GOD Visitation TV

GOD Visitation TV Huu ni Ukurasa Maalumu kwa Madhumuni ya Kumuhubiri Mungu Asiyeshindwa Chini ya Huduma ya Kimataifa ya Mtembeleo wa Mungu.

(GOG VISITATION INTERNATIONAL MINISTRY). Ikiongozwa na Senior Prophet Shepherd Mbise

MKESHA Mkubwa sana Kufanyiki Katika Kanisa La GVM CHURCH DODOMA MICHESE31/3/2023 Kuanzia Saa 3 Usiku na kuendeleya.Kuna ...
27/03/2023

MKESHA Mkubwa sana Kufanyiki Katika Kanisa La GVM CHURCH DODOMA MICHESE
31/3/2023 Kuanzia Saa 3 Usiku na kuendeleya.

Kuna wakati Unajiuliza Mbona Kila Ninalo Lifanya Haliendi na Kila Ninalo lishika Halishikiki.

Ukweli Ni Kwamba Kila atuwa unayotakiwa kuipiga Nilazima Utahitaji NGUVU ya Mungu Ili kukuvusha. Usione walio fanikiwa ukajua na wao walikuwa wakinun'gunika k**a wewe. Walipo Amuwa kufanikiwa katika Mambo Yao waliacha kunun'gunika Nakuitafuta Nguvu ya MUNGU ALIYE Hai.

Prophet Max Mbise Baba Yetu MUNGU Amempatia Mafunuo juu ya Mkesha huu wa kihistoria Wewe utakaye UDHURIA PROPHET MBISE ATAWAOSHA MIGUU NA MIKONO YAKO Kwa Maji ya UPAKO na wewe Utaingia Mwezi wa Nne ukiwa na UMILIKI WAKO.

Zaburi 37:23-24
Hatua za mtu zaimarishwa na BWANA,
Naye aipenda njia yake.
Ajapojikwaa hataanguka chini,
BWANA humshika mkono na kumtegemeza.

NJOO NA MUNGU ATAKUTEGEMEZA KWA MKONO WAKE NA WEWE UTAPA KUMILIKI BARAKA ZAKO MWEZI WA NNE.

Acha kuliya Kizembe Njoo MUNGU Bado Yupo na Nguvu zake ATAKUTEGEMEZA na Utakuwa MSHINDI

A very big vigil to be held at GVM CHURCH DODOMA MICHESE
31/3/2023 Starting at 3 PM and continuing.

There are times when you wonder why everything I have doesn't go and everything I have doesn't hold.

The truth is that every obstacle you have to overcome, you will need the POWER of God to overcome it. Don't see those who are successful and you know they were complaining like you. When they decided to be successful in their affairs, they stopped complaining. I seek the power of the living God.

Prophet Max Mbise Our Father GOD has given him Revelations on this historic Eve You who will attend PROPHET MBISE WILL WASH YOUR FEET AND HANDS WITH ANOINTING WATER and you will enter the Fourth Month with YOUR OWNERSHIP.

Psalm 37:23-24
A man's steps are strengthened by the LORD,
And he loved his way.
When he stumbles he will not fall down,
The LORD holds his hand and supports him.

COME AND GOD WILL SUPPORT YOU WITH HIS HAND AND YOU WILL OWN YOUR BLESSINGS IN THE FOURTH MONTH.

Stop crying in Kizembe. Come, GOD is still there and His strength will support you and you will be WINNER

SHEPHERD MBISESomo: KWA NINI UNAMDANGANYA ROHO MTAKATIFU?Haleluya -  Napenda leo tena nikufundishe kitu mtu wa MUNGUMate...
02/09/2022

SHEPHERD MBISE

Somo: KWA NINI UNAMDANGANYA ROHO MTAKATIFU?

Haleluya - Napenda leo tena nikufundishe kitu mtu wa MUNGU

Matendo ya Mitume 5:1-5
Lakini mtu mmoja jina lake Anania, pamoja na Safira mkewe, aliuza mali.

Akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake, mkewe naye akijua haya, akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume.

Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja?

Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.

Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.

Anania na Safira mkewe wanaingia hemani kwa Bwana / Kanisani wakiwa na sadaka yao au matoleo yao pungufu na MUNGU anawaua wanazikwa.

Nataka uelewe kwanini Mungu aliwaua wanandoa hawa.

Kumbuka walipoingia kanisani hawakumuona Roho Mtakatifu, MUNGU wala Malaika hawakuwepo pale kanisani aliyekuwepo kwa wakati huo ni Mtume Petro ambae alimwakilisha Jehova.

Petro alijua kila kitu kilichokuwa kikiendelea kati ya MBINGU na hawa wanandoa na ndiyo sababu ya Petro kuwauliza maswali haya Anania na mkewe

Kwanini mnamdanganya Roho Mtakatifu?
EPUKA HII LAANA JAMANI

Kwanini mmeficha sehemu ya fedha baada ya kuuza Ardhi?

Ukisoma utakuta kwamba wote wawli walikufa / waliuawa na Roho Mtakatifu wakazikwa.

Najua waweza kuwa mara kadhaa umesoma sehem hiyo leo napenda usome upya na ufatilie fundisho langu kwako kwa makini.

Kwanini Roho mtakatifu aliwaua kwa ajili ya pesa? Kwanini MUNGU anaruhusu wafe kwa ajili ya pesa?

kumbuka hapakuwa na purukushani ya wao kukabwa, hapakuwa na kisu wala panga wala siraha ya aina yoyote bali ni neno lililotoka kinywani mwa mtume Petro likawaua, maana yake ni kwamba kulikuwa na nguvu na utiisho wa hali ya juu sana kwenye maneno ya Petro.

Kulikuwa na uhusiano mkubwa kati ya kilichofanywa na Anania na mkewe na Roho wa Mungu na ndiyo maana Roho yule yule aliyekuwa ndani ya Petro anajua kiasi ambacho aridhi iliuzwa, kiasi kilichofichwa na kilichotoletwa hemani.

Petro anauliza kwanini Mmemjaribu Bwana kwa nini Mmejaribiwa ? Kulikuwa na kiwango Maalum ambacho Anani ana mkewe walipaswa kukileta hemani mwa Bwana na ndiyo maana walipoficha kingine Roho aliwauliza kiko wapi kingine.

Sababu ya roho kuwaua hawa ndugu siyo kuleta pesa chache Sababu ya wao kufa ni hii.

Walimshirikisha Mungu / Roho Mtakatifu kuhusu biashara yao na wakati huo ilikuwa kila mtu anaweza kuuza kitu chake akaleta hemani pesa yote aliyouzia so inawezekana kabisa aridhi yao ingeuzwa mda mrefu bali haikuuzwa mpaka pale kulipotokea kua na ahadi baina ya MUNGU na wanandoa hao kwamba endapo watauza aridhi yao basi watajenga ufalme wa MUNGU kwa pesa yote itakayopatikana.

Roho Mtakatifu akaleta mteja ambae hatuoni k**a alibishana nao kuhusu bei that means alilipa k**a walivyotaka kulipwa kwa nguvu ya Roho Mtakatifu wakauza walipopokea pesa tu mawazo yao yakageuka wakapatana kwa siri wafiche kiasi flani wakaficha na ikawapelekea kufa.

Una jambo umemlilia MUNGU kwa Mda mrefu patana na MUNGU weka agano nae uone k**a MUNGU hatatimiza kwako.


Jifunze kitu ni mara ngapi umemwambia MUNGU nifanyie jambo flani nami nitafanya jambo hili, wapo wengi ambao wanatabia k**a ya Anania na mkewe umemwomba Mungu kazi ukaahidi akikupa kazi basi sehemu ya mapato yako utamtolea ukapata kazi na mapato yako umekula mwenyewe.

Uliomba mtoto Ukapata na mpaka leo hujampa Mungu ahadi yako
sikiliza mwana wa Mungu Anania na safira walikufa na kuzikwa hata wewe leo ni Umekufa japo unaishi Mungu amepiga Uchumi wako, kazi yako imepingwa, baishara yako inakufa, watoto wako wamepingwa.

