Apostle Allen Kipangula Teachings

Apostle Allen Kipangula Teachings HUU NI UKURASA UNAOTUMIWA NA MTUMISHI WA MUNGU APOSTLE ALLEN KIPANGULA KUFUNDISHA NENO
0756057068

[SEHEMU YA NNE] NAMNA YA KUMSHUGHULIKIA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYEANDIKO LA MSINGI.1 Petro 5:8-9[8]Mwe na kiasi na ku...
07/03/2026

[SEHEMU YA NNE] NAMNA YA KUMSHUGHULIKIA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYE

ANDIKO LA MSINGI.

1 Petro 5:8-9
[8]Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.
[9]Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

Kuna ufanano mkubwa kati ya Shetani na simba kiutendaji.

Kulingana na picha iliyotumiwa katika 1 Petro 5:8–9. Mtume Petro hakusema Shetani ni simba halisi, bali “k**a simba angurumaye”, akitumia mfano kueleza tabia na namna anavyofanya kazi.

Tutazame kwa pamoja namna simba anavyofanya kazi.

4. Simba hulenga kula / kumeza mawindo

Lengo la simba kukaa karibu na kundi la swala, pundamilia, nyumbu au nyati SIO KUOMBA MSAMAHA WALA KUJENGA URAFIKI NAO bali ana nia ya DHATI YA KURARUA na KULA MAWINDO.

Kuna wakati simba anaweza kumk**ata mnyama mdogo na akaanza kumchezea bila kumla hii haina maana ameokoka ni mtego anataka mama wa yule mnyama mdogo ajitokeze na mwisho awale wote.

Ndivyo pia Shetani anavyotafuta:
-Atakuvuta kwa raha ya dhambi kabla hajakuharibu jumla.

-Atakuacha uendelee kutenda dhambi huku ukiimba, ukihubiri, na uendelee na maisha mazuri ili usahau madhara ya dhambi mpaka utakapokua umezama sana , umezoea dhambi na huwezi kuziacha hapo ndipo utajua SHETANI SIO BABU YAKO WALA BIBI YAKO

-Unapopewa rushwa, kufurahia raha ya ngono na mambo ya namna hiyo usije kusahau ukweli huu lengo la shetani lipo pale pale ANAMTAFUTA MTU AMMEZE!

Baada ya muda utagundua
-Ameharibu imani yako.

-Amekuangusha kiroho.

-Amekutenga na Mungu wako.
-Amekuharibia maisha yako jumla!

Yohana 10:10
[10]Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.

-Delila alikua anambembeleza Samsoni ili ampe siri ya nguvu zake, alipodanganywa na kutoa siri alik**atwa, akatobolewa macho, akapewa kazi ngumu ya kusaga ngano na mwisho akafa.

Mwisho wa dhambi sio raha,ni MAUTI.
Yakobo 1:14-15
[14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
[15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa MAUTI.

SHETANI SIO BIBI YAKO WALA BABU YAKO NI ADUI YAKO UKICHEZA NAYE UTALIA WEWE!

Sehemu ya 5 inakuja......

Apostle Allen Kipangula
0756 057 068
ABC GLOBAL MOSHI

[SEHEMU YA TATU] NAMNA YA KUMSHUGHULIKA NA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYEANDIKO LA MSINGI.1 Petro 5:8-9[8]Mwe na kiasi na...
07/03/2026

[SEHEMU YA TATU] NAMNA YA KUMSHUGHULIKA NA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYE

ANDIKO LA MSINGI.

1 Petro 5:8-9
[8]Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.
[9]Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

Kuna ufanano mkubwa kati ya Shetani na simba kiutendaji.

Kulingana na picha iliyotumiwa katika 1 Petro 5:8–9. Mtume Petro hakusema Shetani ni simba halisi, bali “k**a simba angurumaye”, akitumia mfano kueleza tabia na namna anavyofanya kazi.

Tutazame kwa pamoja namna simba anavyofanya kazi.

3. Simba hushambulia kwa ghafla.
-Shetani muda wote hutafuta muda utakaolala na kujisahau.

Anasubiri muda utakaokua;
-Umeacha kuomba
-Umeacha kufunga
-Umeacha kukesha
-Umeacha kusoma Neno.
-Umeanza kupuuza umuhimu wa ibada na kuhisi upo salama nje ya kanuni za Mungu, hapo ndipo hushambulia kwa ghafla.

Mathayo 13:24-25
[24]Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
[25]lakini watu WALIPOLALA, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
1 Wathesalonike 5:3
[3]Wakati wasemapo, KUNA AMANI na SALAMA, NDIPO UHARIBIFU UWAJIAPO KWA GHAFULA, k**a vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala HAKIKA HAWATAOKOLEWA.

Simba anaweza kujificha kisha kushambulia kwa haraka bila mawindo kutarajia.

Shetani pia mara nyingi hujaribu kwa ghafla kupitia:

-majaribu
Mwanzo 39:11-12
[11]Ikawa, siku moja, akaingia nyumbani atende kazi yake, wala hapakuwa na mtu katika watu wa nyumbani humo ndani;
[12]huyo mwanamke akamshika nguo zake, akisema, Lala nami. Yusufu akaiacha nguo yake mkononi mwake, akakimbia, akatoka nje.

