26/02/2026
[SEHEMU YA KWANZA]UTAJIRI WA KWELI
TRUE RICHES
MAANDIKO YA MSINGI
Luka 16:11
[11]Basi, k**a ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli?
If therefore ye have not been faithful in the unrighteous mammon, who will commit to your trust the TRUE RICHES?
Ufunuo wa Yohana 3:17-18
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
Katika dunia hii yenye ushindani wa utajiri wa vitu ambapo watu wameshindana kumiliki nyumba magari na ndege na sasa wanakimbizana kumiliki watu, ni rahisi sana kupoteza uelekeo na ukajikita kufukuzia kinachodaiwa ni utajiri na ukasahau kwa habari ya utajiri wa kweli.
Ukisoma Neno la Mungu na kulitafakari kwa kina utagundua kuwa ;
1.Utajiri wa kweli si fedha, dhahabu au mali mtu anazoweza kuwa nazo ingawa utajiri wa kweli huvuta hivyo vitu pia.
2. Mtu anaweza kuwa na mali zinazothaminiwa katika dunia hii na bado akawa maskini.
3. Utajiri wa vitu (mali) mara nyingi hutumika kufunika umaskini halisi ambao mtu anao , umaskini ambao huambatana na unyonge, mashaka, hofu, upofu na uchi (kukosa utukufu wa Mungu).
ambaye hajaoga anaweza kuuficha uchafu wake kwa kujipaka mafuta na kuvaa nguo nzuri lakini haitachukua muda kwa harufu mbaya kumuumbua kuwa ni mchafu ndivyo kwa mtu aliyemaskini anayejisitiri kwa vitu.
Utajiri wa kweli ni nini ?
Utajiri wa kweli ni mvuto wa kimungu (thamani) anaoweka juu ya mtu unaowalazimisha watu wamtendee mema na kumhudumia kwa mali zao.
Isaya 43:4
[4]Kwa kuwa ulikuwa wa THAMANI machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.
Tuangalie mifano angalau miwili.
a)Mfano wa mfalme Suleiman.
Mungu alimtokea kwenye ndoto na akamwambia AMEMPA utajiri(sio atampa) na hii ilikua baada ya Suleman kuomba apewe hekima.
1 Wafalme 3:11-13
[11]Mungu akamwambia, Kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala hukutaka roho za adui zako; bali umejitakia akili za kujua kuhukumu;
And God said unto him, Because thou hast asked this thing, and hast not asked for thyself long life; neither hast asked riches for thyself, nor hast asked the life of thine enemies; but hast asked for thyself understanding to discern judgment;
[12]basi, tazama, nimefanya k**a ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu k**a wewe, wala baada yako hatainuka mtu k**a wewe.
Behold, I have done according to thy words: lo, I have given thee a wise and an understanding heart; so that there was none like thee before thee, neither after thee shall any arise like unto thee.
[13]Na mambo yale usiyoyaomba NIMEKUPA, MALI na fahari, hata hapatakuwa na mtu katika wafalme k**a wewe, siku zako zote.
And I HAVE ALSO GIVEN THEE that which thou hast not asked, both RICHES, and honour: so that there shall not be any among the kings like unto thee all thy days.
Kwahiyo Sulemani aliamka kutoka kwenye ndoto ni tajiri lakini hakua na mali yoyote mkononi kutoka kwenye ndoto hiyo maana Mungu alisema NIMEKUPA.
Utajiri hapa ulikua ni mvuto wa kiungu ambao Mungu aliweka juu ya Sulemani ili watu wamtendee mema k**a ambavyo tunaona kwenye andiko linalofuata.
1 Wafalme 10:1,3,10
[1]Na malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani juu ya jina la BWANA, ALIKUJA ILI AMJARIBU KWA MASWALI YA FUMBO.
[3]Naye Sulemani akamfumbulia maswali yake yote; wala hakukuwa na neno alilofichiwa mfalme asimwambie.
[10]Basi akampa mfalme TALANTA ZA DHAHABU MIA na ISHIRINI, na manukato mengi, mengi sana, na vito vya thamani; wala haukuja tena wingi wa manukato, k**a hayo malkia wa Sheba aliyompa mfalme Sulemani.
