New me, New life

New me, New life Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from New me, New life, Religious organisation, Mwanza.

23/03/2023

MARAFIKI

WANANDOATunawakaribisha ALHAMISI, 15.09.2022Tutakuwa na MAOMBI MAALUMU kwa ajili ya wanandoa. Ndoa zilizoko kwenye hali ...
14/09/2022

WANANDOA

Tunawakaribisha ALHAMISI, 15.09.2022
Tutakuwa na MAOMBI MAALUMU kwa ajili ya wanandoa. Ndoa zilizoko kwenye hali zote. Zenye afya tele, dhaifu, zilizo ICU, zinazobadilika badilika, zilizobaki jina tu nk

Zaburi 107:20
Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.

Tutakuwa LIVE
INSTAGRAM NA YOUTUBE
Anointed Room Ministry
SAA MBILI USIKU saa za Afrika Mashariki

Tukuombe mwana wa MUNGU sambaza taarifa hizi njema kwa wote. Share, TAG, post and repost, na Yesu akubariki.

Lets win differently

HE is HERE

Beatrice & Colle
ANOINTED ROOM MINISTRY
0754440139/0655623588

NI NDEFU LAKINI KUNA KITU AU VIWILI UTAPATATHE STORY OF A WHEELCHAIR Tulipopost kuhusu ndugu zetu tuliowabariki na wheel...
20/07/2022

NI NDEFU LAKINI KUNA KITU AU VIWILI UTAPATA

THE STORY OF A WHEELCHAIR

Tulipopost kuhusu ndugu zetu tuliowabariki na wheelchairs, tulikwambia tutarudi na “Story of a Wheelchair” vile ambavyo BABA alitaka tuwashirikishe ili pamoja tujifunze.

Huyu mama tulikuwa tumpelekee wheelchair siku ya ijumaa baada ya kutoka kumpatia mama yetu mwingine huko Gongolamboto. Lakini kwasababu tulikuwa na huduma ya watumishi saa tisa, ilibidi tuahirishe njiani baada ya kuona tutachelewa na ile traffic jam ya Dar es Salaam. Tukakubaliana naye tutajitahidi tumpelekee siku ya jumamosi asubuhi ambayo ndiyo siku ya prayer gathering Dar es Salaam. Siku ya jumamosi tukafanikiwa kupeleka kwa mwingine mmoja na kwake ikashindikana tena kwa sababu ya muda. Tukakubaliana tena siku ya jumapili. Ilipofika tulianza na shule ya Jangwani, tukaenda na Kimara na mwisho wa siku ilishindikana tena kwa mara ya tatu. Tukakubaliana tena tutaenda jumatatu kwasababu bado tutakuwa Dar es Salaam kukamilisha baadhi ya vitu.

Mhubiri 3:1&11a
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake

Siku ya jumatatu tulianzia kwake. Tulipofika walitupokea vizuri sana. Tulifurahi kumkuta mama huyu akiwa na FURAHA SANA, uso wake una nuru mpaka ilitupa shida kwanza kujua kwani ni huyu tunayemfuata au muhusika bado hajatoka chumbani? Kumtambua ilikuwa ni kazi sana kwa sababu ya uso uliojaa NURU. Kumbuka, miguu yake iko kawaida tu (haijapinda) ila haiwezi kufanya chochote.

“Wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya BWANA ni nguvu zenu”(Nehemia 8:10)

Tulianza kuzungumza naye, na ndipo BABA alipotuambia
“SIKILIZENI KWA MAKINI SANA KILA ANACHOONGEA, NATAKA MJIFUNZE NA MKAWAFUNDISHE WENGINE”

Mama huyu ni mgonjwa wa FIGO. Anasema alikuwa anaendelea na maisha yake tu k**a kawaida na kwenye ujauzito wa mwisho hali ilibadilika na akagundulika kwamba FIGO hazifanyi kazi. Anasema alipopelekwa clinic ya figo mara ya kwanza, alijikuta moyo wake unaugua sana sana juu ya

NENO LA HEKIMALEO, tunapenda kuongea TENA na WAAJIRIWA. Iwe ni serikalini, kwenye sekta binafsi nk. K**a ulipitwa na pos...
19/07/2022

NENO LA HEKIMA

LEO, tunapenda kuongea TENA na WAAJIRIWA. Iwe ni serikalini, kwenye sekta binafsi nk. K**a ulipitwa na post yetu ya kwanza kuhusu waajiriwa pitia post za nyuma ina kichwa WAAJIRIWA.

