06/04/2020
Na, Amedeus J. Shio
*HIVI MWAMKE KUJIPAMBA NI DHAMBI?*
*NI KWELI BIBLIA IMEKATAZA MWANAMKE KUJIPAMBA?*
📖📖📖📖📖📖📖📖📖📖
Isaya 61 : 10 - Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, k**a bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na *k**a bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.*
📡📡📡📡📡📡📡📡📡📡
Hivi kuvaa hereni, mikufu, bangili, vikuku, ni dhambi?
Kusuka rasta na mitindo mingine ya nywele nayo ni dhambi?
Kupaka rangi, shedo, wanja, poda nk. Nako ni dhambi?
Upi ukweli wa mambo haya?🤔
Baada ya kuyachunguza maandiko kwa mda mrefu, k**a mwanafunzi wa biblia, na kupata uhakika wa mambo yale yaliyokuwa tata kwangu, naligundua ukweli ufuatao.👇
Kibiblia, hakuna dhambi yoyote katika hayo.
Biblia haijakataza mwanamke kujipamba.
Wanaokataza kujipamba ni watu tu kwa aidha kukosa tafsiri sahihi ya maandiko, au kuridhisha nafsi zao.
Yaani mtu anaweza akakataza kitu kwa kuwa tu yeye binafsi hapendi..na kwa sababu anataka aaminike, anatafuta maandiko ya kumuunga mkono hoja yake, hata kwa kuyalazimishia.
👇👇
Yeremia 23 : 16 - "Bwana wa majeshi asema hivi, Msisikilize maneno ya manabii wakiwatabiria; huwafundisha ubatili; *hunena maono ya mioyo yao wenyewe;* hayakutoka katika kinywa cha Bwana."
Biblia inasema tunapaswa kuhubiri neno la Mungu kwa uaminifu.👇👇
Yeremia 23 : 28 - "Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na *yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu.* Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema Bwana."
Tusilitangue neno kwa mapokeo yetu ya kidini. Tuache mapokeo ya kidini, tuhubiri ukweli wa biblia.👇👇
Marko 7 : 13 - *"huku mkilitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyopokeana;* tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo."
Lengo la somo hili si kushawishi watu kujipamba, bali ni kuuleza ukweli wa swala hili katika biblia.
K**a nilivoeleza hapo juu, narudia tena kusema, kujipamba sio dhambi kibiblia.
Mwanamke ni kawaida kabisa kujipamba, na biblia haijakataza swala hilo.
Lakini kabla ya kujipamba jiulize maswali yafuatayo👇👇
*1.* Je! Kujipamba kwangu kunaharibu mahusiano na ukaribu wangu na Mungu?
Mathayo 18 : 8 - "Basi mkono wako au mguu wako *ukikukosesha, ukate ukautupe mbali nawe;* ni afadhali kuingia katika uzima hali umepungukiwa na mkono au mguu, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele."
K**a kwa sababu ya kujipamba unachelewa kanisani, unashindwa kujiachia ukiwa kwenye maombi, unashindwa kumwabudu Mungu kwa kuogopa kuharibu make-up, nakushauri ni bora uache.
Bora uache kujipamba kuliko kuharibu mahusiano yako na Mungu.
Paulo aliiona hiyo hatari kwenye kanisa moja, akaamua kuwaonya kwa hilo. Aliona walikuwa wakijipamba lakini mahusiano yao na Mungu hayakuwa mazuri.
Walikuwa wakiacha kutilia mkazo mambo ya rohoni, badala yake wako busy na mambo ya mwilini k**a kuvaa mavazi ya gharama nk..
Tunasoma, 👇👇
1 Timotheo 2 : 9 - "Vivyo hivyo *wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;"*
Ukisoma hapo kwa makini👆utagundua paulo hakukataza kujipamba. Anasema, *"Wanawake na wajipambe"* , kwa hiyo Hakukataza wasijipambe.
Ila alitaka wazingatie katika kujipamba kwao, mambo matatu:
🔐Mavazi ya kujisitiri
🔐Adabu nzuri
🔐Moyo wa kiasi
Hebu tuone na Petro anasemaje 👇👇
1 Petro 3 : 3 - 4 "Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu."
Petro anasisitiza mambo mawili katika kujipamba: roho ya upole, na roho ya utulivu.
Hajakataza kujipamba. Alimaanisha waanze na mapambo ya ndani kwanza(moyoni), ndipo kujipamba kwa nje kutakuwa na maana.
Wao walijipamba tu nje, lakini ndani yao hawakuwa sawa.
Ok, ngoja labda nikuletee tafsiri ya kiingereza kwenye hiki kifungu, utanielewa tu..👇👇
"Your adornment must not be *merely external*—with interweaving and elaborate knotting of the hair, and wearing gold jewelry, or [being superficially preoccupied with] dressing in expensive clothes; but let it be [the inner beauty of] the hidden person of the heart, with the imperishable quality and unfading charm of a gentle and peaceful spirit, [one that is calm and self-controlled, not overanxious, but serene and spiritually mature] which is very precious in the sight of God."