-mawazo mabaya.

Luka 22:3-4
[3]
Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskariote, naye ni mmoja wa wale Thenashara.
[4]Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao.

-mazingira yasiyotarajiwa.
Shetani atamtumia huyo huyo unayemwita kaka yangu au dada angu katika Bwana kukuangusha usipokua makini. -Jifunze kumwamini Mungu wanadamu ni vyombo dhaifu (unstable) -Usijiamini kupita kiasi

Sehemu ya nne inakujia.....

Apostle Allen Kipangula
0756 057 068
ABC GLOBAL MOSHI

[SEHEMU YA PILI] NAMNA YA KUMSHUGHULIKA NA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYEANDIKO LA MSINGI.1 Petro 5:8-9[8]Mwe na kiasi na...
07/03/2026

[SEHEMU YA PILI] NAMNA YA KUMSHUGHULIKA NA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYE

ANDIKO LA MSINGI.

1 Petro 5:8-9
[8]Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.
[9]Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

Kuna ufanano mkubwa kati ya Shetani na simba kiutendaji.

Kulingana na picha iliyotumiwa katika 1 Petro 5:8–9. Mtume Petro hakusema Shetani ni simba halisi, bali “k**a simba angurumaye”, akitumia mfano kueleza tabia na namna anavyofanya kazi.

Tutazame kwa pamoja namna simba anavyofanya kazi.

2. Simba huzunguka akitafuta mawindo dhaifu

●Simba mara nyingi huchagua mnyama aliyedhoofika, aliyejitenga, au asiye makini.

Ndivyo pia Shetani:

-hutafuta mtu asiyekesha kiroho, aliye mbali na ushirika wa waamini wengine, au mwenye imani dhaifu.
👉Ndiyo maana andiko linasema: “mwe na kiasi na kukesha.”
-Kuwa makini na mlango wowote wa dhambi kumbuka mazungumzo mabaya huharibu tabia njema (1kor15:33) na taa ya mwili ni jicho likitiwa giza kwa kutazama vitu vichafu maisha yako yote yatapoteza mwelekeo.

👉Usijitenge na ibada au makusanyiko ya wana wa Mungu kufanya hivyo ni kujihatarisha na kumpa shetani nafasi ya kukushambulia.

Maandiko yanasema:
-Waefeso 4:27
[27]wala msimpe Ibilisi nafasi.

-Waebrania 10:25
[25]wala tusiache kukusanyika pamoja, k**a ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

-Waebrania 3:12-13
[12]Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai.
[13]Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.

USIKOSE IBADA KWA SABABU YOYOTE ILE.

"Huwezi kuacha kupumua kwa kiteteo cha kuchoka—utakufa"

Sehemu ya tatu inakujia....

Apostle Allen Kipangula
0756 057 068
ABC GLOBAL MOSHI

[SEHEMU YA KWANZA] NAMNA YA KUMSHUGHULIKA NA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYEANDIKO LA MSINGI.1 Petro 5:8-9[8]Mwe na kiasi ...
07/03/2026

[SEHEMU YA KWANZA] NAMNA YA KUMSHUGHULIKA NA SHETANI K**A SIMBA ANGURUMAYE

ANDIKO LA MSINGI.

1 Petro 5:8-9
[8]Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.
[9]Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

Kuna ufanano mkubwa kati ya Shetani na simba kiutendaji.

Kulingana na picha iliyotumiwa katika 1 Petro 5:8–9. Mtume Petro hakusema Shetani ni simba halisi, bali “k**a simba angurumaye”, akitumia mfano kueleza tabia na namna anavyofanya kazi.

Tutazame kwa pamoja namna simba anavyofanya kazi.

1. Simba hunguruma kuogopesha mawindo yake

●Simba hutumia kunguruma ili kutisha na kuvunja moyo wa mawindo yake kabla hajayashambulia.
● Hofu inamfanya anayewindwa akose uelekeo asielewe cha kufanya maana hajui adui yuko wapi au hata akijua aogope.

👉Vivyo hivyo, Shetani hutumia hofu, vitisho, na mawazo mabaya ili kumfanya mtu awe dhaifu kiroho.
👉Anajaribu kumfanya mtu aogope, akate tamaa, au aache imani.

👉Mtu akishashambulia na hofu anapoteza imani kwa Mungu na Neno lake.
👉Anaanza kutafuta mbinu za kimwili za kumsaidia na hapo ndipo anapopoteza pambano kwa kuingia uwanda ambao shetani yuko vizuri zaidi.

UKWELI WA KUKUSAIDIA.

Ukiona simba ananguruma ujue yafuatayo.
1. Simba hunguruma pale anapohisi kutishiwa au kuogofywa na kitu.

2. Simba hutumia mngurumo pale anapohisi adui yake ni mkubwa au ana uwezo kumzidi.

3. Simba hutumia mngurumo pale ambapo hajui mawindo yako wapi anataka hofu iyatoe mawindo mahali pake pa maficho na salama ili ayaone na kushambulia.

