mwanadamu katika kumiliki na aliendelea kuwa mmiliki wa kweli wa ulimwengu, walezi wa vitu vyake (Zab 24:1)

*Wakili ni mtu* “aliyekabidhiwa uangalizi wa mali ya mtu mwingine” Uwakili ni nafasi , majukumu. Kwa mkristo uwakili una maana jukumu la mwanadamu kuwa na matumizi ya chochote alichokabidhiwa na Mungu- Uhai, mwili, muda, talanta na uwezo, mali fursa ya kuwahudumia wengine na ujuzi wake wa kweli. Wakristo hutumika k**a waangalizi ( Mameneja) wa mali za Mungu na kuangalia maisha k**a fursa ya kimbingu, kujifunza kuwa waaminifu katika uwakili,hutufanya tufae kwa uwakili uliotukuka zaidi na umilele wa maisha ya baadae.

```Katika upana wake hivyo basi, uwakili unahusisha matumizi ya busara na k*tokuwa wabinafsi wa maisha.```

*NAMNA YA KUTAMBUA UWAKILI WA MUNGU.*

Maisha yaweza kugawanyika katika sehemu kuu nne za msingi na kila sehemu ni zawadi ya Mungu kwetu.

Mungu ametupatia mwili, uwezo, muda pamoja na umiliki wa mali pamoja na hayo twapaswa k*tunza mazingira ya dunia ambayo Mungu ametupatia.

*SEHEMU YA KWANZA- UWAKILI WA MWILI*

Watu wa Mungu ni mawakili wa wao wenyewe twapaswa kumpenda Mungu kwa mioyo yetu yote na kwa nguvu zetu zote na akili zetu zote (Luka 10:27).

Wakristo wamepewa fursa ya kukuza nguvu zao za kimwili na kiakili kwa ngazi ya juu. Kwa kufanya hivyo huleta heshima kwa Mungu na kuwakilisha baraka kuu wanadamu wenzao.

Mungu ametuita k**a Wakristo kuwa watu wenye afya tele kwani miili yetu ni hekalu la Roho mtakatifu.

Iko mibaraka tele ambayo Mungu ametupatia kuweza kuwa na afya bora. Mibaraka hiyo ni k**a ifuatavyo:-

- Mibaraka ya mazoezi
- Mibaraka ya mwangaza wa jua
- Mibaraka ya maji
- Mibaraka ya Hewa safi
- Mibaraka ya kuwa na kiasi
- Mibaraka ya kupumzika.

Uwakili wa mwili ni pamoja na kuuvika mwili mavazi yanayostahili. Wakati ulimwengu unakwenda na mavazi yasiyofaa, wakristo mameitwa kuinua hadhi ya mavazi katika kiwango cha Ukristo.

Sisi tu mali ya Mungu , mwili nafsi na Roho kwa hiyo ni wajibu wetu wa kidini kushika sheria za afya, kwa ajili ya vyote, hali njema na furaha yetu sisi wenyewe, na pia kwa ajili ya huduma yenye ufanisi kwa Mungu na kwa wanadamu wenzetu. Hamu ya kula chakula sharti idhibitiwe. Afya hutumiwa kwa kuzingatia akili kwa kanuni za afya zinazohusiana na hewa safi, upitishaji wa hewa safi,nguo zifaazo,usafi,mazoezi ya kufaa na maburudisho,usingizi tosha na pumziko na lishe tosha iletayo siha. Mungu amempa mwanadamu chakula chema cha aina nyingi ili k*tosheleza kila hitaji la lishe; matunda, nafaka, njugu na mboga zilizoandaliwa kwa njia rahisi pamoja na maziwa………………. hufanya lishe yenye afya mno” (Christian Temperancy and Bible Hygene Uk 47).

Wakristo waepuke kuonyesha urembo na madoido mengi ikiwezekana nguo ziwe za namna bora na rangi zinazopendeza na zifaazo kwa huduma. Zichaguliwe k*tokana na kudumu kwake kuliko kwa ajili ya onyesho.Uvaaji udhihirishe na adabu nzuri heshima na zinazofaa kwa onyofu wa asili (Messages to Young people Uk 352).

Neno la Bwana linabakia pale pale, likisema “ Ninyi ni nuru ya Ulimwengu mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango, nayo yawaangaza wote walioko nyumbani. Vivyo hivyo Nuru yenu na iangaze mbele ya watu wapate kuyaona matendo yenu mema wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni” (Matayo 5: 14:16)

Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri, kujisikia na k*tenda kulingana na kanuni za mbinguni. Ili Roho aumbe upya ndani yetu tabia ya Bwana wetu twapaswa kujihusisha tu katika mambo yale ambayo yatazaa katika maisha yetu usafi unaofanana na Kristo, hii italeta afya na furaha katika maisha yetu. Hii inamaanisha kwamba maraha na maburudisho yetu yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji na uzuri wa Kikristo. Huku tukitambua tofauti za Kiutamaduni, mawazo yetu yanapaswa yawe ya kawaida si ya anasa na safi yanayostahili wale ambao uzuri wao wa kweli asili yake sio mambo ya nje bali asili yake ni mapambo yasiyoharibika yenye Roho ya upole na utulivu. Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa miili yetu ni mahekalu ya Roho mtakatifu yatunapasa k*tumia kwa akili. Pamoja na mazoezi tosha na mapumziko, yatupasa kuchagua lishe yenye afya. Kwavyovyote vile twapaswa kuepuka vyakula vilivyo najisi vilivyotajwa kwenye maandiko matakatifu. Kwa vile madawa hudhuru miili yetu, yatupasa kuepukana navyo pia. Badala yake tunapaswa kujishughulisha na chochote kile kinacholeta mawazoni mwetu na miili yetu nidhamu ya Kristo ambaye hutamani uzima wetu , furaha na wema.

Mafungu ya ziada

Warumi 12:1, 2. 1Yoh 2:6, Waef 5:1-2; Waf 4:8 2 Kor 10:5, 6 14-7, 1 Pet 3:1-4; 1 Wakr 6: 19,20 10:31; Walawi 11: 1-4, 7, 3 Yoh 2

*SEHEMU YA PILI-WAKILI WA TALANTA*

Kila mmoja wa watoto wa Bwana amepewa uwezo; mmoja aweza kupewa uwezo wa uimbaji, mwingine uwezo wa Biashara au ufundi wa magari au mmoja aweza k*tengeneza marafiki kwa urahisi lakini mwingine hutenda kazi kwa ukimya lakini k*tenda kazi kwa umakini na kwa uzuri wote.

Kila uwezo waweza k*tumika kumtukuza mwenye k*tumia au kumtukuza yeye aliyeitoa ambaye ni Mungu wa mbinguni.

Maneno ya Yesu mwenyewe aliyoyasema kabla hajapaa kwenda Mbinguni alisema “Enendeni Ulimwenguni mwote” aliwaagiza wanafunzi wake kuhubiri injili kwa kila kiumbe. Mungu anapotoa kazi hutoa pia vitendea kazi, alipowaagiza kuwa watu waende aliwapa uwezo.

Kusudi la vipawa vya Roho kwa Wakristo ni kuwawezesha k*timiza utume wa kanisa pamoja na ukuaji wake.

Mungu huwakirimia washiriki wote wa kanisa lake katika kila kizazi karama za kiroho ambazo kila mshiriki atatumia katika huduma ya upendo kwa ajili ya mema ya kawaida ya kanisa na wanadamu zikitolewa kwa wakala wa Roho mtakatifu, ambaye humgawia kila mshiriki k**a apendavyo yeye, karama hizo hutoa uwezo wote na huduma zinazohitajiwa na kanisa katika k*tekeleza shughuli zake zilizoamuriwa na Mungu kulingana na maandiko, karama hizi hujumuisha huduma k**a imani, uponyaji, unabii, mahubiri, mafundisho na ufadhili kwa ajili ya msaada na faraja kwa watu.

Baadhi ya washiriki huitwa na Mungu na kukirimiwa na Roho kwa ajili ya shughuli zinazotambuliwa na kanisa katika uchungaji,uinjilisti, utume na huduma za kufundisha zinazohitajika hasa kuwapatia zana washiriki kwa ajili ya huduma, kulijenga kanisa hadi ukomavu wa Kiroho na kukuza umoja wa imani na maarifa ya Mungu. Pale washiriki wanapozitumia karama hizi za kiroho k**a mawakili waaaminifu wa neema mbalimbali za Mungu, Kanisa hulindwa dhidi ya mivuto miharibifu ya mafundisho ya uongo na hukua kwa ukuaji unaotoka kwa Mungu na kujengeka imara katika Imani na Upendo (Warumi 12:4-8; Wakor 12:9-11, 27, 28 Waef 4:8, 11:1-6; Mdo 6:1-7; Tim 3:1-13; 1 Pet 4:10,11).

*SEHEMU YA TATU-WAKILI WA WAKATI (MUDA)*

Mungu ametupatia wakati. Muda wapaswa k*tumika kwa angalifu. Biblia inasema “Lolote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, k**a kwa Bwana wala si kwa wanadamu mkijua ya kuwa kwa Bwana kuna ujira wa urithi” (Kol 3,23,24).