Kila jambo kwako ni shida Jiulize ni ahadi gani ulipeana na MUNGU ukaamua kuingia mitini unalalamika hupandi cheo kazini kwako mmmhhh hakuna mchawi bali ni ile ahadi yako kwa MUNGU.

Umezaa mara Moja unataka watoto zaidi MUNGU amefunga uzao kumbuka ni wapi ulimdanganya kwenye uzao wako wa kwanza, unataka kazi hupati na umesoma vizuri una Cv nzuri anakuja mtu mwenye uwezo mdogo kwako anapewa kazi
Kumbuka ulimwahidi nini MUNGU kwenye kusoma kwako.

Mungu angeweza kukuua k**a alivyowaua Anania na Safira bali Unaishi kwa Neema tu ya MUNGU

Mungu amenipa kibali cha kukufungua, kukutoa mahali uliposhikia laana hiyo Amenifanya kuwa Petro kwako ili nikuvushe mahali flani.

ROHO MTAKATIFU alitaka pesa yote ya Anania na Safira ipelekwe hemani ndiyo maana wanaulizwa na Petro kwanini Wameficha sehemu ya mauzo hayo?

Hata leo unaulizwa kwanini Umendanganya MUNGU anakuuliza kwanini ulimpa ahadi usitimize? Mtu wa MUNGU chunguza hatua zako ili MUNGU akuachilie kwenye hilo Teso la Laana.

Kwa Neema ya MUNGU Nitakuwa nikikuletea hapa GVM SAA YA UREJESHO Kila kitu ambacho ROHO WA BWANA ataniongoza kukuletea Kwa Jina la YESU.

HALELUYA UBARIKIWE SANA

HAKIKA UKIFANYA IVI UTAFIKA MBALI

Ukiamua Na kulisimamia Kusudi la Mungu Ndani yako; Hakika nakuambia Mungu yupo karibu yako.
25/02/2022

Ukiamua Na kulisimamia Kusudi la Mungu Ndani yako; Hakika nakuambia Mungu yupo karibu yako.

Senior~PROPHET SHEPHERD MBISE Tare 1/11/2021TAMKO LA KINABII:Natangaza MWEZI HU WA 11 UWE WA BARAKA  kwako na familia ya...
01/05/2021

Senior~PROPHET SHEPHERD MBISE

Tare 1/11/2021

TAMKO LA KINABII:

Natangaza MWEZI HU WA 11 UWE WA BARAKA kwako na familia yako
kwaa Jina la Yesu.

Mkono MWEMA wa BWANA
Uwe juu yako na familia yako kwaa Jina la Yesu.

MWEZI HU WA 11 Utakwenda UTUKUFU hadi UTUKUFU kwaa Jina la Yesu.

Ninaona MILANGO ISIYOTARAJIWA INAFUNGULIWA kwako, Mbingu imeamua kukukumbuka msimu huu! KWA JINA LA YESU.

Bwana atamtegemeza alipo Mgonjwa kitandani. Katika ugonjwa wake umemtandikia.
Zaburi 41:3
NAKUTAMKIA KILA UGONJWA KATIKA MOYO WAKO,MIFUPA YAKO,NGOZI YAKO,DAMU YAKO,KILA MAJERAHA YOYOTE NDANI YAKO...NINA KUTAMKIA UMEPONA KWA JINA LA YESU..

MWEZI HU WA 11 UWE NI MWEZI WA WAKUPITA JUU YA MAADUI ZAKO KWA JINA LA YESU....

SEMA NAPOKEA KWA JINA LA YESU...NA UAMINI YATAKUA YA KWAKO....

13/04/2021

Hebrews 11:1
Now faith is the substance of things hoped for, the evidence of things not seen.
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

Kuna wakati Mungu anaweza kusema nawewe UFANYE JAMBO FULANI Kwenye mazingira mabovu na wewe ukayaangali hayo mazingira ukajikuta unakata tamaa. Ninachoweza kusema kwako ni hiki IMANI NI KUA NA UWAKIKA NA MAMBO YATARAJIWAYO LAKINI KWA WAKATI HUO HAYAONEKANI...

