06/06/2018
NI SABATO KWA AJILI MWANADAMU AU MWANADAMU KWA AJILI YA SABATO?
Bwana Yesu apewe sifa na utukufu wote,
Moja ya swali ambalo watu wengi wamekuwa wakiuliza ni juu ya siku ya sabato. Kuna maandiko mengi ambayo Biblia imeyatoa juu ya “siku ya sabato.” Hatuwezi kupitia maandiko yote ila tutapitia machache.
Naamini yatakusaidia kuelewa zaidi. Binafsi watu wengi wamekuwa wakiuliza “siku sahihi ya kuabudu” ni ipi? Kwanza kuabudu hakuko katika siku. Wanaoabudu halisi ni wale wanaomuabudu Mungu katika Roho na kweli (Yohana 4:24).
K**a mtu hana Roho Mtakatifu na kweli ya Mungu haimo ndani yake, haijalishi anaenda kusali siku ipi, hawezi kumwabudu Mungu “katika Roho na kweli.” Kuwa na “kweli ya Mungu” siyo mtu kuwa na maandiko.
Mtu haingii katika ufalme wa Mungu kutokana na siku anayoenda kuabudu. Mtu anaingia katika ufalme wa Mungu kwa sababu amezaliwa mara ya pili, amezaliwa katika maji, na katika Roho (Yohana 3:3,5).
Hivyo k**a mtu hajazaliwa mara ya pili, hana neno wala Roho Mtakatifu, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu haijalishi anaenda kusali wapi na anasali siku ipi.
Turudi kwenye “Siku ya Sabato:”
Nataka tuangalie sabato k**a “sehemu ya agano.” “BWANA akasema na Musa, na kumwambia, Kisha nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi” (Kutoka 31:12—13).
Mungu anaendelea kumpa Musa maagizo na kumwambia atakayeinajisi Sabato hakika atauawa (Kutoka 31:14—15). “Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato, kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele” (Kutoka 31:16).
Maandiko haya yanatuambia kuwa kuiangalia Sabato “ni agano la milele.” Kumbuka agano ni makubaliano kati ya pande mbili au zaidi.
SWALI: Mungu anasema kuishika Sabato na kuiangalia “ni agano la milele.” JE NI AGANO LA MILELE KATI YA MUNGU NA NANI? Kati ya “Mungu na Israeli” au “Mungu na kanisa?” Kumbuka Mungu hakufunga agano lolote na kanisa.
Neno linasema, “Angalia, siku zinakuja, asema BWANA, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema BWANA” (Yeremia 31:31—32).
Nilitaka uone kuwa “agano jipya” Mungu alilifanya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
Hivyo kushika Sabato k**a “agano la milele” Mungu aliwaambia wana Israeli, siyo kanisa. Katika Agano la Kale kulikuwa hakuna kanisa. Kanisa limeanza Yesu alipofufuka. Kwa sababu hiyo, sabato yetu k**a kanisa “ipo kwa Yesu, siyo katika siku.”
Yesu alisema, “Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato” (Mathayo 12:8).
Maneno haya Yesu aliyasema baada ya Mafarisayo kuona wanafunzi wa Yesu walipokuwa wanavunja masuke na kuyala na kumwambia Yesu kuwa wanafunzi wake wanafanya lisilo halali “siku ya Sabato.”
Kwa Mafarisayo na watu wengine wa dini, k**a ilivyo sasa, Sabato ipo katika siku, siyo kwa Yesu. Lakini Sabato yetu ni katika Kristo kwani kila kitu (pamoja na Sabato) kiliumbwa kwa ajili ya Kristo (Wakolosai 1:16; Yohana 1:3).
Yesu, ambaye ni Mwana wa Mungu, aliyatenda mapenzi ya Mungu siku zote (hata siku ya Sabato) kwani Yeye ndiye “Bwana wa Sabato.”
“Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato. Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi” (Yohana 5:17).
Kitu cha msingi ambacho watu wanasahau ni kwamba hatukuumbwa kwa ajili ya Sabato bali Sabato iliumbwa kwa ajili yetu. Kuna watu wanaishi kana kwamba waliumbwa kwa ajili ya Sabato.
Yesu alipokuwa anajadiliana na watu wa dini juu ya Sabato, neno linasema, “Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya Sabato” (Marko 2:27).