Neno la Bwana linatuambia tusiwe wajinga tuwe werevu,tukiukomboa wakati kwa sababu zamani hizi ni za uovu. (Waefeso 5: 15, 16) K**a Yesu twapaswa kuwa kwenye shughuli za Bwana (Luka 2:49).

Muda ni zawadi k*toka kwa Mungu. Muda umetolewa k*tengeneza tabia kwa ajili ya ufalme wa Mbinguni.


Njia nne za kupoteza muda:-

- K*tofanya chochote
- K*tofanya kile ulichopaswa kufanya
- Kufanya vitu kwa uzembe
- K*tofanya vitu kwa wakati.

Ili kuonekana mawakili waaminifu Wakristo wanapswa kujiondoa wenyewe katika hali za namna hiyo.

Wakati ndani ya Biblia Marko 1:15,

- Zawadi ya Mungu kwa wanadamu
- Mungu hufanya kazi kwa wakati
- Kristo mhimili wa wakati
- Mtu hapaswi kufanya lolote atakalo bali apaswa kufanya pale Bwana anapomuagiza.

Mungu ndie mtoaji wa muda Zab: 10: 12 “ Utufundishe kuzihesabu siku zetu

Mungu yuko makini na muda Zab: 31: 16 muda wangu u mkononi mwako, Daniel 2:21 Yeye ndie anayeweza kubadili nyakati.

Kila jambo na wakati wake. Muhub 3:1, 8:6

*SEHEMU YA NNE-UWAKILI WA MALI*

Mungu aliwapatia wazazi wetu wa kwanza jukumu la kuitawala Dunia k*tawala wanyama kwa aina zake pia k*tunza Bustani ya Eden (Mwan 1:28; 2:15) Hii yote ilikuwa sio kufurahia bali pia kuangalia (Manage), jambo moja lilikuwa k**a sharti kwao lilikuwa k*tokula mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mti huu ulikuwa kwa ajili ya kuwa kumbusha kuwa Mungu mmiliki na wenye mamlaka ya mwisho Duniani hapa. Kwa k*tunzasharti hili wawili hawa walionyesha imani yao na utii wao kwao.

Baada ya kuanguka Mungu hakuweka kipimo cha utii katika mti. Lakini bado wanadamu walihitaji kukumbushwa kuwa Mungu ni chanzo cha vitu vyote vyema (Yakobo 1: 17) na kuwa yeye ametupatia nguvu kupata tulivyo navyo. (Kumbku 8:18) Ili k*tukumbusha kuwa yeye ni chanzo cha kila mbaraka, Mungu alianzisha mfumo wa zaka na sadaka.

*Zaka* – k**a vile moja ya saba ya muda wetu tunavyouweka kwa Bwana, vivyo moja ya kumi ya mali zetu twaziweka kwa Bwana pia. Biblia inatuambia zaka ni “Takatifu kwa Bwana” ikiashiria kuwa yeye ni mmiliki wa kila kitu. (Kumb 27:30,32)

Mungu anapoitisha zaka (Mal 3:10) hafanyi hivyo k**a shukrani au ukarimu. Ingawa shukurani yapaswa kuwa sehemu ya kumwonyesha Mungu. Tunatoa zaka kwa kuwa Mungu ameamuru hivyo. Zaka ni ya Bwana na ameagiza tumrudishie.

- Mifano ya utoaji wa zaka

Mwan 14:20 – Abraham alitoa zaka wa Melkzedeki

Mwab 28:22 – Yakobo pia alitoa zaka.

Kumb 27:30 – 32

Heb 18:24,26,28 Israel wanaagizwa k*toa zaka.

Nyakati 12:6,11,17

*Sadaka* - Wakristo wenye shukurani hawawekewi mipaka katika michango yao kanisani.
👉🏼Katika Israel hekalu lilijengwa kwa sadaka za hiari ya moyo (k*t 36:2 -7), Nyakati 29:14).
👉🏼Sadaka maalumu zilisaidia kufanya matengenezo katika sehemu za Ibada (K*to 30:12 – 16) 2 Falme 12:4,5; Kumb 24:4 -13; Nehemia 10:32,33).

_Leo pia Mungu anatuita k*toa kwa kadri tulivyobarikiwa. Sadaka zahitajiwa kujenga na kukarabati makanisa. Hii ikiwa ni pamoja na kuendesha shughuli mbalimbali za kanisa katika k*timiza utume._

*SEHEMU YA TANO-UWAKILI WA KUTUNZA DUNIA.*

Katika miaka ya hivi karibuni wanasayansi na wana mazingira wamegundua kuwa Dunia inaharibiwa na hivyo k**a matokeo ya uharibifu huu Dunia itakuwa sio mahali pa kuishi.

*MIBARAKA YA UWAKILI.*

Mungu ametupatia jukumu la uwakili kwa ajili ya manufaa yetu na wala sio kwa manufaa yake.

- *Mibaraka binafsi.*

