Efatha Church Kilimanjaro

Efatha Church Kilimanjaro Welcome to the OFFICIAL facebook account of EFATHA Church Kilimanjaro | Healing & Deliverance by the blood of JESUS.

.

MAMBO YA KUZINGATIA ILI UINGIE KATIKA UFALME1. Kuzaa Matunda; katika kuzaa sio watoto tu, bali mashamba, majumba, kampun...
04/06/2026

MAMBO YA KUZINGATIA ILI UINGIE KATIKA UFALME

1. Kuzaa Matunda; katika kuzaa sio watoto tu, bali mashamba, majumba, kampuni na kadhalika.. Ruhusu akili yako itafute uzao, lazima uwe na uzao usitembee vilevile Januari mpaka December. Kanisa k**a haliongezeki kwa kuleta watu kwa Yesu haliwezi kuwa na furaha ya kweli kwani katika kuzaa ipo furaha.

2 .Kuongzeka, Mungu anapoanza kuona unaongezeka anakuona wewe k**a yeye hivyo anaruhisu mazingira yake, nguvu na uwezo viwe vya kwako. Usikubali kuwa na kitu kimoja bali sababisha kingine kizaliwe kupitia hicho kimoja kwani unapoongezeka ufalme unaona umeelewa unapokwenda.

3. Kujaza
Hakikisha Kila unachokifanya kinajaa, kila kitu unachofanya hakikisha kinajaa yaani unakikamilisha k**a ni biashara, kazi unafanya kwa uaminifu na ukamilifu wake.

4. Kutiisha; kutiisha kwa sababu yupo anayetishia, maandiko yanasema shetani ni k**a Simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, k**a hutokua na bidii ya kutiisha utakuwa unatishiwa tu na ibilisi, kazi za shetani ni kuua na kuharibu.

Watu wanapotishiwa wakatishika mambo yao yanaharibika lakini sasa lazima ubadilike kwa sababu iko mamlaka juu yetu tutiishe nguvu za ibilisi.

02_Tarehe 04_06_2026

: Mchungaji Baraka Lyimo
: UFALME_KWANZA

04/06/2026
  02_Tarehe 04_06_2026📍Kanisa_La_Efatha_Sayuni_Moshi_KDC📍Mhubiri: Mchungaji Baraka Lyimo🔥SOMO: UFALME_KWANZAUFALMEK**a u...
04/06/2026

02_Tarehe 04_06_2026
📍Kanisa_La_Efatha_Sayuni_Moshi_KDC
📍Mhubiri: Mchungaji Baraka Lyimo
🔥SOMO: UFALME_KWANZA

UFALME
K**a umeokoka ufalme uko ndani yako, lakini hauwezi kuonekana mpaka kuna kitu kwanza kimetokea kwa kuweka bidii kwenye huo ufalme.

Ukipata ufalme utaanza kuona mabadiliko kwanza ndani yako kwanza na ndipo utaanza kudhihirika nje.
Ufalme ukiwa ndani yako utaheshimika.

Mithali 8:17"17]Nawapenda wale wanipendao,
Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.

Unatakiwa uweke BIDII katika kusikia sauti ya Mungu, pia tamani kusikia na kuona kile amesema Mungu kinatimia kwako. Kusikia ni kufanya kazi lile ulilolisikia kwa bidii hadi kuona matokeo ya kile ulichosikia kinatokea.

Kutunza kile ulichosikia, hapa ndipo unapoiona ile nguvu ya Mungu iliyoko ndani yako inatembea na wewe. Na popote unapokanyaga unakuwa na yeye, ufalme unakuwa ndani yako, wale wanaokuwa kinyume chako ile nguvu ndani yako inapambana nao.

Kufanya kile ulichosikia. Mwanzo 4:7"7]K**a ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde."

Ukiwekwa bidii katika kutenda vyema unapata kibali. wapo wanaofanya kazi ya Mungu hovyo hovyo ndio maana wanakosa kibali. Lakini unapofanya vema unapata kibali cha kustawi katika kila eneo la maisha yako.

K**a kuna jambo la Mungu hakikisha akili yako iko pale, nguvu zako ziko pale na moyo wako uko pale na chochote unachokifanya katika moyo lazima Mungu aonekane.

Hakikisha unafanya kazi ya Mungu kwa nguvu zako kwa sababu amelaaniwa nayemtumikia Bwana kwa ulegevu. Lazima tufanye tofauti ili kupata kibali. Kibali kinaudhihirisha ufalme ulioko ndani yako.

04/06/2026


Day 02_ june04_2026
04/06/2026

Day 02_ june04_2026

  🔥 Don't Plan to miss it !! 💯
03/06/2026



🔥 Don't Plan to miss it !! 💯

TUNAPATAJE UFALME ?!Ni pale tunapobadilisha mtazamo kuhusu mazingira yetu.Mfano wa yule mwanamke aliyetokwa na damu miak...
03/06/2026

TUNAPATAJE UFALME ?!

Ni pale tunapobadilisha mtazamo kuhusu mazingira yetu.
Mfano wa yule mwanamke aliyetokwa na damu miaka12 alibadilisha mtazamo wake, akadhamiria kupata uponyaji wake alipoweka bidii na kugusa pindo la Yesu.

Tarajia kupokea kile ulichodhamiria katika semina hii kwa kubadili mtazamo wa kile kilicho ndani yako iwe ni magonjwa, kazi, elimu, biashara, ndoa itakua unavyotaka wewe.

Daudi aliangalia anataka kufanya nini na Mungu anamwambia nini, akamshinda Goliati, ili ushinde lazima uhame mahali pa kuogopa changamoto.

Mtu anayetaka kuona ufalme wa Mungu, lazima akubali kuifia imani yake , kile unachokiogopa ndio kitakachokuua , kile unachokikabili ndicho unachoshinda.

Ufalme wa Mungu unapatikana kwa yule aliyeokoka, na ili aupate lazima awe na bidii, IMANI na asiogope changamoto. Wakati wanafikiri unaanguka kumbe unazidi kuinuka viwango vya juu zaidi.



Baraka Lyimo

  YA KWANZA_Tarehe 3_6_2026📍SEMINA YA UFALME KWANZA📍MHUBIRI: MCHUNGAJI BARAKA  LYIMOKila mtu ana kitu ambacho anakihitaj...
03/06/2026

YA KWANZA_Tarehe 3_6_2026

📍SEMINA YA UFALME KWANZA📍

MHUBIRI: MCHUNGAJI BARAKA LYIMO

Kila mtu ana kitu ambacho anakihitaji ndani ya ufalme, lakini ili akipate ni lazima awe kwenye huo ufalme.

Mathayo 6:33 "33]Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa."

Mbingu zinapoona unafanya zaidi katika Ufalme, zinaachilia ufalme kwako.

Mithali 8:27"27]Alipozithibitisha mbingu nalikuwako; Slipopiga duara katika uso wa bahari; "

Ukiokoka ufalme unakua ndani yako. Kwanini uutafute? ni kwasababu kuna kitu cha kujifunza ambacho kinahitaji bidii yako. Wale ambao wamedhamiria jambo litokee, bidii yao inadhihirisha huo ufalme.

BIDII ilimfanya Elisha kupata anachokitaka, ukiwa na bidii utaona yale yaliyo ndani yako. Chochote unachokihitaji kiko ndani ya ufalme, hivyo ulikuona ufalme lazima uwe na bidii katika mambo ya ufalme na hapo utaanza kuishi maisha ya tofauti.

Address

Efatha Church Kilimanjaro
Moshi
1058

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Kilimanjaro posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share