Kuna watu ambao wameshika Sabato na wanajaribu kuishi chini ya sheria ya Musa lakini imani yao kwa Yesu haipo.
Kumbuka kuwa hakuna wokovu katika torati ya Musa. Hatuhesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali ni kwa imani katika Kristo. Torati ni inakusaidia “kutambua dhambi” (Wagalatia 2:16; Warumi 3:20).
Hivyo sababu ya wana wa Israeli kuishika sabato ni kwamba kwao ni “agano la milele.”
SWALI: Je sisi wa mataifa tunapookoka na kumpokea Kristo k**a Bwana wetu tunatakiwa tuishi kwa kushika sabato na sheria zingine ambazo Mungu alimpa Musa kwa ajili ya wana wa Israeli? Tuangalie maandiko yanasemaje:
“Lakini baadhi ya madhehebu ya Mafarisayo walioamini wakasimama wakisema, Ni lazima kutahiri na kuwaagiza kuishika torati ya Musa. Mitume na wazee wakakusanyika kulifikiri neno hili” (Matendo 15:5—6).
Nilitaka uone mjadala wa “kuishika torati ya Musa” haujaanza leo. Ulianza tangu kanisa la kwanza na chimbuko lake ni “madhehebu ya Mafarisayo” na siyo Kristo. Hata wakati wa Yesu huo mjadala ulikuwepo (kumbuka hakuna jipya chini ya jua [Mhubiri 1:9]).
Maagizo ambayo wale wamataifa tulipewa ni “kujiepusha na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu” (Matendo 15:20).
Mitume walisema, “Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima, yaani, mjiepeshe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongelewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu” (Matendo 15:28—29).
Hayo ni maagizo ambayo mitume waliyatoa na ilimpendeza Roho Mtakatifu. Kumbuka neno linasema, “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni” (Waefeso 2:20).
Hivyo mambo ambayo ni ya LAZIMA kwetu sisi mataifa tuliomwamini Yesu hayo hapo juu. Maana yake mengine “siyo ya lazima” kwa ajili ya wokovu. Hii ni pamoja na kuishika Sabato kwa jinsi ya mwili na torati ya Musa.
SWALI: Je siku sahihi ya kuabudu ni ipi? Mara nyingi swali hili wanauliza ambao ni “wachanga kiroho” kwa sababu wanadhani Mungu anaabudiwa “katika siku” au “walioshika dini ya Mafarisayo” hivyo wanatafuta kuhesabiwa haki kwa sababu “wanaishika Sabato.”
Kinachotofautisha kwa nini kuna “wanaokusanyika” jumapili au jumamosi ni hiki: Kwa sababu wana wa Israeli walipewa maagizo ya kuishika Sabato k**a “agano la milele,” wao wamekuwa wakikusanyika Jumamosi.
Kwa wa mataifa ambao wamepewa neema ya wokovu na kumjua Kristo, wamekuwa wakikusanyika Jumapili kwa sababu kanisa lilianza baada ya Yesu kufufuka.
Neno linasema, “Ikawa jioni, siku ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwanu; k**a Baba alivyonituma mim, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu” (Yohana 20:19; 21—22).
Siku hii ya kwanza (Jumapili) ndiyo siku ambayo Yesu alifufuka na ndiyo siku aliyowavuvia wanafunzi wake wakapokea Roho Mtakatifu. Kwa sababu hii, wengine wamekuwa wakikusanyika siku ya Jumapili.
Lakini kitu cha msingi kuliko vyote ni kuelewa kwamba kuabudu halisi siyo Jumapili wala Jumamosi. K**a tulivyoona, waabuduo halisi wanaabudu katika Roho na Kweli. Ukiwa na hivi viwili, utaweza kumuabudu Mungu k**a Mungu anavyotaka kuabudiwa. Ukiwa huna hivi, utamuabudu kwa kufuata mapokeo ya dini (ya wanadamu).
Mtu anaweza kuwa anakusanyika na wenzake Jumamosi au Jumapili na mwisho wa siku bado akaenda jehanum. Hivyo ni muhimu kuelewa kuwa uhalisia wa mahusiano yako na Mungu hautegemei siku ipi unayoenda “kusali.”