4. Simba hutumia mungurumo k**a njia ya kuonyesha nguvu zake ili yamkini amtishe hata mnyama aliye na nguvu kuliko yeye.

5. Mngurumo wa simba hauui kinachopelekea kuua ni kitendo ambacho mnyama anayewindwa atafanya k**a mwitikio wa hofu.

UNAPOHISI KUOGOPA AU KUTISHWA NA ADUI KWA NAMNA YOYOTE FANYA YAFUATAYO:

1. Mpinge kwa kutumia Damu ya Yesu na Neno la ushuhuda.
-Muonyeshe ulishatakaswa kwa damu ya Yesu,ulishaokolewa kutoka nguvu za giza, uko huru na hakuna cha kukudhuru.
-Achilia maandiko kinyume chake , Neno la Mungu ndio makombora rohoni dhidi ya adui .
-Kufyatua kombora tumia Neno imeandikwa na liachilie hilo andiko !
Mathayo 4:10-11
[10]Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
[11]Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.

Ufunuo wa Yohana 12:11
[11]Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

Zaburi 107:1-2
[1]Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema,
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
[2]Na waseme hivi waliokombolewa na BWANA,
Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi.

2. Mkabili na kumkemea kwa mamlaka ya jina la Yesu.
-Our enemy is powerless against the authority of the name of Jesus.
Luka 4:41
[41]Pepo nao waliwatoka watu wengi, wakipiga kelele na kusema, Wewe u Mwana wa Mungu. Akawakemea, asiwaache kunena, kwa sababu walimjua kuwa ndiye Kristo.

Wafilipi 2:9-11
[9]Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
[10]ili kwa jina la Yesu KILA GOTI LIPIGWE, la VITU vya MBINGUNI, na VYA DUNIANI, na VYA CHINI YA NCHI;
[11]na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.

Yakobo 4:7
[7]Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Sehemu ya pili inakuja...

Apostle Allen Kipangula
0756 057 068
ABC GLOBAL MOSHI

[SEHEMU YA KWANZA]UTAJIRI WA KWELITRUE RICHESMAANDIKO YA MSINGILuka 16:11[11]Basi, k**a ninyi hamkuwa waaminifu katika m...
26/02/2026

[SEHEMU YA KWANZA]UTAJIRI WA KWELI

TRUE RICHES
MAANDIKO YA MSINGI

Luka 16:11
[11]Basi, k**a ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli?
If therefore ye have not been faithful in the unrighteous mammon, who will commit to your trust the TRUE RICHES?

Ufunuo wa Yohana 3:17-18
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

Katika dunia hii yenye ushindani wa utajiri wa vitu ambapo watu wameshindana kumiliki nyumba magari na ndege na sasa wanakimbizana kumiliki watu, ni rahisi sana kupoteza uelekeo na ukajikita kufukuzia kinachodaiwa ni utajiri na ukasahau kwa habari ya utajiri wa kweli.

Ukisoma Neno la Mungu na kulitafakari kwa kina utagundua kuwa ;

1.Utajiri wa kweli si fedha, dhahabu au mali mtu anazoweza kuwa nazo ingawa utajiri wa kweli huvuta hivyo vitu pia.

2. Mtu anaweza kuwa na mali zinazothaminiwa katika dunia hii na bado akawa maskini.

3. Utajiri wa vitu (mali) mara nyingi hutumika kufunika umaskini halisi ambao mtu anao , umaskini ambao huambatana na unyonge, mashaka, hofu, upofu na uchi (kukosa utukufu wa Mungu).
ambaye hajaoga anaweza kuuficha uchafu wake kwa kujipaka mafuta na kuvaa nguo nzuri lakini haitachukua muda kwa harufu mbaya kumuumbua kuwa ni mchafu ndivyo kwa mtu aliyemaskini anayejisitiri kwa vitu.

Utajiri wa kweli ni nini ?

Utajiri wa kweli ni mvuto wa kimungu (thamani) anaoweka juu ya mtu unaowalazimisha watu wamtendee mema na kumhudumia kwa mali zao.

Isaya 43:4
[4]Kwa kuwa ulikuwa wa THAMANI machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.

Tuangalie mifano angalau miwili.

a)Mfano wa mfalme Suleiman.

Mungu alimtokea kwenye ndoto na akamwambia AMEMPA utajiri(sio atampa) na hii ilikua baada ya Suleman kuomba apewe hekima.

1 Wafalme 3:11-13
[11]Mungu akamwambia, Kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala hukutaka roho za adui zako; bali umejitakia akili za kujua kuhukumu;
And God said unto him, Because thou hast asked this thing, and hast not asked for thyself long life; neither hast asked riches for thyself, nor hast asked the life of thine enemies; but hast asked for thyself understanding to discern judgment;
[12]basi, tazama, nimefanya k**a ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu k**a wewe, wala baada yako hatainuka mtu k**a wewe.
Behold, I have done according to thy words: lo, I have given thee a wise and an understanding heart; so that there was none like thee before thee, neither after thee shall any arise like unto thee.
[13]Na mambo yale usiyoyaomba NIMEKUPA, MALI na fahari, hata hapatakuwa na mtu katika wafalme k**a wewe, siku zako zote.
And I HAVE ALSO GIVEN THEE that which thou hast not asked, both RICHES, and honour: so that there shall not be any among the kings like unto thee all thy days.

Kwahiyo Sulemani aliamka kutoka kwenye ndoto ni tajiri lakini hakua na mali yoyote mkononi kutoka kwenye ndoto hiyo maana Mungu alisema NIMEKUPA.