UNAJUA, shida kubwa ya waajiriwa ni kwamba wengi bado hamjajua kwamba hapo mlipo mnamtumikia Mungu na mmesimama k**a mawakili wake. Wengi sana wanatilia maanani mwisho wa mwezi tu. Lakini tunakwambia kabisa, ukibadili mtazamo na kujua kwamba hapo ulipo wewe ni mwakilishi wa Mungu, kuna mambo mengi sana mazuri yatatokea kwenye maisha yako na kuna mambo mengi sana mabaya utaepuka.

Tito 2: 9 - 10
Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu, wasiwe WAIBAJI; bali wauonyeshe UAMINIFU mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.

NINYI waajiriwa wengi wenu sio WAAMINIFU na hamna uchungu kabisa na MALI za ofisi. Mnazitumia tu vile mpendavyo na wala hakiwaumizi. Kuna watu mnabeba tu vifaa mbalimbali kutoka maofisini yani k**a vile ni vyenu. Bahasha, kalamu, office pins, karatasi wengine mpaka stapler na punch machines, huo ni wizi.

Wengine mna-print mambo yenu binafsi kutumia printer za ofisi, wino wa ofisi, karatasi za ofisi bila huruma. Mambo yenu binafsi sijui network marketing report, wengine application letters na CVs za kwenda kuapply kazi sehemu nyingine mnaprint hapo hapo. Wengine upuuzi puuzi tu. Hivi wewe umeajiriwa na mshahara unalipwa, kwanini usiwe mwaminifu tu nenda stationery print lipa.

Wengine wana misuse tu, unaweza kuhitaji page moja tu ya kwanza, lakini unaprint page zote 7, halafu zile 6 zote zinaishia kwenye dustbin. Au document moja una print mara 3, kwanini usiwe mwangalifu? Jamani hata k**a ofisi sio yako hivi husikii uchungu hata kidogo wewe mwakilishi wa Mungu? Unamwakilishaje Mungu kwa wizi na kukosa uaminifu?

Wengine mnabeba mpaka toilet papers. Yani wewe unabeba chochote kinachobebeka. Wengine mnafanya kazi store yani ninyi ndio wakati wote mnaangalia namna ya kuiba vitu.

13/07/2022

BEHIND COMFORT ZONE

Kwenye COMFORT ZONE ni wapi?
Ni aina fulani ya maisha uliyoizoea na inakufanya usikie RAHA au AT EASE kuwa hapo.
Kuna aina fulani ya kazi umeizoea.
Aina fulani ya watu ndio unasikia raha kuwa nao around.
Aina fulani ya mazingira ndio umeyazoea.
Aina fulani za tabia.
UNERIDHIKA

UMEZOEA kufanya kazi za aina fulani, ukipewa zingine au zaidi husikii raha tena, tena unaanza kulalamika.

UMEZOEA kuwa kwenye mazingira fulani hivi. Ukihamishwa mazingira husikii raha tena. Umezoea kule kwasababu you feel comfortable. Umezoea maisha ya miji mikubwa mikubwa Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Dodoma nk. Ukipelekwa Kakonko, Kigoma au Namtumbo, Ruvuma au Nangurukuru, Lindi, humu ndani kunaanza kufurukuta.

Umezoea hapo hapo kwenye hiyo ofisi. Ukihamishwa ofisi huna raha tena.

UMEZOEA maisha ya kulala saa tatu usiku mpaka asubuhi. That’s your comfort zone. Ukiambiwa amka saa nane uombe tayari huna raha. You love your sleep.

UMEZOEA kula milo mitatu kila siku. That’s your comfort zone. Yani ikitokea umekosa mlo mmoja tu, mambo yanabadilika kabisa. Habari za kufunga hutaki kusikia. Umezoea kula. That’s your comfort zone.

