EAGT Nyakato - Canaan Gospel Center

EAGT Nyakato - Canaan Gospel Center GOSPEL CENTER

01/06/2026

Tunamshukuru Mungu kwa ajili ya matendo yake makuu aliyoyatenda katika wiki hili la kwaya na kwenye wiki hili tulikuwa na semina kuanzia jumatano na jumapili ilikuwa ni hitimisho ya semina.

Mnenaji wa semina alikuwa ni mchungaji Shadrack Reuben kutoka kanisa la Mito Ya Baraka(Kishiri)......

Tumejifunza katika siku zote za semina(Jumatano,Ijumaa,Jumapili) somo kuhusu Nguvu ya Mungu Katika Uimbaji na andiko kuu la semina limetoka kitabu cha

Yohana 4:24

Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Ahsante sana kwa kuhudhuria semina hii na Mungu akubariki.

Nikukaribishe kwenye ibada ya kesho Jumapili 03/5/2026, Itakuwa ibada ya SIFA, MAABUDU NA SHUKRANI kwa Mungu wetu.Itaanz...
02/05/2026

Nikukaribishe kwenye ibada ya kesho Jumapili 03/5/2026, Itakuwa ibada ya SIFA, MAABUDU NA SHUKRANI kwa Mungu wetu.

Itaanza saa 3:00 asubuhi mpaka saa 7:30 mchana,
Kanisa lipo Nyakato, National jirani na shule ya msingi Mzigu (Almaarufu k**a kanisa la vioo)

Watu wote mnakaribishwa sana, tutafurahi kukuona.

HAPPY INTERNATIONAL LABOR DAY
01/05/2026

HAPPY INTERNATIONAL LABOR DAY

IBADA YA JUMAPILI 26/04/2026MNENAJI: DANIEL SADICKSOMO: UTII​MAANA YA UTII:​Utii ni zaidi ya kusikia tu; ni tendo la moy...
28/04/2026

IBADA YA JUMAPILI 26/04/2026

MNENAJI: DANIEL SADICK
SOMO: UTII

​MAANA YA UTII:
​Utii ni zaidi ya kusikia tu; ni tendo la moyoni na vitendo.

​Kitendo cha kukubali kufanya maelekezo au maagizo unayopewa: Hii inahusisha kufanya yale unayoelekezwa na aliye juu yako, iwe unapenda au hupendi.
​Kukubali maelekezo unayopewa na kuitia: Utii wa kweli unahitaji utekelezaji wa haraka na ukamilifu.

​LENGO LA SOMO:
​Ni namna gani tunaweza kutii maagizo ya Mungu?

​Maandiko ya kurejea:
​Yakobo 4:7 ("Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.")

​Wafilipi 2:8 (Kuhusu unyenyekevu na utii.)

​KIELELEZO CHA UTII: Yesu Kristo
​Yesu ndiye mfano wetu mkuu wa utii kwa Baba.

​Yesu alitii na kukubali mapenzi ya Mungu.
​Aliyanyenyekea maagizo yote na kile ambacho Mungu alimwagiza akifanye hapa duniani.

​SABABU ZA WATU KUTOFANIKIWA NA KUPATA HITAJI LA MAOMBI YAO
(BARAKA):

​Mara nyingi kizuizi kikubwa cha baraka ni ukosefu wa utii.
​Ni kwa sababu ya kutokutii maagizo ya Mungu. Tunaposhindwa kufuata kile Mungu anachosema, tunajizuia kupokea majibu yetu.

​Maandiko ya kurejea:
​2 Wafalme 5:1–14 (Habari ya Naamani aliyepona baada ya kutii agizo la kuoga mtoni mara saba.)
​1 Wafalme 17:1– (Habari ya Eliya na utii katika kipindi cha njaa.)

MADHARA YA KUTOKUTII:
​Kutokutii kuna gharama kubwa na huleta matokeo hasi katika maisha ya kiroho na kimwili.

