Efatha Church Mtwara

Efatha Church Mtwara Efatha Church: Healing & Deliverance by the Blood of JESUS CHRIST.

ASANTE KWA KUABUDU NASI Leo tumejifunza kuwa Neno la Mungu linatupa uzima, nguvu na furaha. Neno ni mkate wa uzima, mwan...
30/08/2026

ASANTE KWA KUABUDU NASI

Leo tumejifunza kuwa Neno la Mungu linatupa uzima, nguvu na furaha. Neno ni mkate wa uzima, mwanga wa miguu yetu, uponyaji na ukombozi, silaha yetu na maji ya uzima.

Imani huja kwa kusikia Neno la Mungu na tunapolipokea ndani yetu, Imani inaumbika na kutufanya kuwa hodari na washindi.

Soma Neno, tafakari Neno, kula Neno na tamka Neno; kwa namna unavyofanya hivyo ndivyo unavyoruhusu Neno likae ndani yako.

Waefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.”

Tunawatakia mwanzo mwema wa wiki, uliojaa nguvu, furaha na ushindi katika Bwana.

Maombi1. MWombe Mungu akupe kiu ya Neno la Mungu ndani yako siku zote za maisha yako ili uweze kulijua, kuliishi na kuli...
30/08/2026

Maombi
1. MWombe Mungu akupe kiu ya Neno la Mungu ndani yako siku zote za maisha yako ili uweze kulijua, kuliishi na kulikiri Neno la Mungu katika maisha yako.

2. Mwombe Mungu akupe wepesi wa kulielewa Neno lake maana Neno lake ndiyo uzima, na kupitia uzima huo kila kilichokufa ndani yako kikawe hai.

30/08/2026
4. Neno linaponya na kukomboa; Zaburi 107:20 “Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.” Katika Neno...
30/08/2026

4. Neno linaponya na kukomboa;
Zaburi 107:20 “Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.”

Katika Neno kuna uponyaji na ukombozi, hivyo katika hali yoyote uliyonayo Neno linaweza kukutoa, k**a unaumwa Neno linaweza kukuponya, k**a umefungwa Neno ni ukombozi wako, kamwe hauwezi kufa katika mateso maana ukiwa na Neno linakukomboa na kukuponya. Kwa namna unavyokula Neno ndivyo unapata nguvu.

5. Neno ni uzima wako; Zaburi 16:11 “Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele.” Neno la Mungu linakuongoza katika uzima wako kamwe hautapotea.

6. Neno ni silaha yako; Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.”

Mtu anayelifahamu Neno anajua mambo mengi: Waefeso 6:13 “Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.” Neno la Mungu ni siraha kuu hapa duniani na hii ndiyo siraha ambayo ibilisi anaiogopa sana kuliko maombi unayoomba. Kwa sababu unapoomba unaiambia mbingu itende kwa ajili yako lakini unapotendea kazi neno wewe unakuwa ndiye mtendaji mkuu.

7. Neno ni maji ya uzima; linaondoa kiu, mashaka, hofu na hali ya kutokuamini; neno lipo ili kusababisha uwe mtendaji mkuu katika ufalme wa Mungu.

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.” Neno k**a maji kazi yake ni kutoa mashaka yako, hofu, uovu wote na linakutakasa. Neno linapokuja kwako linakutakasa na kukufanya uwe mtakatifu.

8. Isaya 11:2 “Na roho ya Bwana atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana;” 10 “Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.”

Kanuni hizi za Imani zilimfanya Musa aamuru watu kuzingatia amri hizi na Neno la Mungu; Kumbu kumbu 28:1-2 “Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.”

Unapoelewa nadharia hii inakupeleka katika Imani, unapozingatia kusikia Neno ndivyo Mungu anakupandisha cheo na kukuinua atakutoa nafasi ya chini na kukupeleka nafasi ya juu.

©Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

Nehemia 8:10 “Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye as...
30/08/2026

Nehemia 8:10 “Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”

Furaha ya Bwana inapokuja ndani yako inakupa nguvu, inakupa kuwa hodari na shujaa kwa nini? Kwa sababu kile ulichokula ndicho kinachokupa furaha, kipi hicho? Neno la Mungu linakupa furaha, na ni nguvu yako. Unapopata hiyo furaha inakupa nguvu na wepesi.

Zaburi 51:12 “Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya wepesi.”

Nini maana ya furaha ya wokovu? Unapokula Neno la Mungu ambalo ni mkate wa uzima linakupa furaha. Roho ya wepesi ni nini? Ni kujua namna ya kufanya mambo kwa haraka na kwa wakati pasipo kupoteza majira yaliyowekwa. Kwa maana kuna muda wako wa kuanzisha biashara, kujenga au kuanziasha jambo fulani sasa kwa wewe kulijua Neno litakupa furaha na hiyo furaha itakusaidia kufanya mambo kwa wepesi na kwa wakati sahihi.

