29/12/2025
Ninachukua fursa hii kumshukuru sana Bwana Mungu Aliyetulinda na kututunza na kutuwezesha kuchukua kombe la timu ya football! Ndugu zangu, hata michezo ikichezwa kwa kumtanguliza Bwana, pia ni *jambo la kiroho!*
Hivyo ninawapongeza sana waandaaji wa mashindano haya, ninawapongeza wote waliohusika kuiandaa timu yetu, ninawapongeza walioifadhili timu yetu kwa namna yoyote ile, ninawapongeza washarika wote, na
SANA SANA, NINAWAPONGEZA SANA WACHEZAJI WETU WALIOCHEZA KWA BIDII KUBWA, BILA KUKATA TAMAA!
Ushindi huu ni wetu sote, na kwa pamoja tunamtukuza Bwana kwa ushindi huu.
Hakika tutaandaa siku ya kuwapongeza mashujaa wetu.
Ninawaombea wachezaji wetu na vijana wote *mzidi kuimarika kiroho na katika michezo!*
Baada ya kupokea kombe, tulirudi Madhabahuni kumshukuru Bwana ππ»
Bwana Mungu Azidi kutubariki sana sisi soteππ»
(Ni maneno ya Mchungaji Kiongozi ).