1 Peter 3:3-4 AMP
Naamii umeona neno merely hapo. Hilo neno limetumika kuonesha kujipamba kwenu kusiwe kwa nje peke yake, yaani kusiwe kujipamba ambako hakuna maana, bali ili kulete maana changanyeni na mapambo ya ndani.
Me nafkiri umeelewa bhana, labda uwe ulijiandaa kutokuelewa..😅
Najua kuna watu dini zimewaingia kiasi kwamba hata kuwaelimisha kweli ya Mungu inakuwa shida kweli. Wameshaweka ngome zao tayari. Watu wa namna hii ni kazi sana.
Ukitaka kuelewa kweli halisi ya biblia ni lazma uvue udini kwanza.
Anyway, tuendelee na somo letu jamani..
Tunza mahusiano yako na Mungu. Angalia mapambo na makeup ambazo hazikuondolea Uhuru wako na Kristo.
Hapa ndipo wengine hupata kitu tunaita personal conviction ya kuacha kabisa kujilamba. Kuna watu Mungu huwazuilia kabisa kujipamba.
K**a na wewe Roho Mtakatifu anakushuhudia kutokujipamba, mtii. Lakini usilazimishe na wengine wawe k**a wewe; umekatazwa wewe kibinafsi.
Ukiamua kujipamba sawa, na ukiamua kutojipamba sawa; cha muhimu tunza mahusiano yako na Mungu.
*2.* Je! Kwa nini nataka kujipamba?(motive behind).
Watu hujipamba kwa sababu mbalimbali:👇
*A).* Kujipamba kwa ajili ya miungu migeni.
👇
Mwanzo 35 : 4 - "Nao wakampa Yakobo miungu migeni yote iliyokuwa mikononi mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu."
Hizo pete za masikioni zinazozungumziwa hapo ni hereni(rings). Lakini walizivaa hizo hereni k**a kinga(hirizi). Ndio maana ilibidi waziondoe ili kutembea na Mungu.
Hebu tusome kwenye tafsiri ya kiingereza, 👇👇
"So they gave Jacob all the [idols and images of the] foreign gods they had and *the rings which were in their ears [worn as charms against evil],* and Jacob buried them under the oak tree near Shechem."
Genesis 35:4 AMP
Naamini umeona hapo👆, walivaa hereni k**a kinga(charms). Otherwise, wasingekuwa na haja ya kuzivua.
Kuvaa hereni sio dhambi. Ilamradi huvai k**a hirizi ya kukulinda. Unavaa ili upendeze.
Kuna watu wanasema ati mapambo ni miungu. Sijui wanasoma biblia gani?!🤷♂️
Hiyo miungu hapo kwenye hilo andiko hayakuwa mapambo jamani, vilikuwa vinyago(idols), na vijisanamu) tu. Walikuwa wamevibeba mikononi.
Someni hilo andiko vizuri mwelewe.👆
Usivae pete, hereni, mikufu, vikuku, ama chochote kwa lengo la kulata majini ya bahati, kuvuta mpenzi wako, kukulinda nk..hayo ni machukizo kwa Mungu.
Huko ni kujiungamanisha na miungu migeni.
Jipambe tu kwa lengo la kupendeza inatosha.
*B).* Kujipamba kwa sababu unahisi Mungu kakuumba vibaya. Yaani unajipamba kwa lengo la kumkosoa Mungu. 👇
Warumi 9 : 20 - "La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, *Kwani kuniumba hivi?"*
Kubali ulivyoumbwa mpendwa. Usijichukie kwa kuwa wewe ni mweupe ama mweusi, au ulitaka kuwa na kichwa cha aina flani.
Usijipambe kwa lengo hilo. Ni lazma ujikubali kwanza, ndipo ujipambe.
Pamba uzuri aliukupa Mungu.
Vyovyote ulivyo, wewe ni mzuri tayari kwa asili. Usipojikubali hivyo, kuna shida si ndogo.
Mapambo hayana maana ya kukupa uzuri ambao huna, bali kupamba uzuri uliopewa na Mungu tayari.
Sema amen, k**a umenielewa..💪
Kujipamba sio kubadili uumbaji wa Mungu, kujipamba ni kupendezesha uumbaji wa Mungu.
Kwanza huwezi kujibadili hata hivyo. Labda ufanyiwe scientific procedures.
Narudia, jikubali kwanza ndipo ujipambe.
Mwanzo 1 : 31 - *"Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana.* Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita."
Kila unapojitazama kwenye kioo, jisemee hili andiko👇
Zaburi 139 : 14 - *"Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.* Matendo yako ni ya ajabu, *Na nafsi yangu yajua sana,"*
Bwana Yesu asifiwe..👍
*C).* Kujipamba kwa ajili ya kuwanasa wanaume au ukahaba. Tunao mfano wa mwanamke Yezebeli. Yeye alijipamba kwa ajili ya ukahaba. Tunasoma, 👇👇
2 Wafalme 9 : 30 - "Hata Yehu alipofika Yezreeli, *Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake,* akachungulia dirishani."