Yohana 17:17 “Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.”
Kwa kulifahamu Neno unakuwa unatenda katika haki na ukamilifu, kwa nini Neno lina nguvu namna hii? Neno lina nguvu ili kukufanya wewe uwe mshindi katika kila eneo la maisha yako.

Neno la Mungu lina maeneo saba ya muhimu sana:-

1. Ukilielewa Neno kamwe hauwezi kuwa masikini,
2. Neno ni mkate wa uzima: linatupa nguvu,
3. Neno ni mwanga wa miguu yetu;
Zaburi 119:105 “Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.”

Soma Neno, tafakari neno, kula neno, tamka Neno, kwa namna unavyofanya hivyo ndivyo unaruhusu neno likae ndani yako, namna unavyotenda na kukiri neno ndivyo linakaa ndani yako na kuanzia hapo kila utakachokitenda kitakaa kwa nini? Kwa sababu neno linakuwa ndani yako.

©Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

Unawezaje kupata uhai? Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.” Neno ndiy...
30/08/2026

Unawezaje kupata uhai?
Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.” Neno ndiyo mkate, ukilisikia Neno la Mungu na ukalipokea ndipo imani inaumbika ndani yako kwa maana hiyo uhai unaumbika ndani yako na Neno linasema “Yote yawezekana kwake aaminiye.”

Sasa je! Kwa nini wewe unakwama k**a unayo imani? Ukiona unakwama maana yake ni kuwa huenda ulionja mkate (Neno la Mungu) haujalila na ndiyo maana kwako hakuna uhai kwa maana k**a ulikula huo mkate (Neno la Mungu) wewe utakuwa hai na kila ulichonacho kitakuwa hai.

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.”

Watu gani wanaruhusa ya kuomba? Yohana 10:9 “Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.”

Yule ambaye anaruhusa ya kuomba ni yule ambaye amekubali kukaa ndani yake mzima mzima, je unaingiaje ndani yake mzima mzima? Kwa namna unavyolifahamu Neno, namna unavyolifahamu neno ndivyo unavyoingia kwake.

1 Yohana 1:1-4 “Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima; (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu)… ”

Ukifikia mahali pa kulijua Neno la Mungu ndipo imani inaumbika ndani yako na uzima unaumbika kwako pia; hapo ndipo furaha inaanza. Tunapozungumzia furaha ya Bwana tunazungumzia uhakika wa kujua kile kilichopo mbele.

©Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

NENO LA UZIMAWaefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.” Huu mstari unaongele...
30/08/2026

NENO LA UZIMA

Waefeso 6:10 “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.”

Huu mstari unaongelea mambo mawili (2) ya kwake:
1. Uwe hodari
2. Uwe katika nguvu na uweza wake,

Haya ndiyo maeneo mawili (2) ambayo unapaswa kuyafahamu ili uweze kuwa mshindi, ua uweze kuwa na nguvu katika Yeye.

Nini maana ya kuwa hodari? Ni kuwa mshindi, yeyote ambaye ana nguvu huwa mshindi daima, mara zote aliye hodari katika mashindano ndiye anayechukua medali ya ushindi, hata darasani yule ambaye anawaongoza wengine anayeelewa masomo kuliko wengine ndiye aliye hodari; kwa nini ni hodari? Ni kwa sababu alielewa; kwa maana hiyo tunakuwa hodari kwa kuelewa.

Nini kinachotupa kuwa hodari?
Marko 9:23 “Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.” Yesu hapa alikuwa anamaanisha nini? Alimaanisha kuwa yeyote aaminiye ni hodari na anakuwa mshindi, kwa nini? Kwa sababu ana imani. Imani inakupa wewe ushindi katika kila jambo.

Luka 1:37 “kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.” Kwa Mungu kila jambo linawezekana hakuna lisilowezekana kwake, hii inamaana kuwa, mimi, wewe au yeyote akiwa na Mungu hakuna lisilowezekana.

Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” Kwa maana hiyo unahitaji nguvu ili uweze kufanya mambo yote na upate kushinda katika hayo yote.

Uweza au nguvu hiyo tunaipataje?
Yohana 6:51 “Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”

Uweza au nguvu hiyo tunaipata kwa kupitia Neno la Mungu ambalo litatupa sisi uzima. Mkate (Neno la Mungu) linatoa uzima, uhai unatoa uhai na mauti inatoa umauti, sasa! je! Wewe umebeba nini?

©Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

2 Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende k**a alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu hum...
30/08/2026

2 Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende k**a alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.”

© Mtume Eliakunda Mwingira

USHUHUDA
30/08/2026

USHUHUDA

30/08/2026

Address

Ligula
Mtwara

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Mtwara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Mtwara:

Shortcuts

Share