Efatha Church Mtwara

Efatha Church Mtwara Efatha Church: Healing & Deliverance by the Blood of JESUS CHRIST.

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA | 31.05.2026Zaburi 84:10"Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ni...
31/05/2026

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA | 31.05.2026

Zaburi 84:10
"Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu."
Karibu Nyumbani

*NAIBARIKI JUMANNE YANGU.*BWANA yu mbele yangu daima; Kwetu kutakuwa Kwema, hakutakuwa na magomvi wala magonjwa wala vif...
26/05/2026

*NAIBARIKI JUMANNE YANGU.*

BWANA yu mbele yangu daima; Kwetu kutakuwa Kwema, hakutakuwa na magomvi wala magonjwa wala vifo, wala ukata.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

Kutoka 23:26"Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza....
24/05/2026

Kutoka 23:26
"Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza."

© MCHUNGAJI JOYMETA MGINA

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 24/06/2026KANISA LA EFATHA MTWARA MCHUNGAJI KIONGOZI JOYMETA MGINASOMO:AINA ZA VIWANGO VYA IMAN...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 24/06/2026
KANISA LA EFATHA MTWARA

MCHUNGAJI KIONGOZI JOYMETA MGINA

SOMO:AINA ZA VIWANGO VYA IMANI

Imani chanzo chake ni kusikia Neno la Kristo.
Imani ni Mungu mwenyewe anayejidhihirisha ndani ya mwanadamu kupitia Neno lake. Mtu akiipokea imani, anaanza kusukumwa kumtafuta Mungu na kutembea katika njia zake.

K**a ilivyoandikwa katika Waebrania 11:6, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Mtu anapoipokea imani, anaanza kuwa mtendaji wa Neno na kufanya mambo yanayomtambulisha Mungu katika maisha yake. Bila imani ni vigumu sana kumtambulisha Mungu kwa matendo na ushuhuda wa maisha.

Baada ya kuipokea imani, mtu anavikwa uwezo wa kufanya yale ambayo yalionekana kuwa magumu au yaliyoshindikana. Imani humwezesha mwanadamu kuona uwezekano pale ambapo wengine wanaona kutowezekana.

Matarajio ni muunganiko wa wazo la mtu pamoja na wazo la Mungu. Wazo ni jambo la ulimwengu wa roho na huumbwa na nia iliyomo ndani ya mtu. Nia ikiwa njema huzaa mawazo mema, na nia ikiwa mbaya huzaa mawazo mabaya. Wazo la mtu linapokutana na wazo la Mungu huzaliwa tarajio, na tarajio hilo huzaa imani isiyotikisika.

Mtu mwenye matarajio anatakiwa kujilinda dhidi ya mambo mawili makubwa ambayo ni hofu na mashaka. Tarajio linapaswa kulindwa mpaka litakapoonekana katika ulimwengu wa damu na nyama. Mtu asikubali chochote kuharibu kile ambacho Mungu ameweka ndani ya moyo wake.

Ili mtu apate na kukua katika imani, anapaswa kujitoa katika kufunga, kuomba na kujitakasa. Mambo haya humsaidia kuingia katika ulimwengu wa roho na kuwasiliana na Mungu kwa urahisi zaidi. Kujitakasa ni mchakato wa kuacha yale yasiyompendeza Mungu na kuishi maisha yanayompendeza yeye.

Mwamini anatakiwa kuishi sawasawa na kiwango cha imani alichopewa na Mungu.

Kiwango cha Kumtumaini Bwana

Hiki ni kiwango ambacho mtu anaweka tumaini lake lote kwa Mungu bila kutegemea akili au nguvu zake mwenyewe.
Danieli 6:13, Marko 10:36

Kiwango cha Imani ya Kuendelea Mbele (Imani ya Musa)

Hiki ni kiwango cha kuendelea mbele bila kuangalia vikwazo vinavyoonekana mbele ya macho. Ni imani inayosukuma mtu kutii sauti ya Mungu hata wakati mazingira yanaonekana kuwa magumu.
Kutoka 14:15-16