MWAMINI MUNGU NA UMWAMINI MTUMISHI WAKE UTAFANIKIWA...

Psalms 76:6At thy rebuke, O God of Jacob, both the chariot and horse are cast into a dead sleep. Kwa kukemea kwako, Ee M...
12/04/2021

Psalms 76:6
At thy rebuke, O God of Jacob, both the chariot and horse are cast into a dead sleep.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.

ONA ROHO YA  UCHAWI ILIVYO WAKA MOTO....KUTOKA 22:18  USIMUACHE  MWANAMKE MCHAWI KUISHI....
08/04/2021

ONA ROHO YA UCHAWI ILIVYO WAKA MOTO....KUTOKA 22:18 USIMUACHE MWANAMKE MCHAWI KUISHI....

Mama Eliza Magita Mkazi wa Lwamlimi Musoma amepata Uponyaji katika Jina la Yesu,Alipofika Katika Kanisa la GVM alikuwa akisumbuliwa na Miguu,Tumbo na Pia kat...

SENIOR ~PROPHET SHEPHERD MBISE NINA AMURU KIBALI KIWE JUU YAKO KWA JINA LA YESU....BWANA YESU AMEKUJALIA KIBALI LEO...Ku...
08/04/2021

SENIOR ~PROPHET SHEPHERD MBISE

NINA AMURU KIBALI KIWE JUU YAKO KWA JINA LA YESU....

BWANA YESU AMEKUJALIA KIBALI LEO...
Kutoka 12:36
BWANA akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara.

MWEZI HUU WATAKUPENDA TU WAPENDE WASIPENDE NASE K**A KUHANI WA BWANA YESU UTAPENDWA:

Ninaamuru na kutangaza NEEMA ya MUNGU juu ya MAISHA YAKO KWA JINA LA YESU.
🔥Favour itafadhili matusi yako ulio tukanwa kazini naona KIBALI

🔥Bila maisha ya KIBALI ni kazi NGUMU Nimaombi yagu leo KIBALI Kidumu ndani yako ninayaona matokeo Makubwa kwako baada kibali kufanya kazi ndani yako.

︎🔥Bila maisha ya NEEMA ni ya kufadhaisha na yaliyojaa mkanganyiko Na dharahu MUNGU AKUTETEE LEO...

🔥Bwana akawapa KIBALI machoni pa Wamisri NA WEWE BWANA AKUPE KIBALI MBELE YA MAADUI ZAKO...

08/04/2021

I PROPHESY IN YOUR LIFE WHEN THE DEMONS SEE YOU KNEEL AND SAY WE ARE WITH YOU SON OF GOD............

SOMO: ROHO MTAKATIFU NINANI KWAKO?JUMA PILI YA KUJAZWA ROHO WA MUNGUTare 21/02/2021UtanguliziRoho Mtakatifu Ni Mwema kwe...
22/02/2021

SOMO: ROHO MTAKATIFU NINANI KWAKO?

JUMA PILI YA KUJAZWA ROHO WA MUNGU
Tare 21/02/2021

Utangulizi
Roho Mtakatifu Ni Mwema kwetu na huyo Roho Mtakatifu ni Roho wa Mungu Ambae Yesu Kristo Alimuomba BABA WA MBINGUNI AWE MSAIDIZI KWETU....

Yohana 14:16-23 … Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni, wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu......

SOMO:
NATAKA Tujifunze Juu ya kazi za Roho Mtakatifu na kukuonyesha namna unavyoweza kumtumia Roho Mtakataifu k**a Msaidizi kupitia kazi zake....

K**a Utakua Mnyenye kevu kwa hili ni Hakika Nitamuona Roho Mtakatifu kwenye maisha yako, Maana ni lazima kwanza uzijue kazi zake...

Tunaona Kua Roho Mtakatifu ni Msaidizi.
Roho Mtakatifu ni nani?
Roho Mtakatifu ni MUNGU, mwenye NGUVU zote, maarifa yote, anayepatikana kila mahali....