Unaweza kuishika sabato, unaweza kuacha kula vyakula fulani k**a Mungu alivyoagiza wana wa Israeli lakini fahamu kuwa wokovu wako haupo katika hivyo. Wokovu wako unategemea na imani yako kwa Kristo. Tunaokolewa kwa neema na ni kipawa kinachotoka kwa Mungu (Waefeso 2:8).
Yesu alisema wanaoingia katika ufalme wa mbinguni ni wale wanaoyatenda mapenzi ya Mungu (Mathayo 7:21). K**a huyatendi mapenzi ya Mungu, haijalishi unaishika Sabato au huishiki; haijalishi unasali lini mwisho ni ghadhabu ya Mungu.
Waandishi na Mafarisayo, walijitahidi sana kuishika torati ya Musa na kuishika sabato lakini pia ndio hao Yesu aliwaambia wanawafungia watu kuingia katika ufalme wa Mungu na ndio hao wanawafanya watu kuwa wana wa jehanum mara mbili zaidi yao wenyewe (Mathayo 23:13,15).
Ndio maana ni hatari sana kushika mapokeo ya dini lakini kiukweli moyoni huna pendo la Mungu ndani yako. Mwana—sheria alipomjaribu Yesu kwa kumuuliza amri kuu “katika torati” ni ipi, Biblia inasema:
“Akawaambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako k**a nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii” (Mathayo 22:37—40).
Watu wa dini walipata shida na Yesu kwani waliona anaitangua torati na haishiki sabato. “Basi baadhi ya Mafarisayo wakasema, Mtu huyo hakutoka kwa Mungu, kwa sababu haishiki sabato” (Yohana 9:16a).
Katika kitabu cha matendo ya mitume, tumeona kuwa “madhehebu ya Mafarisayo” ndiyo walikuwa wanasema watu wanatakiwa kuishika torati ya Musa. Hivyo kwa wao, waliona k**a Yesu “anaivunja torati.”
Hata sasa “madhehebu ya Mafarisayo” yapo na wao wanachoangalia k**a wewe ni wa Mungu au sio ni kuishika sabato na torati ya Musa. Sasa unaweza kuelewa kwa nini watu wengine ukikutana nao swali la kwanza atakuuliza ni hili: “unasali siku gani” au “siku sahihi ya kusali/kuabudu ni ipi?”
Kuna watu wanaamua wewe ni wa Mungu au siyo kutokana na siku unayoenda kusali. Hili dhehebu lilianza na mafarisayo wakati wa Yesu.
Kumbuka Yesu ambaye ndiye Bwana wa Sabato hakuja kuitangua torati wala manabii bali kutimiliza (Mathayo 5:17). Watu wa mataifa wakiamua kuishika torati ya Musa na sabato wanaweza lakini hii haiwafanyi “kuwa wana wa Israeli” na kuwa sehemu ya “agano la milele” ambalo Mungu alimwambia Musa.
Hivyo ndugu mpendwa, hakikisha una nafasi katika ufalme wa Mungu. Tafuta kujua nafasi yako ndani ya Kristo na una nguvu ya “kujiingiza katika ufalme wa Mungu.” “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu” (Luka 16:16).
Mungu haabudiwi Jumamosi au Jumamosi, bali anaabudiwa katika Roho na Kweli. Kuna watu wengi sana wanakusanyika Jumamosi au Jumamosi lakini wanaishi maisha ya dhambi na ndani ya mioyo yao wamejaa uovu. Watu hawa hawamwabudu Mungu.
Kuna mambo ambayo Biblia inasema kanisa lazima liyashike. Hakikisha umeyashika hayo. Ila unaruhusiwa kuishika torati ya Musa aliyopewa kwa ajili ya wana wa Israeli (sheria zote 613). Ila hutahesabiwa haki kwa kuwa chini ya sheria bali tunaishi kwa imani.
Neno linasema, “kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; kwa maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye. Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani. Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo” (Wagalatia 3:10—12).
Ukiendelea neno linasema, “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti” (Wagalatia 3:13). Kwa hiyo anayechagua kuwa chini ya torati na kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria yuko chini ya laana na hawezi “kuishi kwa imani.”
Je! Wewe sabato yako ipo katika siku (Jumamosi) au ipo katika Kristo (Bwana wa Sabato)? Je! Unaishi kwa imani au chini ya matendo ya sheria?
Ubarikiwe,