Utajiri hapa ulikua ni mvuto wa kiungu ambao Mungu aliweka juu ya Sulemani ili watu wamtendee mema k**a ambavyo tunaona kwenye andiko linalofuata.

1 Wafalme 10:1,3,10
[1]Na malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani juu ya jina la BWANA, ALIKUJA ILI AMJARIBU KWA MASWALI YA FUMBO.
[3]Naye Sulemani akamfumbulia maswali yake yote; wala hakukuwa na neno alilofichiwa mfalme asimwambie.
[10]Basi akampa mfalme TALANTA ZA DHAHABU MIA na ISHIRINI, na manukato mengi, mengi sana, na vito vya thamani; wala haukuja tena wingi wa manukato, k**a hayo malkia wa Sheba aliyompa mfalme Sulemani.

Zingatia yafuatayo;
1. Malkia wa Sheba hakua na tatizo lolote analohitaji kutatuliwa na Suleman alikuja kumjaribu ili kupima uwezo wake k**a ni kweli ana uwezo k**a avyosikia.

2. Chochote ambacho Malkia alimpa Sulemani hakikua ni malipo ya kutatuliwa changamoto ilikua ni zawadi ya kumuonyesha namna anavyomkubali.

Sasa tuachane na zawadi nyingine tupige mahesabu thamani ya dhahabu pekee kwa fedha za kitanzania.

1talanta=26kg
120talanta =3120kg
Ambazo ni sawa na
3120,000grams.

1gram (dhahabu safi) =Tsh419,500/=

Kwahiyo
3120,000gram=Tsh1,308,240,000,000

Tirioni 1.3 za kitanzania mtu kapewa k**a malipo ya Interview ya siku moja hatujapigia mali nyingine ambazo alipewa.

Mara zote mali hutoka mikononi mwa maskini wenye mali na kuwaelekea matajiri wasio nazo lakini wenye utajiri wa kweli.

Mfano wa pili:Mwanampotevu

Mwanampotevu alikua ni maskini anayeishi kwa baba tajiri.

Yeye alijua kwa kuondoka na mali nyingi alizopewa na baba yake tayari amekua tajiri.

Ilichukua muda mchache kuufunua umaskini wake aliokua anauficha kwa mali za baba yake.

Luka 15:13-16
[13]Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
And not many days after the younger son gathered all together, and took his journey into a far country, and there wasted his substance with riotous living.
[14]Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye AKAANZA KUHITAJI.
[15]Akaenda akashik**ana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
[16]Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala HAPANA MTU ALIYEMPA KITU.

MAMBO YA KUZINGATIA.
i)Utajiri wa vitu unaweza kuisha.
ii)Utajiri wa vitu unaweza kuliwa na watu waliokuzunguka.
iii)Utajiri wa Vitu unaweza ukapukutika kutokana na majanga (mf njaa) na ukapotea.
iv)Ni utajiri wa kweli pekee ndio unaweza kustahimili na kudumu nyakati zote.

Mwana mpotevu hakua na utajiri wa kweli (thamani/mvuto wa kiungu) ndio maana mali zilipoisha hakukua na mtu wa kumpa kitu kiasi kwamba hata aliyemwajiri kumlishia nguruwe wake hakumpa chakula.

Hii ni zero mvuto.

Kuna watu sasa ni matajiri wa vitu lakini hawana utajiri wa kweli, wana marafiki wengi kwa sababu ya mali ila zikipotea hizo mali ndio utagundua ni maskini wa kutupwa.

K**a hujajitajirisha kwa Mungu hata k**a ni tajiri wa mali ni suala la muda tu utagundua ni maskini aliyebahatika kuwa na vitu.

Ukiona mtu anasema nilipokua na hela nilikua na marafiki wengi niliwasaidia lakini baada ya kufilisika hakuna hata mmoja anayenikumbuka , ujue huyu mtu alikua maskini tangiapo.

Mfano wa tatu:Yesu alipozaliwa.
Yesu alipozaliwa kwa nje alikua ni maskini lakini ndani tajiri kumbuka utajiri wa kweli sio vitu ni mvuto au thamani ya kiungu juu ya mtu inayoweza kuvuta watu na vitu.

Yesu alikua na utajiri wa kweli!

Utajiri wake uliwafanya mamajusi kutoka mashariki ya mbali kusafiri kwa siku kadhaa ili tu wamwone na kumsujudia.

Walipomfikia hawakumpa "baby diapers" walimletea dhahabu na manukato yaliyomfanya baba yake Yusufu asiwaze kusafiri kwenda Misri kukaa huko na kurudi baada ya Herode kufa.

Mathayo 2:1-2,10-11
[1]Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,
[2]Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
[10]Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.
[11]Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

Tafuta kuutafuta UTAJIRI WA KWELI na utajiri wa mali utakujilia.

Niishie hapa kwa sasa...

