Efatha Church Mpwapwa

Efatha Church Mpwapwa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Efatha Church Mpwapwa, Church of Christ, Mpwapwa.

Mtu yeyote, iwe umeajiriwa au umejiajiri, usisahau jambo hili: Mungu ndiye aliyekupa kazi uliyonayo. 🙏Ameona uwezo wako,...
10/08/2026

Mtu yeyote, iwe umeajiriwa au umejiajiri, usisahau jambo hili: Mungu ndiye aliyekupa kazi uliyonayo. 🙏

Ameona uwezo wako, vipaji vyako na kile unachoweza kufanya. Amekuamini kwamba utaitenda kazi yako kwa uaminifu, bidii na kwa ubora unaostahili.

Kwa hiyo, usiidharau kazi yako kwa sababu tu haijafikia kiwango unachotamani. Ifanye kwa moyo wote, kwa sababu hata kazi ndogo inaweza kuwa sehemu ya mpango mkubwa wa Mungu katika maisha yako. ❤️

Leo Jumatatu, jiulize:👉 Je, ninaifanya kazi yangu kwa moyo wa shukrani au kwa mazoea tu?



'swill

KUNDI LA WANAWAKE LILILOONGOZANA KATIKA KABURI KWENDA KUMPAKA BWANA YESU MAFUTA:Ni wakina nani hao? Luka 24:9-10 “Wakaon...
09/08/2026

KUNDI LA WANAWAKE LILILOONGOZANA KATIKA KABURI KWENDA KUMPAKA BWANA YESU MAFUTA:

Ni wakina nani hao? Luka 24:9-10 “Wakaondoka kaburini, wakarudi; wakawaarifu wale kumi na mmoja na wengine wote habari za mambo hayo yote. Nao ni Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo, na wale wanawake wengine waliokuwa pamoja nao;”

Pale wanaume walipokuwa wamejawa hofu lakini hawa wanawake waliamka asubuhi na mapema wakaenda kumpaka Yesu mafuta, hawakuuliza wanaume wako wapi, bali waliamka na kwenda moja kwa moja kwa Bwana wao.

MWANAMKE WA EFATHA:
Wewe mwanamke wa Efatha onesha upendo wako kwa Kristo mwokozi wako;
Luka 23:28 “Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.” Nakuita wewe mwanamke wa Efatha, k**a biblia isemavyo kuwa wanawake ni jeshi kubwa, onesheni hivyo.

Wagalatia 6:7-8 “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.”

Kile utakachoenda kufanya mbele za Baba yako wa mbinguni usifanye katika mwili bali katika roho maana katika mwili utavuna uharibifu lakini katika roho utavuna uzima wa milele kwako na wa kizazi chako.

© MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

SOMO: MWANAMKE WA EFATHAZaburi 68:11 “Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;” Biblia inase...
09/08/2026

SOMO: MWANAMKE WA EFATHA

Zaburi 68:11 “Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;”

Biblia inasema wanawake ni jeshi kubwa, maana yake ni kuwa; kuna nguvu kubwa inayowasukuma wanawake. Wamama wanapokuwa wanajifungua wanatumia nguvu sana ili kusukuma mtoto atoke, k**a wanawake wanaweza kusukuma mtoto mpaka atoke basi elewa kuwa wana nguvu kubwa na Mungu anatambua hilo na ndiyo maana akasema “Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa”

Kutoka 1:9 “Wazalisha wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si k**a wanawake wa Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia.”

Hivyo wanawake wanazo nguvu za kujihudumia; wanawake wana nguvu ndani yao ya kujisaidia wenyewe, maana yake wao si k**a wanaume, wanaume wana nguvu za mwili; wanawake hawana misuli ya nguvu lakini wana nguvu ndani yao, ndiyo maana huweza kusukuma jambo lolote na likatokea, hivyo wakiwa mahali popote wanasababisha mambo yaende. Wanawake ninyi ni jeshi kubwa na mnazo nguvu, kwa maana Mungu mwenyewe ametangaza kuwa wanawake ni jeshi kubwa.

Wamisri waliwatambua wanawake wa Kiebrania ya kwamba wanazo nguvu katika kutoka anasema “wazalisha wakamwambia Farao, ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si k**a wanawake wa kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia.”

