06/03/2024
*KUGEUZWA KUWA MTU MWINGINE*
DAY 19: *MBUZI KUWA KONDOO...*
Mwl Triple J
"...Mataifa Yote Watakusanyika Mbele Zake; Naye Atawabagua K**a Vile MCHUNGAJI Abaguavyo KONDOO na MBUZI; *atawaweka KONDOO Mkono Wake wa KUUME, na MBUZI Mkono Wake wa KUSHOTO."*
(Mathayo 25:32-33)
..Kwa Wachungaji Wanajua Ukitoa Ng'ombe, Basi Kundi *Jingine Kubwa la Wanyama ni KONDOO na MBUZI*
..Kiukweli, Hakuna KAZI Ngumu K**a Kuchunga MBUZI, *Heri Upewe KONDOO 1000 Kuliko Kupewa MBUZI 10!*
*SIFA 5 ZA MBUZI...*
-Hawasikii
-Wasumbufu
-Hawatulii Sehemu Moja
-Hawafati Maelekezo
-Walafi Sana
*SIFA KUU 3 ZA KONDOO...*
-Wasikifu
-Watulivu na Wapole
-Wafuasi wa Mchungaji Wao
..Ndivyo Hata Kanisa, Limejaa Watu Wa Aina Mbili, *Wale Yesu Anawaita KONDOO na Wengine ni MBUZI*
I). *WATU AINA YA KONDOO...*
-Wasikivu kwa Mchungaji Wao (Yesu)
-Watiifu Kwa Mchungaji
-Wanafata Kile Neno Limesema
-Sio Wakaidi Katika Neno
-Sio Walafi Wala Wakorofi
-Wanaogozwa na Neno, Hawajiogozi Wenyewe
-Wapole na Wanyenyekevu
-Wanajulikana kwa Mungu
-Wanawajali Wengine hasa Wagonjwa, Wafungwa n k
ii). *WATU AINA YA MBUZI...*
-Hawasikii Chochote Kuhusu Mchungaji Wao
-Walafi Kupitia Kiasi
-Hawatulii Na Mke/Mme Mmoja
-Wanahudhuria Semina, Jumuiya na Kanisani Lakini Hawana badiliko Lolote!
-Hawako Tayari Kuwasaidia Wengine Hasa Wahitaji
-Leo Utawakuta Kanisa Hili, Kesho Wako Kwa Kanisa Jingine
-Maneno na Matendo Yao Haviendani
-Hawatii Amri Wala Sheria ya Mchungaji Wao (Yesu)
-Wabinafsi Kwa Karama Walizojaliwa
-Wakorofi na Wagomvi
Mungu Asema Wazi...
"KONDOO Wangu WAISIKIA SAUTI Yangu; *Nami NAWAJUA, Nao WANIFUATA."*
(Yoh 10:17)
*JIULIZE MWENYEWE...*
-Wewe ni Msikifu ?
-Wewe Mungu Anakujua?
-Wewe ni Mfuasi wa Kweli?
K**a Jibu ni NDIO Basi Wewe ni KONDOO, *K**a Jibu ni HAPANA Tambua Wewe ni MBUZI-MTU!*
..Na MBUZI Mwisho Wao ni Katika MOTO wa MILELE *pale Mungu Atakavyowabagua na Kuwatenga!*
"...Atawaweka KONDOO Mkono wake wa KUUME, *na MBUZI Mkono wake wa KUSHOTO."* (Math 25:33)
..Kwaresma Ni Muda Wa Mabadiliko.