Wabeloya-Aict Buhongwa Sunday School. - Children Ministry

Wabeloya-Aict Buhongwa Sunday School. - Children Ministry Inajihusisha na kutoa elimu ya kikristo kwa vijana na watoto

26/02/2022

KUWA SHAHIDI..!

Mathayo 10:32-33
[32]Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

[33]Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.

• Moja Ya Kanuni Muhimu Ambayo Unapaswa Kuikumbuka Katika Maisha Yako Ya Wokovu, NI KANUNI YA KUMTAMBULISHA BWANA YESU!

• Kanuni Hii Ni Muhimu Mno Na Haipaswi K*tekelezwa Kwenye Baadhi Ya Matukio Ya Maisha Yako, Bali Ni Kanuni Inayopaswa K*tekelezwa Kwenye Kila Eneo La Maisha Yako Bila Kujali Upo Kwenye Mazingira Gani..!

• Katika Maisha Yangu Ya Wokovu Nimejifunza Jambo Hili; USITARAJIE KUONA MUNGU AKIDHIHIRIKA KWENYE MAISHA YAKO ZAIDI YA KIWANGO CHAKO CHA KUMDHIHIRISHA KWENYE MAISHA YAKO YA KILA SIKU..!

• Usitarajie Kuona YESU Akijitukuza Katika Maisha Yako Ilihali Umekuwa MTU WA KUONA HAYA HATA KUSEMA KUWA UMEOKOKA!!

• Unapaswa Kuhakikisha Maisha Yako Yanamtambulisha Bwana Yesu Kwa K*mkiri, Mwenendo N.k Bila K*muonea Haya Yeye Aliyekufia Msalabani Bila Aibu Yoyote!! YEYE ALIIDHARAU AIBU ILI WEWE UOKOLEWE...!

• Bwana Yesu Atadhihirika Kwenye Maisha Yako Na Kwenye Kila Ambacho Utautia Mkono Wako Kukifanya!!

- USIMUWEKE YESU MFUKONI!!!
- MTAMBULISHE BWANA YESU!!
- KUWA SHAHIDI!

# TAFAKARI KWA KINA, AMUA KWA BUSARA #

- Ahsante Kwa Kunielewa -

21/02/2022

Tafakari ya neno la Mungu siku ya leo Jumatatu tarehe 21/02/2022 na siku ya 052/365.

Danieli 9 : 3

"Nikamwelekezea BWANA Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu."

Tafakari ya kujifunza:

▶️Aya hii katika sura ya 9 ni uamuzi wa Danieli kuchukua hatua ya kufanya maombezi kwa ajili ya mji wa Yerusalemu. Uamuzi wa Danieli unaifunua tabia yake nyingine ya kutokuwa mbinafsi.

▶️Sura ya 9 imetawaliwa na maombezi ya Danieli. Maombezi ni maombi matakatifu ya kuamini na kustahimili ambapo mtu humsihi Mungu kwa niaba ya mwingine au wengine ambao wanamhitaji sana Mungu aingilie kati kwa haraka.

▶️Biblia katika agano la kale na agano jipya imeandika habari za maombezi ya wacha Mungu wengi wanaume, wanawake, Yesu Kristo, na Roho Mtakatifu.

▶️ Danieli katika sura ya 9 anaomba kwa dhati kwa ajili ya urejesho kwa Yerusalemu na taifa zima. Anaonyesha kuwa na huruma, mzigo wa huduma kwa ajili ya watu wengine.

▶️Pamoja na kuwa kiongozi mkubwa serikalini akishika nafasi ya tatu baada ya mfalme Dario ambapo leo hii katika serikali yetu tungempa nafasi ya waziri mkuu. Nafasi hiyo ilimfanya kuwa na kila kitu mfano mali, ulinzi, heshima, watumishi, nk. Lakini bado aliwakumbuka jamii ya taifa lake na kumuomba Mungu kwa huzuni.

▶️Yesu wakati wa huduma yake hapa duniani alilia katika hali ya kupondeka kuhusu mji wa Yerusalemu (Luka 19: 41). Aliwaombea wanafunzi wake mmoja mmoja (Luka 22 :32) na k**a kundi (Yohana 17 : 6 - 26).

▶️Yohana anamwita Yesu "Mwombezi kwa Baba" (1 Yohana 2:1).

▶️Pamoja na mfano wa Yesu, wapo watu wa Mungu wengi k**a Danieli waliotumika kwa ajili ya kufanya maombezi ya watu mbalimbali tazama : Ibrahimu kwa ajili ya Ishmaeli (Mwanzo 17:18) na kwa ajili ya Sodoma na Gomora (Mwanzo 18: 32 - 32); Daudi kwa ajili mtoto wake (2 Samweli 12 : 16; 1 Nyakati 29: 19), Ayubu kwa ajili ya watoto (Ayubu 1:5); Musa naye alikuwa mwombezi wa Waisraeli (Hesabu 14: 13 - 19) nk.

▶️Kila mara huduma ya maombezi Mungu a

09/07/2021
JINSI YA KUBOMOA MADHABAHU ZA KISHETANI ZINAZOKUTESAK*t 34:13 “Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, ...
13/04/2021

JINSI YA KUBOMOA MADHABAHU ZA KISHETANI ZINAZOKUTESA

K*t 34:13 “Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, na kuyakata-kata maashera yao.”

