04/06/2026
MAMBO YA KUZINGATIA ILI UINGIE KATIKA UFALME
1. Kuzaa Matunda; katika kuzaa sio watoto tu, bali mashamba, majumba, kampuni na kadhalika.. Ruhusu akili yako itafute uzao, lazima uwe na uzao usitembee vilevile Januari mpaka December. Kanisa k**a haliongezeki kwa kuleta watu kwa Yesu haliwezi kuwa na furaha ya kweli kwani katika kuzaa ipo furaha.
2 .Kuongzeka, Mungu anapoanza kuona unaongezeka anakuona wewe k**a yeye hivyo anaruhisu mazingira yake, nguvu na uwezo viwe vya kwako. Usikubali kuwa na kitu kimoja bali sababisha kingine kizaliwe kupitia hicho kimoja kwani unapoongezeka ufalme unaona umeelewa unapokwenda.
3. Kujaza
Hakikisha Kila unachokifanya kinajaa, kila kitu unachofanya hakikisha kinajaa yaani unakikamilisha k**a ni biashara, kazi unafanya kwa uaminifu na ukamilifu wake.
4. Kutiisha; kutiisha kwa sababu yupo anayetishia, maandiko yanasema shetani ni k**a Simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, k**a hutokua na bidii ya kutiisha utakuwa unatishiwa tu na ibilisi, kazi za shetani ni kuua na kuharibu.
Watu wanapotishiwa wakatishika mambo yao yanaharibika lakini sasa lazima ubadilike kwa sababu iko mamlaka juu yetu tutiishe nguvu za ibilisi.
02_Tarehe 04_06_2026
: Mchungaji Baraka Lyimo
: UFALME_KWANZA