Radio Sauti Ya Injili Moshi

Radio Sauti Ya Injili Moshi Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Radio Sauti Ya Injili Moshi, Evangelical church, 777, Moshi.

UCB yazindua mikopo kwa mama Lishe na baba Lishe Kilimanjaro Moshi Benki ya Uchumi Commercial Bank (UCB) imezindua mikop...
28/08/2026

UCB yazindua mikopo kwa mama Lishe na baba Lishe Kilimanjaro

Moshi

Benki ya Uchumi Commercial Bank (UCB) imezindua mikopo ya fedha na nishati safi kwa Mama Lishe na Baba Lishe, mpango unaolenga kuwawezesha wajasiriamali hao kukuza shughuli zao za kiuchumi na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara.

Uzinduzi wa mpango huo, unaojulikana k**a UMALITA, umefanyika katika Soko la Manyema mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukabiliana na changamoto ya mitaji na matumizi ya nishati safi miongoni mwa wafanyabiashara hao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi Commercial Bank Limited (UCB), Cornel Alois, amewataka Mama Lishe na Baba Lishe kujiunga katika vikundi ili kurahisisha upatikanaji wa mikopo hiyo.

Amesema mikopo hiyo inaweza kutolewa bila wafanyabiashara kuhitajika kuwa na dhamana ya mali, hatua inayolenga kuwawezesha wajasiriamali ambao mara nyingi hukabiliwa na changamoto ya kukosa dhamana wanapohitaji mikopo kutoka taasisi za fedha.

Mikopo hiyo inajumuisha mkopo wa fedha kwa ajili ya kuendeleza na kukuza biashara, pamoja na mkopo wa mitungi ya gesi kwa wafanyabiashara wanaotaka kutumia nishati safi katika shughuli zao za upishi.

Kwa upande wake, Afisa Tarafa wa Moshi Mashariki, Halima Idrisa, akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi, ameipongeza UCB kwa kuiunga mkono serikali katika kuwawezesha wajasiriamali hao na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Naye Mama Lishe, Asha Olotu, ameishukuru Serikali na UCB kwa kuliona na kulikumbuka kundi hilo, akisema mikopo hiyo itawapa fursa ya kukuza biashara na kujikwamua kiuchumi.

Uzinduzi huo unatarajiwa kuwa chachu kwa Mama Lishe na Baba Lishe kuongeza uzalishaji, kuboresha biashara zao na hatimaye kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa jamii na taifa kwa ujumla.

28/08/2026

Watafiti Watakiwa Kutumia Matokeo Ya Tafiti Kuboresha Sera Na Huduma Za Jamii

Moshi

KILIMANJARO: Watafiti nchini wametakiwa kuhakikisha matokeo ya tafiti zao hayabaki kwenye majarida ya kisayansi pekee, bali yanatumika kuboresha sera, huduma za jamii na kusaidia viongozi kufanya maamuzi yenye tija.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu, Profesa Said Abood, wakati akizungumza katika Kongamano la Tatu la Kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu KCMC mkoani Kilimanjaro lililotoa fursa kwa watafiti kuwasilisha matokeo ya tafiti mbalimbali wanazozifanya.

Profesa Abood amesema sayansi, teknolojia na utafiti vina nafasi muhimu katika kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku akisisitiza umuhimu wa matokeo ya tafiti kuwafikia watunga sera na kutumika kuleta mabadiliko katika jamii.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu KCMC, Profesa Efatha Kaaya, amesema tafiti zinazofanywa chuoni hapo zinalenga kuboresha sekta ya afya, ikiwemo katika magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza, pamoja na matumizi ya teknolojia katika ugunduzi wa magonjwa.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwajengea uwezo vijana katika masuala ya utafiti, akisema wataalamu wenye uzoefu wanapaswa kuwaongoza na kuwalea vijana ili kujenga kizazi kipya cha watafiti kwa manufaa ya taifa.

Baadhi ya washiriki wa kongamano hilo kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda na Tanzania wamesema limewapa fursa ya kujifunza mambo mapya, kubadilishana uzoefu na kufahamu maendeleo mbalimbali katika tafiti za kisayansi.

Kongamano hilo la Tatu la Kisayansi limewakutanisha watafiti, wataalamu wa afya, wanafunzi na wadau mbalimbali, kwa lengo la kujadili na kuwasilisha matokeo ya tafiti yanayolenga kuboresha afya na kuchangia maendeleo ya jamii.

MWISHO.

