29/12/2023
SOMO: KANISA NI MWILI WA KRISTO NA KRISTO NI KICHWA CHAKE
UTANGULIZI
Yesu ana mwili mmoja tu, na haugawanyiki. Yesu ni kichwa cha huo mwili, na ametoa nguvu kubwa na urithi wenye utukufu kwao walio ndani ya mwili wake.
Tunahitaji kuelewa ni nani walio viungo vya huu mwili mmoja, ndipo kwamba tutaweza kuwa na ushirika mkamilifu na nguvu za Yesu Kristo katika maisha yetu.
Kiungo cha mwili huwa hai na chenye nguvu tu pale kinapokuwa kimeungana na viungo vingine (mwili); hii ina maana kwamba, tutakuwa hai na wenye nguvu za Yesu ikiwa tutadumu katika ushirika na wengine walio katika Kristo. Hii ni sawa na tawi linapokuwa hai na kuzaa matunda kwa sababu limeshik**ana na shina. Hupaswi kujitenga na ushirika wa kanisa lako, wala umoja wa kanisa, wala kukiacha kichwa, yaani Kristo, ambaye ni mzizi na shina lako pia – Yh. 15:1-8.
I. KWELI YA MAANDIKO
A. Waefeso 1:18 – Mungu ametoa urithi wa utukufu wake kwa watakatifu.
B. Waefeso 1:19-20 – Ametoa nguvu za uweza wake zisizo za kawaida kwetu tuaminio.
C. .Waefeso 1:21 – Yesu Kristo ni kichwa kwa kila kitu kwa ajili ya Kanisa
D. Waefeso 1:23 – Kanisa ni mwili wa Yesu Kristo.
II. MAFUNDISHO
A. Mungu ametoa urithi wa utajiri wa utukufu wake kwa watakatifu.
1. Mungu ametuita kupitia tumaini la ufufuo wa wafu – Efe. 1:18, 1 Kor. 15:1-4.
2. Mungu ametupatia urithi na nguvu zilizo katika Yesu aliyefufuka – Efe. 1:18, Yud. 1:1.
B. Mungu hudhihirisha uweza na Nguvu zake kwa njia ya imani.
1. Zipo kwa ajili yao waaminio – Efe. 1:19, Mdo. 26:18.
2. Zilidhihirishwa kwetu katika ufufuo wa Yesu Kristo – Efe. 1:20, Flp. 3:8-11.
3. Zinapatikana kwa wote walio waaminifu kwa Yesu – Efe. 1:20 na 23.
C. Mungu alimfanya Yesu kuwa kichwa cha kanisa.
1. K**a kichwa, Yesu ameketi mkono wa kuume katika kiti cha Mungu Baba – Efe. 1:20, 1 Pet. 3:22).
2. K**a kichwa, Yesu amepewa mamlaka yote mbinguni na duniani – Efe. 1:21, Mt. 28:18, Yh. 1:1-3.
3. Yesu ni kichwa chetu na anatawala vitu vyote kwa ajili yetu – Efe. 1:22, Kol. 1:16-20.
D. Mungu amemfanya Yesu kuwa mwili (Kanisa ni mwili wa Yesu Kristo) – Efe. 1:23, 1 Kor. 12:13.
1. Yesu katika uhai wake duniani alikuwa na mwili na Roho ndani yake – Mt. 4:1
2. Alipokwenda mbinguni alimtuma Roho wake kuja kukaa ndani ya miili yetu – Mdo. 2
3. Roho wa Yesu anakaa ndani yetu ili tufanyike mwili wa Yesu – 1 Kor. 3:16-17
4. Tumefanyika mwili wa Kristo duniani – Efe. 5:23-27
III. MATUMIZI
A. Mungu anataka Kanisa tumpe utukufu – Efe. 3:10.
1. Urithi wetu na tumaini letu la milele linapatikana katika Kanisa – Efe. 1:18).
2. Tafuta kuwa sehemu ya Kanisa ili ufanyike kiungo katika mwili wa Kristo – Flp. 3:8-11.
B. Kanisa ni familia ya Mungu iliyoitwa kutoka ulimwengu uliopotea kwa njia ya Injili – Rm. 1:16, 1 Kor. 1:21, Yh. 20:31.
1. Mungu huzidisha watu katika Kanisa pale wanapoonyesha imani Kwake – Mdo. 2:47, 1 Kor. 12:13.
2. Wote walioitii Injili ni viungo vya mwili, yaani ni sehemu ya Kanisa – Mdo. 5:32.
C. Tunza muunganiko wako kwenye Kanisa (mwili).
1. K**a unataka kuendelea kuwa hai katika Yesu Kristo – Rm. 6:17-18
2. K**a unataka kumzalia Mungu matunda – Yh. 15:1-14.
D. Kamwe usishirikiane wala kuungwa na walimu wa uongo au manabii wa uongo.
1. Ambao wanakataa kumkiri Yesu k**a Bwana na Mwokozi wao – Yh. 5:39-40.
2. Ambao wanaukataa ujumbe wetu wa Injili ya wokovu na nguvu zake zinazopatikana kwa njia ya imani katika msalaba, yaani kifo, kuzikwa na kufufuka kwa Yesu Kristo - 2 Yh. 1:6-11);
3. Ambao wanazikana nguvu za jina la Yesu na kutumia nguvu na miujiza ya uongo – Mdo. 4:12
4. Ambao wanajitukuza wenyewe kwa wenyewe na utukufu wa Mungu hawautafuti – Yh. 5:41-44
E. Si kila kitu kiingizwacho na wanadamu katika Mwili wa Kristo kwamba mwamini atakikubali - taz. Rm. 13-15.
IV. AYA YA KUKARIRI: Waefeso 1:22-23