Viwawa parokia ya Mt.Yohana mwinjili Usagara mwanza

Viwawa parokia ya Mt.Yohana mwinjili Usagara mwanza Kueneza neno la Mungu kwa watu wotena kuwaleta vijana karibu wamjue Mungu

08/12/2024
01/10/2023

Ni mwezi wa Mama Bikra Maria tusali rozari kila siku

Endelea kupumzika kwa amani Fr Mapunda
03/06/2022

Endelea kupumzika kwa amani Fr Mapunda

Vijana wakatoriki Wafanyakazi (viwawa) Parokia  ya usagara Jimbo kuu la Mwanza
22/05/2022

Vijana wakatoriki Wafanyakazi (viwawa)
Parokia ya usagara Jimbo kuu la Mwanza

01/05/2022

Heri ya sikukuu ya wafanyakazi
Vijana tufanye kazi

 Parokia ya Mt. Yohane Mwinjili Usagara
27/02/2022



Parokia ya Mt. Yohane Mwinjili Usagara

Viwawa parokia ya usagara
08/01/2022

Viwawa parokia ya usagara

Happy Merry Christmas
26/12/2021

Happy Merry Christmas

26/12/2021

Tunawatakia sherehe njema kwa niaba ya viwawa wote wa Mt. Yohana Mwinjili usagara

Kristu....!!!Kesho 14/11/2021 ni Dominika ya 33 ya Mwaka B wa KanisaSomo la 1 ni Dan 12:1-3Zab 16:5,8-11Somo la 2 ni Ebr...
13/11/2021

Kristu....!!!
Kesho
14/11/2021 ni Dominika ya 33 ya Mwaka B wa Kanisa

Somo la 1 ni Dan 12:1-3
Zab 16:5,8-11
Somo la 2 ni Ebr 10:11-14,18
Injili ni Mk 13:24-32
Nawatakia Dominika njema nyote.
Tumsifu Yesu Kristu......!!

07/11/2021

MASOMO YA MISA NOVEMBA 7, 2021
DOMINIKA YA 32 MWAKA B

MWANZO:
Zab. 88:2

Maombi yangu na yafike mbele zako, uutegee ukulele wangu sikio lako, ee Bwana.

SOMO 1
1 Fal. 17:10-16

Eliya aliondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa. Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako. Naye akasema, K**a Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika p**a, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe. Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye k**a ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile p**a la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya k**a alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi. Lile p**a la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 146:6-10 (K) 1

(K) Ee nafsi yangu, umsifu Bwana.

Bwana huishika kweli milele,
Huwafanyia hukumu walioonewa.
Huwapa wenye njaa chakula;
Naye huwafungua waliofungwa. (K)

Bwana huwafumbua macho waliopofuka,
Naye huwainua walioinama.
Bwana huwapenda wenye haki,
Naam, huwahifadhi wageni. (K)

Bwana huwategemeza yatima na mjane,
Bali njia ya wasio haki huipotosha.
Bwana atamiliki milele milele,
Mungu wako, ee Sayuni, kizazi hata kizazi. (K)

SOMO 2
Ebr. 9:24-28

Kristu hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu; wala si kwamba ajitoe mara nyingi, k**a vile kuhani mkuu aingiavyo katika patakatifu kil

Address

Mwanza

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Viwawa parokia ya Mt.Yohana mwinjili Usagara mwanza posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share