21/03/2020
*KESHA LA ASUBUHI.*
Jumamosi, Machi 21,2020.
*NITAKUWA MKRISTO NYUMBANI.*
📖 *[Upendo] haukosi kuwa na adabu hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya.1 Wakorintho 13 : 5.*
✍️ *Mengi yanaweza kupatikana kwa kuishi kwa nidhamu nyumbani.... Hebu kila mmoja ayafanye maisha kuwa ya furaha kwa mwenzake kwa kadiri inavyowezekana. Kuwepo adabu katika maongezi. Dumisha umoja na upendo. Shetani hatakuwa na nguvu juu wale wanaojitawala kikamilifu nyumbani*
✍️ *Inatupasa kuwa na Roho wa Mungu, vinginevyo hatutakuwa na mwafaka nyumbani.... Inatupasa kujali sana upendo nyumbani, kwa kuwa nyumbani, ikiwa Roho wa Bwana yupo hapo, panakuwa mbingu ndogo.... Kitu chochote kinachoelekea kuharibu amani na umoja wa familia kisiendekezwe kamwe. Uungwana na upendo, roho ya kujali na uvumilivu, idumishwe. Pale mtu mmoja anapokosea, mwingine aoneshe uvumilivu wa Kikristo.*
✍️ *Yeyote anayeonesha roho ya upole, uvumilivu, na upendo atagundua kuwa roho ile ile itaoneshwa kwake.... Ikiwa Kristo ameumbika ndani, tumaini la utukufu, kunakuwa na umoja na upendo nyumbani. Kristo aliyeko ndani ya moyo wa mke anapatana na Kristo aliyeko ndani ya mume. Watakuwa wakijiandaa pamoja kuishi katika majumba ambayo Kristo alikwenda kuwaandalia wampendao.... Inapasa upendo wa kirafiki udumishwe daima kati ya mume na mke, wazazi na watoto, kaka na dada.... Ni wajibu wa kila mmoja katika familia kuwa na furaha, kuongea vizuri.*
✍️ *Nyumba ambayo ina upendo ndani yake, ambapo upendo unaelezwa kwa maneno, kwa mwonekano, na matendo, ndipo mahali ambapo malaika hupenda kuonekana na kuangaza kwa miale ya nuru ya utukufu… Inapasa upendo uonekane katika mwonekano na tabia na isikike katika sauti. Kujitawala kwa kila mmoja wa wanafamilia kutaifanya familia kufanana sana na paradiso.*
*MUNGU AKUBARIKI UNAPOTAFAKARI NENO LAKE.*
🙏🙏
UWE NA SABATO NJEMA.