Tanzania Dira2050

Makamu wa Rais Dkt Immanuel Nchimbi atangaza kujiuzulu
25/08/2026

Makamu wa Rais Dkt Immanuel Nchimbi atangaza kujiuzulu

13/08/2026

KCMC kuandaa wataalamu wa imunolojia kwa utafiti na chanjo

Moshi

Chuo Kikuu KCMC kwa kushirikiana na chuo kikuu Cha Copenhagen nchini Dermark wameanza Mpango wa programu ya uzamili katika taaluma ya imunolojia, ikiwa ni hatua ya kuongeza idadi ya wataalamu wanaohitajika nchini katika utafiti na maendeleo ya chanjo na mifumo ya kinga ya mwili.

Akizungumza katika semina ya siku tatu inayowakutanisha wataalamu wa afya kutoka Tanzania, Ghana na Denmark, Dkt. Godfrey Temba amesema Tanzania ina uhitaji mkubwa wa wataalamu wa imunolojia, hivyo kuanzishwa kwa programu hiyo kutasaidia kuzalisha wataalamu wenye uwezo wa kufanya tafiti na kutoa mchango katika kukabiliana na changamoto za afya.

Amesema mpango huo ni sehemu ya juhudi za KCMC kuimarisha mafunzo na utafiti katika sekta ya afya, huku ukilenga kuongeza uwezo wa Tanzania kuwa na wataalamu wanaoweza kushiriki katika maendeleo ya teknolojia za afya, ikiwemo chanjo.

Dkt. Temba amesema chuo hicho kinaweka mipango ya kuandaa programu hiyo ya uzamili, ambayo itatoa fursa kwa wataalamu kupata mafunzo ya juu katika eneo la imunolojia.

Kwa upande wake, mmoja wa wanufaika wa mradi huo, Dkt. Emmaculate Gabriel, amesema mafunzo hayo yatawajengea uwezo wa kufanya tafiti na kuchangia katika maendeleo ya chanjo na teknolojia za kinga ya mwili, ambazo zinaweza kuwa na manufaa kwa Tanzania na dunia kwa ujumla.

Naye Dkt. Ashraf Mahmoudi amesema mafunzo hayo yatawawezesha kuwa watafiti na kusambaza maarifa kwa wataalamu wengine, hatua ambayo amesema inaweza kusaidia kuleta maendeleo katika sekta ya afya na jamii kwa ujumla.

Mpango huo unatajwa kuwa sehemu ya jitihada za Chuo Kikuu KCMC kuwaandaa wataalamu wa afya wenye uwezo wa kutumia utafiti na ubunifu kutatua changamoto za kiafya na kuunga mkono azma ya Tanzania ya kujitegemea katika sekta ya afya.

Mkutano mkuu wa 19 Wanawake KKKT umemchagua Ruth Kaaya kuwa mwenyekiti wa wanawake KKKT
07/08/2026

Mkutano mkuu wa 19 Wanawake KKKT umemchagua Ruth Kaaya kuwa mwenyekiti wa wanawake KKKT

26/07/2026

Walimu Wavuna Zaidi ya Milioni 30 , Tuzo za Moshi DC Teachers Samia Award

Moshi

Historia mpya imeandikwa katika sekta ya elimu ya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi baada ya walimu 202 kutoka shule za msingi na sekondari za serikali na binafsi kunufaika na zaidi ya shilingi milioni 30 pamoja na vyeti vya pongezi kupitia mpango wa kwanza wa Moshi DC Samia Teachers Award, ulioanzishwa kwa ushirikiano wa Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, Mhe. Moris Makoi, na Mbunge wa Jimbo la Vunjo, Mhe. Enock Koola.

Hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wadau wa elimu na walimu, huku mgeni rasmi akiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dkt. Festo Dugange.

Akizindua rasmi mpango huo, Dkt. Dugange alisema utoaji wa tuzo kwa walimu wanaofanya vizuri katika mitihani ya taifa ni hatua muhimu ya kuongeza ari ya kazi, kuhamasisha ushindani chanya na kuendelea kuboresha matokeo ya wanafunzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.

25/07/2026

Kuthamini mwalimu ni kuwekeza kwa mtoto na jamii - CWT

Moshi

Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Moshi Vijijini kimesema jitihada za kuwathamini na kuwapa motisha walimu hazipaswi kuonekana k**a zawadi kwa walimu pekee, bali ni uwekezaji mkubwa kwa jamii nzima kutokana na nafasi yao katika kujenga msingi wa maendeleo ya watoto na taifa kwa ujumla.

Akizungumza kuhusu mpango wa Moshi DC Samia Teachers Award, Katibu wa CWT Wilaya ya Moshi Vijijini, Caroline Ngereshi, amesema walimu wanafanya kazi kubwa ya kulea, kufundisha na kuwaandaa watoto kuwa viongozi wa baadaye, hivyo jamii inapaswa kutambua mchango huo na kushirikiana nao.