Kiwango cha Ujasiri na Moyo wa Uhodari

Hiki ni kiwango cha kusimama imara katika mapenzi ya Mungu kwa ujasiri na uthabiti. Watu wenye kiwango hiki cha imani hawarudi nyuma kwa sababu ya changamoto, bali husonga mbele kwa kutegemea ahadi za Mungu.
Yoshua 1:7

Kiwango cha Kumtegemea Mungu

Hiki ni kiwango ambacho mwamini anatambua kuwa nguvu zake, uwezo wake na mafanikio yake yanatokana na Mungu. Katika kiwango hiki mtu anakuwa mshirika na mtendaji pamoja na Mungu.
Wafilipi 4:13, 1 Yohana 4:4

Kiwango cha Uvumilivu na Kujifunza

Hiki ni kiwango cha imani ambacho mtu huendelea kusimama hata anapokutana na changamoto nyingi. Ni kiwango cha kujifunza, kukomaa na kuendelea kumwamini Mungu katikati ya majaribu mpaka ushindi upatikane.

"Nimekuja kuabudu, si kwa sababu ya nilichonacho, bali kwa sababu ya Yeye alivyo. Yeye ndiye sababu ya maisha yangu; bil...
24/05/2026

"Nimekuja kuabudu, si kwa sababu ya nilichonacho, bali kwa sababu ya Yeye alivyo. Yeye ndiye sababu ya maisha yangu; bila Yeye mimi si chochote. Utukufu wote ni Wake milele.
Efatha Church Mtwara

Nalifurahia waliponiambia twende nyumbani, hakika Mungu anastahili kupewa sifa siku zote za Maisha kwakua tunaona Mkono ...
24/05/2026

Nalifurahia waliponiambia twende nyumbani, hakika Mungu anastahili kupewa sifa siku zote za Maisha kwakua tunaona Mkono wa Mungu ukihusika kwenye Maisha yetu.

Ibada ya ufunguzi kanisa la Efatha church MtwaraKutoka 33:13[13]Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, un...
24/05/2026

Ibada ya ufunguzi kanisa la Efatha church Mtwara

Kutoka 33:13
[13]Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, unionyeshe njia zako, nipate kukujua, ili nipate neema mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako.
Gerald

Zaburi 27:4"Neno moja nimelitaka kwa Bwana, nalo ndilo nitakalolitafuta; Nikae nyumbani mwa Bwana siku zote za maisha ya...
24/05/2026

Zaburi 27:4
"Neno moja nimelitaka kwa Bwana, nalo ndilo nitakalolitafuta; Nikae nyumbani mwa Bwana siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, na kutafakari hekaluni mwake."

*SIKU YA ISHIRINI NA TATU YA KUFUNGA NA KUOMBA*Katika muendelezo wa safari yetu hii, inatukumbusha kuwa kungojea kwa Mun...
23/05/2026

*SIKU YA ISHIRINI NA TATU YA KUFUNGA NA KUOMBA*

Katika muendelezo wa safari yetu hii, inatukumbusha kuwa kungojea kwa Mungu ni tendo la imani. Tunangojea si kwa woga, bali kwa tumaini lenye uhakika, tukijua kwamba Mungu wetu husikia na kujibu.

Katika kipindi hiki cha kufunga na kuomba, kila dakika ya kumtafuta ni ushuhuda kwamba tunauamini wakati Wake na majibu Yake. Hata k**a bado hatujaona majibu, yanakuja.

Na leo iwe siku ya kujisalimisha na kumtumainia Mungu. Yeye hachelewi kamwe na kwa wakati wake, utashuhudia majibu ya maombi yako.

Zaburi 38:15 (SUV) “_Kwa kuwa nakungoja Wewe, Bwana, Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu_.”

IBADA YA MAOMBI NA MFUNGO | SIKU YA 22 | 22.5.2026Somo : kumuomba mungu kulejeshewa kibali chako kilicho ibiwa na ibilis...
22/05/2026

IBADA YA MAOMBI NA MFUNGO | SIKU YA 22 | 22.5.2026
Somo : kumuomba mungu kulejeshewa kibali chako kilicho ibiwa na ibilisi
@ pastor JOYMETER MGINA

Address

Ligula
Mtwara

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Mtwara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Mtwara:

Share