Radio Sauti Ya Injili Moshi

Radio Sauti Ya Injili Moshi Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Radio Sauti Ya Injili Moshi, Evangelical church, 777, Moshi.

01/06/2026

Wahitaji 160 Wanufaika na Huduma za Diakonia Himo

MOSHI

Katika juhudi za kuwasaidia wenye uhitaji, jumla ya watu 160, wakiwemo wazee, watoto, na watu wenye ulemavu, wamepatiwa misaada mbalimbali ikiwemo matibabu bure pamoja na mahitaji mengine ya nyumbani , huku watoto zaidi ya 100 wakigharamiwa ada na michango mingine ya shule.

Msaada huo umetolewa wakati wa Ibada Maalumu ya Diakonia iliyofanyika kwa mara ya tano sasa katika Usharika wa Himo, Jimbo la Kilimanjaro Mashariki, Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT).

Akizungumza ​katika ibada hiyo mchungaji kiongozi wa usharika huo George Mamuya amesema , jumla ya wahitaji 160 wamepatiwa huduma za afya ikiwemo matibabu na dawa, huku watoto wakilipiwa ada pamoja na michango ya shule ili kuwawezesha kuendelea na masomo.

Mwenyekiti wa Diakonia katika Usharika huo wa Himo, Dorkasi Moshi, ameeleza kuwa changamoto kubwa wanayokabiliana nayo kwa sasa ni ongezeko la kasi la watu wenye shida ambapo amesema maadhimisho ya Siku ya Diakonia husaidia kwa kiasi kikubwa kukusanya nguvu ya pamoja ili kuwafikia wahitaji wengi zaidi.

Baadhi ya wazee pamoja watu wenye mahitaji maalumu wameeleza kufurahishwa na huduma hiyo wakitaja kuwa faraja kubwa kwao, kwani licha ya misaada ya vitu walivyopewa, fursa ya kukusanyika, kusali pamoja, na kujisikia sehemu ya jamii imewapa nguvu mpya na kuwatoa katika upweke unaowakabili.

31/05/2026

Usharika wa Himo wawafariji mamia ya wenye uhitaji Siku ya Udiakonia

Moshi

Katika kuadhimisha Siku ya Udiakonia, Usharika wa Himo uliopo Jimbo la Kilimanjaro Mashariki, Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), umewakutanisha na kuwafariji mamia ya watu kutoka makundi yenye uhitaji maalum.

​Maadhimisho hayo yaliyofanyika leo Jumapili, Mei 31, 2026, yamehusisha wazee, watoto yatima, wajane, pamoja na watu wenye ulemavu, ambao mbali na kupokea misaada, wepata fursa ya kushiriki ibada ya pamoja na kutoa sadaka ya shukrani ili kuendeleza huduma hiyo

​Katika tukio hilo la kipekee, wahitaji hao wameshiriki Sakramenti Takatifu ya Meza ya Bwana na kupatiwa huduma za matibabu bila malipo bure pamoja na kugawiwa mahitaji mbalimbali ya msingi ya nyumbani k**a vile Mchele, mahindi, maharage, sukari, sabuni pamoja na nguo

​Akihubiri katika ibada hiyo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Himo, George Mamuya, ametoa wito mzito kwa jamii kubadili mtazamo wao dhidi ya watu wenye uhitaji kwa kutowabeba k**a mzigo Katika jamii Bali k**a Fursa ya mafanikio na baraka Katika maisha yao

​Baadhi ya washiriki wa huduma hiyo waliozungumza na Dira ya Leo wameeleza kufurahishwa na kuguswa kwao na jambo hilo, wakitaja kuwa limekuwa faraja kubwa kwao, kwani licha ya misaada ya vitu walivyopewa, fursa ya kukusanyika, kusali pamoja, na kujisikia sehemu ya jamii imewapa nguvu mpya na kuwatoa katika upweke unaowakabili.

​Siku ya Udiakonia katika makanisa ya KKKT imekuwa ikitumiwa k**a mfumo wa kurejesha upendo na huduma za kijamii kwa vitendo, ikiongozwa na misingi ya kuwajali wasiojiweza huku misaada hiyo ikiwa ni kutoka kwa wadau mbalimbali wenye moyo wa kujitolea.

30/05/2026

Maadhimisho ya CCT Kilimanjaro yafanyika Yasisitiza Umoja kuelekea kilele chake kitaifa Njombe

Same

Ikiwa Leo ni maadhimisho ya siku ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa mkoa wa Kilimanjaro imeelezwa toka kuanzishwa kwake imekuwa nguzo muhimu katika kutoa huduma za kiroho, kimwili na kijamii kutokana na misingi thabiti iliyowekwa.