Yeye anayo nafsi na ameamua kuishi ndani ya mwili wa Mwanadamu. Kusudi kubwa la ujio wake ni kuwa Msaidizi wa Mwanadamu kwenye ulimwengu huu wa mwili, ili kumsaidia kuishi katika Mapenzi ya Mungu....

Roho Mtakatifu amemamua kuishi ndani ya mwili wa mtu kwa sababu, Mungu hana namna ya kutawala kwenye ulimwengu wa kimwili bila kuwa na mwili wa damu na nyama, kwa kuwa yeye ni Roho (Yohana 4:24). Hivyo hana budi kuingia kwenye mwili wa mtu na kufanya makao yake hapo, ili kutawala na kumuongoza mwanadamu katika mapenzi yake....

JE! UMEMKARIBISHA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO?
Ufunuo wa Yohana 3:20
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.....

1Wakorinto 3:16-17, 6:19).
Kinachotusaidia kujua kwamba Roho Mtakatifu ana nafsi, ni tabia zake, maana kwenye kila nafsi kuna hisia, nia, kumbukumbu, akili nk....

Baadhi ya sifa na tabia za Roho Mtakatifu ni; anapatikana kila mahali Na kwa Mwanadamu yoyote aliye Amuwa kumfungulia Kuingia ndani yake...

Zaburi 139:7, Ana maarifa anajua yote...1 Wakorinto 2:10-11, ni mwenye nguvu zote Ni wa umilele

Mwanzo 1:2, ni Mtakatifu, Luka 11:13, ana hisia Waefeso 4:30, Mwanzo 6:3 Na Wala msimuhuzunishe Roho wa Mungu…

Roho Wa MUNGU Haitashindana na Mwanadamu Kamwe Hata milele,1Wakorinto 12:11 Piya Hutenda kazi k**a apendavyo....

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
Kufundisha,Ni Mwalimu (Yohana 14:26) … Atawafundisha yote…

Kuongoza, Ni Kiongozi (Warumi 8:14, Yohana 16:13) Atawaongoza awatie kwenye kweli yote, wote wanaoongozwa na Roho hao ndio Wana WA MUNGU … Mfano (Matendo ya Mitume 13:4, Acts 8:29)

Ni mfunuaji wa mambo (MAFUMBO) yani siri za MUNGU...

(1Wakorinto 2:10)
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote. Usipoteze muda kumtaka Mungu akufunulie siri zake, wewe mwambie Roho Mtakatifu Maana hiyo ndiyo kazi yake...

Yeye Ni Muombezi (Warumi 8:26) – Roho Mtakatifu Hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa...

Ni Mtoa Habari za mambo yajayo (Yohana 16:13f) – Na mambo yajayo atawapasha habari yake ndio kazi yake...

Ni msemaji wa mambo ya MUNGU(Yohana 15:26, 2 Petro 1:21)

Yeye atashuhudia Wanadamu wayanena yaliyotoka kwa MUNGU WAKIONGOZWA na Roho Mtakatifu.

Ni mtetezi Na msemaji wa mambo yetu (Marko 13:11) Kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu.

Ni mkumbushaji wa yale uliyojifunza au uliyoagizwa na Mungu (Yohana 14:26) Atawakumbusha yote niliyowaambia.

HUWAPA NGUVU watu wake,UWEZO (Matendo1:8) Lakini mtapokea NGUVU akisha kuwajilia juu yenu ROHO MTAKATIFU …

Kuuhakikisha (convict, make aware, sadikisha) ulimwengu kwa habari ya dhambi, haki na hukumu (Yohana 16:8) UNAJUAJE kwamba kuna hukumu? Warumi 8:16

Naam kazi hizi za Roho Mtakatifu zinatufikisha mahali pa kujua kwamba jukumu lake kubwa ni kuwa Msaidizi wa mwanadamu...

Kufanyika msaada wa mwanadamu katika mambo hayo hapo juu pale mwanadamu atakapohitaji msaada huo....