Apostle Allen Kipangula
0756 057 068
ABC GLOBAL MOSHI

2. MALEZI YA KIROHO ni NJIA YA MUNGU ya KUWAANDAA WATU NA KUWAFANYA KUWA BORA KWENYE WALICHOITIWA.Matendo ya Mitume 18:2...
09/02/2026

2. MALEZI YA KIROHO ni NJIA YA MUNGU ya KUWAANDAA WATU NA KUWAFANYA KUWA BORA KWENYE WALICHOITIWA.

Matendo ya Mitume 18:24-26
[24]Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko.
[25]Mtu huyo alikuwa AMEFUNDISHWA NJIA YA BWANA; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye ALIJUA UBATIZO wa YOHANA TU.
[26]Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila WALIPOMSIKIA WAKAMCHUKUA KWAO, WAKAMWELEZA NJIA YA BWANA KWA USAHIHI ZAIDI.

Hata k**a unasikia moto unawaka au msukumo wa kuwa mtu fulani kwenye maisha itakugharimu kukaa chini ya malezi kuwa mtu huyo.

Hauwi mtu fulani kwa kuwa umetamani kuwa, unakuwa kwa sababu umetengenezwa kuwa.

HABARI NJEMA KWA WATU WA KILIMANJARO.Mchungaji kiongozi wa kanisa la Assembly of Believers Church Moshi anakukaribisha k...
07/02/2026

HABARI NJEMA KWA WATU WA KILIMANJARO.

Mchungaji kiongozi wa kanisa la Assembly of Believers Church Moshi anakukaribisha kwenye ibada maalumu ya UJAZO WA ROHO MTAKATIFU, UPONYAJI NA KUFUNGULIWA.

YESU ATAWAFUNGUA WOTE:
●WANAOTESWA NA DHAMBI NA WANASHINDWA KUACHA.

●WALIOFUNGWA KWENYE TABIA SUGU K**A ULEVI, UVUTAJI SIGARA/BANGI/MADAWA YA KULEVYA.

●WALIOVUNJIKA MIFUPA ITAUNGWA NA WATATEMBEA.

●WANAOTESWA NA MAGONJWA SUGU K**A KISUKARI, SARATANI, SHINIKIZO LA DAMU N.K

●WANAOTESWA NA MADENI SUGU YASIYOLIPIKA.

TUKUTANE MOSHI, MJOHORONI UKUMBI WA CHAKITO.

SAA 2 KAMILI ASUBUHI.

TUTAKUA NA IBADA MOJA TU.

MJULISHE YEYOTE ALIYEKO MOSHI ASIKOSE NEEMA HII.

Unayekuja nijulishe kwa namba zifuatazo

APOSTLE ALLEN KIPANGULA
0756 057 068 /0711 990 492

MCHUNGAJI KIONGOZI-ABC MOSHI

USHINDI WA ZINAAMimi ni kijana mwenye umri wa miaka 22 sasa nimeteswa na zinaa tangu nikiwa sekondari hadi  chuoni na ha...
04/02/2026

USHINDI WA ZINAA

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 22 sasa nimeteswa na zinaa tangu nikiwa sekondari hadi chuoni na hata baada ya kumaliza chuo hii hali imekuwa ikitawala faham zangu kila wakati hasa nilikuwa nikitaka kufanya maendeleo tu hiyo hali inajitokeza ya kutamani kufanya zinaa hadi kupelekea kupoteza fedha nyingi sana nikiamini kuwa kesho ipo.

Nilijaribu kutafuta msaada kwa wachungaji kazaa wakanifanyia maombi mwingine akaniambia ili hiyo roho initoke ni lazima nitoe sadaka ambayo itanenewa maombi ili isirudi tena nikawa nimetulia baada ya mda nikajikuta nimeanguka tena kwa kasi kuliko hata mwanzo nilifikia hatua ya kulala na mabinti zaidi ya mmoja kwa siku.

Ile hali ilikuwa inaniumiza sana baada tu ya lile tendo maana miaka inazidi kwenda na sijatengeneza chochote ambacho kinaweza kunipa hatua ila siku tarehe 19 mwezi wa kwanz nikaona pengine nimtafute Baba yangu huyu wa kiroho apostle Allen nikamuelezea hali husika akawa ameniombea na kuniambia kwanzia muda huo nimefunguliwa na hiyo roho imenitoka kabisa.

Kiukweli baada ya hapo nilianza kufanya maendeleo, nikajenga banda la biashara lakini pia kabla ya siku ya ujenzi nilipatwa na homa kali sana ilioambatana na maumivu ya kichwa baada kupimwa nikakutwa na malaria.

Nakumbuka nilikuwa sijala toka asubuhi nilijaribu kula vijiko viwili tu vya wali wakati huo nikiwa nimenunua dawa ya malaria sikuitumia nikakumbuka kuna Mungu alienitoa katika zinaa nikamuuliza Baba jinsi naweza kuishi bila kuumwa akanifundisha mda huo huo kwa imani nikapiga magoti na kuomba uponyaji hapo hapo homa ikapona na kichwa kikaacha kabisa kuniuma na dawa nilizonunua hadi leo sijazitumia niligawa na kesho yake nikaendelea na ujenzi maana ningekaa nyumbani basi ela zingekuwa zinatoka tu kwaiyo nisingeweza kuendelea lakini ka ukombozi wa Baba wa mbinguni kupitia mtumishi wake Apostle Allen ambae ni Baba yangu wa kiroho hadi hivi sasa nimekamilisha kujenga kibanda changu kwaajili ya kuuzia nguo na jana nimeagiza cherehani maana banda ni kubwa kwaiyo namtukuza sana Baba wa mbinguni alieniletea mtu atakaesimamia hatima yangu maana mimi ni mtoto wa kwanza na wadogo zangu kusoma pia wananitazamia mimi maana hata Baba yangu mzazi hajali chochote kabisa kuhusu wao ila naamini k**a Mungu amenipitisha katika hili hakika nitashinda.