K*m 12:3 “nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.”

1. Tambua madhabahu gani zipo kwako au kwenu.

2. Tambua sababu iliyo nyuma ya uwepo wa madhabahu hizo.

3. Jitiishe kwa Mungu ili uwe salama. Hakikisha Yesu ni Bwana na Mwokozi wa maisha yako!

4. Omba Mungu akupe uwezo wa kupambanua.

5. Mpinge shetani. Usiwe na urafiki na shetani. Shetani asiwe na haki fulani katika maisha yako.

6. Omba kinabii na kwa nguvu. Tambua mamlaka yako katika Bwana na kuitumia.

7. Waue makuhani wa madhabahu hizo. Tambua kwamba katika madhabahu za shetani kuna makuhani wanaohuisha maagano.

8. Jiondoe kwenye madhabahu hizo. Ondoa jina lako, picha, nguo, nembo nk kutoka kwenye madhabahu za uovu.

9. Miliki milki zako. Usisahau kuchukua kilicho halali yako. K**a madhabahu zilikuzuia kufanikiwa, sasa anza shughuli za kipato hata k**a awali ulishindwa.

10. Mpe Mungu sifa. Mtukuze Mungu kwa ushindi aliokupatia.

NB: Hata hivyo vipengele hivi vinahitaji muda wa kutosha na uongozi wa Roho wa Mungu. Usivitaje tu na kudhani umemaliza. Ndiyo maana ni muhimu kushiriki vipindi vyetu vya kubomoa madhabahu ili ujue k**a una nguvu za kutosha kukabiliana na madhabahu za kwenu. Hata Bwana Yesu alionya tabia ya kwenda kichwakichwa katika vita. Lk 14:31,32 “ Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? Na k**a akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.”

MWONGOZO MFUPI WA MAOMBI:
1. Ee Mungu nifunulie ni madhabahu gani zilizok**ata maisha yangu na ya ndugu zangu.
2. Ee Mungu nisaidie kutambua kwanini madhabahu hizo zimekuw

SOMO LA LEO3 YOHANA 1;22 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavy...
21/03/2021

SOMO LA LEO
3 YOHANA 1;2

2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo.
Bwana Yesu asifiwe mtu wa Mungu!
Wakati tukiwa bado tuko katika msiba mzito wa kifo cha rais wetu, napenda nikupitishe katika maneno ya uzima ambayo japo kwa sehemu yakaufanye moyo wako kujengwa kiimani!
Wakati mtumishi wa Mungu mzee Yohana anaandika walaka huu alikuwa ni mzee wa siku(umri).
Ni wakati ambao alikuwa ametoka katika mapito ya kutupwa katika kisiwa cha kutisha na kuachwa peke yake kwa lengo la kuangamizwa na warumi jambo lililoonekana si kitu katika uhai ulikuwa wake aliopangiwa na Mungu.
Anaandika waraka huu akiwa ni shahidi wa upendo wa Yesu Kristo tangu akiwa mwanafunzi wake na ndiye aliyekuwa ni mdogo kuliko wote(na sasa ana umri mkubwa kuliko wote duniani kwa mitume wengine waliomtangulia).
Mtume Yohana anatoa baraka ya kufanikiwa katika mambo yote ambayo anahitaji wafanikiwe.
Unajua ni kwanini anaanza hivi?
Anaacho kimaanisha ni BARAKA!
Watu wengi wanazani baraka ni jumla ya mambo yote waliyo nayo na kuyamiliki,mfano pesa,majumba,magari n.k
Nikupe swali kidogo!
Unakumbuka wakati Ibrahim anaambiwa atoke kwenye nyumba ya baba yake aende mpaka mahali atakapooneshwa?
Unakumbuka kile kilichomfanya Yakobo mpaka kuchukua mbaraka wa ndugu yake kwa baba yake Isaka? Je, alichukua sehem yoyote ya mali pale nyumbani ili kuoneshwa amebarikiwa? Alitafuta nini pale katika kunenewa!
Watu wengi hutamani sana kuwa marafiki wa watu walio na pesa na magari ila hawajibidiishi kuwa marafiki wa watu walio BARIKIWA!
KUWA NA VYOTE HIVYO SI BARAKA ILA NI MATOKEO YA BARAKA!
Ila matokeo ya vitu hivyo yanaweza kuwepo ila wakati huo usiwe na BARAKA ZA MUNGU!
Bwana Yesu asifiwe!
Yohana anasema "naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo"
Naona hapa hajataja habari za vitu wa umiliki wa vitu halisia......

02/01/2019

TUNAENDELEA KUMSHUKURU MUNGU NA TUNAWAOMBA MZIDI KUIOMBEA HUDUMA HII.
AMEN

13/12/2018

We proceed!!

Kanisa la leo na kesho likiwa darasani!
29/12/2017

Kanisa la leo na kesho likiwa darasani!

We thanks God to all steps we pass through
14/09/2017

We thanks God to all steps we pass through

Certificate to complete safari kuu studies!!
14/09/2017

Certificate to complete safari kuu studies!!

14/09/2017

Address

Buhongwa
Mwanza

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wabeloya-Aict Buhongwa Sunday School. - Children Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Wabeloya-Aict Buhongwa Sunday School. - Children Ministry:

Share