13/08/2026
DAY 04 -HUKUMU YA HAMAN
Esta 6:1 “Usiku ule mfalme hakupata usingizi; akaamuru aletewe kitabu cha maandiko ya taarifa, nayo yakasomwa mbele ya mfalme.”
Mordekai alifanya kazi ya kumlinda Mfalme kutoka kwa Bigthana na Tereshi lakini hakupata heshima anayostahili kwa muda mrefu, hii inalandana na maisha ya kawaida kuwa mtu anaweza kufunga kitabu chako na usipate yale ambayo unastahili.
Kuna roho zimeapa kuwa kitabu chako kisifunguke kwenye maisha yako na kuna namna ambayo Shetani anaweza kubadilisha kurasa za kitabu chako mfano kwenye kitabu cha biashara anaweza akakuwekea kwenye kurasa zako madeni, hasara n.k. na hii hupelekea unakuwa kwenye sehemu moja bila mafanikio. Lakini Mordekai hakusimama bila maombi aliomba na Mungu alimuheshimisha upya.
Maombi machache ya kusimama nayo siku ya leo
- Kufungua kitabu chako kilichofungwa na Roho za Haman miaka na miaka kiende kufunguka leo
- Kila heshima yako iliposhushwa ikarejee kwenye maisha yako (Modekai alichukuliwa kwa hali ya kawaida kutokana na kazi alikuwa anaifanya lakini baada ya kitabu chake kufunguka heshima ilirudi )
NI MAOMBI YANGU KWAKO KUWA KILA KITABU CHAKO KILICHOFUNGWA( NDOA, HABARI NJEMA, FURAHA, AMANI, HESHIMA, BIASHARA) KIKAFUNGUKE NA KILA KURASA MBAYA ZILIZOWEKWA NA SHETANI ZIKACHANIKE KWA JINA LA YESU
MAOMBI YA MCHANA BADO YANAENDELEA NSSF GHOROFA LA NNE KUANZIA SAA SITA NA NUSU MCHANA MPAKA SAA NANE KAMILI MCHANA (12:30pm-2;00pm).
Prophet Shepherd Bushiri
Prophetess Mary Bushiri
ECG The Jesus Nation Church Tanzania
Mtalemwa Dionis Rweyemamu
Boneka Adolph Boneka