Kuna tabia umezoea kuzifanya. Zinakufanya ujisikie raha. Kuangalia tamthilia, movies nk. Kupiga umbea na yule rafiki yako fulani hivi, unasikia raha. Kazi yenu ni kusema watu tu. Usipofanya hivyo unahisi kuna kitu kinakosekana. Umezoea kupoteza muda kwenye mambo yasiyo ya msingi.

NYUMA YA COMFORT ZONE KUNA NINI?
Nyuma ya COMFORT ZONE kuna MAUTI.
Mauti ya hatma za watu. Mauti ya MAONO. Mauti ya VIPAWA. Mauti ya KARAMA. Mauti ya MAWAZO MAKUBWA nk. Wengi wamepotea kwasababu ya kung’ang’ania COMFORT zone. Wengi mmebaki hapo hapo miaka nenda miaka rudi kwasababu ya kupenda comfort zote. Wengi mmeshuka viwango. Mambo hayaendi kwasababu mmebweteka hapo hapo. Hamtaki maisha zaidi ya yale mliyoyazoea. Umezoea kuomba lisaa limoja tu mwaka wa nne sasa wewe ni wa hivyo hivyo.

MUNGU anataka tuwe HODARI (Joshua 1:9). Kuwa hodari hakuwezi kuja kwa k

13/07/2022

Yohana 16:24[

Yohana 16:24
[24]Hata sasa HAMKUOMBA NENO KWA JINA LANGU; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.

Kuna Siri YESU KRISTO ANATUAMBIA HATA SISI LEO KUWA HATA SASA HAUJAOMBA LOLOTE KWA JINA LAKE🙈😭🙈😭

Angalia roho zakujihesabia haki zinavyoanza kukuhubiria kuwa Mimi mbona huwa nikiomba nasema KWA JINA LA YESU KRISTO au nikiwa namalizia sala zangu namaliza katika jina la YESU KRISTO nimeomba nakuamini, Amen🤷🏻‍♂️🤷🏻‍♂️ si ndio hivyo?! Mie huwa nafanya

Sikia SIO HIVYO Kuna TOFAUTI ya KUSEMA NA
KUOMBA✍🏼✍🏼

KANUNI ya KUOMBA wengi hawaijui au hawaifanyi japokuwa wameona wameokoka au wameshakaa kanisani muda mrefu wengine wakishapewa na ule utenda kazi kanisani kuhudumia watu nk ndo kwisha habari yeye ameshajua yote na amekomaa🤣

Neno hili ni rahisi Sana kulisema ila kiutendaji ni tofauti kabisaaa

Mathayo 7:7
[7]Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa

Wengi wamechanganywa saana na wanazidi kujipoteza na kupoteza wengine kwenye kauli hii

OMBENI, NANYI MTAPEWA✍🏼✍🏼
Wengi wamefundishwa na kuishia kuona kwajicho moja tu kuwa MUNGU ANATOA VITU TU (Tangible)
Wamezuia upande wapili warohoni kupata wamejikita mwilini tu

Angalia maombi yetu mengi yalivyo na huku tunaendelea kusonga mbele tukisema TUNAPOKEA VITU AU TUNASUBIRI KUPOKEA VITU

Yakobo 4:1
[1]Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?
[
Yakobo 4:1
[1]Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?
[
Kuna sehemu yetu iko VITANI NA WENGI HAWAJUI Hilo wakidhania ukiokoka kila kitu kinaokoka badala yaku scan ulimwengu wetu wa roho ukoje.

VITA HAVITOKI HUMU?!
Katika TAMAA ZETU ZINAZOFANYA VITA katika viungo vyetu?!
- mkono unataka saa nzuri kucha nzuri, Pete nzuri nk
- shingo inataka rangi nzuri, cheni nzuri, urembo mzuri?!
- mguu unahitaji kiatu aghali, sandles za kisasa, kucha, rangi nk

Address

Mwanza

Telephone

+255766802023

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when New me, New life posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share