Ikiwa na wewe unateseka na zinaa nitafute nikusaidie kwa kukukutanisha na Yesu na utafunguliwa.

0756 057 068 (WHATSAPP)
0711 990 492

ABC GLOBAL MOSHI

USHUHUDA WA USHINDI DHIDI YA DHAMBI.Huu ni ushuhuda wa binti ambaye alikuja na changamoto ya zinaa na kutoa mimba nikamw...
04/02/2026

USHUHUDA WA USHINDI DHIDI YA DHAMBI.

Huu ni ushuhuda wa binti ambaye alikuja na changamoto ya zinaa na kutoa mimba nikamwombea na kumpa audio ya somo la TOBA YA KWELI na huu ulikua mrejesho wake.

Pastor nimeisikilizaaa vizur hii audio mpaka mwisho hakikaa nilikuwaa naruka baadhi ya stage kwenye kuomba Toba. Hakika nilikuwaa bint ambaye siyo kwamba mafundisho siyajui na siyo kwamba huduma nilikuwaa sifanyi za kanisan nilikuwaa nafanya ili Hali nazini na kutoa mimba na kanisan sikuwahi kukosa hata mara Moja lakini nimefanya madhambi yote haya nikiwa humo humo kanisan na naabudisha k**a kawaida lakini hii dhambi ya kutoa mimba ilikuwa inanitafuna . Ikafika hatua nikaanza kuona aibu mpaka kuimba praise and worship mbele ya wauminj niliona k**a napoteza muda tuu mbingu sitokaa niione nikiishi haya maisha. But tangu nipate haya mafundisho nimekuwa mtu wa aina tofauti kabisa moyo wangu umekuwa na amani saaana kwa Kila kitu na Nina nguvu kabisa kuomba bila wasiwas, nilikuwaa nawaza naomba Nini wakati na dhambi nilihisi Mungu hawezi jibu maombi yangu . Asante saaana apostle Mungu akubariki na uendelee kunihudumiaa

HII NI HALI YA WENGI MAKANISANI.

-Unatafunwa na dhambi kimya kimya huku kwa nje unajitahidi kutunza mwonekano wako uendelee kuonekana uko sawa.
-Huyu dada yeye alikua anateswa na Dhambi ya zinaa na kutoa mimba lakini bado kila Jumapili bila kukosa anahudumu ibadani.

-Kwako inaweza isiwe dhambi hizo inaweza kuwa kiburi,wivu, kinyongo, uchungu, na mambo yanayofanana na hayo kwa sababu eti ni kiongozi au mhudumu unaogopa kutafuta msaada badala yake unaendelea kuigiza, hii ni mbaya na itakugharimu mbele ya safari.

-Ukiona peke yako umeshindwa kuvuka tafuta msaada , Neno la Mungu liko wazi.

Yakobo 5:16
[16]Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

Mhubiri 4:9-10,12
[9]Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja;
Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
[10]Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
[12]Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.

-Mtu huyu wa kukuvusha ni vizuri akawa kiongozi wako wa kiroho/mchungaji lakini si lazima. K**a una mchungaji aliyekomaa na mwenye kifua ni vizuri zaidi, point ya msingi ni kuvuka sio nani umemshirikisha.

-Kuna watumishi kwenye hili hawajakomaa unamshirikisha ulipokwamia Jumapili kwenye matangazo anakusimamisha anasema mnamwona huyu ameanguka kwenye dhambi kwahiyo kuanzia leo nimemtenga kibaya zaidi hakusaidii chochote kwenye kutoka hapo.

Yote kwa yote ni hatari kuishi na mizigo ya dhambi na ukaendelea kuwahudumia watakatifu wa Mungu ni sawa na kujua kuwa mikono yako ina kinyesi na badala ya kuiosha kwanza unaitumia hiyo hiyo kumlisha mtoto.

Huu ni wito wa toba, Yesu anataka upone.INAWEZEKANA KUPONA.

0711 990 492
0756 057 068 (whatsapp)

Niko hapa kukusaidia.

ABC GLOBAL MOSHI
Apostle Allen Kipangula

MGEUKO MKUU WA MAISHA YANGU.Nikitazama nyuma naona  jinsi maisha yangu yangekua k**a mambo yafuatayo yasingenipata kwa m...
02/02/2026

MGEUKO MKUU WA MAISHA YANGU.