- ```Uwakili hutusaidia kuondoa tabia za uchoyo ambazo Yesu amezikemea. (Luke 12:15).```

*Kwa habari ya zaka na sadaka Bwana ameahaidi baraka tele hata isiwemo nafasi ya k*tosha au la,*

04/05/2022

UNYENYEKEVU – KUUTAFUTA - KUGEUKA.

“Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” – 2 Nyakati 7:14.

"Toba, unyenyekevu, roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Mungu hataudharau." (Review and Herald, 12/19/1899)

Changamoto ya Moyo.

Dhambi ni mbaya sana na ya k*tisha, kiasi kwamba hakuna kitu tunachoweza kufanya, hakuna kiasi cha mambo mema kinachoweza kuondoa makovu yaliyosababishwa na dhambi. Lakini Mungu katika rehema yake isiyokuwa na kikomo hatuambii kwamba tufanye kile tunachoweza kufanya wenyewe. Anakubali hali ya kujitoa kwa kawaida, kwenye unyenyekevu kwamba tunamhitaji.
Je, unahisi kuhitaji msamaha wake? Uponyaji wake? Unaweza kuwa na huo uponyaji, tena leo hii! Unachotakiwa kufanya ni kumgeukia Yesu sasa hivi na kuomba huku ukiungama dhambi zako. Kisha chagua kuamini neema yake toshelevu ili ikuwezeshe k*tembea kadiri unavyoupatia kisogo udhaifu na kugeukia haki yake.

Mambo ya Kuombea:

• Omba Mungu akudhihirishie hitaji lako kuu la nerma yake.

• Omba Mungu akusaidie kuamini nguvu zake na kupata ushindi katika jitihada zako za kila siku dhidi ya dhambi.

• Omba kwa ajili ya kumwagwa kwa Roho Mtakatifu kwa Mchungaji wa kanisa lako.

• Omba Mungu arekebishe mahusiano yaliyovunjika katika Maisha yanayohitaji kurejeshwa na kukupatia moyo wa toba na unyenyekevu wa kweli ikiwa ulikuwa umewajeruhi wengine.

HAKUNA MUUJIZA WA UAMSHO UTATOKEA PASIPO KUOMBA HIVYO NI LAZIMA KUDAI KWA DHATI AHADI HII MUHIMU YA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.

MUNGU HUJIBU MAOMBI TUNAPOOMBA KWA IMANI NA KWA UNYENYEKEVU MWINGI.

TUWE NA SIKU NJEMA YA MAOMBI.
🙏🙏🙏🙏

04/05/2022

*KESHA LA ASUBUHI*

*JUMATANO, MEI 4, 2022*

*SIKU SITA KWA AJILI YETU, MOJA TU KWA MUNGU*

" _Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA Mungu wako.... Kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa_ ." K*toka 20:8-11.

▶️ Mwanzoni kabisa mwa amri ya nne, Mungu alisema, "Kumbuka," akijua kuwa wanaume na wanawake, katika wingi wa wasiwasi na mashaka yao, wanaweza kujaribiwa kujipatia udhuru wenyewe k*totimiza matakwa kamili ya sheria au, katika msongo wa shughuli za kidunia, wangesahau umuhimu wake mtakatifu. "Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote," shughuli za kawaida za maisha, kwa ajili ya faida au raha za dunia. Maneno haya yako wazi kabisa; hakuwezi kuwa na makosa.

▶️ Kaka K, unawezaje k*thubutu kukiuka amri nzito hivyo na ya muhimu? Je! Bwana amefanya jambo la pekee ambalo kwa hilo wewe umeepushwa toka kwa sheria aliyoitoa kwa ulimwengu? Je! Maovu yako yameondolewa k*toka katika kitabu cha kumbukumbu? Je! Amekubali kusamehe k*totii kwako wakati mataifa yatakapokuja mbele Zake kwa hukumu? Usijidanganye mwenyewe hata kidogo kwa mawazo kuwa dhambi yako haitaleta adhabu inayostahili. Makosa yako yatapatilizwa kwa fimbo, kwa sababu ulikuwa na nuru, lakini ukatembea kinyume kabisa nayo. "Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana."