Huyu Yezebeli alijipamba kwa sababu ya ukahaba. Je! Wewe unajipamba kwa sababu gani?
Hata leo makahaba hujipamba vile vile ili waweze kunasa wanaume kwa urahisi, na wanafanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Kujipamba ukiwa na nia mbaya k**a hii ni bure kabisa katika ukristo wako. Utaona k**a wanaume wanakusifia lakini wanakudanganya tu wakuchezee na kukuacha. Hebu soma hapa..👇👇
Yeremia 4 : 30 - "Na wewe, utakapotekwa, utafanyaje? Ujapojivika mavazi mekundu, *ujapojipamba mapambo ya dhahabu, ujapojitia wanja machoni, unajifanya kuwa mzuri bure tu; wapenzi wako wanakudharau; wanakutafuta roho yako."*
Kujipamba ili uangushe wanaume, biblia inasema, wanaume hao wanakudharau tu. Huna lolote. Hiyo ni nia mbovu kabisa.
Usijipambe kwa mavazi ya kikahaba👇
Mithali 7 : 10 - "Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana *mavazi ya kikahaba,* mwerevu wa moyo;"
Vaa mavazi ya kujisitiri(modest apparel).
Hata k**a ni suruali, iwe ya kusitiri(modest).
Uwe na nia njema unapojipamba. Hakikisha kwa ujumla wake, unajipamba kwa utukufu wa Mungu.👇
1 Wakorintho 10 : 31 - "Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, *fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.*"
Wakolosai 3 : 17 - "Na *kila mfanyalo,* kwa neno au kwa tendo, *fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu* Baba kwa yeye."
1 Wakorintho 6 : 20 - "maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, *mtukuzeni Mungu katika miili yenu.*"
Hakikisha unajipamba ili upendeze kwa lengo la kumtukuza Mungu. Otherwise recheck the motivation behind adornment.
Bila shaka tumeelewana hapo.
*3.* Je! Kujipamba kwako kunakwaza wengine?
Je! Unajipamba kiasi cha kuwafanya watu wasiendelee mbele na Yesu?
Luka 17 : 1 - "Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini *ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!"*
Jifunze kujipamba kwa kiasi mpendwa.
Biblia inasema tuwe na kiasi katika mambo yote.👇
2 Timotheo 4 : 5 - "Bali wewe, *uwe na kiasi katika mambo yote,* vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako."
Mambo yote ni pamoja na kujipamba. Jipambe kwa kiasi.
Utajuaje hicho kiasi ndio sawa?!
Roho mtakatifu atakuambia. We mwulize kila unapojipamba, utapata ushuhuda wa Roho ndani yako.
Warumi 8 : 14 - "Kwa kuwa wote *wanaoongozwa na Roho wa Mungu,* hao ndio wana wa Mungu."
Ukijifunza kujipamba kwa kiasi, huna haja ya kuwekewa sheria.
Wagalatia 5 : 23 - "upole, *kiasi; juu ya mambo k**a hayo hakuna sheria."*
Bila shaka umenelewa kwa uzuri. Hallelujah!
Hayo yalikuwa ni baadhi ya maswali machache ya kujiuliza kabla ya kuchukua msimamo wa kujipamba.
Mwanamke kujipamba sio dhambi. Tusifiche ukweli kwa sababu za kifarisayo.
Wanawake wengi wanaokatazwa kujipamba kwenye dini zao, mioyoni mwao wanatamani ila basi tu. Wameamua tu kuishi kinafiki. Hiyo ni mbaya zaidi. Nawashauri waache unafiki na waishi uhalisia wa wanachokiamini.
Wanaambiwa waachane na kujipamba lakini asili inagoma.(woman nature).
Wameumbiwa kujipamba..👇👇
Yeremia 2 : 32 - *"Je! Mwanamwali aweza kusahau mapambo yake,* au bibi arusi mavazi yake? Lakini watu wangu wamenisahau mimi kwa muda wa siku zisizo na hesabu."
Anasahauje kwa mfano?!😇
Anyway, somo letu limeishia hapo kwa sasa.
Wale mliochukizwa na somo hili sababu ya misimao yenu ya kidini, niwaulize swali, 👇
Wagalatia 4 : 16 - *"Je! Nimekuwa adui wenu kwa sababu nawaambia yaliyo kweli?"*🤷♂️
Biblia inasema, 👇
Yohana 8 : 31 - 32 "Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; *tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru."*
Uhuru wa kweli unapatikana ndani ya Neno, sio kwenye misimamo ya kidini.
Bwana Yesu akubariki mpendwa..🙋♂️
Prepared by,
Amedeus J. Shio
0766 120 520
03/04/2020.