15/12/2022
VIJUE VYANZO VYA NDOTO NA KUVIOMBEA IPASAVYO.
CHANZO CHA KWANZA: NDOTO KUTOKA KWA MUNGU.
Ayu.33:14-15”Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu,
Katika usingizi kitandani;”
Hes.16”...Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA,… Nitasema naye katika ndoto.”
Zab.89:19”Ndipo ulipowaambia watakatifu wako kwa njozi(Ndoto),Ukasema...”
MAOMBI:Omba Mungu akusaidie kusikia k**a kile kitu kimetoka kwa Mungu. (Omba upate kusikia na kuelewa k**a kweli jambo hilo limetoka kwa Mungu).
CHANZO CHA PILI:SHETANI AU NDOTO KUTOKA KWA SHETANI.
Kumb.13:1-4”Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda BWANA, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.Tembeeni kwa kumfuata BWANA, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushik**ana naye.
MAOMBI:Jifunze kuombea lango la ndoto katika ulimwengu wa roho kwa kulifunika na damu ya Yesu ili Shetani asipitishe ndoto zake.
CHANZO CHATATU:NDOTO KUTOKA KWENYE MAZINGIRA YA SHUGHULI NYINGI.
Mhu.5:3”Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno”
MAOMBI;Jifunze kumwomba Mungu akupangilie siku yako na aongoze siku yako.
CHANZO CHA NNE:NDOTO KUTOKA KWENYE HALI YA KIROHO YA MAHALI ULIPOLALA.
Mwa.28:10-12”Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani.Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.”
Yakobo aliota ndoto mahali alipolala palipokua na madhabahu(Betheli) Mungu aliyehai aliyoijenga babu yake mzee Ibrahimu.
Yakobo alilala mahali ambapo paliunganishwa na mbingu umewahi jiuliza umelala sehemu yenye umiliki au maagano na miungu mingine ya kishetani hali yako itakuwaje?
MAOMBI: Jifunze kuombea hali ya kiroho ya mahali unapolala kabla ya kulala hapo.