Hivyo ni jukumu lako kumpa nafasi kwa kuboresha mahusiano yako na yeye ili akusaidie.

Hata hivyo Roho Mtakatifu Huitwa Msaidizi haina maana kwamba ndio umvunjie heshima Mtu, bali fahamu kwamba, Roho Mtakatifu ni Msaidizi kwa namna ambayo bila yeye mimi na wewe hatuwezi kutenda neno lolote....

Kazi hizi zinatupa kujua kwamba Roho Mtakatifu yupo tayari kutusaidia katika kila eneo la maisha yetu.

Ni jukumu letu kumpa nafasi hiyo na kutambua kwamba bila msaada wake sisi hatuwezi lolote.

Watu wengi leo hawaoni msaada wa Mungu kwao kwa sababu ya kutokumpa ROHO MTAKATIFU nafasi ya kuwasaidia katika maisha yao na pia kwa kutokujua maeneo ya kumtumia ROHO MTAKATIFU k**a Msaidizi...

Je, unahitaji msaada wa ROHO MTAKATIFU eneo gani la maisha yako?, ni ndoa, kazi, madeni, huduma, kanisa, utawala nk MPE nafasi akusaidie, akufundishe na kukuongoza katika kweli yote....

Kumbuka yeye ni MUNGU ambaye ni Mwalimu na Kiongozi MIMI na wewe hatuwezi NENO lolote Bila yeye Roho Mtakatifu...

Unataka kumjua MUNGU, kuwa na maombi yenye matokeo mazuri na kufanikiwa katika maisha yako kiroho na kimwili pia mwambie ROHO MTAKATIFU Akusaidie...

Msaada wa Roho Mtakatifu hauna mipaka maadam unahitaji msaada katika yale ambayo ni mapenzi ya MUNGU...

Hivyo haijalishi unapita katika jambo gani mpe nafasi Roho Mtakatifu akusaidie....

Na ili uweze kuthamini msaada wa ROHO MTAKATIFU JIFUNZE siku zote kufikiri kwa dhana kwamba bila msaada wake wewe huwezi lolote, na kwa sababu hiyo utaona umuhimu wa yeye kukusaidia katika maisha yako....

Usisubiri mambo yako yaharibike au usiachague mambo unayofikiri magumu ndio umshirikishe akusaidie, yeye anataka kuwa BWANA WA MAISHA YAKO, akusaidie kwa kila kitu hata mambo madogo kabisa kwenye maisha yako....

MUNGU ASIYE SHINDWA HUUMIA kuona watoto wake chini ya jua wanahangaika katika maisha yao, wakati yeye amemleta ROHO MTAKATIFU ili awasaidie katika maisha hayo....

Tumia vizuri fursa ya ROHO MTAKATIFU SASA MAADAM ANAPATIKANA, KUNA WAKATI HATAPATIKANA TENA KWENYE MAISHA YETU...

POKEA NGUVU YA ROHO WA MUNGU KWA JINA LA YESU.......

SOMODalili za mtu ambaye amekuwa attack na nguvu za gizaMathayo 16:231-kukosa Amani ghafla na kuwa muoga au hofu 1 Yohan...
17/02/2021

SOMO
Dalili za mtu ambaye amekuwa attack na nguvu za giza
Mathayo 16:23
1-kukosa Amani ghafla na kuwa muoga au hofu 1 Yohana 4:18
2-kukosa Uhuru WA kufanya utakacho,Bali kulazimishwa na nguvu iliyopo ndani yako
3:Kuota ndoto za majitu ya kutisha au namna ya kivuli kutaka kukukaba au kukudhuru
4Vitu kutembea mwilini
5-kusahau kusiko kawaida na uzito kichwani
6:kupiga miayo hovyo tena mfululizo bila kuchoka
7:kumchukia mume au mke bila sababu
8- kusisimka mwili ayubu 4:15
9kuhisi unabeba mizigo isiyoonekana

Address

Gvminternationaltv@gmail. Com
Musoma
10111986

Telephone

+255745796567

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GOD Visitation TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to GOD Visitation TV:

Share