​Hayo yamebainishwa leo Jumamosi, Mei 30, 2026, na Mwenyekiti wa CCT mkoa wa Kilimanjaro, Askofu Charles Mjema, wakati wa ibada maalum ya maadhimisho ya siku ya jumuiya hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Dayosisi ya Pare KKKT wilayani Same

Vilevile ​Askofu Mjema amesema kuwa matarajio ya jumuiya hiyo kwa sasa ni kuendelea kuimarisha umoja huo na kuhakikisha wanatekeleza kikamilifu malengo makuu yaliyowekwa na waasisi wa CCT.

Akihubiri kwenye maadhimisho hayo, Mchungaji Kanoni Lucas kutoka Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Mount Kilimanjaro, amewataka Wakristo kujihoji k**a wanaishi kulingana na mapenzi ya Mungu, huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha Umoja.

​Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wa ibada hiyo, akiwemo Mchungaji David Tekwa na Emma Msuya, wameeleza kuwa maadhimisho hayo yamekuwa fursa muhimu ya kujifunza na kukumbushana wajibu wao katika jamii na kanisa hasa suala la Umoja.

​Maadhimisho haya ya ngazi ya mkoa ni maandalizi ya kuelekea kilele cha maadhimisho ya CCT Kitaifa, yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili, Mei 31, mkoani Njombe huku lengo likiwa ni kukumbushana misingi na umuhimu wa Umoja wa makanisa na vyama wanachama wa CCT Katika ngazi zote .

25/05/2026
22/05/2026

Rombo

Diwani wa kata ya Marangu Kitowo Simon Massawe amewataka wahitimu wa kidato Cha sita kutumia elimu waliyoipata k**a nyenzo ya kuleta maendeleo binafsi na ya jamii.

Diwani Simon ametoa ushauri huo wakati akiwa Mgeni rasmi katika mahafali ya kidato cha sita ya mwaka 2026 katika shule ya Sekondari Shauritanga,

Mhe. Simon Rogath Massawe, amesema vijana wanapaswa kuwa na nidhamu, kujituma na kuwa waadilifu wanapoanza hatua mpya ya maisha baada ya kuhitimu masomo yao ya sekondari.

Aidha, amewaasa wahitimu hao kuepuka vitendo vinavyoweza kuharibu mustakabali wao, ikiwemo matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, dawa za kulevya, makundi yenye ushawishi mbaya pamoja na kutokata tamaa wanapokutana na changamoto za maisha kwani mafanikio yanahitaji uvumilivu, bidii na maamuzi sahihi.

18/05/2026

Askofu Shoo amstaafisha kwa heshima Mchungaji Lord Macha

Moshi

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini, Dkt. Fredrick Shoo, amemstaafisha kwa heshima Mchungaji Lord Macha, baada ya kulitumikia kanisa hilo kwa uaminifu kwa kipindi cha miaka 24.

​Ibada hiyo ya kihistoria imefanyika Jumapili, Mei 17, 2026, katika Usharika wa Pumuani, Jimbo la Kilimanjaro Mashariki, mkoani Kilimanjaro.

​Akisoma wasifu na historia ya utumishi wa Mchungaji Macha, Katibu Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini, Mhandisi Zebadia Moshi, ameeleza kuwa mchungaji huyo amekuwa nguzo muhimu katika injili, akitumikia kwa unyenyekevu katika sharika mbalimbali kwa zaidi ya miongo miwili.

​Akitoa neno la shukrani na itikio la kustaafu kwake, Mchungaji Lord Macha amemshukuru Mungu kwa ulinzi na neema katika kipindi chote cha utumishi wake huku akibainisha kuwa tangu alipoitwa na Mungu hawajawahi kujutia wito huo badala yake ametumika kwa uaminifu

​Katika ibada hiyo, Askofu Dkt. Shoo pia aliongoza zoezi la kuweka jiwe la pembe katika jengo jipya la ibada la Mtaa wa Sayuni ambapo amewataka Wakristo kuwa na unyenyekevu na utulivu katika maombi, huku akiwasisitiza kufanya toba ya kweli ili kutoka katika shimo la dhambi bila kujali mazingira yaliyowaingiza humo.

Ibada hiyo ambayo ilihudhuriwa pia na Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Godfrey Mzava, ameliomba kanisa kuongeza nguvu katika kushirikiana na serikali kupiga vita vitendo vya ukatili akibainisha kuwa kuna ongezeko kubwa la matukio hayo katika jamii kwa sasa.