Nikitazama nyuma naona jinsi maisha yangu yangekua k**a mambo yafuatayo yasingenipata kwa mkono wa Mungu lakini kabla ya hapo nikuelezee maisha yangu kwa ufupi:

KUZALIWA KWANGU.
Nilizaliwa k**a mtu ambaye tayari alizaliwa kufa—nilijuaje hili ? Siku moja nikiwa katika hali ya kujiuliza maswali mengi kuhusu kwa nini napitia mambo magumu kwenye maisha yangu Mungu alinionyesha jambo la kushangaza. Alinionyesha kwamba nilizaliwa k**a mtu aliyekwisha kufa na yeye akaniokoa kwahiyo ilikua kana kwamba nimehukumiwa kunyongwa halafu nikatolewa kwa msamaha wa Rais. Nilijivika ujasiri kumuuliza mama nini kilitokea lakini hakuonyesha ushirikiano maana kwetu mtoto kumuuliza mzazi masuala ya uzazi kwa wakati huo ilikua ni k**a jambo la aibu, baadaye nikamwambia hata usiponiambia Mungu ameshanionyesha ikabidi aniambie tu. Kwa namna alivyonieleza nilimuelewa kuwa nilizaliwa nikiwa nimefungwa fungwa na umbilical code kwa wakati huo kulikua na mchezo wa kichawi unafanyika ,ukiwa mjamzito na wachawi wamekuweka kwenye dhabaha yao basi wanamnyongea mtoto tumboni. Lakini Mungu aliniokoa.

MAKUZI YANGU.
Nilikua katika mazingira mabaya, nakumbuka nikiwa na miaka mitano kuelekea sita tayari nilikua nimekutana na masuala ya ushoga , ilikuaje? Ilikua hivi, nilikua na marafiki ambao walikua wanasoma "international school" kumbe kule walikua wanajifunza mambo machafu sana. Siku moja tukiwa tunacheza mchezo wa kombolela (hide and seek game ), mimi ndio nilikua natafuta wao wamejificha katika kutafuta nikawakuta wawili wao wanafanya ushoga, wakati huo ilikua kila jambo jipya au la hatari nilikua najaribu kulifanya lakini mpaka leo sijui ilikuaje jambo hili lilinipita.

SIKU NILIYOONJA UMEME
Ili ufahamu kwamba nilikua mtu wa kujaribu vitu hatari siku moja nilionja umeme kwa ulimi (240v). Ilikuaje ? Kipindi kile tulikua tunawaibia wazazi bulb ndogo💡 zilizokua kwenye baiskeli halafu tunaunganisha na betri zilizotupwa baada ya kutumika sasa ili kujua k**a ni bulb ndio imeungua au betri ndio halina chaji tulikua tunaunganisha waya kwenye betri upande mmoja halafu unaweka ulimi kati ya waya na upande mwingine wa betri. K**a betri lina chaji basi utasikia ladha k**a uchachu fulani hivi.

Siku moja wazo baya likanijia , ikiwa umeme mdogo wa betri ya volt 1.5 ina kuwa na uchachu kiasi hiki je umeme wa majumbani wa 220 volt utakua na uchachu kiasi gani ?

Nikakata waya wa umeme uliokua unatoka kwenye socket ya umeme kwenda kwenye redio halafu nikalamba zile nyaya mbili za umeme nilizokata, sikumbuki k**a nilipata ladha yoyote ila nachokumbuka cha kwanza nilihisi ulimi wangu k**a umebanwa na unavutwa nje ukiwa na mizizi iliyoenda mwili mzima na hasa kwenye moyo. Kwahiyo nilihisi k**a moyo nao unavutwa kwa namna ile ile ulimwi ulivutwa kilichofuatwa sikumbuki ila nilijikuta niko mwisho wa kitanda upande wa pili na kitanda kilikua sita kwa sita nahisi ukuta ulinisaidia kunizuia. Siwezi kusema moja kwa moja k**a nilirushwa kwa nguvu maana kilichotokea hapo kati kati sikumbuki.

Nimewahi kupata ajali mara 3 ambazo moja kwa moja zilikua zichukue uhai wangu nikapona. Mara moja nilitumiwa popo kichawi ili anishambulie aliwaacha watu wote akanifuata mimi tu watu wote wakiwa wanashuhudia (haikua maono) nilipoita jina la Yesu akatoweka mbele ya macho yangu.

Nilishafanya majaribio kadhaa ya kutaka kujiua kwa maji ,Mungu alimtumia mama yangu kuniokoa kila nilipowaza hivyo mama yangu alinizuia kutoka kabisa hata kwenda kucheza na wenzangu bila yeye kujua kwanini alifanya hivyo.

Hayo ni baadhi ya mambo machache niliyoyapitia ambayo k**a usingekua mkono wa Mungu historia yangu leo ingekua tofauti kabisa.

MAMBO AMBAYO YALILETA MGEUKO MKUU KWENYE MAISHA YANGU.

1. KUMPOKEA YESU K**A BWANA NA MWOKOZI WANGU KWA DHATI.

Sitasahau siku hiyo, ulikua ni uzoefu wa namna ya kipekee sana. Allen yule aliyekua mgomvi, mwenye hasira, mcheza ndomboloo, nikawa mpole,mstaarabu k**a ndio nazaliwa.

Nilikua na furaha isiyo kifani maana nilikua nasikia sauti ikiniambia wewe ni mwanangu nitakushika mkono na kukusaidia machozi tu yalikua yakinitoka. Sina hamu ya kuongea, sina hamu ya kucheza na rafiki zangu wale wakorofi nikawa addicted na Biblia. Nilikua natembea na biblia kila mahali yaani kila mahali!

