07/11/2021
MASOMO YA MISA NOVEMBA 7, 2021
DOMINIKA YA 32 MWAKA B
MWANZO:
Zab. 88:2
Maombi yangu na yafike mbele zako, uutegee ukulele wangu sikio lako, ee Bwana.
SOMO 1
1 Fal. 17:10-16
Eliya aliondoka, akaenda Sarepta; hata alipofika langoni pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni; akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo chomboni nipate kunywa. Alipokuwa akienda kuleta, akamwita akasema, Niletee, nakuomba, kipande cha mkate mkononi mwako. Naye akasema, K**a Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika p**a, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe. Eliya akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye k**a ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate mdogo ukaniletee; kisha ujifanyie nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile p**a la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya k**a alivyosema Eliya; na yeye mwenyewe na Eliya, na nyumba yake, wakala siku nyingi. Lile p**a la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa kinywa cha Eliya.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 146:6-10 (K) 1
(K) Ee nafsi yangu, umsifu Bwana.
Bwana huishika kweli milele,
Huwafanyia hukumu walioonewa.
Huwapa wenye njaa chakula;
Naye huwafungua waliofungwa. (K)
Bwana huwafumbua macho waliopofuka,
Naye huwainua walioinama.
Bwana huwapenda wenye haki,
Naam, huwahifadhi wageni. (K)
Bwana huwategemeza yatima na mjane,
Bali njia ya wasio haki huipotosha.
Bwana atamiliki milele milele,
Mungu wako, ee Sayuni, kizazi hata kizazi. (K)
SOMO 2
Ebr. 9:24-28
Kristu hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu; wala si kwamba ajitoe mara nyingi, k**a vile kuhani mkuu aingiavyo katika patakatifu kil