South Eastern Diocese SED ELCT

South Eastern Diocese SED ELCT KKKT- Dayosisi ya Kusini Mashariki ni Dayosisi yenye eneo la Mikoa Miwili Lindi na Mtwara

Matukio mbalimbali katika picha leo tar 17/12/2022 Ibada ya kuwabariki watheolojia kuwa wachungaji. Baada ya ibada Baba ...
17/12/2022

Matukio mbalimbali katika picha leo tar 17/12/2022 Ibada ya kuwabariki watheolojia kuwa wachungaji. Baada ya ibada Baba Askofu Lucas Mbedule Judah alipanda mti wa kumbukumbu kwa ajili ya watheolojia waliobarikiwa kuwa Wachungaji.

Baba Askofu wa KKKT DAYOSISI ya KUSINI MASHARIKI Lucas Mbedule Judah. Siku ya Leo amebariki watheologia kuwa Wachungaji ...
17/12/2022

Baba Askofu wa KKKT DAYOSISI ya KUSINI MASHARIKI Lucas Mbedule Judah. Siku ya Leo amebariki watheologia kuwa Wachungaji katika Usharika wa Magomeni Mtwara. Waliobarikiwa ni Neema Chiputa, Joseph Kikoti, Vumilia Mgaya na Thadei Mohele.
UJUMBE WA NENO LA MUNGU kutoka kwa Baba Askofu ulikuwa
2 Timotheo 4:5
[5]Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.
But watch thou in all things, endure afflictions, do the work of an evangelist, make full proof of thy ministry
Baba Askofu aliwaasa Wachungaji kwa kusema , "Mnaingia kwenye huduma ya Kichungaji wakati dunia imechanganyikiwa, nchi imechanganyikiwa, na jamii imechanganyikiwa na Kanisa limechanganyikiwa.
Hivyo nendeni mkamtumikie Mungu kwa uaminifu, mkatafute majibu ya changamoto zilizopo katika makundi yote. Hali kadhalika aliwaasa Wachungaji hao kumtegemea Mungu katika huduma yao.
Tuendelee kuwaombea watumishi hawa ili huduma yao iendelee kuleta matunda kwa Kanisa la Mungu.

Kwaya ya Wamama na Betheli wa usharika wakihudumu kwa nyimbo usharika wa Magomeni kwenye ibada ya kuwabariki watheolojia...
17/12/2022

Kwaya ya Wamama na Betheli wa usharika wakihudumu kwa nyimbo usharika wa Magomeni kwenye ibada ya kuwabariki watheolojia kuwa Wachungaji.

17/12/2022
17/12/2022

Ibada Takatifu ya kuwabariki Watheolojia
Neema Chiputa, Joseph Kikoti, Vumilia Mgaya, Thadeo Mhole kuwa Wachungaji. Ilikuwa ni ibada iliyoambata na Baraka za kipekee katika Dayosisi yetu ya Kusini Mashariki. Ibaya hiyo ilifanyika usharika wa Magomeni Mtwara.

Picha kutoka Maktaba yetu, tar 12/12/2021 Usharika wa Newala Mch Geofrey John Mposola alipopata daraja la Kichungaji. Tu...
12/12/2022

Picha kutoka Maktaba yetu, tar 12/12/2021 Usharika wa Newala Mch Geofrey John Mposola alipopata daraja la Kichungaji. Tuendelee kumuombea ili Mungu azidi kumtumia katika viwango alivyokusudia.
🙏🙏🙏🎂

Siku ya Leo ilifanyika Ibada ya Ndoa Takatifu baina ya Vasco Andrea na Atupelye Kiulamagulu iliyofanyika katika Usharika...
09/12/2022

Siku ya Leo ilifanyika Ibada ya Ndoa Takatifu baina ya Vasco Andrea na Atupelye Kiulamagulu iliyofanyika katika Usharika wa Masasi Mjini, Picha katika matukio ni Baba Askofu Lucas Mbedule Judah akiendelea kukamilisha shughuli hiyo.
Neno la Mungu lilikuwa ni Waefeso 5:15-17
[15]Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si k**a watu wasio na hekima bali k**a watu wenye hekima;
See then that ye walk circumspectly, not as fools, but as wise,
[16]mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
Redeeming the time, because the days are evil.
[17]Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

Asanteni sana

Tukio la Pili Leo Tar 4/12/2022Matukio katika picha ni Mh Baba Askofu pamoja na Msaidizi wa Askofu wakipokea hati ya kiw...
04/12/2022

Tukio la Pili Leo Tar 4/12/2022
Matukio katika picha ni Mh Baba Askofu pamoja na Msaidizi wa Askofu wakipokea hati ya kiwanja kutoka kwa Familia ya Bw & Bi Maliki ambao wametoa ardhi kwa ajili ya Kujenga Kanisa eneo la Mbawala Chini.

Tukio la kwanza kupokea hati ya kiwanja.Picha katika matukio mbalimbali, eneo la Mbawala chini ambapo leo tar 4/12/2022 ...
04/12/2022

Tukio la kwanza kupokea hati ya kiwanja.
Picha katika matukio mbalimbali, eneo la Mbawala chini ambapo leo tar 4/12/2022 Baba Askofu Lucas Mbedule Judah aliambata na Msaidizi wa Askofu Mch Yericko Ngwema pamoja na Mch wa Usharika Nuru Mwakapsuya kupokea hati ya makabidhiano ya nyaraka za shamba la Kanisa ambalo lilitolewa familia ya Godfrey Nkya. Kwenye matukio hayo anaonekana Mama Nkya akikabidhi nyaraka hizo kwaajili ya matumizi ya Kanisa.

Matukio katika picha ya jumapili ya Tar 13/11/2022 yakionesha Ibada ya kipaimara katika usharika wa Masasi. Tendo hilo l...
30/11/2022

Matukio katika picha ya jumapili ya Tar 13/11/2022 yakionesha Ibada ya kipaimara katika usharika wa Masasi. Tendo hilo la Baraka Iilioongozwa na Baba Askofu Lucas Mbedule Judah akishirikiana na Mkuu wa jimbo la Magharibi. Ibada hiyo ilifanyika kwenye jengo jipya la ibada ikiwa ni kwa mara ya kwanza. Pia ibada hiyo iliambatana na baraka nyingine k**a CHAKULA Cha bwana na UBATIZO .

Ibada ya kipaimara usharika wa Kilwamasoko  tar 14/11 jumatatu jioni ilikuwa ni ibada ya Kipaimara, ibada hiyo iliongozw...
30/11/2022

Ibada ya kipaimara usharika wa Kilwamasoko tar 14/11 jumatatu jioni ilikuwa ni ibada ya Kipaimara, ibada hiyo iliongozwa na Baba Askofu akishirikiana na Mch wa Eneo la Missioni ya Kilwa Mch Mabala. Baada ya ibada ilifanyika sherehe ya pamoja nje ya Kanisa ( viunga vya kanisa).

Baba Askofu akiwa na watheologia walio masomoni, Makumira University, Tar 27/11/2022.
30/11/2022

Baba Askofu akiwa na watheologia walio masomoni, Makumira University, Tar 27/11/2022.

Address

S. L. P. 469
Mtwara

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when South Eastern Diocese SED ELCT posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share