Kaka yangu aliyeniongoza sala ya toba alikua masomoni na sina namna ya kuwasiliana naye mara kwa mara kwahiyo nilikua kana kwamba sina mtu wa kunilea kiimani.

Maombi mengi na kusoma biblia kwingi kukawa ndio kiongozi changu k**a Neno la Mungu lisemavyo.

Zaburi 119:105
[105]Neno lako ni taa ya miguu yangu,
Na mwanga wa njia yangu.

Yeremia 31:9
[9]Watakuja kwa kulia, na kwa maombi nitawaongoza; nitawaendesha penye mito ya maji, katika njia iliyonyoka; katika njia hiyo hawatajikwaa; maana mimi ni baba wa Israeli, na Efraimu ni mzaliwa wa kwanza wangu.

Tangu hapo sijawahi kufurahia maisha ya dhambi wala kutafuta kujitetea kukaa dhambini nimemfuata Bwana kwa moyo wangu wote.

2. KUTAMBUA KUSUDI LA KUUMBWA KWANGU
Hili ni jambo la pili la muhimu kunipata.Nilianza kutambua kile nilichoumbiwa kufanya kwenye mwaka wa 2009 na tangu hapo niliyaweka maisha yangu kumtumikia Mungu kwa asilimia k**a 90 naweza kusema. Ilikua kawaida kwangu kukosa muda wa kusoma kwa sababu ya kujishughulisha sana na masuala ya kiroho na wakati mwingine katika kuzunguka shule jirani na makanisani kuhubiri .

Pamoja na hayo nilifaulu kwa ufaulu wa juu. Katika kusoma kwangu nilijua mapema kuwa si kusoma kwangu ndio kutanipelekea nifanikiwe kwenye maisha, niliona kusoma ni fursa ya kuwafikia watu kwa injili ya Yesu. Wale niliosoma nao na walimu walionifundisha hasa kuanzia sekondari watakua mashahidi wa hili pia maana wengi wao si kwamba ni mashuhuda bali nawalea kiroho hata sasa.

3. KUMPATA BABA YANGU WA KIROHO.
Hili liliniletea nafuu kubwa sana, kumbuka hapo kabla sikupata mtu wa kunilea moja kwa moja kwenye masuala ya kiroho. Kaka yangu wa kuzaliwa Mwalimu Nickson Kipangula ndiye aliyeniongoza sala ya toba na alinisaidia sana kiroho ingawa changamoto ilikua muda wa kuwa naye ulikua mchache kwa sababu naye alikua masomoni tunakutana mara chache wakati wa likizo.

Ila mgeuko ulikuja kutokea Mungu aliponikutanisha na baba yangu wa kiroho Bishop Dickson Cornel Kabigumila huyu alinisaidia sana kujua kuwa masuala ya kiroho si mambo ya kubahatisha au yasiyoeleweka bali kuna KANUNI halisi zinazoongoza matukio ya kiroho na unaweza kuzijua ukitaka.

Akaanza kunihimiza umuhimu wa kusoma vitabu ,kusikiliza audio na video za mafundisho ya Neno la Mungu.

Nikatoka kwenye kubahatisha mambo na kuanza kujua mambo yanavyofanyika. Baba yangu huyu amenifanya kuwa na ujasiri kwenye eneo la uponyaji na kufungua watu. Mfano ukimleta mtu amevunjika mguu mbele yangu si suala tena la kubahatisha kwamba atatembea najua atatembea kwa sababu nimemwona akishughulikia matatizo ya namna hiyo na pia nimejua kanuni nyuma ya uponyaji.

Au ukamleta mtu mwenye addiction yoyote mfano ma********on (kujichua),kutazama picha chafu (pornogragh), ulevi au uvutaji wa aina yoyote sio natumaini Mungu atamfungua nina uhakika. Ilimradi awe anataka kuacha hata k**a amejaribu na ameshindwa kwanini nina ujasiri huo ninajua kanuni nyuma ya miujiza.

Haya nimeyapata k**a matokeo ya malezi. Baba alikua ananitumia watu wenye kesi nzito nzito nikawa nawaza kwanini asiwaombee yeye na maupako yote aliyonayo ananitumia mimi ? Ila nampenda mno baba yangu kwahiyo nikawa natii nawaombea kwa moyo mpaka wanafunguliwa.

Kiukweli zile kesi kwa hiari yangu nisingethubutu kuhangaika nazo lakini kwa sababu baba yangu amezisukumia kwangu sikua na namna ya kuzikwepa kwa kadri nilivyokua nafanya nilikua napata siri nyuma ya changamoto hizo na nikazidi kuwa bora mpaka leo.

Mambo haya niliyoyasema yanaweza kumletea mtu yeyote katika hali yoyote mahali popote mgeuko akiamua kuyafanyia kazi.
Kwa leo niishie hapo.....

K**a una changamoto na ungetamani niombe pamoja na wewe au unataka KUOKOKA nitumie ujumbe whatsapp kwa namba 0756 057 068.

Ukitaka kutuma zawadi ya birthday tumia
0711 990 492 mixx by Yas

ABC GLOBAL MOSHI

Address

Kiboriloni
Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Apostle Allen Kipangula Teachings posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Apostle Allen Kipangula Teachings:

Share