​Maandiko ya kurejea:
​1 Samweli 15:1– (Habari ya Mfalme Sauli aliyekataliwa na Mungu kwa sababu ya kutokutii agizo kamili la Mungu.)

KUMBUKA: Utii ni ufunguo wa kufungua milango ya baraka na kudumisha uhusiano mzuri na Mungu. K**a ilivyo kwa Naamani, wakati mwingine agizo linaweza kuonekana dogo, lakini matokeo yake ni makuu.

Pia kupitia kutii kutakufanya ule mema ya nchi,
Isaya 1:19
Yoshua 1:8

IDARA YA HABARI 2026.

Karibu katika ibada ya maombi Njoo tuombe pamoja tulete haja zetu na mahitaji yetu mbele ya Baba yetu wa Mbinguni. Yerem...
17/04/2026

Karibu katika ibada ya maombi

Njoo tuombe pamoja tulete haja zetu na mahitaji yetu mbele ya Baba yetu wa Mbinguni.

Yeremia 29:12-13
Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.

Kanisa lipo

📍Nyakato,National Mwanza
Karibu na Mto(Kanisa la Vioo)

Karibuni Sana.

16/04/2026

"Umeinuliwa Bwana, zaidi ya milimaaa
Wema wako Bwana kwetu, kweli washangaza..........."

Maneno ya kwenye wimbo "MWENYE NGUVU" kutoka kwa Canaan Revival Choir (CRC).

Kwaya ya kanisa la EAGT NYAKATO, CANAAN "A" GOSPEL CENTER

Wana Album yao iendayo kwa jina la *KISHINDO CHA WAKOMA* na huu ukiwa ni moja ya wimbo kwenye album hiyo.

Kupata flash wasiliana na viongozi wa kwaya hii kwa namba
0788 665 557
0753 334 749
0767 685 073

Au Fika kanisa ujipatie flash hiyo kwa bei nafuu sana.

na Mungu akubariki sana.

Ibada ya JumatanoTulikuwa na mama yetu akitufundisha kuhusu upendo kwa Mungu wetu na kwa wanadamu.Tukaona na kusoma andi...
16/04/2026

Ibada ya Jumatano

Tulikuwa na mama yetu akitufundisha kuhusu upendo kwa Mungu wetu na kwa wanadamu.

Tukaona na kusoma andiko katika kitabu cha

1 Petro 4:7-14

Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.Zaidi ya yote iweni na bidii kubwa katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi. Mtu akisema, na aseme k**a asemaye maneno halisi ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

Akatusihi kuweka juhudi katika kumpenda Mungu(kutoa,kuhudhuria ibada) na kupendana sisi kwa sisi na mwisho kujifanyia tathmini ya maisha yetu kwa maana Bwana Yesu anarudi.

15/04/2026

Kila kilichochukuliwa na kupokonywa kikarudishwe kwako kwa Jina la Yesu

Ona maandiko haya 👇

2 Wafalme 7:3-7

Basi walikuwapo watu wanne wenye ukoma, penye lango la mji; wakasemezana, Mbona tunakaa hapa hata tufe?

Tukisema, Tutaingia mjini, mjini mna njaa, nasi tutakufa humo; nasi tukikaa hapa, tutakufa vile vile. Haya! Twende tukaliendee jeshi la Washami; wakituhifadhi hai tutaishi; wakituua, tutakufa tu.

Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu.

Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, k**a kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi.

Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile k**a kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao.

Mungu asikizishe kishindo kwenye uchumi wako,biashara yako,kwenye mahali unapofanyia kazi ili uvune mali mahali ambapo hawakutarajia.

13/04/2026

Tunamshukuru Mungu kwa ibada ya Sifa na Kuabudu. Hakika tulimuona yeye na alituhudumia.

Asante pia kwa wote mliofika na Mungu awabariki sana.

05/04/2026

Tutakuwa live muda sio mrefu
Katika Ibada ya Pasaka

Address

Mahango, Mhandu
Mwanza
33125

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when EAGT Nyakato - Canaan Gospel Center posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to EAGT Nyakato - Canaan Gospel Center:

Share