Nakutangazia leo wewe mwanamke wa Efatha kuwa wewe siyo k**a mwenye dhambi, unazo nguvu katika roho, unazo nguvu ndani ya moyo wako, unaweza kuomba pasipo kukoma, una uwezo wa kushuhudia pasipo kuogopa chochote. Simama na chukua nafasi yako, wewe una nguvu.

© MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

SIKU YA PARAPANDA:Siku ile itakuwa ni siku makini sana, dunia yote itanyamaza kimya, wakati wana wa Mungu wanainuliwa, s...
09/08/2026

SIKU YA PARAPANDA:

Siku ile itakuwa ni siku makini sana, dunia yote itanyamaza kimya, wakati wana wa Mungu wanainuliwa, siku ile ni siku ya kitisho, tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu hakujawahi kutokea tetemeko la aina hiyo, tetemeko la ajabu litaitikisa dunia wakati wana wa Mungu wanaondoka.

Kwa nini dunia itatikisika? Ni ili kuruhusu makaburi kufunguka na watu watoke huko, kuruhusu bahari kutoa watu waliyoko huko.
Huu siyo wakati wa kuwaandaa watu wanene kwa lugha mpya au waponywe magonjwa yao, la! Bali ni ili kuwaandaa watu kwa ajili ya unyakuo.

Usifikiri kanisani ni mahali pa mzaha mwana wa Mungu, bali ni mahali makini sana, una heri wewe unayesikia kile ambacho anaongea mtumishi wa Mungu na kutenda sawa sawa, yale unayoshindwa sawa lakini yale unayoweza kuyafanya na ukakataa kufanya hiyo ni mbaya sana. Una heri wewe ambaye utaiona siku ile na kuingia. Wewe uliyepata neema ya kuokoka ndani ya Efatha usije ukadharau au kusahau kile ulichokipata Efatha.

© MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira tayari yupo mubashara ili kufundisha Neno la Mungu litakalokupa uzima, faraja, tu...
09/08/2026

Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira tayari yupo mubashara ili kufundisha Neno la Mungu litakalokupa uzima, faraja, tumaini na imani ndani yako.

Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira tayari yupo mubashara ili kufundisha Neno la Mungu litakalokupa uzima, faraja, tu...
09/08/2026

Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira tayari yupo mubashara ili kufundisha Neno la Mungu litakalokupa uzima, faraja, tumaini na imani ndani yako.

Zaburi 20:1-9 “Bwana akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na...
09/08/2026

Zaburi 20:1-9 “Bwana akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue. Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni. Azikumbuke sadaka zako zote, Na kuzitakabali dhabihu zako. Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote. Na tuushangilie wokovu wako, Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. Bwana akutimizie matakwa yako yote. Sasa najua kuwa Bwana amwokoa masihi wake; Atamjibu kutoka mbingu zake takatifu. Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la Bwana, Mungu wetu. Wao wameinama na kuanguka, Bali sisi tumeinuka na kusimama. Bwana, umwokoe mfalme, Utuitikie siku tuitayo.”

Mwana wa Mungu unapaswa kutambua kuwa unapotoa sadaka zako mbele za Bwana Yesu si bure, bali huwa inazungumza mbele za Bwana. Unapotoa matoleo yako kwa usahihi mbele za Bwana Yesu, Yeye atakukumbuka, atakumbuka sadaka zako na atakufanyia usaidizi pindi pale utakapokuwa una uhitaji.

© MTUME ELIAKUNDA MWINGIRA

OFFERING SESSION
09/08/2026

OFFERING SESSION

Neema ya Kristo Yesu yatosha katika maisha yetu; shuhuda hii itakupa kupokea tumaini la Mungu, unapomwomba anasikia na a...
09/08/2026

Neema ya Kristo Yesu yatosha katika maisha yetu; shuhuda hii itakupa kupokea tumaini la Mungu, unapomwomba anasikia na atakuponya kwa yale yote unayopitia katika maisha yako.

Katika matoleo ndipo ziliko baraka za Mungu katika maisha ya mwanadamu; kupitia shuhuda hii utatambua nguvu ya matoleo k...
09/08/2026

Katika matoleo ndipo ziliko baraka za Mungu katika maisha ya mwanadamu; kupitia shuhuda hii utatambua nguvu ya matoleo katika kupokea mafanikio aliyotuandalia Mungu. Kuwa mwaminifu katika matoleo yako.

Address

Mpwapwa
41601

Telephone

+255627892420

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Mpwapwa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share