05/07/2022
2 falme 4:-5
Basi, mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha, akasema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha BWANA; na aliyemdai amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa. Elisha akamwambia, Nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani? Akasema, Mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani, ila chupa ya mafuta. Akasema, Nenda, ukaazime vyombo huko nje kwa jirani zako wote, vyombo vitupu; wala usiazime vichache. 4Kisha uingie ndani, ukajifungie mlango wewe na wanao, ukavimiminie mafuta vyombo vile vyote; navyo vilivyojaa ukavitenge.
ni roho sio kitu cha kawaida cha kuzoeleka, Biblia inasema “ mdaiwa ni mtumwa wa anayedai”. Hii inamaana mtu anayekudai anaweza kukutumikisha anavyotaka, atakuwekea masharti anayoyataka yeye na utayafuta sababu uko chini ya deni. Anayekudai atakuwekea hata kiwango cha ukomo cha amani yako, Hii ndiyo sababu unapokutana na mtu anayekudai moyo wako unakosa amani.
☑️ Wapo wengi wamehama makanisa Kwa sababu ya kudaiwa. unajisikiaje unapokaa ikaribu na mtu anayekudai wakati wa kumwabudu Mungu kanisani?. Hii ndiyo sababu Mungu anasema Kumb 28 “utakopesha wala hutakopa”.
Sio watu wengi hutazama madeni k**a roho, ndiyo sababu ni rahisi kunaswa katika mkono wa madeni. Roho ya madeni haichagui mtu wa kumvaa na kumwendesha, haijalishi ni mtu mkubwa au mdogo, maskini au tajiri unapovamiwa na roho hii unakuwa mtumwa. Kuna watu ambao hawawezi kuishi bila kudaiwa, hata k**a hawapendi kwasababu hii ni roho, itahakikisha baada ya kupata fedha unatumia haraka ili ukope tena, itahakikisha ukishalipa deni unakuwa na kiu ya kukopa tena.
Sasa maandiko hapo juu ya utaona kuna mtu aliitwa Elisha na alikutana na mmoja wa wake za manabii ambaye mume wake alifariki.
Mama huyu alikuwa anadaiwa katika namna ambayo k**a asingeweza kulipa watoto wake wangishia utumwani. Ndipo alipokutana na Elisha nabii ambaye aliachilia Neema ya utele iliyoshinda roho ya madeni. Hii inatudhihirishia ya kuwa mtu anaweza kutoka katika roho ya madeni kwa Neema ya Mungu inayoleta utele.
Habari njema ni kuwa leo roho ya madeni itakomeshwa kabisa kwenye maisha yako katika jina la Yesu Kristo.
Karibu maombi na maombezi kanisani
Neema Lutheran Church Mtwara Dangote
Nyuma ya kituoa Cha Mafuta Cha Olympic Petroleum msijute / hiyali Dangote ( kwa kweka)
Muda wa ibada kila jumapili Saa tatu asubuhi