29/07/2024
MWINJILISTI HUDHIHIRISHA ROHO NJEMA ILIYO HALISI KATIKA HUDUMA
(Soma ujumbe huu mpaka mwisho.)
NENO KUU:
2 Timotheo 1:7 "Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi."
UTANGULIZI
Mwinjilisti ni mtumishi wa Injili anayepaswa kutumia vema nguvu za Mungu na mbinu ziokoazo nafsi.
Mungu huwapa watoto wake Roho ya nguvu na upendo na kiasi (kujitambua). Wakati Timotheo alipokea nguvu ya Roho kwa kuwekewa mikono ya Paulo na kwa maombi, ndivyo nasi tunavyoweza kupokea nguvu ya Roho na mitazamo yake pale tunapotumia kile Mungu ametufundisha na kufanya mapenzi yake katika maisha yetu. Lazima tuitendee kazi Roho halisi ya Yesu Kristo kwa kujifunza Biblia, kuomba, kutafakari, kufuata na kuweka kwenye vitendo imani na maisha ya Kristo tuliyojifunza kutoka kwake.
Soma maandiko haya na utunze kweli hizi moyoni
- 2 Timotheo 1:7 inatufundisha Roho njema hutoka kwa Mungu, siyo kwetu sisi.
- 2 Timotheo 1:12 inatufunulia kweli kuwa Roho njema hutufanya tuziamini na kuzitegemea nguvu za Mungu.
- 2 Timotheo 2:24-26 inatuonyesha tabia za Roho njema kuwa ni upole na kuvumilia mabaya.
- 1 Timothy 6:11-14 inatukumbusha kwamba tunahitaji kuitendea kazi Roho njema.
MAFUNDISHO
Wainjilisti ni watu wa Mungu waliopewa Roho njema ya Mungu na wanaotakiwa kuidhihirisha kwa vitendo katika namna tatu zifuatazo:
I. Roho ya nguvu:
Hii ni roho ya ujasiri ambayo hutolewa na Mungu kwetu:
A) Roho ya nguvu imo ndani ya Injili tunayoihubiri – Rm. 1:15-17; 1 Kor. 15:1-4.
B). Ina msingi wake katika nguvu za Mungu, siyo juhudi zetu - 1 Kor. 2:1-5; 2 Kor. 1:810.
C) Hupatikana kwa imani na maombi – Efe. 1:16-17; Flp. 1:9-11.
D). Huimarishwa pale tunapokiri udhaifu wetu, kwamba tunahitaji nguvu - 2 Kor. 12:9-10; Yk.5:16-18; 1 Yh. 1:8-9.
E). Hutumika pamoja na unyenyekevu, upole na uvumilivu - 2 Tim. 2:24-26; Gal. 6:1-3.
II. Roho ya upendo:
Hii ni roho ya utii na huduma ambayo hutolewa na Mungu kwetu:
A) Roho ya upendo imo ndani ya Yesu Kristo tunayemtangaza – 1 Yh. 4:8-16
B). Upendo ndio lengo la maagizo yote ya Mungu kwetu sisi - 1 Tim. 1:15; Rm. 13:8-10.
C) Lazima tuitendee kazi Roho ya Upendo - 1 Tim. 6:11; 2 Pet. 1:3-11.
D) Roho ya Upendo ndicho kipaumbele chetu kikuu na cha kwanza - 1 Kor. 13:1-8.
E). Ina kiini chake kwenye unyenyekevu na kutoa huduma – Yh. 13:5-17, 34-35.
III. Roho ya kiasi:
Hii ni roho ya nidhamu na kujidhibiti ambayo hutolewa na Mungu kwetu.
A) Ni njia salama ya jinsi gani tunapaswa kufikiri na kutenda vema – Tit. 1:8; 2:2-6, 12.
B) Hulenga katika tegemeo letu kwenye nguvu za Roho – Rm. 8:5-7; Gal. 3:1-3; 2 Kor. 3:5-6.
C) Ina mtazamo wa Kristo – Flp. 2:5-8; Kol. 3:1-4.
D) Haivuki mipaka, haivunji sheria za Roho na hudhibiti tamaa zetu za mwili – Gal. 5:16, Rm. 8:1-2
MATUMIZI
1. Mwinjilisti ni Mkristo aliyepewa Roho ya nguvu, na upendo na kiasi. Mshukuru Mungu kwa kukupatia hii Roho njema – Efe. 1:16-17; Kol. 1:9-14.
2. Nguvu au Ujasiri utakuwezesha kumhubiri Kristo na kutenda mapenzi ya Mungu.
3. Upendo utakuwezesha kumkaribia Mungu na kuwahudumia watu wengine.
4. Kiasi kitakusaidia kujitawala mwenyewe na kuwa na nidhamu kibinafsi.
5. Kila siku kumbuka kwamba Mungu ni chanzo cha kila mtazamo mzuri tulionao, kisha mruhusu Roho wake kufinyanga tabia, maisha na mitazamo yako yote – Flp. 3:7-10; Efe. 1:3.
6. Kila siku fanya kazi ya kumzika “mtu wa kale” aliyemo ndani yako kwa sababu alikufa na Kristo msalabani ili afufuke naye katika Roho njema – Rm. 6:11; Efe. 4:17-22; Gal. 5:19-21; 2 Pet. 3:1114.
7. Usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu Yesu Kristo - 2 Tim. 1:7-12; Rm. 1:16.
8. Usione aibu kuhubiri Injili ya Yesu Kristo
9. Usiwaonee haya watakatifu au watu wa Mungu unapowaona wanahitaji huduma yako au msaada wako.
10. Kumbuka kwamba Mungu ndiye hutupatia mahitaji kwa ajili ya kutimiza kazi yake - 2 Kor. 9:8-15.
11. Anza kujifunza kufikiri kuhusu kuwa jasiri, mwenye upendo, kiasi na mawazo mema kwa sababu Roho njema ya Kristo uliyonayo sasa inataka uwe na mtazamo mzuri – Kol. 3:1-4; Flp. 4:6-9.
12. Utakapotumia ujasiri ulionao, tegemea watu wengine kukuchukia lakini kwa Kristo utatukuzwa.
13. Unapoacha kuwa jasiri utakuwa unamzimisha Roho aliyemo ndani yako.
HITIMISHO
Ujasiri ukitumiwa pamoja na upendo na kiasi ni Roho njema. Daima uwe jasiri lakini uwe na kiasi na upendo unapotaka kuutumia ujasiri wako vibaya.
Mungu akubariki sana.
*Shea ujumbe huu kwenye magrupu.