​Kwa upande wake, Mkuu wa Jimbo la Siha, Mchungaji Elisa Kileo, akihubiri katika ibada hiyo, amewasihi Wakristo kutokata tamaa na badala yake wadumu katika maombi kwani ndio silaha pekee ya kushinda vita vya kiroho na kutokukubalia aina yeyote ya ukatishwaji wa tamaa.

16/05/2026

Jimbo la Kilimanjaro Mashariki lazindua Juma la Pentekoste, wahubiri watakiwa kusimamia imani kukesha na maombi

Moshi

Jimbo la Kilimanjaro Mashariki la Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limezindua rasmi Juma la Pentekoste, huku watumishi waliopata nafasi ya kuhudumu wakitakiwa kusimamia kwa vitendo kaulimbiu ya mwaka huu inayohamasisha waumini kusimama katika imani , kukesha na kuomba.

Akizungumza leo Jumamosi Mei 16, 2026 wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika usharika wa Samanga Marangu ,Mkuu wa Jimbo la Kilimanjaro Mashariki, Mchungaji Calvin Koola amesema maandalizi ya juma hilo tayari yamekamilika na kilichobaki ni wahubiri kuanza kupita katika vituo mbalimbali kwa ajili ya kuhubiri Injili ya Kristo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Elimu ambaye pia ni mratibu wa semina za mikutano ya Pentekoste na Nuru ya Injili, Mchungaji Fadhili Kiwera amesema kwa mwaka huu maadhimisho hayo yanafanyika kimajimbo tofauti na ilivyozoeleka hapo awali.

Amesema jumla ya vituo 293 pamoja na wahubiri 438 wameandaliwa kuhudumu katika sharika 177 za Dayosisi ya Kaskazini, lengo likiwa kuwafikia waumini wengi zaidi kupitia mafundisho ya Injili.

Naye Mdiakonia Elirehema Kaaya, akihubiri katika ibada hiyo ya ufunguzi , amewataka wahubiri hao kuhakikisha wanazingatia maombi, kuwa na imani pamoja na kumuomba Roho Mtakatifu awaongoze na kuwapa nguvu wanapotekeleza kazi ya kuhubiri Injili katika maeneo mbalimbali watakayohudumu.

Kwa upande wa watumishi waliotumwa kuhudumu katika Juma hilo wamesema wako tayari kuifikisha Injili kwa jamii kwa lengo la kuleta uponyaji wa kiroho, kuimarisha imani za waumini na kuendeleza kazi ya Mungu katika maeneo mbalimbali watakayohudumu.

14/05/2026

Dayosisi ya Kaskazini KKKT na NCA zaivisha Jeshi la kupambana na ukatili wa kijinsia.

Moshi

​Washiriki wa semina maalum ya siku nne kuhusu mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia (GBV), wameahidi kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii kufuatia kuongezeka kwa vitendo hivyo nchini.

​Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na shirika la Norwegian Church Aid (NCA) kwa kushirikiana na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini , yamehusisha viongozi wa dini, wasaidizi wa kisheria (paralegals), na watoa huduma ndogo ndogo za kifedha.

​Akizungumza leo Alhamisi, Mei 14, 2026, Msaidizi wa Mkuu wa Jimbo la Siha, Mchungaji Godwin Msele, pamoja na shekhe Abdalah Mfaume, wamesema semina hiyo imewapa mwanga mpya wa namna ya kubaini na kukabiliana na ukatili unaofanyika hata ndani ya nyumba za ibada.

​Kwa upande wao Christina Lema ambae ni Katibu wa DIVA kutoka wilaya ya Hai, na Monica Mathayo, msaidizi wa kisheria kutoka Babati, wamesisitiza kuwa kikwazo kikubwa ambacho wamekuwa wakikabiliana nacho ni uoga na ukimya hivyo mafunzo hayo yamewajengea ujasiri wa kuvunja ukuta wa huo

Hata hivyo ​Mratibu wa NCA mkoani Kilimanjaro, mchungaji Andrew Munisi, amebainisha kuwa semina hiyo imefichua uwepo wa matukio mengi ya ukatili yanayofumbiwa macho kutokana na​ Mila potofu, ukosefu wa Elimu pamoja na uoga ndani ya jamii.

​Amesema Mategemeo Yao baada ya semina hiyo ni kuona washiriki wa mafunzo hayo wanakuwa mstari wa mbele kupaza sauti ili jamii iweze kuishi kwa amani na furaha, bila hofu wala wasiwasi.

Address

777
Moshi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Sauti Ya Injili Moshi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Radio Sauti Ya Injili Moshi:

Share