05/05/2025
MAMBO YAKAYOKUSAIDIA KUWA NA UFANISI KATIKA HUDUMA YA VIJANA.
Ili uwe na Ufanisi katika kuwahudumia vijana inabidi uwe na mambo yafuatayo ;
1. HUDUMA YA VIJANA NI KURITHISHA MAARIFA YA KIMUNGU KIZAZI KIMOJA KWENDA KINGINE.
Mungu amekupa agizo hilii wewe uwaandae watumishi wakubwa wajao. Ukiwa k**a mwl au mchungaji wa vijana, Mungu amekupa neema ya kuwarithisha shuhuda na matendo makuu ya Mungu uliyoyaona katika maisha Yako.
Zaburi 48:12-13
[12]Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji, Ihesabuni minara yake,
[13]Tieni moyoni boma zake, Yafikirini majumba yake, Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja.
Zaburi 71:17-18
[17]Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo.
[18]Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako.
Zaburi 78:4,6
[4]Hayo hatutawaficha wana wao, Huku tukiwaambia kizazi kingine, Sifa za BWANA, na nguvu zake, Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.
[6]Ili kizazi kingine wawe na habari, Ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao.
Mambo ya Walawi 3:17
[17]Neno hili litakuwa amri ya daima, katika vizazi vyenu vyote, ndani ya nyumba zenu zote, ya kwamba hamtakula mafuta wala damu kabisa.
Huduma ya vijana ni Mwendelezo wa kufanya kile ambacho Mungu anafanya kwenye kizazi hiki kiweze kufanyika hata Kwa kizazi kinachokuja. Ipo hasara kubwa sana ya kuacha watoto wasipate kujua matendo makuu ya Mungu aliyoyatenda kwani hii ndyo sababu ya kuinuka kizazi kisicho mjua Mungu kabisa.
Waamuzi 2:7-11
[7]Watu hao wakamtumikia BWANA siku zote za Yoshua, na siku zote za hao wazee walioendelea siku zao baada ya Yoshua, hao waliokuwa wameiona hiyo kazi kubwa ya BWANA yote, aliyokuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli.
[8]Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa BWANA, akafa, naye alipata umri wa miaka mia na kumi.
[9]Nao wakamzika katika mpaka wa urithi wake katika Timnath-heresi, katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu, upande wa kaskazini wa mlima wa Gaashi.
[10]Tena watu wote wa kizazi hicho nao walikusanywa waende kwa baba zao; kikainuka kizazi kingine nyuma yao, ambacho hakikumjua BWANA, wala hawakuijua hiyo kazi ambayo alikuwa ameitenda kwa ajili ya Israeli.
[11]Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya BWANA, nao wakawatumikia Mabaali.
Kizazi kisicho mjua Mungu ni kizazi gani?
🌷Ni kizazi kisicho jua matendo makuu ya Mungu baba na ukuu wake.
🌷Ni kizazi chenye maarifa mengi ya kidunia kuliko ya Ki-Mungu
🌷Ni kizazi chenye ukaidi.
Inafaa sana vijana wadogo wajifunze utumishi. Kwani ipo faida kubwa ya kutumika ukiwa kijana mdogo.
Daudi alimuua Goliati akiwa. Kijana mwenye umri wa miaka 15 na 17, Yusufu aliota ndoto kubwa akiwa kijana wa miaka 17, yohana aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu alianza kimfuata Yesu akiwa na miaka 16. Pia hata Yesu mwenyewe alianza kukaa barazani na kuhojiana neno la Mungu akiwa na miaka 12.
2. KUWA KIONGOZI AMBAYE NI MFANO WA KUIGWA ( Role Model)
K**a mtumishi uliyeitwa kutumika Kwa vijana, unapaswa kuwa mfano kwako Kwa kuyaishi Yale unayofundisha. Watoto na vijana wote hujifunza hasa Kwa mifano, Kwa hyo wewe utakuwa mtu wa kuigwa k**a utakuwa na tabia Inayoendana na kile unachokisema.
Mara nyingi Yesu alifundisha Kwa kuonyesha mfano halisi ili nao wafanye, Paul anasema nifuateni Mimi k**a ninavyo mfuata kristo.
Maeneo matatu ya chaguzi za maisha ya vijana unapaswa kuwasaidia.
i. Vocational choice ( uchaguzi wa fani au kazi ya kufanya )
Vijana hujiuliza sana nitafanya kazi gani kwenye maisha Yangu? ( who am I going to do with my life ).
K**a mtu uliyeitwa kufundisha vijana unapaswa kuwaongoza vijana wawe na chaguzi zilizo sahihi Kwa kuwasaidia kujua nini Mungu ameweka ndani Yao kufanya wawapo hai.
ii. Life- mate choice ( uchaguzi wa mwenza wa maisha).
Vijana wengi hupata shida sana kujua nani atamuoa au ataolewa naye ( who am I going to marry)
Simama ukiwaelekeza ili wawe kufanya maamuzi yaliyosahihi katika eneo Hilo.
iii. Value selection ( Nini wataamini kwenye maisha Yao yote?)
Hii inahusu ni kitu gani Wana amini na kukishika K**a hukumu ya utu wao wa ndani.
Vijana wengi hukosa mwelekeo thabiti wa kiimani ambapo hufanya Kila mmoja awaze na kuamua kivyake tu. Wengi wao wakiishia kuamini miungu kwenye maisha Yao.