Amesema mafanikio ya sekta ya elimu hayawezi kupatikana kwa juhudi za walimu pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa wazazi, viongozi, wanafunzi na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia yanapatikana.

“Tunawashukuru wabunge wetu wa Jimbo la Moshi Vijijini na Vunjo kwa kuona jambo hili jema la kufanya motisha kwa walimu. Walimu wanafanya kazi ngumu sana, lakini kazi hii itakuwa rahisi k**a jamii itaelewa kazi hiyo na kuikubali,” amesema Ngereshi.

Amesema kutambuliwa kwa walimu kupitia mpango huo kutawapa nguvu mpya ya kuongeza juhudi katika utekelezaji wa majukumu yao, jambo litakalosaidia kuongeza ufaulu wa wanafunzi na kujenga kizazi chenye maarifa.

Kwa mujibu wa Ngereshi, thamani ya mwalimu inapoongezeka mbele ya jamii, walimu nao hupata ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi kwa kuwa wanaona mchango wao unatambuliwa.

“Motisha hii si ya walimu peke yake, ni kwa ajili ya jamii. Walimu watafanya kazi kwa bidii zaidi ili waweze kupata matokeo bora zaidi k**a ambavyo wamekuwa wakifanya siku zote,” amesema.

Aidha, CWT imewataka viongozi wa kisiasa kutumia nafasi zao kuendelea kufikisha changamoto zinazowakabili walimu katika maeneo mbalimbali ili Serikali iweze kuzifanyia kazi na kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu.

Kwa mtazamo wa CWT, kumthamini mwalimu si tu kumpongeza mtu anayefundisha darasani, bali ni kuwekeza katika mustakabali wa mtoto, familia na maendeleo ya taifa.

25/07/2026

Waalimu Wataanza Kuhamia Moshi Kuboresha Elimu - Dennis Tarimo

Moshi

Mpango wa kutoa tuzo kwa walimu wanaofanya vizuri umeelezwa kuwa unaweza kuwa kichocheo cha kuvutia walimu wenye uwezo kutoka maeneo mbalimbali nchini kuhamia Moshi, hatua inayolenga kuongeza ubora wa elimu katika wilaya hiyo.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya Moshi DC Samia Teachers Award, mmoja wa maafisa Elimu kata ,Denis Tarimo, amesema kutambuliwa kwa walimu kupitia tuzo hizo kutajenga mazingira ambayo yatawafanya walimu kuona thamani ya kufanya kazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.

Amesema kwa muda mrefu baadhi ya walimu wamekuwa wakiona taaluma hiyo haina motisha ya kutosha kutokana na juhudi zao kutotambulika, hivyo mpango huo unatarajiwa kubadilisha mtazamo huo na kuongeza ari ya walimu kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Kwa mujibu wa Tarimo, baada ya kuanza kwa utaratibu huo, ushindani wa kitaaluma unaweza kuongezeka na kufanya walimu wengi wenye uwezo kutoka maeneo mengine kuvutiwa kuja kufanya kazi Moshi ili kushiriki katika mazingira yanayothamini mchango wao.

“Tunatarajia kupitia tukio hili la kwanza kufanyika walimu wataendelea kuwepo, na kutakuwa na msukumo wa walimu wengi kutoka vijijini au maeneo mengine kuhamia Moshi kwa ajili ya kuboresha maeneo ya elimu katika jamii yetu,” amesema.

Hata hivyo Amepongeza wabunge wa Jimbo la Moshi Vijijini na Vunjo, Moris Makoi na Enock Koola, kwa kuwezesha mpango huo akisema ni mfano wa namna viongozi wanaweza kushirikiana na sekta ya elimu katika kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabili walimu.

Mpango wa Moshi DC Samia Teachers Award unaotarajiwa kufanyika tarehe 25 Julai 2026 katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi unalenga kutambua walimu waliofanya vizuri katika majukumu yao ya ufundishaji.

Kwa mujibu wa waandaaji, lengo la muda mrefu ni kujenga mazingira yatakayofanya Moshi kuwa eneo linalovutia walimu wenye weledi, huku ushindani wa kitaaluma ukiendelea kuchochea maboresho katika sekta ya elimu

21/07/2026

Mabo yalikuwa moto Tamasha na Bonanza la vijana Jimbo Kilimanjaro Mashariki Dayosisi ya Kaskazini KKKT

21/07/2026

Bonanza la vijana Jimbo la Kilimanjaro Mashariki Dayosisi ya Kaskazini KKKT

Address

777
Moshi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Sauti Ya Injili Moshi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Radio Sauti Ya Injili Moshi:

Shortcuts

Share