15/12/2025
Kanuni za msingi za uinjilisti wenye ufanisi.
1. Jenga mahusiano na watu:
Pata kuwajua watu, sikiliza habari zao, tafuta mambo yanayofanana na wao na uwaombee kabla ya kukutana nao ili kuwashirikisha imani yako.
2. Ishi Imani Yako:
Weka matendo yako (uadilifu, ukarimu, upendo) yaakisi tabia za Kristo (injili), na kuifanya hiyo tabia iwe ya kuvutia kwa wengine.
3. Hubiri Injili na hadithi yako:
Kila mara unapohubiri kumbuka kutoa ushuhuda wako mweyewe wa jinsi Kristo alivyokubadilisha.
4. Omba moyoni uwezeshwe na Roho:
Tegemea mwongozo wa Mungu wakati wote unapoachilia maneno unayohubiri au kufundisha, ukimwachia Mungu matokeo yake maana yeye ndiye hukuza mbegu tuipandayo mioyoni mwa watu.
5. Kuwa Mwema:
Kuwa mkarimu, mkweli na mwenye adabu, kiasi na mipaka; epuka lawama au kuunda msuguano au kashfa.