Waelekeze chaguzi iliyosahihi ya kumwamini Yesu kristo katika maisha Yao Kwa kuwaonyesha uzuri wa kuwa na Yesu kwenye maisha Yao pia kuwafundisha juu ya hukumu ya Mungu Kwa watu wote wasio mwamini kristo kwani yeye ndye njia pekee ya kweli na uzima .
3. KUFUNDISHA NENO LA MUNGU( Teaching God's word)
Mathayo 28:19-20
[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
[20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Andiko hili linatupa agizo kuu la kufanya kwetu Kwa MUNGU, kuwafundisha wengine amri za Mungu yaani neno la Mungu k**a sisi alivyotufundisha.
Kwanini tunapaswa kufundisha neno la Mungu Kwa vijana?
I. Huduma ya vijana imejengwa katika fundisho la neno la Mungu. Ambapo itawasaidia Kujenga msingi imara ( solid foundation) Kwa ajili ya maisha Yao.
Msingi imara Kwa vijana unajengwa Kwa neno la Mungu, kijana akijaza neno la Mungu itampa Kushinda majaribu na Hila za adui shetani.
Luka 6:46-49
[46]Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?
[47]Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
[48]Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri.
[49]Lakini yule aliyesikia ila hakutenda, mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ukaishukia kwa nguvu, ikaanguka mara; na maangamizi yake nyumba ile yakawa makubwa.
Mfundishe kijana neno la Mungu ili dhoruba na mafuliko yakija asianguke katika jina la Yesu...
Mambo mhimu ya kujua na kujiandaa k**a mtumishi Kwa vijana.
Katika filosofia ya kigiriki walimu walipaswa kujua mambo haya wanapokuwa wanaenda kufundisha, hatuna budi nasisi kuweza kuyajua haya ili yatusaidie katika kuwajenga vijana katika neno la Mungu.
I. Pathos
Maana yake ni kwamba mwl. Anapaswa na shauku ya ndani ( deeply passion) ya kutaka kufundisha vijana.
Mara nyingi watu hufundisha waooo na vijana sababu tu wanaona hawana kazi na wapo tu huru, unakuta unaenda kufundisha ukiwa k**a umelazishwa bila kuwa na mwito na msukumo wa ndani wa kutaka kuwajenga watoto walijue neno la Mungu.
K**a mwl. Na mtumishi wa MUNGU Kwa watoto na vijana Jenga shauku na Nia dhabiti ya kutaka kufundisha vijana.
ii. Logos
Logos maana yake neno la Mungu, unapaswa kujiandaa vizuri Kwa neno la Mungu, usikurupuke na kwenda kufundisha vijana hakikisha una neno ulilojiandaa kuwafundisha watoto siku hyo.
iii. Ethos
Imani na matendo Yako Kwa kufuata kile unachofundisha. Mwl. Unapaswa kukiishi unachofundisha kijana. Yesu alifundisha mambo ambayo ni maisha yake ya Kila siku.
4. PANGA SHUGHULI ZITAKAZO WASHIRIKISHA WOTE KWA PAMOJA.
Waebrania 10:24
[24]tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri;
Mwl. Au mchungaji wa vijana panga matukio ambayo yatawafanya vijana wote washiriki, hii inaweza kupangwa Kwa kusudi la kujuana na kufahamiana zaidi kwani vijana wakifahamiana ni rahisi kujengana Kwa tabia njemaa. Pia inapunguza Kwa kuwa na makundi au urafiki na. Watu ambao hawana Imani sawa yaani hawajaokoka. Kumbuka vijana wengi huharibika sababu ya kuwa na shughuli za pamoja na vijana ambao hawajaokoka huko nje.
1 Wakorintho 15:33
[33]Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
K**a mazungumzo mabaya yanaharibu tabia njema, pia mazungumzo mazuri yanaweza Jenga tabia nzuri zaidi Kwa vijana.
Shughuli hizi ni pamoja na ;
.Michezo (. Kuimba, dance ) Chakula Drama.
5. WAPE NAFASI YA KUTUMIKA ( opportunities for Christians services)
Baada ya kuwafundisha vijana wape nafasi ya kutumika kanisani, inaweza kuwa kwenye kanisa la watoto au kanisa kubwa k**a kufanya usafi kanisani, kupanga viti na kutoa sadaka pia hata huduma za nje k**a ushuhudiaji na umisheni.
Kusudi la Yesu wakati akiwa duniani ilikuwa ni kuwafundisha wanafunzi ili wawe k**a yeye, ndivyo ilivyo kwetu pia,. Tunafundisha vijana ili wafanye k**a sisi tunavyofanya.
Yesu alifundisha Kwa njia ifuatayo ambayo nasisi yaatupasa kuifuata ili kuwakuza vijana kwenye utumishi.
I. Unafundisha, yeye akisikiliza
ii. Nafanya, yeye Akiwa anaangalia.
iii. Anafanya nikiwa namwangalia, ( hapa akikosea namrekebisha ili afanye Kwa ubora zaidi)
iv. Anafanya na kuniletea taarifa.
6. FANYA KILA JAMBO KWA KIASI.
Fanya kwa kiasi mambo yote k**a vile mafundisho ya biblia, shughuli za nje, kutumika na maombi.
Hii ni Kwa sababu vijana Wana kikomo Cha umakini ambao wanaweza kuwa nao wakati wa kujifunza biblia, kuomba, na kutumika. Kwa hiyo Fanya Kwa kiasi tu ili wawe na shauku ya kukusimiliza kesho Tena. Ukifundisha Kwa muda mrefu itafika wakati hawata kuelewa unachofundisha.
SOMA ZAIDI KITABU
EFFECTIVE YOUTH MINISTRY
.
.