Zingatia yafuatayo;
1. Malkia wa Sheba hakua na tatizo lolote analohitaji kutatuliwa na Suleman alikuja kumjaribu ili kupima uwezo wake k**a ni kweli ana uwezo k**a avyosikia.
2. Chochote ambacho Malkia alimpa Sulemani hakikua ni malipo ya kutatuliwa changamoto ilikua ni zawadi ya kumuonyesha namna anavyomkubali.
Sasa tuachane na zawadi nyingine tupige mahesabu thamani ya dhahabu pekee kwa fedha za kitanzania.
1talanta=26kg
120talanta =3120kg
Ambazo ni sawa na
3120,000grams.
1gram (dhahabu safi) =Tsh419,500/=
Kwahiyo
3120,000gram=Tsh1,308,240,000,000
Tirioni 1.3 za kitanzania mtu kapewa k**a malipo ya Interview ya siku moja hatujapigia mali nyingine ambazo alipewa.
Mara zote mali hutoka mikononi mwa maskini wenye mali na kuwaelekea matajiri wasio nazo lakini wenye utajiri wa kweli.
Mfano wa pili:Mwanampotevu
Mwanampotevu alikua ni maskini anayeishi kwa baba tajiri.
Yeye alijua kwa kuondoka na mali nyingi alizopewa na baba yake tayari amekua tajiri.
Ilichukua muda mchache kuufunua umaskini wake aliokua anauficha kwa mali za baba yake.
Luka 15:13-16
[13]Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
And not many days after the younger son gathered all together, and took his journey into a far country, and there wasted his substance with riotous living.
[14]Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye AKAANZA KUHITAJI.
[15]Akaenda akashik**ana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
[16]Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala HAPANA MTU ALIYEMPA KITU.
MAMBO YA KUZINGATIA.
i)Utajiri wa vitu unaweza kuisha.
ii)Utajiri wa vitu unaweza kuliwa na watu waliokuzunguka.
iii)Utajiri wa Vitu unaweza ukapukutika kutokana na majanga (mf njaa) na ukapotea.
iv)Ni utajiri wa kweli pekee ndio unaweza kustahimili na kudumu nyakati zote.
Mwana mpotevu hakua na utajiri wa kweli (thamani/mvuto wa kiungu) ndio maana mali zilipoisha hakukua na mtu wa kumpa kitu kiasi kwamba hata aliyemwajiri kumlishia nguruwe wake hakumpa chakula.
Hii ni zero mvuto.
Kuna watu sasa ni matajiri wa vitu lakini hawana utajiri wa kweli, wana marafiki wengi kwa sababu ya mali ila zikipotea hizo mali ndio utagundua ni maskini wa kutupwa.
K**a hujajitajirisha kwa Mungu hata k**a ni tajiri wa mali ni suala la muda tu utagundua ni maskini aliyebahatika kuwa na vitu.
Ukiona mtu anasema nilipokua na hela nilikua na marafiki wengi niliwasaidia lakini baada ya kufilisika hakuna hata mmoja anayenikumbuka , ujue huyu mtu alikua maskini tangiapo.
Mfano wa tatu:Yesu alipozaliwa.
Yesu alipozaliwa kwa nje alikua ni maskini lakini ndani tajiri kumbuka utajiri wa kweli sio vitu ni mvuto au thamani ya kiungu juu ya mtu inayoweza kuvuta watu na vitu.
Yesu alikua na utajiri wa kweli!
Utajiri wake uliwafanya mamajusi kutoka mashariki ya mbali kusafiri kwa siku kadhaa ili tu wamwone na kumsujudia.
Walipomfikia hawakumpa "baby diapers" walimletea dhahabu na manukato yaliyomfanya baba yake Yusufu asiwaze kusafiri kwenda Misri kukaa huko na kurudi baada ya Herode kufa.
Mathayo 2:1-2,10-11
[1]Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,
[2]Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.
[10]Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.
[11]Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.
Tafuta kuutafuta UTAJIRI WA KWELI na utajiri wa mali utakujilia.
Niishie hapa kwa sasa...
Apostle Allen Kipangula
0756 057 068
ABC GLOBAL MOSHI