ELCT - ELVD

ELCT - ELVD East of Lake Victoria Diocese (ELVD) is part of the Lutheran Church in Tanzania (ELCT).

Contacts:
Bishop Andrew Petro Gulle: [email protected]
General Secretary Rogath Lewis Mollel: [email protected]
Assistant Bishop Oscar Lema: oscarlema11yahoo.com

Leo Juni 03, 2026 watumishi wa  kituo cha ushauri wa kisaikolojia-Nyakato wamewajengea uwezo wanafunzi  wa Mwanza Luther...
03/06/2026

Leo Juni 03, 2026 watumishi wa kituo cha ushauri wa kisaikolojia-Nyakato wamewajengea uwezo wanafunzi wa Mwanza Lutheran Secondary School kuhusu afya ya akili.

Naibu Katibu Mkuu-Fedha Adria Temba amefungua mafunzo ya kuomba malipo katika kanzi data ya Dayosisi (ELVD MIS) kwa waku...
01/06/2026

Naibu Katibu Mkuu-Fedha Adria Temba amefungua mafunzo ya kuomba malipo katika kanzi data ya Dayosisi (ELVD MIS) kwa wakuu wa Idara, wakuu wa vitengo, wakuu wa vituo na wahasibu leo Juni 01, 2026 katika Ukumbi wa Charming Bungalow-Nyakato.

Mafunzo haya yameandaliwa na Idara ya Mipango na Uwekezaji kwaajili ya kujifunza kufanya malipo kwa njia ya mtandao kwa waombaji wenye uhitaji wa malipo.

ZIARA YA KAZI YA KATIBU MKUU KKKT-DMZVKatibu Mkuu wa KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria akishirikiana na Mkuu wa I...
28/05/2026

ZIARA YA KAZI YA KATIBU MKUU KKKT-DMZV
Katibu Mkuu wa KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria akishirikiana na Mkuu wa Idara ya Mipango na Uwekezaji na Huduma za Jamii leo tarehe 28, Mei wamefanya ziara katika Usharika wa Emanueli-Sengerema ya kukutana na watumishi wa jimbo, usharika na mradi wa ACHIEVE Pamoja na kukagua shughuli za uhitimishaji wa mradi.

Pia ziara hii imefika katika Usharika wa Tumaini-Kasamwa kuona shughuli mbalimbali zinazoendelea pamoja na utekelezaji wa mpango mkakati. Vilevile ziara iliendelea mpaka mtaa wa Penueli-Nampalahala kuona na kukagua kazi mbalimbali ikiwemo mpango kazi wa mtaa, uendelevu wa shughuli za mradi wa utunzaji mazingira (CCAP), mradi wa uchimbaji wa visima, mradi wa uwekaji vioo na vigae katika usharikani na mradi wa ufugaji nyuki unaoendelea.

Ziara hii imekua na matokeo makubwa sana baada ya vikao vya mrejesho na majadiliano ya namna ya kuboresha kazi hizi za taasisi.

Idara ya Huduma za Jamii kupitia Kituo cha afya Nyakato Leo Mei 25, 2026 imepokea ugeni toka Makao Makuu ya Kanisa(KKKT)...
25/05/2026

Idara ya Huduma za Jamii kupitia Kituo cha afya Nyakato Leo Mei 25, 2026 imepokea ugeni toka Makao Makuu ya Kanisa(KKKT), Kurugenzi ya Afya na Diakonia. Ziara hii imeangazia namna bora ya Kanisa kuihudumia jamii kupitia Huduma shufaa (Palliative Care),utekelezaji na ubora wa huduma mbalimbali zinazotolewa katika
kituo hicho, kuimarisha mifumo ya rufaa, ukusanyaji wa taarifa, ufuatiliaji wa huduma na ushirikiano kati ya hospitali na jamii. Kwa kutambua umuhimu wa ubora wa huduma katika mchakato wa utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote, ziara hii pia imelenga kufanya tathmini ya kina ya utayari wa vituo vya huduma za afya, pamoja na kuandaa mikakati shirikishi ya uboreshaji itakayowezesha kufikia malengo ya utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote kwa ufanisi na uendelevu.

25/05/2026
MAANDALIZI YA KUZALIWA DAYOSISI MPYA YAANZA MKOANI GEITA.Katibu Mkuu wa Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria Bwana  Joshu...
24/05/2026

MAANDALIZI YA KUZALIWA DAYOSISI MPYA YAANZA MKOANI GEITA.

Katibu Mkuu wa Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria Bwana Joshua Kyelekule Amemtambulisha Mkuu wa Jimbo la Magharibi kati Mchungaji
Daniel Kaijunga kuwa mratibu wa shughuli zote za uanzishwaji wa Dayosisi mpya mkoani Geita.

Ibada ya utambulisho huo imefanyika jumapili hii ya tarehe 24/05/2026 katika usharika wa Upendo-Geita uliopo Jimbo la Magharibi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali .

Akifanya utambulisho huo Katibu Mkuu Bwana Kyelekule amewaomba wajumbe wa k**ati ya kuratibu uanzishwaji wa Dayosisi mpya,Wachungaji pamoja na washarika wote kumuunga mkono Mchungaji Kaijunga ili kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa kwa viwango vya juu zaidi.