▶️ Mungu ametupatia siku sita ambazo kwazo tunafanya kazi zetu na kuendelea na shughuli za kawaida za maisha; lakini anadai siku moja, ambayo aliitenga maalum na kuitakasa. Anatupatia hiyo sisi k**a siku tunayoweza kupumzika k*toka katika kazi na kujitolea kuabudu na kuboresha hali zetu za kiroho. Ni kitendo cha ukatili mkali jinsi gani kwa sisi kuiba siku moja iliyotakaswa ya Yehova na kuitumia kwa makusudi yetu binafsi!

🔘 Ni ufidhuli mkubwa kabisa kwa viumbe wanaoweza kufa k*thubutu kuingilia mapatano na Mungu ili kupata masilahi yao madogo, ya muda. Ni uasi wa kikatili wa sheria k*tumia Sabato mara kwa mara kwa shughuli za kidunia k**a ilivyo kuikataa kabisa; kwa kuwa hilo linafanya amri za Bwana kuwa jambo rahisi aonavyo mtu.

11/12/2021

Mithali 7 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁷ Nimetia kitanda changu manukato, Manemane na udi na mdalasini.
¹⁸ Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.
¹⁹ Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;
²⁰ Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.
²¹ Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.
²² Huyo akafuatana naye mara hiyo, K**a vile ng'ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;
²³ Hata mshale umchome maini; K**a ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.
²⁴ Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.
²⁵ Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake.
²⁶ Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.
²⁷ Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.

29/08/2021

*KESHA LA ASUBUHI.*

Jumapili, 29/08/2021.

*BUSARA YA KIKRISTO.*

*Kwa kuwa Bwana MUNGU asema hivi; Mji uliotoka nje wenye watu elfu, utasaziwa watu mia, na mji uliotoka wenye watu mia, utasaziwa watu kumi, kwa nyumba ya Israeli. Amosi 5:3.*

▶️Tahadhari inapaswa kuchukuliwa kwa maombi na kila mtu anayeuamini ukweli. Kuna matukio ya kujaribu mbele yetu, na inatubidi kuchukua tahadhari kubwa, huku tukiutunza mlango wa midomo yetu wakati waovu wanapokuwa mbele yetu. Itabidi tuk*tane katika uzoefu wetu na watu wenye ari iliyokithiri ambao watawachochea wale wanaochukia ukweli na itakuwa muhimu kudumisha hali ya utulivu na sio kusema yote tunayoyajua, kwa kuwa fikra zitafanywa katika akili za wanadamu ambazo, chini ya uwezo wa Shetani, zitakua kufikia viwango vikubwa.

▶️Kuna haja ya kukesha na kuomba. Uovu ambao tutak*tana nao muda mrefu umekuwa ukijikusanya na k**a dhoruba, utawajia wengi wakati hawautarajii kabisa. Ingawa hawawezi kushutumiwa kwa kuusababisha uovu huo, waliuhimiza. Mash*taka yatatolewa ambayo waumini hawawezi kukanusha, kwa sababu hawakuonesha hekima katika matumizi ya kalamu na sauti.

▶️Sheria nyingi zinatungwa kwa serikali za mataifa, zilizokusudiwa kukandamiza; na sheria za zamani ambazo kiutendaji hazifai tena, zitafufuliwa. Tunapaswa kusonga mbele katika kazi yetu kwa ufahamu na kwa imani, chini ya ustadi wenye hekima wa usimamizi wa Yesu Kristo. Kazi kubwa inapaswa k*tendwa kwa ajili ya Bwana katika k*tangaza ujumbe wa mwisho wa rehema kwa ulimwengu wetu, na tunategemea mamlaka na wenye madaraka katika kupata njia k*toka mwisho mmoja wa ulimwengu hadi mwingine, na maadamu tunawategemea wenye mamlaka, hatupaswi kujitenga k*toka kwao, kwa sababu huu ni ujumbe wa ulimwengu wote.

▶️ *Tunapaswa kwenda mbele kimyakimya, na njia yetu inapofungwa katika mwelekeo mmoja hatupaswi kuwalaumu wenye mamlaka, kwani kwa kufanya hivyo tunazifundisha mamlaka zingine jinsi ya kufanya ili kukinga njia yetu. Hatupaswi kuchochea nguvu za upinzani au kuchochea ulipizaji wa kisasi. Kilele kitakuja hivi karibuni sana. Tayari kinakuja k**a mwizi usiku. Na tunaweza kusema ukweli wa Biblia ambao hautaweka mivuto inayopingana kazini.*

*MUNGU ATUBARIKI SOTE.*
🙏🙏🙏🙏

Address

Kiseke
Mwanza

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kiseke SDA Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share