Ikumbukwe kuwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria (DMZV) kilichokaa Aprili 29 na 30 mwaka 2026 kilipitisha jina la Mchg.Daniel Kaijunga kuwa Mratiibu wa shughuli zote za kuanzishwa kwa dayosisi mpya ambayo inatarajiwa kuanza Mwaka 2029.

Aidha zoezi la utambulisho huo limeambatana na kukagua ujenzi wa Kanisa Kuu la Dayosisi hiyo mpya linalojengwa katika usharika wa Upendo pamoja na maeneo mengine ya kujengwa Ofisi za Dayosisi na nyumba ya Askofu.

Kwa sasa Dayosisi .ashariki ya Ziwa Victoria DMZV ina jumla ya mikoa miwili ambayo ni Mwanza na Geita na kukamilika kwa Dayosisi mpya kutaufanya mkoa wa Mwanza ujitegemee na Geita itajitegemea.

Baba Askofu Oscar I. Lema leo Mei 17, 2026 ni miaka 37 ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria...
17/05/2026

Baba Askofu Oscar I. Lema leo Mei 17, 2026 ni miaka 37 ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria amehudumu kwa njia ya mahubiri katika Usharika wa Imani Kanisa Kuu.
Askofu amesisitiza wakristo juu ya kuomba kulingana na mapenzi ya Mungu na kutumika ili kumfata Kristo
Katibu Mkuu wa KKKT Bwana Rogath Mollel ameshiriki ibaada hii na kutoa salamu kutoka KKKT Makao Makuu.

MAADHIMISHO YA SIKU YA FAMILIA DUNIANI. Leo Mei 15, 2026 ni siku ya familia duniani. Wadau wa maendeleo  ya mkoani Mwanz...
15/05/2026

MAADHIMISHO YA SIKU YA FAMILIA DUNIANI.
Leo Mei 15, 2026 ni siku ya familia duniani. Wadau wa maendeleo ya mkoani Mwanza wameadhimisha siku hii kwa kuandaa mdahalo wa wadau wa sekta ya maendeleo ya jamii.

Mgeni rasmi katika kongamalo hili alikuwa Bi Witness Malero aliyetoa neno la Ufunguzi katika mdahalo huo.

Mdahalo huu umeandaliwa na wadau kutoka Halmashauri ya jiji la Mwanza, KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Viktoria kupitia Idara ya Jinsia na Maendeleo ya Jamii, Rafiki wa watoto (RAWATO), Railway Children in Africa na Inland Media.

Lengo la mdahalo huu ni kujadiliana jinsi migogoro ya kifamilia inavyoadhiri watoto, vijana na familia kwa ujumla.

Washiriki katika mdahalo huu ni viongozi wa dini (Wachungaji &Shekhe), Maafisa Maendeleo ya Jamii, Dawati la Jinsia Mkoa, Walimu kutoka Shule za Msingi na Sekondari, Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia ( Samia Legal Aid), Afisa Mradi na malezi toka Railway Children, Babu na Bibi kutoka KKKT-DMZV(wazee wenye umri wa miaka 60 na zaidi), mwakilishi wa baraza la watoto (Taifa), wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari, Inland media na Jambo media.

Halmashauri ya Wachungaji imefanya kikao chake cha kikatiba kuanzia tarehe 11 na 12 Mei 2026, katika Chuo cha Kilutheri ...
12/05/2026

Halmashauri ya Wachungaji imefanya kikao chake cha kikatiba kuanzia tarehe 11 na 12 Mei 2026, katika Chuo cha Kilutheri Nyakato.

Leo katika kikao hicho kimehudhuriwa na watumishi kutoka KKKT-Makao Makuu Bi Patricia Mwaikenda kwaajili ya kukusanya maoni ya mradi mpya utakao jikita na vijana watakao tekeleza mradi huu katika Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria.

UZINDUZI WA JIWE LA MSINGI MTAA WA REHOBOTH-ILALILABaba Askofu Oscar I. Lema leo Mei 10, 2026 ameweka  jiwe la msingi ka...
10/05/2026

UZINDUZI WA JIWE LA MSINGI MTAA WA REHOBOTH-ILALILA

Baba Askofu Oscar I. Lema leo Mei 10, 2026 ameweka jiwe la msingi katika Mtaa wa Rehoboth-Ilalila. Mtaa huu unatunzwa na Usharika wa Imani Kanisa Kuu.
Askofu Lema amewahasa wakristo wanapaswa kumuomba Mungu siku zote k**a sala ya Bwana inavyoelekeza na sio kupayuka payuka na watu waendelee kufanya kazi ya Mungu kwa kujitoa kwa moyo.
Mtaa wa Rehoboth-Ilalila ina jumla ya washarika sitini (60).
Makamu Mkuu wa Chuo cha Biblia Nyakato Mchg. Mimi Brown amepata nafasi ya kuwakaribisha wakristo wote wanaopenda kusoma na wenye watoto, ndugu, jamaa na marafiki wajiunge na Chuo chetu kinachotoa kozi ya maendeleo ya jamii kwa ngazi ya cheti na diploma.

Address

P. O. Box 423
Mwanza

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELCT - ELVD posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to ELCT - ELVD:

Share